Leo nimetafakari sana kifo cha Rais Benjamin Mkapa

Leo nimetafakari sana kifo cha Rais Benjamin Mkapa

Status
Not open for further replies.
Nikiri mbele yenu wanajamvi wenzangu mimi ni mvivu tena "nyambole" kabisa wa kusoma nyuzi ndefu humu jf japo kwingineko nasomagasomagapo si haba, Leo kwa Mara ya kwanza nimesoma Uzi mpaka mwisho na komenti zake zote, hakika mtoa mada ametafakari na amenitafakarisha na Mimi.

Amenikumbusha reflection ya mtaalamu mmoja wa maisha ya kiroho (bado yu hai) aliyewahi kuhoji uhalali wa maneno "Bwana ametoa na Bwana ametwaa...." Kutumika ktk misiba hasa ya wakristo akidai kuna mahala maneno hayo yanatumika kimakosa kwani misiba mingine iko dhahiri "Bwana hajatwaa" akitolea mfano wa vifo vitokanavyo na ajali hasa za bodaboda (kugongwa ama kugonga).

Imani inafundisha kuwa "kifo ni mpango wa Mungu" na hivyo ukihoji sana mambo mengine unaweza kujikuta "unamkufuru Mwenyezi" lakini kadiri ya mang'amzi ya tawala za kibinadamu "mambo kama haya" yanakuwagepo wakati mwingine, Mwisho wa nyakati zitakapofunuliwa siri zote za mioyo ya watu, tutafahamu pasi na shaka....

#RIP BWM.
 
MTANZANIA HANA KAWAIDA KUSOMA VITABU HICHO KITABU HAWAJAKISOMA NDUGU WENGI WAMEPEWA WAMEWEKA KWENYE KABATI KAMA UREMBO
 
Ni miezi takriban minne sasa tangu Rais Mstaafu BWM atutoke. Bila ubishi, Rais Mkapa alikuwa na ushawishi mkubwa ndani ya siasa za CCM, na ni ukweli usio na shaka kuwa outcome ya siasa za CCM za uchaguzi wa mwaka 2015 ambazo yeye alishiriki kikamilifu ndizo leo hii tunaishi kwa consequences zake. Pamoja na hayo nimetafakari sana juu ya kifo chake na kujaribu kufikiria leo angekuwa hai angekuwa na fikra gani au angeshawishi vipi mwenendo wa serikali hii pamoja na chama chake. Nimetafakari sana pia urais wa huyo mheshishimiwa.

1. Ni mwaka 1995,Mkapa achaguliwa kuwa rais, ala kiapo na kisha kusema wapinzani ni mkono mmojawapo katika mikono yake miwili ya kufanya kazi
Mwaka 1995 baada ya kuapishwa pale uwanja wa uhuru, Mkapa atoa hotuba na kulihutubia Taifa, asema Wapinzani ni watu muhimu kwa maendeleo ya Taifa, Asema mawazo mbadala katika nchi ni kitu chanya kwa Taifa na akasema Wapinzani ni kama mkono mmoja katika mikono yake miwili, na kuwa chama chake ni kama mkono wa pili wote wanahitajika kwa ajili ya usitawi wa nchi.

Miaka 25 baade tumepata rais Mwingine, anayeonekana ana nia ya kuua upinzani, anayewaambia wananchi kuwa pindi wakichagua wasimchanganyie, anawaambia wananchi kuwa wakichagua upinzani katika maeneo yao hatopeleka maendeleo!. Hii ndo Tanzania ya leo, tofauti na miaka 25 iliyopita!. Najiuliza je Mkapa angekuwa hai leo hii akashuhudia aliyoshiriki kuyaasisi mwaka 2015 angekaa kimya ndani ya Chama? - Naamini angemwambia John bila kupepesa macho kuwa John hili unalofanya siyo sahihi badilika!

2. Mkapa atoa kitabu ajuta Mauaji ya Zanzibar
Mwaka mmoja au miwili nyuma kabla ya kifo chake rais Mkapa atoa, kitabu, ajuta kwelikweli ndani ya kitabu hicho mauaji ya watu wasio na hatia huko Zanzibar. Mauaji yale yawa mzigo kwenye mtima wake, yamkosesha raha. Miaka 19 baadae, mauaji yanatokea tena, wananchi wa Zanzibar wauawa, wateswa sababu tu ili Tanganyika iweze kuendelea kuweka mtawala inayemtaka huko Zanzibar. Je Mkapa angekuwepo hai, leo hii angemueleza John kitu gani? - Angemwambia John kuwa uko sahihi well done endelea hivyohivyo? au angemwambia John kuwa usirudie makosa niliyofanya mimi mwaka 2001 waachie Wazanzibari wamchague wanayemtaka?

