Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

Muungano ulikuwa na matatizo toka siku ya kwanza ya kuundwa kwake.
Utavunjika tu siku ccm itatoka madarakani, kama ccm itaendelea kuwepo tusitegeemee mabadiliko yoyote yale.
Nakubaliana nawe kuwa ulikuwa na matatizo, kwa mawazo yangu muungano wowote ni kitu chema iwe ulianza vizuri au vibaya. Cha kufanya ilikuwa kurekebisha matatizo ya kuuweka sawa, ila hawa jamaa ukiwaangalia sicho wanachotaka. Wanataka kwanza nchi yao halafu waamue waungane na nani, kitu ambacho si kibaya ila wanaitaka toka kwa nani ndio shwali. Kwanini wasijaribu kujiondoa wenyewe waone kama kuna mtu atawashika mkono?

Ila mimi nina wasiwasi kuwa hawa jamaa kuna janja ndani yao, taarifa ya habari ya Channel Ten Mzee Mwinyi akiwa na umati mkubwa wanawakebehi wanaotaka kuvunja muungano. Kwani hawajuani!, si mchezo unaochezwa hapa? ili waendelee kuonewa huruma kama wanaonewa kweli na maisha yawe ya kuvyonza tu.
Hata kama unamdai mtu kitu, hapa achukue message ipi, hamtaki au mnataka?. Kama hawataki kweli wachukue ushauri waliopewa.
 
I support this movement na tena wafanye haraka.Ikiwezekana wabunge wao kutoka zanzibar wasije kabisa kwenye kikao kijacho. Tumewachoka na lazima walielewe hilo
 


Mwanakijiji and . co umekuwa na ka huu ugonjwa wa Zanzibari , nilikuuliza zamani kama unaunga mkono

muungano au unawapinga uamsho ni jambo gani linawazuia kuweka muhadhara mukawaeleza watu hayo mnayoyaona ni bora ,

Sio kila mtu ana access na internet au kununua gazeti , wengi wa wale wanaohudhuria mihadhara , uwezo wa kupata mlo mmoja unawashinda.

Uamsho wanatumia haki yao kikatiba au nyinyi mumenyimwa haki hiyo ??? mnapita vichochoroni kama wezi tu!!!!

Kama mnazo hoja teremkeni uwanjani msitie mafitina ya kanisa muwape watu nafasi ya kuwahoji

AU TAYARISHENI MDAHALA NA UAMSHO WATU WAAMUE UKWELI UKO WAPI
 
Pasco, JF ikinyooshewa kidole nitashangaa sana! wale wa UAMSHO waliochoma hadi nyumba za ibada hakuna aliyeshtakiwa kwa uhaini. Mzalendo.net si tu wanatoa maoni bali wana video unazopaswa kuziangalia watoto wakiwa wamelala. Ni matusi kashfa tuhuma n.k

Tutauliza kama JF inachochea na ni uhaini,basi Jussa alitakiwa awe katika kifungo cha maisha n.k

Naunga hoja mkono

Let Zanzibar go, if possible July 1 2012
 

yaani umeandika upuuzi mtupuuuuu yaani kama ni mtihani bac 0+++=000000000000000000000, unajua watz wengi ni wajinga hawajui haki zao linapo kuja swala la kudai haki zao watawala ni rahisi sana kubadili upepo hoja sio nani ananufaika na muungano nani hanufaiki wananchi wa znz wanataka mabadiliko ya mfumo wa muungano wameona mfumo uliokuwepo hauna faida kwao je ni kosa kisheria?

Wanataka kura ya maoni iitishwe ili tusipoteze pesa na muda kuwalazimisha watu kuunda katiba wakati muungano wenyewe haupo kisheria kwa ujinga wetu watz maendeleo tutaendelea kuyaona kwenye tv tu aibu tupu
 
Pasco, katiba ya JMT kwa sasa imakiukwa sana, i.e tuna makamo wawili wa rais vs chief minister.

Naunga mkono kwamba sasa wanzanzibari wafanye hima ili waipate nchi yao, ni haki yao kabisa, wasikubali kunyonywa tena na Tanganyika.
 
Last edited by a moderator:
Kwa wasiojua ukweli wa mambo, msingi mkuu wa muungano ni dhima ya Nyerere na Karume in good faith!.

Baada ya dhima ikafuatia kitendo cha kuungana rasmi kwa kuchanganya udogo na kusaini zile hati za muungano.

Baada ya hapo muunngano huo uliridhiwa bara tuu (ratified) kwa bunge la Tanganyika kuupitisha mkataba huo uliokuwa na mambo 11 hivyo kupata nguvu za kisheria!.

