Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

Maneno yangu matatu tu: "LET ZANZIBAR GO." OOOUUUTTT haraka sana hata leo.

Kwanza wanatusaidia nini sisi zaidi ya kutupunguzia mapato ya kodi ya Ushuru wa Forodha? Kupitisha mzigo bandari ya zanzibar bei chee kulinganisha na Dar. Watoke haraka ili mwaka ujao wa fedha tuongeze makusanyo ya kodi.

Wapemba walioko Tanganyika watachukuliwa kama Wawekezaji wengine wa kigeni, hii itaongeza mapato yatokanayo na sekta ya uwekezaji. Kata umeme unaoenda kule bure au watozwe malipo ya umeme kwa viwango stahiki, itasaidia kwenye Balance of Payments kutokana na ongezeko la Exports. In fact Watanganyika tutafaidika sana kiuchumi na kijamii Muungano huu ukivunjika.

Hima Wazanzibari daini visiwa vyenu ingawa mnakaa wenyewe. Ifike mahali na sisi tupumue, tunatukanwa eti tunainyonya Zanzibar, kwa maziwa yapi iliyonayo?
 
Bw, Nonda

Muungano una maana kubwa zaidi kwa hao watu uliyowataja hapo (kwenye red) . Kwao wao wananufaika moja kwa moja kwa sababu ni watumishi wa kitengo cha propaganda cha Muungano. Wanalipwa mishahara kufaya shughuli zao. Vile vile ni sehemu ya ibada kwa Bwana Mungu wao (Nyerere) .
Takashi, angalau basi umma ungekuelewa kama ungejibu hoja. Kama ni propaganda onyesha basi wapi propaganda zilipo, hasira na dharau ni silaha ya mwisho ya mtu asiye na hoja, ni silaha dhaifu ya kupambanisha hoja na ni silaha nzito kubebwa na mwerevu.

Mathalani, nimesema bajeti ya Zanzibar ni bilioni 648, bilioni 307 ni matumizi ya serikali na Bilioni 341 ni za maendeleo.
Katika pesa hizo, hakuna bajeti ya vyombo vya ulinzi, elimu ya juu, wabunge, viongozi na mishahara ya SMZ kwa uchache. Sasa hapo wapi propaganda ilipo? Kama kuna bajeti tuambie chanzo chake

Zanzibar ambayo uchumi wake ni sawa na bajeti ya wizara ya akina mama na watoto haichangii chochote katika kuendesha muungano. Kinyume chake inapewa asilimia 7 ya mapato kutoka hazina Dar. Hapo propaganda ipo wapi

Zanzibar yenye bajeti ya bilioni 648 haiwezi kutoa bilioni 50 kulipa umeme kwasababu hiyo ni asilimia 8 ya pato la taifa.
Umeme unatumika Ikulu ya Zanzibar, Baraza la wawakilishi, baraza la mapinduzi na wakazi wote ni matokeo ya kodi ya mlima nyanya wa Mtimbira morogoro na mlima mpunga wa kidatu morogoro. Hapo propaganda ipo wapi

Kwamba Zanzibar inayosema ni nchi ikiwa na bendera, wimbo wa taifa, BLW,BLM,ahakama,Rais na makamu wawili haiwezi kuandaa mswada wa kuiondoa chini ya ukoloni. Hapo propaganda ipo wapi.

Tunaposikia Tanganyika ni Land locked country inatukumbusha hadithi za BOKO HARAM-ZANZIBAR BRANCH zinazosema ZNZ ilikuwa na maendeleo kwa kuwa na TV ya Rangi hata kama hakuna chuo kikuu na madhara yake tunayaona sasa.
Si hesabu, jiografia au historia inayoeleweka vema kwa Wazanzibar.

Mkuu Joka kuu, mi nadhani njia ya kudai Tanganyika si kwa kubeba madumu ya petroli kama wanavyofanya Boko haram(Z). Tanzania ipo na tunakiti kila taasisi kimataifa.

Tunachotakiwa ni kuwaambia kuzuia bunge lisipeleke ruzuku Zanzibar. Halafu tutawaambia watu kuwa mzanzibar akiwa popote huyo ni kupe na kupe anaondolewa.

Maalim Seif ambaye ni mshiriki mkubwa wa boko haram(z) amesita kutamka neno muungano uvunjwe! kashindwa kusema
Ahmed Rajab UAMSHO mwingine naye kashindwa kuandika neno hatutaki muungano, amebaki na hadithi za kipuuzi za seriakali 3, mkataba na uhusiano maalumu.
Ally Saleh UAMSHO kindaki ndaki amegoma kujitoa katika tume ya katiba.
Raza wa sultan ameshindwa kusema Zanzibar inajitoa, sasa tuwasaidije ninyi watu.