3. Ni Siku chache kabla ya kifo chake, Wastaafu waitwa dodoma kujadili mtu wa kumpa kijiti cha kuongoza Zanzibar, Mkapa naye ahudhuria
Ni siku chache tu kabla ya kifo chake, Mkapa alikuwa na wenzie, Ali, Jakaya John, Shein na Mama Maria, moja ya kitu walichojadili ni mtu wa kumpa uraisi huko Zanzibar. Kitu kiichoniijia kichwani, hivi Mkapa alikubaliana kweli na wenzie wampe mtoto wa Ali uraisi? - Mkapa huyuhuyu ambaye Sumaye anasema kuwa wakati wakiwa madarakani walikubaliana wasiwape watoto wao vyeo ili kuondoa nepotism ndo eti atakuwa alikubaliana na wenzie kuleta na kulea utamaduni wa Kisultani nchini? - Akili yangu inaniambia kuwa Mkapa lazima alikataa hilo wazo, haiwezekani Mkapa huyu anayejuta kutokana na maafa ya kuwapandikizia Wazanzibar mtawala mwaka 2000 eti akubali tena kurudia dhambi ileile iliyopelekea kuuawa Wazanzibari huko Pemba mwaka 2001. Kwa hiyo akili yangu inaniambia kuwa Mkapa hakuwa onboard kwenye wazo la kumfanya Hussein kuwa Sultan huko Zanzibar.

4. Mkapa afariki, hatukutangaziwa na mkuu wa nchi ugonjwa uliomuua
Mkapa afariki, sheria inasema anapofariki kiongozi mstaafu lazima umma utangaziwe na rais aliyeko madarakani, na katika tangazo hilo mtangazaji inabidi aeleze kilichomuua mgonjwa. Sisi kwetu kweli tulitangaziwa msiba, lakini katika tangazo lile hatukuambiwa mgonjwa kafia nyumbani au kuambiwa jina la hospitali husika kama kafia hospitali. Nimetafakari sana kwa nini taarifa hizo hazikuwa kwenye tangazo? - kwa mujibu wa sheria, Umma si ulikuwa na haki ya kujua hizo info?, kwa nini zilikuwa vague sana?

5. Maombolezo yafanyika, Msiba haukuwa na kiongozi high profile kutoka nje ya nchi
Nimetafakari sana hili suala, nikasema kwa nini viongozi wa nchi jirani hawakuja? Nikasema labda ni Korona, lakini nikafikiria tena, Burundi nao sera yao ya korona si ilikuwa kama sisi na ni marafiki wetu wakubwa kwenye ukanda huu? Kwa nini rais mpya Ndaisheye hakuja? Sijapata jibu.

Kama ni Korona mbona basi raisi Museveni baadae alikuja na convoy yae wamevaa mask kwa ajili ya mradi wa Bomba la Mafuta wakati nchini kwake bado wanapambana na Korona? Kwanini baadae kabla ya uchaguzi Mkuu rais wa Burundi alikuja TZ? Mbona na rais wa Malawi alikuja baadae kipindi cha Kampeni?

6. Maombolezo yaendelea na watu waendelea na shughuli zao utadhani hakuna msiba
Nimetafakari sana hili, wakati mwili wa Marehemu umelala uwanja wa Uhuru hapo Dar, hakuna hata siku moja shule za msingi au sekondari au vyuo zilifungwa ili watoto na walimu wakatoe heshima kwa rais wao wa zamani, Lakini John alipokuwa akienda kwenye kampeni katika jimbo la uchaguzi basi shule zitafungwa, watumishi wa serikali watapewa notice ya lazima wahudhurie mikutano yake, Najiuliza serikali ya John ilishindwaje kuwapa ruhusa maalum watumishi wa serikali kwenda kuuaga mwili wa BWM kama heshima kwake? - Sitegemei jibu liwe eti Jumamosi au Jumapili watu wangeweza kwenda kutoa heshima zao za mwisho, hizo kwa wengine bado ni siku za kwenda kwenye ibada!

7. Ben alitaka tume huru ya uchaguzi
Kabla ya kifo chake, ndani ya kitabu chake, Ben ni kama anaungama, kuna kitu anakisema, kinamuuma roho. Anaona wazi kuwa taratibu za chaguzi nchini haziko fair, hazina haki. Ben anataka tume huru ya uchaguzi ili wananchi wachague viongozi wao haki bin haki - Je Ben angekuwa hai leo hii akajionea hii tume ya John na Mahera wake, Ben angesemaje? - Naamini Ben angemwambia John kuwa Mwanangu sasa hii unachofanya umezidisha hatuendi hivyo!! , hebu achana na uharibifu huu haukusaidii wewe wala nchi!

8. Swali moja ambalo bado nahaingaika nalo, JE BEN ANGEUNGA MKONO MOVE YOYOTE YA KUBADILI VIPINDI VYA UTAWALA KWENYE KATIBA? - Hell no, maana huko nyuma amewahi kusimama kidete kumzuia Salmin Amour kubadili katiba kuendelea kuitawala Zanzibar!

