Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

Wapeni kura ya maoni ili tupate kushughulikia matatizo ya watu 40 milioni
Kura hawataki wanasema na bara nao wapewe kura hiyo!

Swali usilotaka kujibu ni kuwa nini kinashindikana kutangaza kuwa muungano umekufa
1. Mna baraza la mapinduzi, kwani kazi yake ni nini?
2. BLW
3.Wabunge
4. Wananchi
5. Wahuni wa UAMSHO
 
Wapeni kura ya maoni ili tupate kushughulikia matatizo ya watu 40 milioni.

Hii miaka hii, wacha tu. Link https://www.jamiiforums.com/habari-...15-british-people-demand-vote-to-quit-eu.html
Mkuu wangu nadhani swala hili la kura ya maoni ni geni kwako kabisa na ndio maana unasisitiza bara tuwape Zanzibar kura ya maoni wakati hiii ni haki yao na kazi yao wenyewe kuitekeleza. Hakuna mtu wala kiongozi bara anayeweza kuwazuia maana Zanzibar ina serikali kamili na kwa maslahi ya Wazanzibar ikiwa ni pamoja na hao UAMSHO.

Labda nikufafanulie na kutoa mfano..Quebec walitaka kujitenga mwaka 1980 wakidai 'Sovereignty' wakapitisha ktk bunge lao na madai yakwa halali wakafanya referendum Quebec tu, tena msafara mkubwa wa Wa quebec walirudi nyumbani kwa sababu ya zoezi hilo tu. Matokeo yake yalikuwa tofauti kabisa na walivyotegemea.. KURA za hapana zilishinda, hawakukubali matokeo wakaendeleza siasa za kujitenga na wakarudia tena mwaka 1995 baada ya mapambano makali ya kisiasa hapo katikati lakini pia kura za hapana zilishinda.

Jambo pekee lililofanyika ktk zoezi hilo kabla ya upiganji kura ni midahalo ya wazi ktk luninga ambayo pande mbili zote walipewa nafasi sawa kuelezea faida na hasara ya Quebec kujitoa ktk muungano huo. Watu walielezwa ukweli matatizo yote watakayo yapata na sii hizi hadithi wanazouza hawa UAMSHO ama kina Jussa maana siku zote ni Uzanzibar lakini hasara zake hazitazamwi hata kidogo. Hivyo kelele za wajomba sijui kina Jussa au UAMSHO haziwezi kubeba nafasi kubwa ya maamuzi ya Wazanzibar hadi mtuonyeshe kwamba Wazanzibar kwa vithibitisho hawautaki muungano nasi tutawapeni hiyo talaka.


Ni jukumu lenu wenyewe kufanya maamuzi na nimesema sana kuhusu Wazanzibar kusimama kidete na viongozi wao ili hoja ya haki yao ipatiwe ufumbuzi. Nakuomba sana soma historia ya Quebec na utakuta kuna mambo fulani fulani yanafanana na Zanzibar maana hawa ni Wafaransa wanaoona wamemezwa na Canada ya Waingereza. Hivyo mkuu wangu mtu akitaka kutalakiwa hakuna sheria inayomlazimisha bwana kumpa ruksa mwanamke akaulize ndugu na jamaa zake hii ni kazi yake yeye mwenyewe na siku akifikia maamuzi ya kutalakiwa na kuiomba talaka kortini mume hana hila zaidi kuitoa talaka. Ama kwa upande mwingine sii mke anayetoa talaka, hututaki unaandika tu talaka maamuzi ya kufikia kuandika ni yako wewe sio kuomba ruksa kwa mke...

Kuhusu EAC, Unashindwa kuelewa kwamba hili ni shirikisho hata hivi tulivyo leo Zanzibar inaweza kuingia pekee ni swala la kufanya amendments tu ktk ushirika huu ambao unalenga zaidi ushirika wa kibiashara ktk kukuza uchumi na kujenga sauti moja ktk ushiriki wetu kimataifa. Hivyo, Nyerere alipozungumzia vile alikuwa na maana kwamba Ushirika wa EAC safari hii utakuwa tofauti na ule tulokuwa nao miaka ya 60 kutokana na kwamba zipo sehemu ambazo hatukubaliani na hizi ndizo zilizopelekea kuvunjika kwa EAC. Makosa yale hayatarudiwa tena, lakini kwa jinsi navyoona kuna harufu kubwa ya kurudia makosa yale yale..

Ndio maana kwa upande mmoja namuunga sana Mkono Mutuz, Le Baharia aliposema lazima tujiulize na kuepuka sababu zilizovunja EAC. Bahati mbaya wabunge wote wanaotuwakilisha ni vijana ambao hawana kumbukumbu wala hawajui kwa nini EAC ilivunjika isipokuwa lawama za mwalimu.
 
Wapeni kura ya maoni ili tupate kushughulikia matatizo ya watu 40 milioni.

Hii miaka hii, wacha tu. Link https://www.jamiiforums.com/habari-...15-british-people-demand-vote-to-quit-eu.html

Nonda,

..lakini hawa walishapiga kura ya maoni kuamua suala la serikali ya umoja wa kitaifa.