Mwisho, Takashi JF hoja hujibiwa kwa hoja. Kama wapo wapiga propaganda basi hilo waachie Watanganyika maana moto uliowashwa utasambaa na Wazanzibar watajuta! Wataikimbia nchi ya sali na maziwa kama walivyoikimbia sasa.

Nonda na Takashi mnatakiwa mujibu kwa hoja, vinginevyo mtakuwa mumeingia mtandao usiowahusu, wenu ni kule Mzalendo.net ambako uanachama umezuiliwa hadi ujulikane kama ni mapinduzi daima au Sultan oyee
Kule unakoweza kusema jua linatoka magharibi aghalab ukapata watu watakaokupigia makofi.

Na mwisho, sisi tunafanya chaguzi zetu kila wakati, hivi Zanzibar wameshwahi kufanya uchaguzi! just curious
 
...Zanzibar ni sehemu ndogo sana kulinganisha na Tanganyika. Hicho tunachotoa kwa wa-Zanzibari hakina athari kubwa kwetu sisi.

..Tunachokataa sisi siyo muungano bali ubaguzi na chuki
Mkuu, wakati mwingine nasikitishwa sana na watu wetu nyinyi wenyewe ambao tunategemea mtusaidie kututoa kwenye hili bonde la uvuli wa mauti, la Muungano.

Nchi yetu ni ya masikini, masikini kapuku, masikini lazima awe makini na kila senti anayotumia, anayopoteza. Umesikia bunge la bajeti wanalalamika kwa uchungu kukua kwa deni la Taifa, serikali na wabunge wanakuna vichwa wapi tutapata vyanzo vya mapato, mpaka wanaanzisha mpango wa kuuza personalized license plates, wanaongeza kodi kwa waendesha vi pikipiki. Utasemaje bilioni hamsini zinaoenda Zanzibar hazina athari kwetu? Wewe unaona ni sawa kuwalipia umeme na mishahara watu wa Zanzibara ambao makusanyo ya TRA kwao yanabaki kwao? Do you find that right kwa kweli???

Unasema "let Zanzibar go" halafu in the same breath unasema "Tunachokataa sisi siyo muungano..." Hivi kwa nini Watanganyika hatuna balls za kuwa straightforward na kusema muungano hatuutaki kwa vile unatunyonya? Kwa nini Watanzania hatuna uchungu na nchi yetu?

Inanisikitisha sana kwa sababu maoni yako ni ya wale Watanzania Bara wachache, wachache mno ambao wanaelewa lopsidedness ya Muungano na Zanzibar, lakini mwisho wa siku nyinyi hao hao ndio mnasema "Tunachokataa sisi siyo muungano..." Of course tunachokataa sisi ni Muungano, kwa sababu nchi ya watu milioni 45 haiwezi kuungana na nchi ya watu milioni moja halafu ukataka kujenga hadhi sawa za kinchi. Haiwezekani.
 
Zanzibar wanaiibia Tanzania kwa makusudi, mfano tu Airport ya Zanzibar watalii wa Italia wanaofika kwa maelfu kila siku na kutoa euro 50 siku wakiingia, na euro 20 siku wakitoka na kulipia dola 5 kila siku watayolala Zanzibar, basi hawagongewi VISA ila kamuhuri tu kuwa ameingia Zanzibar, kwa VISA zilizopo ni za Tanzania
 
Takashi, angalau basi umma ungekuelewa kama ungejibu hoja. Kama ni propaganda onyesha basi wapi propaganda zilipo, hasira na dharau ni silaha ya mwisho ya mtu asiye na hoja, ni silaha dhaifu ya kupambanisha hoja na ni silaha nzito kubebwa na mwerevu.

Mathalani, nimesema bajeti ya Zanzibar ni bilioni 648, bilioni 307 ni matumizi ya serikali na Bilioni 341 ni za maendeleo.
Katika pesa hizo
, hakuna bajeti ya vyombo vya ulinzi, elimu ya juu, wabunge, viongozi na mishahara ya SMZ kwa uchache. Sasa hapo wapi propaganda ilipo? Kama kuna bajeti tuambie chanzo chake

Lakin pia nimeipenda sana sana hapo nilipo BLUE. Lakin ningekushauri uangalie hizo pesa za zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo ni % kiasi gani zimetengwa kuondoa umasikini na % ngapi kukuza uchumi? Hapo utakuwa umeleta kitu cha maana sana katika usemi wako hususan unapozungumzia maendeleo. Na ukilinganisha na Bajeti ya JMTz.