Tangulia Ben, Kifo chako kinaniachia maswali mengi kuliko majibu!!!
Kuna tabia ya kuanza ku edit historia watu wakifariki.

Ukweli ni kwamba, kuna consistency katika kubana uhuru Tanzania kutoka Nyerere mpaka Magufuli.

Mkapa ndiye Godfather wa Magufuli. Miaka yote hiyo Magufuli alivyominya upinzani Mkapa alishindwa nini kukemea?

Marais wawili ambao kidogo walijaribu kujiondoa kwenye kuminya mawazo mbadala ni Mwinyi na Kikwete. Mwinyi zaidi.

On a large scale, hakuna ambacho anafanya Magufuli leo ambacho Nyerere hajafanya. Tofauti pekee ni kwamba, Magufuli anafanya kwa nguvu na kijinga, na Nyerere alifanya kwa siasa ya hali ya juu na ujuzi wa hila za Ki Makaveli.

Magufuli kaminya vyama vya upinzani? Nyerere alivifuta kabisa. Kwa miaka takribani 30.

Magufuli kawafanya wapinzani wakimbie nchi? Nyerere alikimbiza kina Kambona na Masha.

Magufuli kaiba kura? Nyerere alibariki matokeo ya chaguzi kubadilishwa Zanzibar tangu enzi za chama kimoja.

Unajiuliza Mkapa angefanyaje?

Huwa sipendi kuhariri historia.

Ila jiulize.

Katika maisha yake alifanya nini kumkemea Magufuli?

Kitu pekee Mkapa alichomkemea Magufuli ni kuita serikali "serikali ya Magufuli" badala ya " serikali ya CCM". Or something to that effect. As if this credit grab is the most atrocious thing Magufuli has done.

Katika mabaya yote ya Magufuli, hilo ndilo aliloliona muhimu kabisa kukemea.

On that topic, bora hata Nyerere alimkemea Mwinyi kwa kuvunja katiba.

Angalau Nyerere alikemeq jambo la msingi. Wazi.

Magufuli amevunja katiba kipindi chake cha kwanza chote, mara nyingi tu, mfano kwa kukataza wapinzani kufanya mikutano.

Mkapa hakumkemea.

Kwa nini unafikiri angemkemea kwenye uchaguzi?
 
meandika sana lakini unakumbuka angalau neno moja mwaka 2000 alipoulizwa ,
"Utajisikiaje ukiamka ukakuta upinzani umekufa"
Alijibu "nitasikitika sana"
Ila kwa bwana yule mambo ni tofauti
nchi inapita ktk kipindi kibaya na cha kutisha kuliko hata tulivyokuwa na mkoloni mweupe!
Viongozi wa dini mna dhambi mbaya kabisa nchi hii na ni aibu kwenu
 
Mtabaki na "speculations" zenu hizo wakati wenzenu CCM washaanza kujiandaa kwa kampeni za 2025. Mkija kushtuka hata wabunge "handfuls" hamtawapata.
Waafrika sisi tuna laana flani hivi si bure...dunia ya leo unafurahia Ccm kujazana wao peke yao bungeni.?

Hivi ulisoma kidogo umuhimu wa checks and balances ilivyo na umuhimu kwenye nchi?

Hao darasa la 7 waliojazana ndio mnategemea hili taifa lipige hatua? Waafrika ni disgrace duniani hapa.
 
Atakumbukwa Dama milele... One of the think tankers...

Aliudhibiti uchumi na kuupaisha juu, kimya kimya bila mbwembwe wala...




Cc: mahondaw
 
Leo kuna rafiki yangu moja yupo jikoni kabisa kwa meko, tulikuwa tunazungumzia uteuzi wa Waziri Mkuu.

Nikawa namuuliza vipi ikatokea Majaliwa asichaguliwe na Magu???,Je Mwaka 2015 majaliwa alikuwa chaguo namba 1 la magu.

Akasema ngoja nikupe kwanza mkanda nikianza na makamu wa Rais ule mwaka 2015,JPM aliambiwa apeleke majina 3 awe ameyapanga kimtiririko kwa umuhimu.

Anasema,katika list yake jina LA kwanza lilikuwa Dr. Hussein Mwinyi-Jina la 2 kuna jamaa nimesahau Nina lake na Jina la 3 alikuwa Mama samia. Wazee wakamuchagua Mama samia.

Alisema Magu na Dr.Hussein hawajakutana barabarani wana common bond kati yao ambapo watu wengi hawafahamu.
..Nje ya mada...
 
Mkapa huyo uliyesema angepinga Hussein Mwinyi kuteuliwa kuongoza Zanzibar kupinga nepotism ndiyo huyo huyo alihusika kumuweka Amani Abeid Karume Zanzibar!!! Amani ni mtoto wa kiongozi wa zamani wa Zanzibar.

Kuwa mtoto wa kiongozi hakunyimi haki na fursa ya kuwa kiongozi mzuri. Muhimu uwe na sifa zinazo stahili.
Amani Karume ndiyo alikuja kuleta muafaka Zanzibar kujaribu kuondoa mgogoro na mpasuko wa nchi yenu Zanzibar.

