monotheist
JF-Expert Member
- Apr 30, 2017
- 830
- 1,449
Nilikua na hamu ya ndizi nyama hivyo kwa kua nalijua jiko nikapita zangu sokoni nikachukua mazaga kadhaa nikaingia jikoni😆 na nitawaelezea jinsi nilivyopika hatua kwa hatua
MAHITAJI;
Carry powder, paprika powder, black pepper, soya souce, tui la nazi (tui la 1 na tui la 2), ndizi mshale 8, nyama nusu, carrot na pilipili hoho (paprika)
Nikachemsha nyama hadi zikaiva na kulainika kabisa mimi huwa sipendi nyama ngumu
Baada nyama kuiva nikabadilisha sufuria maana ilikua ndogo nikaweka ndizi zilizokatwa vipande vidogo kisha nikachanganya paprika powder, black pepper, carry powder, soya souce na chunvi
Baada ya kukoroga na kuhakikisha viungo vimekolea vizuri nikaweka nyama na tui la nazi la pili
Kisha nikaweka mchuzi wa nyama
Baada ya hapo nikafunika ili mchanganyiko wangu uive kwa muda fulani
Baada ya mchanganyiko kuiva nikaongeza hoho, carrot na tui la kwanza (tui zito)
Kisha nikafunika tena kwa dakika kadhaa ili mchanganyiko uive vizuri baada ya dk kama nane chakula chetu kilikua tayari kwa kuliwa
Chkula kilikua chamoto sana na kitamu chenye radha nzuri na kinanukia
Natamani niwaonjeshe utamu wa hiki chakula ila ndo hivyo tena haiwezekani😜 na pia wengi watajiuliza ulikunaje nazi? Jibu nilitumia blender kisha nikaichuja
Wale tulio single bila wapenzi tuwe na mazoea ya kupika tukipata muda vyakula vya mama ntilie vipo kibiashara zaidi na pia vina kasoro nyingi mno
Mimi ni mtu wa pwani napenda sana chakula kilichopikwa kwa mchanganyiko wa nazi juzi nilitoka mafia nikambebea mama nazi za kutosha chache nikabaki nazo
MAHITAJI;
Carry powder, paprika powder, black pepper, soya souce, tui la nazi (tui la 1 na tui la 2), ndizi mshale 8, nyama nusu, carrot na pilipili hoho (paprika)
Nikachemsha nyama hadi zikaiva na kulainika kabisa mimi huwa sipendi nyama ngumu
Baada nyama kuiva nikabadilisha sufuria maana ilikua ndogo nikaweka ndizi zilizokatwa vipande vidogo kisha nikachanganya paprika powder, black pepper, carry powder, soya souce na chunvi
Baada ya kukoroga na kuhakikisha viungo vimekolea vizuri nikaweka nyama na tui la nazi la pili
Kisha nikaweka mchuzi wa nyama
Baada ya hapo nikafunika ili mchanganyiko wangu uive kwa muda fulani
Baada ya mchanganyiko kuiva nikaongeza hoho, carrot na tui la kwanza (tui zito)
Kisha nikafunika tena kwa dakika kadhaa ili mchanganyiko uive vizuri baada ya dk kama nane chakula chetu kilikua tayari kwa kuliwa
Chkula kilikua chamoto sana na kitamu chenye radha nzuri na kinanukia
Natamani niwaonjeshe utamu wa hiki chakula ila ndo hivyo tena haiwezekani😜 na pia wengi watajiuliza ulikunaje nazi? Jibu nilitumia blender kisha nikaichuja
Wale tulio single bila wapenzi tuwe na mazoea ya kupika tukipata muda vyakula vya mama ntilie vipo kibiashara zaidi na pia vina kasoro nyingi mno
Mimi ni mtu wa pwani napenda sana chakula kilichopikwa kwa mchanganyiko wa nazi juzi nilitoka mafia nikambebea mama nazi za kutosha chache nikabaki nazo