Je unafahamu uwekezaji?
Je unajuwa Znz ilitoa kiasi gani kuanzisha BOT?
Je Tanganyika ilitoa kiasi gani?
Je unafahamu mambo mliokubaliana katika Mkataba wenu wa Muungano?

Kwa kujibu masuala hapo juu nafikiri utakuwa umefunguka sana kiakili na kujua uchumi ni nini na maana ya muungano wenu.

 
Takashi, angalau basi umma ungekuelewa kama ungejibu hoja. Kama ni propaganda onyesha basi wapi propaganda zilipo, hasira na dharau ni silaha ya mwisho ya mtu asiye na hoja, ni silaha dhaifu ya kupambanisha hoja na ni silaha nzito kubebwa na mwerevu.

Mathalani, nimesema bajeti ya Zanzibar ni bilioni 648, bilioni 307 ni matumizi ya serikali na Bilioni 341 ni za maendeleo.
Katika pesa hizo, hakuna bajeti ya vyombo vya ulinzi, elimu ya juu, wabunge, viongozi na mishahara ya SMZ kwa uchache. Sasa hapo wapi propaganda ilipo? Kama kuna bajeti tuambie chanzo chake

Zanzibar ambayo uchumi wake ni sawa na bajeti ya wizara ya akina mama na watoto haichangii chochote katika kuendesha muungano. Kinyume chake inapewa asilimia 7 ya mapato kutoka hazina Dar. Hapo propaganda ipo wapi...

Mkuu Nguruvi3,

Hivi inapotokea kuwa umemhifadhia mtu amana yake ya 11.5 na halafu ukamrudishia 4.5 na baada ya kupiga kelele sana unampa 7. Kwa akili zako za kichumi tendo hilo litaitwa nini?
Utapeli? Wizi? Hadaa? Ukibaka? au "kuwabeba mayakhe"?


Serikali ya Zanzibar inakosa majibu juu ya suala la mgao wa Muungano wa asilimia 4.5 ambao kwa muda mrefu yametolewa mapendekezo ya asilimia 11.5 lakini BOT bado halijatekelezeka hadi sasa.

Alisema jambo linaloshangaza kuona baada ya kupelekwa mapendekezo hayo serikali ya Muungano imeipatia gawio la asilimia 7.8 huku kukiwa hakuna muendelezo wa hatma ya suala hilo.

Link mtandaousiowahusu
 
Nonda,

..Tanganyika ipo, na wa-Tanganyika wapo. Kilichotokea, na kinachowanganya watu akili, ni kwamba shughuli za utawala ktk Tanganyika zilikasimiwa kwa serikali ya muungano mwaka 1964.

..Inawezekana kabisa kujadili haki za wa-Tanganyika ndani ya muungano huu. Wahusika wanajitia vichwa maji tu lakini sina shaka kabisa kwamba hilo linawezekana.


..Pia siamini ktk kuwafukuza au kuwasumbua wa-Zanzibar walioko ktk ardhi ya Tanganyika. I am on the record hapa JF kupendekeza kwamba wa-Zanzibar walioko Tanganyika wapewe nafasi ya kuwa wakazi wa kudumu kwa kipindi maalum wakisubiri kuamua wanataka kuwa raia wa upande gani -- Tanganyika au Zanzibar.

Mtu ngapi zina muono kama wako?

Pitia hapa thereisnosuch
 
Lakin pia nimeipenda sana sana hapo nilipo BLUE. Lakin ningekushauri uangalie hizo pesa za zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo ni % kiasi gani zimetengwa kuondoa umasikini na % ngapi kukuza uchumi? Hapo utakuwa umeleta kitu cha maana sana katika usemi wako hususan unapozungumzia maendeleo. Na ukilinganisha na Bajeti ya JMTz.Je unafahamu uwekezaji?
Je unajuwa Znz ilitoa kiasi gani kuanzisha BOT?
Je Tanganyika ilitoa kiasi gani?
Je unafahamu mambo mliokubaliana katika Mkataba wenu wa Muungano?

Kwa kujibu masuala hapo juu nafikiri utakuwa umefunguka sana kiakili na kujua uchumi ni nini na maana ya muungano wenu.
Baru baru Salaam, Tafadhali sana naomba ufute hiyo quote ya pili (namba 5) post yako # 285. Hayo si maneno yangu na wala sijaandika na kama nimeandika hebu iweke hiyo post namba. Hujanitendea haki kunibambikizia maneno

Baada ya hapo nitaweza kuendelea na mjadala wa BoT n.k.
 
Bw Nguruvi3

Hakuna hoja ya Mzanzibar yeyote yule kwako wewe ikawa hoja, sio ya Maalim Seif, Jussa, Allly Saleh ,Uamsho na wengineo. Kwako wewe mzanzibar ni mtu duni na asiyejua haki yake kwahiyo wewe (nyinyi), ndio mnajipa haki ya kuwaamlia nini kitawafaa.