Marekani na demokrasia yao yote walimchagua George Walker Bush kuwa raisi wao wakati baba yake alikuwa raisi wa zamani wa nchi yao na hatukusikia malamiko ya nepotism.

Tusiwe na double standard kwenye kukosoa, kukemea na kupongeza, au kuiga demokrasia ya watu wa magharibi.

Mtoto wa raisi au wa kiongozi yeyote Naye ni binadamu ana haki ya kuishi bila ndoto na haki zake kuathiriwa na historia ya familia yake.
 
Ni miezi takriban minne sasa tangu Rais Mstaafu BWM atutoke. Bila ubishi, Rais Mkapa alikuwa na ushawishi mkubwa ndani ya siasa za CCM, na ni ukweli usio na shaka kuwa outcome ya siasa za CCM za uchaguzi wa mwaka 2015 ambazo yeye alishiriki kikamilifu ndizo leo hii tunaishi kwa consequences zake. Pamoja na hayo nimetafakari sana juu ya kifo chake na kujaribu kufikiria leo angekuwa hai angekuwa na fikra gani au angeshawishi vipi mwenendo wa serikali hii pamoja na chama chake. Nimetafakari sana pia urais wa huyo mheshishimiwa.

1. Ni mwaka 1995,Mkapa achaguliwa kuwa rais, ala kiapo na kisha kusema wapinzani ni mkono mmojawapo katika mikono yake miwili ya kufanya kazi
Mwaka 1995 baada ya kuapishwa pale uwanja wa uhuru, Mkapa atoa hotuba na kulihutubia Taifa, asema Wapinzani ni watu muhimu kwa maendeleo ya Taifa, Asema mawazo mbadala katika nchi ni kitu chanya kwa Taifa na akasema Wapinzani ni kama mkono mmoja katika mikono yake miwili, na kuwa chama chake ni kama mkono wa pili wote wanahitajika kwa ajili ya usitawi wa nchi.

Miaka 25 baade tumepata rais Mwingine, anayeonekana ana nia ya kuua upinzani, anayewaambia wananchi kuwa pindi wakichagua wasimchanganyie, anawaambia wananchi kuwa wakichagua upinzani katika maeneo yao hatopeleka maendeleo!. Hii ndo Tanzania ya leo, tofauti na miaka 25 iliyopita!. Najiuliza je Mkapa angekuwa hai leo hii akashuhudia aliyoshiriki kuyaasisi mwaka 2015 angekaa kimya ndani ya Chama? - Naamini angemwambia John bila kupepesa macho kuwa John hili unalofanya siyo sahihi badilika!

2. Mkapa atoa kitabu ajuta Mauaji ya Zanzibar
Mwaka mmoja au miwili nyuma kabla ya kifo chake rais Mkapa atoa, kitabu, ajuta kwelikweli ndani ya kitabu hicho mauaji ya watu wasio na hatia huko Zanzibar. Mauaji yale yawa mzigo kwenye mtima wake, yamkosesha raha. Miaka 19 baadae, mauaji yanatokea tena, wananchi wa Zanzibar wauawa, wateswa sababu tu ili Tanganyika iweze kuendelea kuweka mtawala inayemtaka huko Zanzibar. Je Mkapa angekuwepo hai, leo hii angemueleza John kitu gani? - Angemwambia John kuwa uko sahihi well done endelea hivyohivyo? au angemwambia John kuwa usirudie makosa niliyofanya mimi mwaka 2001 waachie Wazanzibari wamchague wanayemtaka?

3. Ni Siku chache kabla ya kifo chake, Wastaafu waitwa dodoma kujadili mtu wa kumpa kijiti cha kuongoza Zanzibar, Mkapa naye ahudhuria
Ni siku chache tu kabla ya kifo chake, Mkapa alikuwa na wenzie, Ali, Jakaya John, Shein na Mama Maria, moja ya kitu walichojadili ni mtu wa kumpa uraisi huko Zanzibar. Kitu kiichoniijia kichwani, hivi Mkapa alikubaliana kweli na wenzie wampe mtoto wa Ali uraisi? - Mkapa huyuhuyu ambaye Sumaye anasema kuwa wakati wakiwa madarakani walikubaliana wasiwape watoto wao vyeo ili kuondoa nepotism ndo eti atakuwa alikubaliana na wenzie kuleta na kulea utamaduni wa Kisultani nchini? - Akili yangu inaniambia kuwa Mkapa lazima alikataa hilo wazo, haiwezekani Mkapa huyu anayejuta kutokana na maafa ya kuwapandikizia Wazanzibar mtawala mwaka 2000 eti akubali tena kurudia dhambi ileile iliyopelekea kuuawa Wazanzibari huko Pemba mwaka 2001. Kwa hiyo akili yangu inaniambia kuwa Mkapa hakuwa onboard kwenye wazo la kumfanya Hussein kuwa Sultan huko Zanzibar.