Zanzibar nao walitakiwa kuuridhia mkataba huo wa muungano kwa kuuratify lakini jambo hili halikufanyika!. Hivyo wanasheria wangeweza kabisa kuishitaki Tanzania kwa kuipora mamlaka Zanzibar na kuikalia kimabavu miaka yote hiyo!.

Kufuatia kukosekana kwa uhalali wa kisheria wa muungano kule Zanzibar, hivyo Wanzanzibar wako huru kujitoa kwenye muungano kwa amani kabisa kwa kung'ang'ana kuwa sheria, taratibu na kanuni, hazikufuatwa!.

Maadam Wanzanzibari wanacholilia ni haki na uhuru wao, nawaombeni tuwateende haki kwa kuwapatia wanachotaka.

Naiunga kauli ya Mzee Mwanakijiji kwa asilimia 100%, "Let them go!."
 
Mkuu Pasco, mimi shida yangu ni hapo kwenye red. Wadai kwa nani, kama hawajui la kufanya wamepewa ushauri wa bure. Hakuna mwenye uwezo wa kuwapa, hasa ukizingatia ni vigeugeu. Kwanza wakubaliane wanachotaka halafu yote yako mikononi mwao wenyewe!
 
Nawaunga mkono wazanzibari, wajitenge wabaki na nchi yao yenye ukubwa wa eneo za kilometa za mraba 2500, watuachie tanganyika yetu yenye ukubwa wa kilometa za mraba 943000.

Naunga mkono pia wazanzibari walioko tanganyika warudi zanzibar bila kudhulumiwa chochote katika kile wanachokimiliki, na pia naunga mkono watanganyika walioko zanzibar warudi tanganyika. Kwa wale watakaoamua kubaki katika nchi isiyo yao basi wakae kama raia wa kigeni, kwa visa maalum- na ofcourse hawawezi kuwa na haki sawa kama wenye nchi yao(raia).

Naunga mkono hoja pia kwamba, ni jukumu la wazanzibari kujitoa katika muungano wao wenyewe, uwezo wa kujitoa wanao, sasa sijui kwa nini wanazunguuka, wakati wakiamua kutumia vyombo vyao kama vile raisi wao, baraza lao la wawakilishi, serikali yao ya mapinduzi, wanaweza kabisa kujitoa.
 

wee iko na problem aisee! bongo yako haiko sawa kabisa.
 
Forget muungano,

The entire idea of a nation-state as alluded in it's genesis at The Peace of Westphalia in 1648 is going extinct.

This idea has been a foreign one that was shoved down our throats from the get go, and now that corporatocracy rules over nation-state sovereignty, and all the flying dual and trio nationalities, and hyphenated Tanzanians working in Canary Wharf and vacationing in Ibiza, it is becoming even less relevant. Lest I am branded an elitist, whether tomorrow or fifty years in the future, this is the trend.

I wrote extensively about this here at JF.

Search for Westphalia. We need to define things, not simply work with given definitions whose genesis did not have us in mind.
 
siku muungano utavujika, nawabie kwamba wa zazibari wataazisha madai megine, mtanibishia sababu wegi mnaburuzwatu hamwelewi mnafanyanya nii
 
Let Zanzibar GO! GO Go. Zanzibar!
Unfortumetelly though, who is a Zanzibari?
 

Pasco, Muungano uliridhiwa Zanzibar kama ulivyoridhiwa Tanganyika na vyombo halali vilivyokuwa na uwezo wa kufanya hivyo na ambavo bado vipo. Wanaosema kwamba Muungano haukuridhiwa Zanzibar wanaandika historia upya; hawajui historia na hawataki kuijua.

Na Wazanzibari wengi hawajui kuwa muungano uliridhiwa kihalali kabisa. Ndio maana wengine tunaona huo muda wa kuwafundisha watu historia hatuna; kama wanataka kuondoka wafunge mizigo, mapakacha na waende; kuna mamia ya Watanganyika walio tayari kushika nafasi zao ambazo wanazishikilia bara.
 