Mimi nadhani bado mna fikra za miaka 60s,70s,80, 90s . Hivyo vitisho na dharau havita mzuwia mzanzibari kudai haki zake ndani ya Muungano. Hivi sasa hapa Zanzibar kumeletwa wanajeshi kutoka Tanganyika kwa kazi maalum ya kuwapoteza viongozi wa Uamsho....Lakini muelewe mauwaji yeyote yatakayofanyika basi na majibu yake yatakuwepo...

Kuhusu hizo hoja zako, wataalam mbali mbali wamezijibu na kwa ufafanuzi zaidi, ila kwako wewe hazitakua hoja alimradi zimetolewa na mzanzibar. SISI TUTAENDELEA KUDAI HAKI ZETU , MPAKA KIELEWEKE...NA KAMA MKOTAYARI KUMWAGA DAMU YA WAZANZıBARI KWA KUDAI HAKI ZAO , BASI FANYENI HIVYO.
 
Nonda,

..Tanganyika ipo, na wa-Tanganyika wapo. Kilichotokea, na kinachowanganya watu akili, ni kwamba shughuli za utawala ktk Tanganyika zilikasimiwa kwa serikali ya muungano mwaka 1964.


..Wazanzibari wanatunyonya wa-Tanganyika ndani ya muungano huu. Tunawalipia umeme. Mishahara ya watumishi inalipwa na wa-Tanganyika. Jambo lolote lile la muungano wanaochangia ni wa-Tanganyika wakati wa-Zanzibari hawatoi chochote. Hebu wewe niambie ni lini umesikia SMZ imetoa fedha fulani kwenye suala lisilohusiana na yale yaliyobainishwa kuwa ni masuala ya muungano kuwasaidia wa-Tanganyika.

..Kwanini wa-Tanganyika hawalalamiki??
..Pia siamini ktk kuwafukuza au kuwasumbua wa-Zanzibar walioko ktk ardhi ya Tanganyika. I am on the record hapa JF kupendekeza kwamba wa-Zanzibar walioko Tanganyika wapewe nafasi ya kuwa wakazi wa kudumu kwa kipindi maalum wakisubiri kuamua wanataka kuwa raia wa upande gani -- Tanganyika au Zanzibar.
JokaKuu,
Hili suala la mapato na matumizi ya mambo ya Muungano lina utata mkubwa. Kama ilivyo kawaida, mapato na matumizi ya shughuli za Muungano(mambo ya Muungano) limefanywa kuwa ni siri kama ulivyo mambo mengi ya muungano wenyewe.

Wengi tunasema kuwa upande mmoja unanyonya mwengine. Tunachukua vigezo vya juu juu kama umeme tunawapa bure, Zanzibar hawachangii chochote. Kauli zetu bado hazitoi jibu sahihi bado zinabaki ni kauli zinazoelea hewani tu.

Upande mwengine,unasema umebanwa na kuwa hawawezi kuingia katika mazungumzo na nchi nyingine kuhusu mikopo ya miradi ya maendeleo kwa yale mambo ambayo si ya muungano au Tanganyika inatumia mgongo wa muungano kujifanyia kile ipendacho bila makubaliano na Zanzibar.

Nilishataja siku za nyuma kuwa kuna kauli kuwa Zanzibar ilichangia 11.5% ya mtaji ulioanzisha benki kuu. Mzee wetu Edwin Mtei angetusaidia sana kama angefunguka kuelezea uhalisia wa dai hili. Hapa tunajua kuwa Zanzibar wanapata mgao wa 4.5 na sasa kufikia 7. Unawekeza 11.5, unavuna 4.5 ni sawa hapo?

Pia kuna kauli aliyoitoa Jussa kuhusu ripoti ya Mshauri mwelekezi kuwa Mapato na matumizi za shughuli za Muungano(mambo ya muungano) yanajitosheleza na kunakuwa na bakaa ya ziada kimapato.
Pitia hapa mapatomatumizi
Hivi vitu viwili tukivipatia majibu, uhalisia au uhakika, tutaweza kusema kwa vinywa vipana kuwa Zanzibar wanatunyonya au tunawagawia, tunawabeba.

Mpaka tutakapopata majibu ya hayo mawili, kauli zetu zinabaki kuwa malalamiko,kupandisha mizuka na kujenga chuki.

Kwa wakazi wa jangwani huona maji kwa mbali(mirage) na wanaposogelea hiyo sehemu huwa ni mchanga moto tu. Na hivyo ndivyo inavyoweza kuwa kwa walalamishi wa pande hizi mbili.