4. Mkapa afariki, hatukutangaziwa na mkuu wa nchi ugonjwa uliomuua
Mkapa afariki, sheria inasema anapofariki kiongozi mstaafu lazima umma utangaziwe na rais aliyeko madarakani, na katika tangazo hilo mtangazaji inabidi aeleze kilichomuua mgonjwa. Sisi kwetu kweli tulitangaziwa msiba, lakini katika tangazo lile hatukuambiwa mgonjwa kafia nyumbani au kuambiwa jina la hospitali husika kama kafia hospitali. Nimetafakari sana kwa nini taarifa hizo hazikuwa kwenye tangazo? - kwa mujibu wa sheria, Umma si ulikuwa na haki ya kujua hizo info?, kwa nini zilikuwa vague sana?

5. Maombolezo yafanyika, Msiba haukuwa na kiongozi high profile kutoka nje ya nchi
Nimetafakari sana hili suala, nikasema kwa nini viongozi wa nchi jirani hawakuja? Nikasema labda ni Korona, lakini nikafikiria tena, Burundi nao sera yao ya korona si ilikuwa kama sisi na ni marafiki wetu wakubwa kwenye ukanda huu? Kwa nini rais mpya Ndaisheye hakuja? Sijapata jibu.

Kama ni Korona mbona basi raisi Museveni baadae alikuja na convoy yae wamevaa mask kwa ajili ya mradi wa Bomba la Mafuta wakati nchini kwake bado wanapambana na Korona? Kwanini baadae kabla ya uchaguzi Mkuu rais wa Burundi alikuja TZ? Mbona na rais wa Malawi alikuja baadae kipindi cha Kampeni?

6. Maombolezo yaendelea na watu waendelea na shughuli zao utadhani hakuna msiba
Nimetafakari sana hili, wakati mwili wa Marehemu umelala uwanja wa Uhuru hapo Dar, hakuna hata siku moja shule za msingi au sekondari au vyuo zilifungwa ili watoto na walimu wakatoe heshima kwa rais wao wa zamani, Lakini John alipokuwa akienda kwenye kampeni katika jimbo la uchaguzi basi shule zitafungwa, watumishi wa serikali watapewa notice ya lazima wahudhurie mikutano yake, Najiuliza serikali ya John ilishindwaje kuwapa ruhusa maalum watumishi wa serikali kwenda kuuaga mwili wa BWM kama heshima kwake? - Sitegemei jibu liwe eti Jumamosi au Jumapili watu wangeweza kwenda kutoa heshima zao za mwisho, hizo kwa wengine bado ni siku za kwenda kwenye ibada!

7. Ben alitaka tume huru ya uchaguzi
Kabla ya kifo chake, ndani ya kitabu chake, Ben ni kama anaungama, kuna kitu anakisema, kinamuuma roho. Anaona wazi kuwa taratibu za chaguzi nchini haziko fair, hazina haki. Ben anataka tume huru ya uchaguzi ili wananchi wachague viongozi wao haki bin haki - Je Ben angekuwa hai leo hii akajionea hii tume ya John na Mahera wake, Ben angesemaje? - Naamini Ben angemwambia John kuwa Mwanangu sasa hii unachofanya umezidisha hatuendi hivyo!! , hebu achana na uharibifu huu haukusaidii wewe wala nchi!

8. Swali moja ambalo bado nahaingaika nalo, JE BEN ANGEUNGA MKONO MOVE YOYOTE YA KUBADILI VIPINDI VYA UTAWALA KWENYE KATIBA? - Hell no, maana huko nyuma amewahi kusimama kidete kumzuia Salmin Amour kubadili katiba kuendelea kuitawala Zanzibar!

Tangulia Ben, Kifo chako kinaniachia maswali mengi kuliko majibu!!!
Tatizo la hawa , akili huwarudia wakishakuwa nje ya system . Subiri hata huyu atakuja kukiogopa kivuli chake .
 
Mkapa huyo uliyesema angepinga Hussein Mwinyi kuteuliwa kuongoza Zanzibar kupinga nepotism ndiyo huyo huyo alihusika kumuweka Amani Abeid Karume Zanzibar!!! Amani ni mtoto wa kiongozi wa zamani wa Zanzibar.

Kuwa mtoto wa kiongozi hakunyimi haki na fursa ya kuwa kiongozi mzuri. Muhimu uwe na sifa zinazo stahili.
Amani Karume ndiyo alikuja kuleta muafaka Zanzibar kujaribu kuondoa mgogoro na mpasuko wa nchi yenu Zanzibar.

Marekani na demokrasia yao yote walimchagua George Walker Bush kuwa raisi wao wakati baba yake alikuwa raisi wa zamani wa nchi yao na hatukusikia malamiko ya nepotism.

