Mzee Mwanakijiji;4005445]Ukiwaskiliza sana baadhi ya wapinga muungano kwa kweli kabisa wamejawa chuki isiyo na kifani na chuki hiyo imezaa matunda meusi katika madhihirisho ya chuki dhidi ya watu wa Bara na Wakristu.
Lakini kitu kimoja ambacho watu wengi hawataki kukifikiria ni kuwa hawa watu wanaopinga Muungano wao wanadai "nchi". Sasa hakuna aliyewauliza kwamba mbona katiba ya Zanzibar imefanyiwa mabadiliko na kuitangaza kuwa Zanzibar ni nchi? Sasa kama tayari Zanzibar ni nchi wanachodai hawa ni nini? Haiwezekani kuwa wanachodai ni nchi kwani nchi tayari wanayo na Katiba ya Zanzibar inasema hivyo! Wanachotaka siyo nchi! Wanachotaka ni kuwa nje ya Muungano! Hivi ni vitu viwili tofauti.
Pendekezo langu ni njia nyepesi za Wazanzibari kujiondoa kwenye Muungano bila kufanya maandamano, mihadhara wala kuwashtumu watu wa Tanganyika. Wazanzibari wakitaka kutoka kweli kwenye Muungano wanaweza kufanya hivyo ndani ya wiki chache tu na wakawa nchi. Nina uhakika serikali ya Muungano haitotumia nguvu kuwalazimisha kubakia! Nyerere mwenyewe alishasema kuwa hawezi kuwalazimisha Wazanzibari kubakia kwenye Muungano.
Njia ya kwanza
Njia ya kwanza na nyepesi zaidi ya kuweza kujitoa kwenye Muungano ni kwa wananchi wa Zanzibar wakiongozwa na hawa wana- uamsho wawatake watendaji wote wa Muungano wenye asili ya Zanzibar kuachia nafasi zao mara moja na kurudi Zanzibar!
Hii ni pamoja na majaji, wabunge, mawaziri, maafisa wa polisi na vyombo vingine vya usalama, na wantedaji wengine ambao wako kwenye Muungano. Badala ya kuililia Tanganyika kila kukicha kuwa inawabana mashehe wa Zanzibari wenye kuongoza vuguvugu la kutoka kwenye Muungano waanzishe mihadhara ya kuwataka Wazanzibari wenzao ambao wanatumikia Muungano waachilie nafasi hizo.
Binafsi ningependekeza kama wataniruhusu waanzishe harakati hizo ili viongozi wote hawa waachilie nafasi zo ifikapo Disemba 10, 2012. Hii ni pamoja na Makamu wa Rais Ghaib Bilal, jaji mkuu na wengine.
Hawa wote wakishawishiwa kuondoka Wazanzibari wajiandae ama kuwapatia pensheni au kuwatafutia nafasi kwenye serikali ya nchi ya Zanzibar.
Sasa hawa wote wakikubali kuondoka kwenye nafasi zao za Muungano Zanzibar itapata wataalamu wengine wengi.
Lakini pia itafungua ajira za Watanganyika wengi ambao wangeweza kushika nafasi zinazoshikiliwa na Wazanzibari.
Mashehe wa uamsho waende mbali zaidi katik akudai nchi yao. Waanze kuwahamasisha Wazanzibari walioko bara kuamua kuondoka bara na kurudi Zanzibar ili kuendesha shughuli zao huko.
Wale Wapemba na Wazanzibari waliona maeneo ya ardhi Bara. Hivi ndivyo ilivyotokea Sudan ya Kusini ambapo baada ya nchi hiyo kujitenga Wasudan ya Kusini waliokuwa wanafanya kazi Khartoum waliacha kazi zao na wengi wao wameamua kurudi kwenye nchi yao kuanza kuijenga.
Hili pia litakuwa na faida kubwa sana kwa Zanzibar kwani itapata watu wengi zaidi wenye uwezo na utajiri mkubwa na vile vile itabidi iwaandalie viwanja vipya vya kilimo na makazi maana vile vya bara itabidi waviachilie kuwapisha Watanganyika ambao wanalalamikia kukosa ardhi au kupatiwa ardhi isiy nzuri. Na pia wafanyabiashara hao wa Kizanzibari watakaporudi Zanzibar na kama watataka kuja kufanya biashara Tanganyika itabidi waje kama wawekezaji
Hivyo hilo ni jjambo la kwanza nawashauri wana uamsho; hamasisheni Wazanzibari waondoke Tanzania bara ili warudi Zanzibar ambako watapatiwa nafasi bora zaidi za ajira. Mtakapofanya hivyo, na watu wa Bara nao itabidi waanze kuondoka Zanzibar japo hapo nina uhakika kutakuwa na kazi kidogo. Watu wa Bara ni kina nani Zanzibar?
Nina uhakika wapo Watanganyika ambao watashukuru sana kwa wao pia kupewa nafasi ya kupumua kuliko kila siku kuimbiwa "Zanzibar, Zanzibar"; Watu wa Bara hatutaki kuonekana tunawang'ang'ania Wazanzibari wakati nguvu yote ya kutoka kwenye Muungano wanayo wao.
Nidhahiri kuwa hakuna mwenye uwezo huo na sasa kilichobakia ni sote kwa pamoja kutoka Bara tuseme nasi pasi ya shaka kuwa LET ZANZIBAR GO- Iacheni Zanzibar iende.