Ni wakati muafaka wa kuudadisi muungano wa Tanganyika na Zanzibar nje ndani, ndani nje, bila ushabiki wala jazba. Nia iwe kutafuta ukweli na kuonesha ukweli na kuusimamia ukweli. Hili tu ndio litaivusha Tanzania salama au litaisambaratisha kama ujanja ujanja utaendelea kuendesha muungano.
 
Mkuu, wakati mwingine nasikitishwa sana na watu wetu nyinyi wenyewe ambao tunategemea mtusaidie kututoa kwenye hili bonde la uvuli wa mauti, la Muungano.

Nchi yetu ni ya masikini, masikini kapuku, masikini lazima awe makini na kila senti anayotumia, anayopoteza. Umesikia bunge la bajeti wanalalamika kwa uchungu kukua kwa deni la Taifa, serikali na wabunge wanakuna vichwa wapi tutapata vyanzo vya mapato, mpaka wanaanzisha mpango wa kuuza personalized license plates, wanaongeza kodi kwa waendesha vi pikipiki. Utasemaje bilioni hamsini zinaoenda Zanzibar hazina athari kwetu? Wewe unaona ni sawa kuwalipia umeme na mishahara watu wa Zanzibara ambao makusanyo ya TRA kwao yanabaki kwao? Do you find that right kwa kweli???

Unasema "let Zanzibar go" halafu in the same breath unasema "Tunachokataa sisi siyo muungano..." Hivi kwa nini Watanganyika hatuna balls za kuwa straightforward na kusema muungano hatuutaki kwa vile unatunyonya? Kwa nini Watanzania hatuna uchungu na nchi yetu?

Inanisikitisha sana kwa sababu maoni yako ni ya wale Watanzania Bara wachache, wachache mno ambao wanaelewa lopsidedness ya Muungano na Zanzibar, lakini mwisho wa siku nyinyi hao hao ndio mnasema "Tunachokataa sisi siyo muungano..." Of course tunachokataa sisi ni Muungano, kwa sababu nchi ya watu milioni 45 haiwezi kuungana na nchi ya watu milioni moja halafu ukataka kujenga hadhi sawa za kinchi. Haiwezekani.

Taso,

..ur 100%. billioni 50 could do a lot of things kwa wa-Tanganyika.

..lakini pia na sisi tumekuwa tunapoteza fedha zaidi ya hizo kwa ufisadi na mambo mengine.

..nilichojaribu kusema mimi ni kwamba wa-Tanganyika hawaoni shida kuwa nchi moja, taifa moja, dola moja, na wa-Zanzibari. ndiyo maana nikasema hatuchukii muungano, bali tunachukia dhuluma, chuki,uzushi, etc etc.

..nadhani sasa umenielewa.
 
Nguruvi3, JokaKuu

Muungano unatumika na wajanja huku Tanganyika kufanya ufisadi, huku Muungano ukiwaacha wengi ya waliokubali kuitwa wabara wasijielewe. Wabara wanafukuza kivuli kama wazanzibari wanavyomtafuta waliyeungana nae.

Angalia hili.Gonga link tunawabebahatujitambui

Kama Tanganyika ingekuwepo, tungejua ni nani wa kumshika shati.

Tumeacha kushughulikia watu 40milioni, tunapiga kelele na watu laki 9.5!!

Wizara ya madini ni ya Tanzania au Tanganyika?

Mwanakijiji na Nguruvi3,JokaKuu, Mkandara tuache kuwazingua wabara(wadanganyika), tudai Tanganyika ,and this Muungano monster will sort itself out!
 
Mkuu Nguruvi3,

Hivi inapotokea kuwa umemhifadhia mtu amana yake ya 11.5 na halafu ukamrudishia 4.5 na baada ya kupiga kelele sana unampa 7. Kwa akili zako za kichumi tendo hilo litaitwa nini?
Utapeli? Wizi? Hadaa? Ukibaka? au "kuwabeba mayakhe"?


Serikali ya Zanzibar inakosa majibu juu ya suala la mgao wa Muungano wa asilimia 4.5 ambao kwa muda mrefu yametolewa mapendekezo ya asilimia 11.5 lakini BOT bado halijatekelezeka hadi sasa.

Alisema jambo linaloshangaza kuona baada ya kupelekwa mapendekezo hayo serikali ya Muungano imeipatia gawio la asilimia 7.8 huku kukiwa hakuna muendelezo wa hatma ya suala hilo.

Link mtandaousiowahusu

Nonda,

..BOT ilianzishwa kutokana na mtaji wa fedha za Tanganyika na Zanzibar tulizopewa na EA currency board.