Tusiwe na double standard kwenye kukosoa, kukemea na kupongeza, au kuiga demokrasia ya watu wa magharibi.

Mtoto wa raisi au wa kiongozi yeyote Naye ni binadamu ana haki ya kuishi bila ndoto na haki zake kuathiriwa na historia ya familia yake.

Mkapa wa 2000 alikuwa tofauti na Mkapa wa 2020, Kabla ya kifo chake busara zilishaongezeka zaidi na kuna mambo alitamani yabadirike nchini!
 
Kuna tabia ya kuanza ku edit historia watu wakifariki.

Ukweli ni kwamba, kuna consistency katika kubana uhuru Tanzania kutoka Nyerere mpaka Magufuli.

Mkapa ndiye Godfather wa Magufuli. Miaka yote hiyo Magufuli alivyominya upinzani Mkapa alishindwa nini kukemea?

Marais wawili ambao kidogo walijaribu kujiondoa kwenye kuminya mawazo mbadala ni Mwinyi na Kikwete. Mwinyi zaidi.

On a large scale, hakuna ambacho anafanya Magufuli leo ambacho Nyerere hajafanya. Tofauti pekee ni kwamba, Magufuli anafanya kwa nguvu na kijinga, na Nyerere alifanya kwa siasa ya hali ya juu na ujuzi wa hila za Ki Makaveli.

Magufuli kaminya vyama vya upinzani? Nyerere alivifuta kabisa. Kwa miaka takribani 30.

Magufuli kawafanya wapinzani wakimbie nchi? Nyerere alikimbiza kina Kambona na Masha.

Magufuli kaiba kura? Nyerere alibariki matokeo ya chaguzi kubadilishwa Zanzibar tangu enzi za chama kimoja.

Unajiuliza Mkapa angefanyaje?

Huwa sipendi kuhariri historia.

Ila jiulize.

Katika maisha yake alifanya nini kumkemea Magufuli?

Kitu pekee Mkapa alichomkemea Magufuli ni kuita serikali "serikali ya Magufuli" badala ya " serikali ya CCM". Or something to that effect. As if this credit grab is the most atrocious thing Magufuli has done.

Katika mabaya yote ya Magufuli, hilo ndilo aliloliona muhimu kabisa kukemea.

On that topic, bora hata Nyerere alimkemea Mwinyi kwa kuvunja katiba.

Angalau Nyerere alikemeq jambo la msingi. Wazi.

Magufuli amevunja katiba kipindi chake cha kwanza chote, mara nyingi tu, mfano kwa kukataza wapinzani kufanya mikutano.

Mkapa hakumkemea.

Kwa nini unafikiri angemkemea kwenye uchaguzi?
Unayosema uko sahihi sana, lakini watu haohao katika nyakati na majira nje ya madaraka wamekuwa na misimamo na mawazo fulanifulani ambayo ni mizuri kwa Taifa lakini haipendezi kwa watawala wa wakati huo. Sasa Whatever the timing ya misimamo yao mipya, It is never too late kutaka kitu sahihi kifanyike au vipi?
 
Kinacho nishangaza mimi ni hawa Watawala wetu ,Baba wa Taifa hili Mwalimu Nyerere nae aliwahi kukiri Ubovu wa Katiba tuliyo nayo nae mpaka anaondoka Madarakani zaidi ya kusema/kukemea hakuweza kubadili Katiba hii.

Mzee Mkapa nae mpaka anaondoka Madarakani ameona Ubovu wa Tume yetu na Suala la Katiba mpya ,haku badili kitu zaidi ya kusema tu.Sijui ni kwa nini Watawala wengi wanaona mapungufu wakiwa nje ya Utawala
CCM ni mzimu aliouacha Nyerere. Utatusumbua waTZ mpaka wote tusalimu amri. Mzimu huu unataka vitu vitatu:
  1. Umasikini kwa watanzania wote
  2. Ujinga kwa watanzania wote
  3. Maradhi kwa watanzania wote.
Utausema na kuukashifu ukiwa nje na ukitoka (kama ulijiunga nao), si vinginevyo.

Hata hivyo aliyekaribia sana kuuharibu na kuutokomeza Mzimu huu ni Dkt Jakaya Kikwete kwa kudiriki kuanza au kufanya yafuatayo:
  1. Kuanzisha mchakato wa katiba mpya (uliofanikiwa kwa karibu 75%, na kutuachia watanzania katiba hiyo mkononi tukiisoma na kuililia).
  2. Kuleta muafaka wa Zanzibar
  3. Kupanua elimu (shule za kata,Kuongeza shule za A- Level kwa wasichana, vyuo vikuu n.k)
  4. Kuwaheshimu wapinzani
  5. Uwazi katika uchaguzi (kubandika matokeo kila kituo).
Hata hivyo, hilo la katiba mwishoni alibadilisha gia angani, pengine kwa kufuatwa na mzimu au kwa shinyikizo la viongozi wenzake. Na la pili aliloshindwa au kubadilsha gia angani ni kufuta matokeo ya Urais Zanzibar. Nia ilikuwa njema lakini , Sorry, Mzimu wa Nyere unatisha!
 