..sasa kinachowazuia kuitisha kura ya maoni kuhusu muungano ni nini?

..my take ni kwamba viongozi wa Zanzibar, watu ambao wana uelewa kuhusu faida za muungano, wanaogopa matokeo ya kura ya maoni.

..also, kupigwa dana-dana kuhusu "kero za muungano" kunatokana na ukweli kwamba kwa hapa tulipofikia Zanzibar imepewa kila kitu, ukiwapa zaidi utavunja muungano. Makamu wa Raisi, na Waziri mwenye portfolio ya muungano, wote ni wa-Zanzibari lakini wameshindwa kupata suluhisho la "kero za muungano."

..mwisho, kwanini hizi "kero za muungano" zimekuwa ni malalamishi ya wa-Zanzibari tu, mbona hatusikii jambo lolote lile kuhusu maslahi ya wa-Tanganyika??
 
Mkuu wangu nadhani swala hili la kura ya maoni ni geni kwako kabisa na ndio maana unasisitiza bara tuwape Zanzibar kura ya maoni wakati hiii ni haki yao na kazi yao wenyewe kuitekeleza. Hakuna mtu wala kiongozi bara anayeweza kuwazuia maana Zanzibar ina serikali kamili ..........
Unasema hakuna kiongozi wa bara(Tanganyika) anayeweza kuwazuia?

Umesahau wakati Jumbe alivyoshughulikiwa? Hali ya hewa imechafuka Zanzibar!

Zanzibar ina serikali kamili? Leo tunasema Zanzibar ina serikali kamili kwa ajili ya kukidhi utashi wa hoja?
Umesahau Zanzibar ilipojiunga na OIC, au wakali ule haikuwa serikali kamili? Serikali kamili isiyotambulikana kimataifa?

Miezi michache au mawiki yaliyopita, Balozi Sefu na wazanzibari wenzake (ujumbe wa serikali ya Zanzibar) walikwenda Israel, liliibuka suali hili:
Nilidhani suala la mahusiano ya mambo ya nje ni la Muungano? au hili kwa vile ni la kilimo (jambo lisilo la Muungano) linawezekana kufanywa na Balozi Idi Seif?
link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...zanzibar-improve-agriculture.html#post3876713
Ukamili wa serikali kamili uko wapi hapo?

Tunasema Zanzibar wanayo bendera yao. Lakini angalia bendera ipi inapepea katika ziara hiyo ya ujumbe wa serikali ya Zanzibar. Picha ya tano katika link hii https://www.jamiiforums.com/habari-...wa-smz-wazuru-israil-kwa-ziara-ya-kikazi.html

Ukamili wa serikali kamili uko wapi hapo?

Bado utakaidi kuwa huu Muungano wa Tanzania (Tanganyika na Zanzibar) ni mazingaombwe? Serikali kamili ya Zanzibar inapeperusha Bendera ya Muungano? Au ndio ukamili wenyewe unaousema hapa?

Mkuu Mkandara sitaki nishuku uelewa wako lakini Zanzibar hakuna serikali kamili. Tuwasaidie , tuwape talaka wapate serikali kamili.

Au tumeridhika na viini macho na usanii?
 
Mkuu wangu nadhani swala hili lakura ya maoni ni geni kwako kabisa ........

Labda nikufafanuliena kutoa mfano..Quebec walitaka kujitenga mwaka 1980 wakidai 'Sovereignty'wakapitisha ktk bunge lao na madai yakwa halali wakafanya referendum Quebec tu, .......

Mkuu Mkandara

Quebec ilishawahi kuwa nchi huru hapo mwanzoni au ni jimbo tu la Canada?
Quebec wana uhusiano upi na Canada?
Quebec imeungana na nchi ngapi? Zipi hizo?

Link Quebec - Wikipedia, the free encyclopedia

Kama Canada ni Muungano, ni muungano wa aina ipi? Wanafata mfumo ,muundo upi?
Mfumo wao ni kama huu wetu wa mazingaombwe? Kiini macho?

Canada ina majimbo mangapi? Canada imeundwa na nchi ngapi?

Muungano wa Tanzania umeundwa na nchi ngapi? au majimbo mangapi?
Nitajie kwa majina nchi zilizounda Tanzanaia.

Kama hatuoni kura ya maoni juu ya muungano ni lazima iridhiwe na serikali ya Muungano ( sio serikali ya bara) ni wazi kuwa hatuelewi aina ya Muungano tulionao.

Pia tunasahau au hatuelewi kauli ya Rais wa Muungano anaposema uwepo au kutokuwepo kwa Muungano ni off-limit.
Mjadala /kelele tu kuwa wanataka kura ya maoni zinaleta sokomoko, je wazanzibari watakapoonesha kuwa sasa wanachukua unilateral decision, wale wanajeshi na vifaru vinavyopelekwa kule wakati wa uchaguzi mkuu si idadi yao itaongezwa maradufu?