..Pamoja na hayo Zanzibar wakaanzisha tena PBZ ambayo toka wakati wa Karume mpaka utawala wa Salmini ndiyo walikuwa wanahifadhi fedha zao humo. Yaani PBZ ndiyo ilikuwa benki kuu ya Zanzibar kwa muda wote huo.

..Sasa suala hili lilishughulikiwa na msuluhishi wa kimataifa ambapo pamoja na mambo mengine alielekeza kwamba Zanzibar iwe inapewa hiyo 4.5% na zaidi ilazimishwe kuweka akiba yake BOT. Baada ya uamuzi huo ndiyo ukaona hata Zanzibar inateua Naibu Gavana wa BOT.

..Mimi sielewi kwanini hii 4.5% imekwenda kuwa 7.8% na sasa inaelekea kuwa 11% na labda baadaye itakuwa 60%. Kwa kweli huko serikalini viongozi wetu wakikaa na wa-Zanzibar they give in to everything. Bora suala hili lingerudishwa kwa msuluhishi wa kimataifa. Ni kwa msingi huohuo ndiyo maana napendekeza Tanganyika isiingie any bilateral agreement na Zanzibar. Mkataba wowote ule na Zanzibar lazima uhusishe nchi multilateral.

..Baada ya kusema hayo naomba unielekeze popote pale ambapo imehalaishwa kwamba Tanganyika ilipie gharama za umeme za Zanzibar, au tuwalipe mishahara SMZ, au tuchangie shughuli za muungano na Zanzibar wasichangie suala lolote lile, au wajumbe toka Zanzibar ktk tume ya katiba walipwe na serikali ya Tanganyika.
 
Nguruvi3, JokaKuu

Muungano unatumika na wajanja huku Tanganyika kufanya ufisadi, huku Muungano ukiwaacha wengi ya waliokubali kuitwa wabara wasijielewe. Wabara wanafukuza kivuli kama wazanzibari wanavyomtafuta waliyeungana nae.

Angalia hili.Gonga link tunawabebahatujitambui

Kama Tanganyika ingekuwepo, tungejua ni nani wa kumshika shati.

Tumeacha kushughulikia watu 40milioni, tunapiga kelele na watu laki 9.5!!

Wizara ya madini ni ya Tanzania au Tanganyika?
Mwanakijiji na Nguruvi3,JokaKuu, Mkandara tuache kuwazingua wabara(wadanganyika), tudai Tanganyika ,and this Muungano monster will sort itself out!
Zanzibar ikindoka Tanganyika ipo. Tanzania ambayo ni Tanganyika kwa tafsiri ya Wazanzibar ipo. Ina kiti UN, AU, EAC, FIFA n.k Hatuna sababu ya kudai Tanganyika irudi.
Ndio maana tunaunga mkono jitihada za kujitoa Zanzibar. Mzanzibar anatakiwa alilie nchi yake maana sisi tupo
Mumesema mara nyingi ninyi ni koloni la Tanganyika sasa unataka Tanganyika ipi tena.
Mumesema Katiba ya sasa ni Tanganyika, sasa mnataka ipi irudi
Mumesema Tanganyika inawanyonya(inanyonya maziwa yasiyokuwepo) sasa mnanyonywa na Tanganyika ipi

Kama Zbar haitajitoa tuna option zifuatazo
1. Kuwa na serikali 1 ya JMT
2. Kuweka mezani nini Zanzibar ianchangia nakama hakuna ima ibaki kama Mkoa au iondoke.

Sisi hatubebi madumu ya petroli, tutawapiga kwa kalam na fikra.
Kipigo cha kwanza ni LET ZNZ GO! Viongozi wote akiwemo Seif wa UAMSHO wamenywea

Tanganyika is there! No question about that
 
Da hatimae umemwaga manyanga chini!!!

Tulishasema waaacheni waende,wakifika uko hawakuwa wamoja tena wataanza upemba na uunguja wakisha anza kutoana nyongo ndio sasa kati yao mmoja ataamua kuja bara kuomba msaaada wa ndugu yake wa damu wa kweli.akija kuomba msaada tunampa kwa kumpa masharti ya kuwa ajue moja kwa moja tunatambua yeye kama sehemu ya Tanzania na kuwa wao watakuwa tayari kuingia kwenye mahusiano na Taifa la Tanzania kama sehemu [MKOA] katika Tanzania na sio tena muungano wa Kinchi.