Waafrika sisi tuna laana flani hivi si bure...dunia ya leo unafurahia Ccm kujazana wao peke yao bungeni.? Hivi ulisoma kidogo umuhimu wa checks and balances ilivyo na umuhimu kwenye nchi? Hao darasa la 7 waliojazana ndio mnategemea hili taifa lipige hatua? Waafrika ni disgrace duniani hapa.
Hapa umemaliza! Asiye na mwana abebe jiwe.

Huu ndio unaitwa Mzimu wa Nyerere, eti unafurahia kuwa na bunge la chama kimoja. Hata kama wangeshinda wapinzani tu bila Mzimu CCM , mimi nisingefurahia.

Hapo ndipo tulipofika, kweli UMASIKINI TUNAUTAKA WENYEWE!
 
Mkapa wa 2000 alikuwa tofauti na Mkapa wa 2020, Kabla ya kifo chake busara zilishaongezeka zaidi na kuna mambo alitamani yabadirike nchini!
Ni kweli, maana kifo kikikaribia, nasikia mabaya yote uliyoyatenda hapa duniani unapenda usiende nayo huko kwenye dunia nyingine. Na mfa maji hakosi kutapatapa, hivyo ukombozi pekee ni kuitamka haki katika ulimi na mdomo wako ukipata nafasi. Kwasababu ukigongwa na pikipiki au ukiwa ndani ya ndege na ikadondoka huna nafasi ya kubwabwaja ya moyoni.
 
Ni miezi takriban minne sasa tangu Rais Mstaafu BWM atutoke. Bila ubishi, Rais Mkapa alikuwa na ushawishi mkubwa ndani ya siasa za CCM, na ni ukweli usio na shaka kuwa outcome ya siasa za CCM za uchaguzi wa mwaka 2015 ambazo yeye alishiriki kikamilifu ndizo leo hii tunaishi kwa consequences zake. Pamoja na hayo nimetafakari sana juu ya kifo chake na kujaribu kufikiria leo angekuwa hai angekuwa na fikra gani au angeshawishi vipi mwenendo wa serikali hii pamoja na chama chake. Nimetafakari sana pia urais wa huyo mheshishimiwa.

1. Ni mwaka 1995,Mkapa achaguliwa kuwa rais, ala kiapo na kisha kusema wapinzani ni mkono mmojawapo katika mikono yake miwili ya kufanya kazi
Mwaka 1995 baada ya kuapishwa pale uwanja wa uhuru, Mkapa atoa hotuba na kulihutubia Taifa, asema Wapinzani ni watu muhimu kwa maendeleo ya Taifa, Asema mawazo mbadala katika nchi ni kitu chanya kwa Taifa na akasema Wapinzani ni kama mkono mmoja katika mikono yake miwili, na kuwa chama chake ni kama mkono wa pili wote wanahitajika kwa ajili ya usitawi wa nchi.

Miaka 25 baade tumepata rais Mwingine, anayeonekana ana nia ya kuua upinzani, anayewaambia wananchi kuwa pindi wakichagua wasimchanganyie, anawaambia wananchi kuwa wakichagua upinzani katika maeneo yao hatopeleka maendeleo!. Hii ndo Tanzania ya leo, tofauti na miaka 25 iliyopita!. Najiuliza je Mkapa angekuwa hai leo hii akashuhudia aliyoshiriki kuyaasisi mwaka 2015 angekaa kimya ndani ya Chama? - Naamini angemwambia John bila kupepesa macho kuwa John hili unalofanya siyo sahihi badilika!

2. Mkapa atoa kitabu ajuta Mauaji ya Zanzibar
Mwaka mmoja au miwili nyuma kabla ya kifo chake rais Mkapa atoa, kitabu, ajuta kwelikweli ndani ya kitabu hicho mauaji ya watu wasio na hatia huko Zanzibar. Mauaji yale yawa mzigo kwenye mtima wake, yamkosesha raha. Miaka 19 baadae, mauaji yanatokea tena, wananchi wa Zanzibar wauawa, wateswa sababu tu ili Tanganyika iweze kuendelea kuweka mtawala inayemtaka huko Zanzibar. Je Mkapa angekuwepo hai, leo hii angemueleza John kitu gani? - Angemwambia John kuwa uko sahihi well done endelea hivyohivyo? au angemwambia John kuwa usirudie makosa niliyofanya mimi mwaka 2001 waachie Wazanzibari wamchague wanayemtaka?