Naomba kuuliza maswali mawili matatu ya kizuushi...kwa kuwa Zanzibar wanayo katiba yao, Raisi wao, bunge lao, serikali yao, bendera yao na wimbo wa Taifa lao na kwa kuwa bunge la Muungano halina nguvu huko;

  1. Ni mamlaka gani hiyo wanayoililia kuwa inawabana mpaka wanashindwa kupumua?
  2. Ni mamlaka gani hiyo inayowashurutisha kubaki ndani ya Muungano kama hawaupendi?
  3. Ni mamlaka gani hiyo inayoizuia Zanzibar kuendesha kura ya maoni kuhusu Muungano?
Mimi naamini kuwa kisiki kinachowakwamisha katika madai yao ni wao wenyewe Wazanzibari kupitia katiba yao, Raisi wao, wawakilishi wao na serikali yao. Kwa nje wanapiga kelele kuwa hawautaki Muungano lakini ndani mioyoni mwao wamemganda Mtanganyika kama kupe ili wazidi kuneemeka kwa chenu chetu lakini chetu chetu!

Wanaogopa kura ya maoni, jambo lililo ndani ya uwezo wao, na badala yake kutafuta kisingizio na kuanza kuwanyooshea vidole watu wasiohusika. UAMUSHO, kwa kutambua huu ukweli kuwa hawawezi kuwashawishi Wazanzibari kupitia ama viongozi wao au serikali yao, hasira zao wanahamishia kwa Kanisa na Watanganyika.

Rai yangu kwa Wazanzibari ni kuwa kama kweli hamuutaki Muungano, njia ni nyeupee...fungasheni virago muone kama kuna Mtanganyika hata moja atakayewalilia. Lakini hii ya kujaribu kukwepa mapungufu na ulafi wenu wa kutaka huku na kule mwataka, uvumilivu wa Watanganyika unakaribia kikomo kwa chokochoko na matusi yenu.
 
Mkuu Pasco, mimi shida yangu ni hapo kwenye red. Wadai kwa nani, kama hawajui la kufanya wamepewa ushauri wa bure. Hakuna mwenye uwezo wa kuwapa, hasa ukizingatia ni vigeugeu. Kwanza wakubaliane wanachotaka halafu yote yako mikononi mwao wenyewe!
Shedafa, kwa vile muungano uliundwa in good faith, vivyo hivyo tuuvunje in good faith!. Wabara walioko Zanzibar wale watakaotaka kurejea, wabebe vinavyobebeka na visivyobebeka tuwaachie zawadi ndugu zetu.

Wale wa bara wenye mizizi Zanzibar, wasifukuzwe bali waachwe, wakipenda kupewa uraia, wapewe na wale wanaopenda uraia wao wa bara, then wapewe resident permits kama wageni!.

Vivyo hivyo, Wanzanzibari walioko huku bara, wale wenye mapenzi ya kubaki bara, kwa sababu zozote zile, wasibughudhiwe wao na mali zao na biashara zao, waachwe huru kuamua kurudi au kubaki.

Watakaoamua kurudi, vile vinavyobebeka, wabebe kilicho chao na visivyo bebeka, wavitoe zawadi kwa ndugu zao!.

Watakaomua kubaki pia watakaotaka uraia tuwape, wasiotaka uraia tuwape resident permit kama wageni wengine wote.

Kwa sisi ni ndugu wa damu, hakuna viza kuingia Zanzibar au kutoka Zanzibar kuingia bara!.

Spirit ya kuvunja muungano iwe smooth with no hurt feelings na tena sisi tuwandee wema ndugu zetu hawa hata kama wao wametutenda!.

Nawaombeni sana tusiwaadhibu Wanzanzibari na Wapemba walioneemeka na muungano kwa makosa ya mafaatani, vichaa na wendawazimu wachache wasiowatakia mema wenzao!.

Let them go!.
 
Kila nikifikiri naishia kuamini kuwa wanzanzibari "wengi" walitaka/wanataka serikali tatu, yaani Serikali ya Zanzibar, serikali ya Tanganyika na serikali ya muungano. Haya yalikuwa mahesabu kama yangekubalika basi wangepata 'vyote' zanzibar huru, na ATM! Maana hainiingii akilini kwa nini wawe na power ya kubalisha katiba yao, wawe na bendera, wimbo lakini washindwe kusema 'sisi ni taifa huru'. Shida iko wapi?

The sooner the better, tumalizane haya mashauri ili mipango mingi na ya gharama kubwa iliyo chini ya muungano iangaliwe upya. Tuna vitambulisho vya utaifa, tuna tume ya katiba. Hivi vyote viko kwenye level ya muungano. Ni vema tujue moja.
 
Nendeni na kamwe msirudi nyuma. Hamna mnachoongeza. Kama beach hata sisi zimejaa tele kule kilwa mafia na ntwara
 
Sasa kama zanzibar ni yenu kinacho wafanya mlielie ni kitu gani?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…