Waaaaaaaaaaacheni waende walioko bara waape rasmi kuwa sasa wao si Wazanzibar Nchi bali watanzania lasmi,wakikataa barabara nyeupe ludisha kwao Zanzibar tubaki na bongo yetu. Simple
 
Kiukweli hawa jamaa wameumbwa kulalamika na hawatakuja kukaa kimya bila kutoa manung'uniko kuwa tunawaonea. Naunga mkono hoja LET THEM GO tumechoka na kelele zao.
 
Bw Nguruvi3

Hakuna hoja ya Mzanzibar yeyote yule kwako wewe ikawa hoja, sio ya Maalim Seif, Jussa, Allly Saleh ,Uamsho na wengineo. Kwako wewe mzanzibar ni mtu duni na asiyejua haki yake kwahiyo wewe (nyinyi), ndio mnajipa haki ya kuwaamlia nini kitawafaa.

Mimi nadhani bado mna fikra za miaka 60s,70s,80, 90s . Hivyo vitisho na dharau havita mzuwia mzanzibari kudai haki zake ndani ya Muungano. Hivi sasa hapa Zanzibar kumeletwa wanajeshi kutoka Tanganyika kwa kazi maalum ya kuwapoteza viongozi wa Uamsho....Lakini muelewe mauwaji yeyote yatakayofanyika basi na majibu yake yatakuwepo...

Kuhusu hizo hoja zako, wataalam mbali mbali wamezijibu na kwa ufafanuzi zaidi, ila kwako wewe hazitakua hoja alimradi zimetolewa na mzanzibar. SISI TUTAENDELEA KUDAI HAKI ZETU , MPAKA KIELEWEKE...NA KAMA MKOTAYARI KUMWAGA DAMU YA WAZANZıBARI KWA KUDAI HAKI ZAO , BASI FANYENI HIVYO.

Watanganyika wamwage damu ya Wazanzibari kwasababu wao wanaupenda saaaana huu muungano eeh? Mnaonaje mkawashawishi viongozi wenu akina Bilal na wenzie wajiuzulu na warudi Zanzibar? Watakapofanya hivyo Serikali ya Muungano haitakuwepo tena. Mtakuwa mmetusaidia sana. Si haki linchi likubwa kama Tanganyika kuuliwa kwa maslahi ya tukisiwa tudogo twenye waarabu na wanyamwezi. Mnadai visiwa vyenu kutoka kwa watanganyika, walivichukua lini? Na wala hakuna haja ya kulilia referendum, nyie ongeeni na viongozi wenu ikiwezekana mjitoe hata kesho. Lifti muombe nyie, dereva mumwelekeze nyie, kasema nani?
 
Watanganyika wamwage damu ya Wazanzibari kwasababu wao wanaupenda saaaana huu muungano eeh? Mnaonaje mkawashawishi viongozi wenu akina Bilal na wenzie wajiuzulu na warudi Zanzibar? Watakapofanya hivyo Serikali ya Muungano haitakuwepo tena. Mtakuwa mmetusaidia sana. Si haki linchi likubwa kama Tanganyika kuuliwa kwa maslahi ya tukisiwa tudogo twenye waarabu na wanyamwezi. Mnadai visiwa vyenu kutoka kwa watanganyika, walivichukua lini? Na wala hakuna haja ya kulilia referendum, nyie ongeeni na viongozi wenu ikiwezekana mjitoe hata kesho. Lifti muombe nyie, dereva mumwelekeze nyie, kasema nani?

kaka ulikuwa unaishi wapi wewe ??? hivi huelewi kinachoendelea ?? ningalikushauri anza kusoma thread zenye masuala ya muungano ndio uje uulize hayo masuali yako
 
kaka ulikuwa unaishi wapi wewe ??? hivi huelewi kinachoendelea ?? ningalikushauri anza kusoma thread zenye masuala ya muungano ndio uje uulize hayo masuali yako

Ningalikushauri anza kusoma historia ya muungano na sababu za uwepo wake ndio usome threads zenye masuala ya muungano.
 
Bw Nguruvi3

Hakuna hoja ya Mzanzibar yeyote yule kwako wewe ikawa hoja, sio ya Maalim Seif, Jussa, Allly Saleh ,Uamsho na wengineo. Kwako wewe mzanzibar ni mtu duni na asiyejua haki yake kwahiyo wewe (nyinyi), ndio mnajipa haki ya kuwaamlia nini kitawafaa.

Mimi nadhani bado mna fikra za miaka 60s,70s,80, 90s . Hivyo vitisho na dharau havita mzuwia mzanzibari kudai haki zake ndani ya Muungano. Hivi sasa hapa Zanzibar kumeletwa wanajeshi kutoka Tanganyika kwa kazi maalum ya kuwapoteza viongozi wa Uamsho....Lakini muelewe mauwaji yeyote yatakayofanyika basi na majibu yake yatakuwepo...