3. Ni Siku chache kabla ya kifo chake, Wastaafu waitwa dodoma kujadili mtu wa kumpa kijiti cha kuongoza Zanzibar, Mkapa naye ahudhuria
Ni siku chache tu kabla ya kifo chake, Mkapa alikuwa na wenzie, Ali, Jakaya John, Shein na Mama Maria, moja ya kitu walichojadili ni mtu wa kumpa uraisi huko Zanzibar. Kitu kiichoniijia kichwani, hivi Mkapa alikubaliana kweli na wenzie wampe mtoto wa Ali uraisi? - Mkapa huyuhuyu ambaye Sumaye anasema kuwa wakati wakiwa madarakani walikubaliana wasiwape watoto wao vyeo ili kuondoa nepotism ndo eti atakuwa alikubaliana na wenzie kuleta na kulea utamaduni wa Kisultani nchini? - Akili yangu inaniambia kuwa Mkapa lazima alikataa hilo wazo, haiwezekani Mkapa huyu anayejuta kutokana na maafa ya kuwapandikizia Wazanzibar mtawala mwaka 2000 eti akubali tena kurudia dhambi ileile iliyopelekea kuuawa Wazanzibari huko Pemba mwaka 2001. Kwa hiyo akili yangu inaniambia kuwa Mkapa hakuwa onboard kwenye wazo la kumfanya Hussein kuwa Sultan huko Zanzibar.

4. Mkapa afariki, hatukutangaziwa na mkuu wa nchi ugonjwa uliomuua
Mkapa afariki, sheria inasema anapofariki kiongozi mstaafu lazima umma utangaziwe na rais aliyeko madarakani, na katika tangazo hilo mtangazaji inabidi aeleze kilichomuua mgonjwa. Sisi kwetu kweli tulitangaziwa msiba, lakini katika tangazo lile hatukuambiwa mgonjwa kafia nyumbani au kuambiwa jina la hospitali husika kama kafia hospitali. Nimetafakari sana kwa nini taarifa hizo hazikuwa kwenye tangazo? - kwa mujibu wa sheria, Umma si ulikuwa na haki ya kujua hizo info?, kwa nini zilikuwa vague sana?

5. Maombolezo yafanyika, Msiba haukuwa na kiongozi high profile kutoka nje ya nchi
Nimetafakari sana hili suala, nikasema kwa nini viongozi wa nchi jirani hawakuja? Nikasema labda ni Korona, lakini nikafikiria tena, Burundi nao sera yao ya korona si ilikuwa kama sisi na ni marafiki wetu wakubwa kwenye ukanda huu? Kwa nini rais mpya Ndaisheye hakuja? Sijapata jibu.

Kama ni Korona mbona basi raisi Museveni baadae alikuja na convoy yae wamevaa mask kwa ajili ya mradi wa Bomba la Mafuta wakati nchini kwake bado wanapambana na Korona? Kwanini baadae kabla ya uchaguzi Mkuu rais wa Burundi alikuja TZ? Mbona na rais wa Malawi alikuja baadae kipindi cha Kampeni?

6. Maombolezo yaendelea na watu waendelea na shughuli zao utadhani hakuna msiba
Nimetafakari sana hili, wakati mwili wa Marehemu umelala uwanja wa Uhuru hapo Dar, hakuna hata siku moja shule za msingi au sekondari au vyuo zilifungwa ili watoto na walimu wakatoe heshima kwa rais wao wa zamani, Lakini John alipokuwa akienda kwenye kampeni katika jimbo la uchaguzi basi shule zitafungwa, watumishi wa serikali watapewa notice ya lazima wahudhurie mikutano yake, Najiuliza serikali ya John ilishindwaje kuwapa ruhusa maalum watumishi wa serikali kwenda kuuaga mwili wa BWM kama heshima kwake? - Sitegemei jibu liwe eti Jumamosi au Jumapili watu wangeweza kwenda kutoa heshima zao za mwisho, hizo kwa wengine bado ni siku za kwenda kwenye ibada!

7. Ben alitaka tume huru ya uchaguzi
Kabla ya kifo chake, ndani ya kitabu chake, Ben ni kama anaungama, kuna kitu anakisema, kinamuuma roho. Anaona wazi kuwa taratibu za chaguzi nchini haziko fair, hazina haki. Ben anataka tume huru ya uchaguzi ili wananchi wachague viongozi wao haki bin haki - Je Ben angekuwa hai leo hii akajionea hii tume ya John na Mahera wake, Ben angesemaje? - Naamini Ben angemwambia John kuwa Mwanangu sasa hii unachofanya umezidisha hatuendi hivyo!! , hebu achana na uharibifu huu haukusaidii wewe wala nchi!

8. Swali moja ambalo bado nahaingaika nalo, JE BEN ANGEUNGA MKONO MOVE YOYOTE YA KUBADILI VIPINDI VYA UTAWALA KWENYE KATIBA? - Hell no, maana huko nyuma amewahi kusimama kidete kumzuia Salmin Amour kubadili katiba kuendelea kuitawala Zanzibar!

Tangulia Ben, Kifo chako kinaniachia maswali mengi kuliko majibu!!!
Wamemtanguliza,walijua atakuwa kikwazo kwa waliyokusudia kuyafanya mwaka huu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom