Leo nimeshiriki tambiko, kumbe wazungu walitudanganya, hamna uchawi wowote kwenye tambiko

Leo nimeshiriki tambiko, kumbe wazungu walitudanganya, hamna uchawi wowote kwenye tambiko

Wazungu ni watu wabaya sana, kumbe tambiko ni ibada kama nyingine na mnyama anayechinjwa anatolewa sadaka na analiwa na wote.

Tambiko lilianza kwa kumuweka ng'ombe kwenye matawi ya mti wa Ululambuli, kisha akachinjwa. Alipochinjwa akachunwa ngozi, akatolewa nyama za kifuani, zikatengenezwa mishikaki, sehemu nyingine zikakatwa katwa.

Nyama ikachomwa kuelekea jua linapotoka, maombi yakafanyika, hatukutaja mashetani, wala hatupandisha majini. Tulimwita Mungu ambaye humwita Sebah.

Baada ya kusali na kila mtu kutaja hitaji la moyo wake, ibada ikaisha, tukaanza kuzila zile nyama za kuchomwa kwa furaha.

Kwa kweli nilifurahi sana kufanya ibada ya kikwetu haswa, sio longolongo za kina Carl Peters na walaghai wengine


Lyubha, Wangaluke, Welelo, Mungu, Sebah.
Mimi nilipata matatizo fulan nikaenda kwa babu yangu kufanyiwa tampico, kiufup nilikua sijui chochote kuhusu tambiko na nilishindwa kukataa kwasababu niliambia tatizo hilo litakwisha.

Kiukweli sikuona kitu cha ajabu sana kama tunavoaminishwa na wahuni wachache wanaopotosha mila zetu , mbuzi alichinjwa kabla ajafa wakamtoboa tumbo wakamtoa sjui ni nini na mavi wakachukua wakawa wanaongea kiluga maneno ambayo kwa tafsir si mabaya ni yakawaida ya kuomba na baadae walinipaka yale mavi ya mbuzi tukala zile nyama na ugali basi .. na mtatizo yale kiukweli yalikwisha kabisa yenyewe
 
Mimi nilipata matatizo fulan nikaenda kwa babu yangu kufanyiwa tampico, kiufup nilikua sijui chochote kuhusu tambiko na nilishindwa kukataa kwasababu niliambia tatizo hilo litakwisha.

Kiukweli sikuona kitu cha ajabu sana kama tunavoaminishwa na wahuni wachache wanaopotosha mila zetu , mbuzi alichinjwa kabla ajafa wakamtoboa tumbo wakamtoa sjui ni nini na mavi wakachukua wakawa wanaongea kiluga maneno ambayo kwa tafsir si mabaya ni yakawaida ya kuomba na baadae walinipaka yale mavi ya mbuzi tukala zile nyama na ugali basi .. na mtatizo yale kiukweli yalikwisha kabisa yenyewe
kabila gani?
 
Wazungu ni watu wabaya sana, kumbe tambiko ni ibada kama nyingine na mnyama anayechinjwa anatolewa sadaka na analiwa na wote.

Tambiko lilianza kwa kumuweka ng'ombe kwenye matawi ya mti wa Ululambuli, kisha akachinjwa. Alipochinjwa akachunwa ngozi, akatolewa nyama za kifuani, zikatengenezwa mishikaki, sehemu nyingine zikakatwa katwa.

Nyama ikachomwa kuelekea jua linapotoka, maombi yakafanyika, hatukutaja mashetani, wala hatupandisha majini. Tulimwita Mungu ambaye humwita Sebah.

Baada ya kusali na kila mtu kutaja hitaji la moyo wake, ibada ikaisha, tukaanza kuzila zile nyama za kuchomwa kwa furaha.

Kwa kweli nilifurahi sana kufanya ibada ya kikwetu haswa, sio longolongo za kina Carl Peters na walaghai wengine


Lyubha, Wangaluke, Welelo, Mungu, Sebah.
Hata ukivunja nazi njia panda hakuna ushirikina wowote. Ni wazungu tu wameharibu akili zetu😂😂😂😂
 
Tambiko langu lilikua Miaka ya early 80 huko.safari ilikua ndefu sana na nilikua bado mdogo ila naona na kuelewa kila kinachofanyika.
Tumefika kabla hata kupumzika tukakuta kila kitu tayari.

Aliletwa Kondoo,akachinjwa pale naona damu inamwagika wakakinga kibuyu bado
kondoo anatapatapa
nikakamatwa nyweshwa damu ile ikiwa moto kabisa km maziwa.
Mi hata sielewi nini hii.
Nililialia kidogo
nyamachoma tayari tukala,wakasali shughuli ikaisha.
Sijawai kupenda nyama ya kondoo tokea hapo mpk leo.
 
Wazungu ni watu wabaya sana, kumbe tambiko ni ibada kama nyingine na mnyama anayechinjwa anatolewa sadaka na analiwa na wote.

Tambiko lilianza kwa kumuweka ng'ombe kwenye matawi ya mti wa Ululambuli, kisha akachinjwa. Alipochinjwa akachunwa ngozi, akatolewa nyama za kifuani, zikatengenezwa mishikaki, sehemu nyingine zikakatwa katwa.

Nyama ikachomwa kuelekea jua linapotoka, maombi yakafanyika, hatukutaja mashetani, wala hatupandisha majini. Tulimwita Mungu ambaye humwita Sebah.

Baada ya kusali na kila mtu kutaja hitaji la moyo wake, ibada ikaisha, tukaanza kuzila zile nyama za kuchomwa kwa furaha.

Kwa kweli nilifurahi sana kufanya ibada ya kikwetu haswa, sio longolongo za kina Carl Peters na walaghai wengine


Lyubha, Wangaluke, Welelo, Mungu, Sebah.
Wewe msukuma? Hakuna msukuma ambaye hana hizo imani. Nakumbuka Dr. Ngwandu alitaka mambo hayo yahalalishwe. Joseph Mihangwa, zamani Rai, naye aliandika sana kutaka uhalali wa hayo makitu.
Kazi sana.
 
Tambiko langu lilikua Miaka ya early 80 huko.safari ilikua ndefu sana na nilikua bado mdogo ila naona na kuelewa kila kinachofanyika.
Tumefika kabla hata kupumzika tukakuta kila kitu tayari.

Aliletwa Kondoo,akachinjwa pale naona damu inamwagika wakakinga kibuyu bado
kondoo anatapatapa
nikakamatwa nyweshwa damu ile ikiwa moto kabisa km maziwa.
Mi hata sielewi nini hii.
Nililialia kidogo
nyamachoma tayari tukala,wakasali shughuli ikaisha.
Sijawai kupenda nyama ya kondoo tokea hapo mpk leo.
Tutalirudia, utapenda tu nyama
 
Back
Top Bottom