Kuhusu hizo hoja zako, wataalam mbali mbali wamezijibu na kwa ufafanuzi zaidi, ila kwako wewe hazitakua hoja alimradi zimetolewa na mzanzibar. SISI TUTAENDELEA KUDAI HAKI ZETU , MPAKA KIELEWEKE...NA KAMA MKOTAYARI KUMWAGA DAMU YA WAZANZıBARI KWA KUDAI HAKI ZAO , BASI FANYENI HIVYO.
Tunachosema hapa ni kuwa tukiweka takwimu wenzetu hawana majibu ila majibu yao ni 'mpaka kieleweke' Katika hoja zangu za jinsi gani ZNZ ni mtegemezi mkubwa wa muungano hujaweza kukanusha hata moja unabaki kusema ni propaganda. Hapo kuna hoja?

Ninaposema hawana hoja nina mfano mzuri sana wa mwana UAMSHO kindaki ndaki Ahmed Rajab. Yeye ni shujaa sana wa kuzusha na kubadili hadithi. Amewachochea Wazanzibar kuwa wakitoka katika muungano watakuwa kama Indonesia, Mlaysia au Mauritius! hajawaambia kuwa wanaweza kuwa kama Comoro au Haiti.

Ahmed anasema Tanganyika inawanyonya Wazanzibar kwa vile kuna TRA na mapato yanachukuliwa kusaidia bara na kuwaacha hoi Wazanzibar. Asichowaeleza ni kuwa Ikulu ya Zanzibar, BWL, Baraza la Mapainduzi, na wananchi wote wanapata mgao wasiochangia hata senti tano. Asichosema ni kuwa gharama za ulinzi na usalama, elimu ya juu, hata mafao ya marais wastaafu wa Zbar ni mzigo wa Mtanganyika.

Ahmed, anaendelea kusema Zanzibar itakuwa paradize kwa bandari huru, asichowaambia ni kuwa ili bandari ifanye kazi kikamilifu nishati kama ya umeme ni muhimu na hiyo inatolewa bure kwa Mzanzibar kuanzia kwa Sheha , Waziri hadi Kisiwandui.

Anajenga hoja kuwa muungano ni jinamizi lisilofaa wakati huo huo anahubiri serikali 3, makataba au mahusiano maalumu.Tunapomuuliza mkataba, serikali 3 au mahusiano yatakuwaje hana hoja anabadili mada na kuendeleza utetezi wa boko haram. Kwamuktadha huo mtu huyu ana hoja gani ya mashiko kama si uchochezi? Kwanini asiwaambie wznz ondokeni katika muungano anabaki kujenga hoja za kuzunguka mbuyu! Lini Ahmed amekuja na suluhu ya muungano zaidi ya chuki zake dhidi ya Watanganyika zinazommaliza kiafya

Maalimu Seif, yeye anasema hataki muungano akiwa uani, hadharani anasema nataka muungano lakini uwe wa mkataba.
Hapa ana hoja gani kama si kuchochea akiwa na lake moyoni.

Jussa, anasema Nyerere ndiye aliyeleta mapinduzi, na kusema Karume alifanya makosa.
Tukimuuliza anakubali mapinduzi au la hana hoja anabaki kusema hawa ni makafir.
Akiwa Dodoma anachukua psoho za bunge nono, haleti mswada, akirudi kwa UAMSHO mdomo sana
Hapa ana hoja?

Wazanzibar kwa ujumla,: Wao wanataka nchi yao. Tumewapa kila mbinu ya kuondoka katika muungano. Hawataki wanachotaka Tanganyika kwanza irudi ili waweze kujenga hoja zao dhaifu na zisizo na mashiko za serikali 3, mkataba au mahusiano. Tukiwauliza mtaweka nini mezani ili tuwe na vitu hivyo hawana hoja wamebaki kusema Nyerere na Watanganyika ni makafir wakubwa. Kuna hoja hapo?

Wakati wanaita Watanganyika Makafir, huku nyuma wanachukua asiliamia 7 ya kodi za makafir, wanapata umeme wa bure wa makafir, wanapata ajira bwerere za makafir, wanafanya biashara nyumbani kwa makafir, wanasoma bure kwa kodi za makafir, hapo wana hoja gani?

Tunasema ZNZ hawana hoja kwasababu hawahitaji ruhusa kutoka katika muungano. Hawakuhitaji kubadili katiba au kuanzisha vyombo vingine. Wana BLW,Mapinduzi, Mahakama, Rais, Wabunge n.k wanachosubiri ni nini, hawana hoja.

Ikifika hapo, sheikh Baru baru huoni ni kweli hawana hoja?
 
Back
Top Bottom