Itaenda wapi zaidi ya kuwa kwenye kivuli cha Tanganyika ndani au nje ya Muungano
HUU NI MWANZO WA "LET ZANZIBAR GO MOVEMENT 2012"; Kama unaunga mkono kuwaacha Wazanzibar wajitoe kwenye Muungano weka kwenye sahihi yako "I support Let Zanzibar Go Movement 2012"! Tuwasaidie waharikishe wajitoe kwani hakuna
Mkandara;4004870] Wazanzibar wanataka kujitoa ktk Muungano wajadili na viongozi wao kisha wakilisheni ombi lenu la kujikata halafu ndipo itapangwa ushirika wa kimataifa kama tulivyo na nchi nyingine iwe Kenya au Uganda. uamuzi ni wenu sisi bara hatuna nongwa kabisa isipokuwa mjue tu ya kwamba ni WATU wanaojenga nchi na sii ARDHI kwa watu wake. Maadam wapo Wazanzibar wengi bara ambao kwa matakwa haya watakuja kuwa wageni wakiishi kwa visa na work permit sijui hapa mtakuja sema nini maana huu mungano mnautazama kwa bendera na ramani.
Uhuru ni wa WATU sii wa ardhi na mipaka yake hata siku moja, maana hata wewe unaweza kuja bara ukanunua ardhi na ikawa yako au waarabu wanaweza kuja Zanzibar nunua ardhi ukahamishwa wewe kama ilivyotokea Palestine.
Sasa kama nyie mnaona ardhi ni bora zaidi kuliko wananchi wenyewe jikateni wala hatuna noma kabisa isipokuwa ktk vichwa vyenu wafikirieni WATU wanaoishi mikoani maana kuna waarabu wenye asili ya Zanzibar (kiOman), Washiraz na Wangazija waliohamia bara na wanajulikana kama Wazanzibar. Kama umegundua hakuna Wabara wanaohamia Zanzibar, wamekuja fanya biashara au kufanya kazi huko lakini wao wanajua kuwa ni wageni kama waphilipino kule Dubai kisha ardhi yenyewe iko wapi? lakini kwa Wazanzibar waliohamia bara au wanaotaka kuhamia bara ardhi kubwa na huru kwao kufanya lolote. Muungano huu ni faida kubwa kwa Wazanzibar kuliko bara kumbuka Palestine, Rwanda na Burundi wanachokiomba ni ardhi zaidi wangemshukuru Mungu, nyie ndio kwanza mnataka kujikata kwa ardhi kidogo wakati mko mamillioWazanzibar
tumewafungulia kila kitabu na kila kurasa. Tunawasaidia, nanyi onyesheni nia ya kujitenga July 1 2012. Hii kampeni ya Let Zanzibar go ndiyo imeanza na mwitikio unatia raha. Pita vijiweni uone jinsi Wabara walivyohamasika na nchi yao.
Hakuna Mzanzibar atakayedaiwa chochote midhali kipo ndani ya begi lake. Wale wenye dhamana zisizohamishika hakikisheni mnapata wanunuzi kipindi hiki ili kuepuka hasara.
Huu ni ukarimu kwasababu hakuna mzanzibar aliyewahi kubeba nyumba ardhi au duka kuja nalo. Lakini hatazuiliwa kuondoka na amana zake pale atakapoziuza.
Ni vema mkaondoka wenyewe kwasababu mtakuwa na wakati wa kujipanga. Mkisubiri kufukuzwa mtajikuta katika wakati mgumu.
Hakuna mbara atakayenyanyua dongo, kijiwe,unyoya au njiti kumpiga mtu.
Wabara hatujafikia kiwango hicho cha upuuzi
Tutatumia njia ifuatayo na ambayo imependekezwa na mwenzetu MM.
Tutaomba serikali moja bila kuwa na Mwanza au Zanzibar. Zote ziwe JMT.
Tunajua mlivyo na uchungu wa nchi yenu hili hamtalikubali na hapo mtaondoka bila matayarisho na mtapata hasara.
Kuna mambo ambayo sasa ni 'off the table''
1. Hakuna serikali 3 kwasababu hamna cha kuchangia katika serikali ya muungano. Hatudhani kama mumegoma kulipa umeme wa bilioni 50 mtaweza kulipa bill ya bilioni 500!
Hata kama mtaweza mtabakisha nini chunguni?
2. Hatuhitaji mkataba. Hatuna kitu ambacho tunadhani tutafaidika kutoka katika mkataba.
Mkataba ni njia ya ulaghai ya chako ni chetu, changu ni changu. Hatuna tutakachofadika
3. Hatuhitaji uhusiano special, tutakutana SADC, EAC, COMESA n.k.
Nashadidia yaliyosemwa,kama mnadhani makamu wa rais na mawaziri ni vibaraka, basi ninyi wafanyakazi wa Zanzibar wazalendo ndani ya muungano onyesheni mfano.
Pisheni huko mlikoajiriwa ili Wabara wafaidi matunda ya nchi yao kama mtakavyofaidi yenu.
Vijana wa bara mnaotembea na bahasha za khaki(CV), hili ni kuwakumbusha kuwa dhiki zenu zinalipwa fadhila na matusi, kejeli na moto wa wazanzibar walioziba nafasi zenu.
Watanganyika, hatuna tunachofaidika na Zanzibar zaidi ya hasara kama Mluguru kulipia bill za umeme kwa UAMSHO
[/QUOTE]
Wazanzibar this is athe point of no return, hamhitaji maandamano wala kelele, nafasi ya kujitoa ipo wazi nasi tutawasaidia
LET ZANZIBAR GO! ZANZIBAR SHOULD GO ASAP!