Hata hivyo, wacha nikubaliane na wewe kwa mantiki ya hoja yako tu kuwa Wazanzibari wanao uwezo wa kuitisha kura ya maoni juu/dhidi ya Muungano lakini wanaogopa au wana sababu wanazozijua wenyewe.

Suali la kujiuliza ni: Je sisi watu milioni 40 tumeridhika na Muungano?

Je sisi watu milioni 40 hatunyonywi na watu laki tisa na nusu? Kama tunanyonywa na wanatutia hasara, je sisi hatutaki kuvunja Muungano?

Au hatutaki kupata maoni ya watu 40 milioni juu ya Muungano ambao unawapendelea wazanzibari?
Au Muungano huu hauwahusu watanganyika bali unawahusu viongozi wao tu?

Na hivi ni kwa nini hakuna kikundi/ watu huku Tanganyika kinachotaka mjadala wa wazi wa Muungano au kutaka kura ya maoni juu/ dhidi ya Muungano?

Hali hii ni ya kawaida kweli? Au tunapata faida gani na Muungano huu kiasi tusiwe tunaudadisi?
Au tunapenda kunyonywa? Au tunapenda kuwabeba Wazanzibari?

Kwa nini kura ya Maoni juu ya muungano si muhimu kwa mtanganyika?

Tunabeba mzigo mzito( Zanzibar) au vipi? Hatutaki kupumzisha mabega yetu?
Kwa nini tuko kimywa sana? Hatupigi ukelele" mnatuumiza" au hatuumii?
 
Hivyo kelele za wajomba sijui kina Jussa au UAMSHO haziwezi kubeba nafasi kubwaya maamuzi ya Wazanzibar hadi mtuonyeshe kwamba Wazanzibar kwavithibitisho hawautaki muungano nasi tutawapeni hiyo talaka. .................

Mkuu Mkandara

Pengine sikukufahamu, umesema kuwa Zanzibar wanaweza kujiondoa katika Muungano bila kunyeshewa na mvua ya risasi?
Kama wanaweza hivyo, huu uwezo wa kutoa talaka tunaupata wapi?

Kama utashikilia kusema "nasi tutakupeni talaka" ni wazi kuwa wao hawana uwezo unaouandika hapa kuwa uamuzi uko mikononi mwao.

Nitafurahi siku moja kusikia Lisu au mbunge mtanganyika anadai kura ya maoni juu ya muungano ndani ya bunge la muungano. Let us stand and be counted!

Kwa nini iwe wazanzibari tu ndio wanalalamika/ wanalalamikia Muungano?

Something fishy here!!!
 
Mkuu wangu ,
Kuhusu EAC, Unashindwakuelewa kwamba hili ni shirikisho hata hivi tulivyo leo Zanzibar inawezakuingia pekee ni swala la kufanya amendments tu ktk ushirika huu ambao unalengazaidi ushirika wa kibiashara ktk kukuza uchumi na kujenga sauti moja ktkushiriki wetu kimataifa. Hivyo, Nyerere alipozungumzia vile alikuwa na maanakwamba Ushirika wa EAC safari hii utakuwa tofauti na ule tulokuwa nao miaka ya60 kutokana na kwamba zipo sehemu ambazo hatukubaliani na hizi ndizozilizopelekea kuvunjika kwa EAC. Makosa yale hayatarudiwa tena, lakini kwajinsi navyoona kuna harufu kubwa ya kurudia makosa yale yale..
.

Mkuu Mkandara.

Umepata uvivu kusoma kijarida: shirikisho ndani ya shirikisho?
Link hii hapa http://www.kituochakatiba.org/index2.php?option=com_docman&task=doc_view&gid=1208&Itemid=27

Ukurasa wa 95-96 utakutana na hii:

Hitimisho lililofikiwa kutokana na maelezo hayo ni kuwa katika uhusiano wa kimataifa kinachotambuliwa ni Jamhuri ya Muungano. Ndani inaweza kuwepo serikali yaZanzibar na Muungano, lakini nje ipo Jamhuri ya Muungano tu. Kwa hiyo
vilevile, Zanzibar katika hali hiyo haina uwezo wa kujadiliana au kufanyamazungumzo kimataifa. Hivyo, serikali ya Muungano inaingiliana na serikali nyingine na vyama vya kimataifa kwa jina la Jamhuri ya Muungano, pamoja na Zanzibar.Hii inahusu vile vile mambo ambayo si ya kisiasa, ya kifedha, ya kiuchumi na michezo, pamoja na shughuli za jumuiya za kiraia kama wale walioohojiwa wanavyoeleza. Hii nipamoja na Umoja wa Mataifa.

Ukurasa 98-99:
Kuhusiana na Jumuiya ya Afrika Mashariki, kwa sababu ya yote mawili, katiba ya Jamhuri yaMuungano na Mkataba wa Afrika Mashariki, Zanzibar si mwanachama rasmi kwasababu Jumuiya ,kama ilivyoelezwa, ni Jumuiya ya nchi na Zanzibar si nchi. "Hakunamwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeitwa Zanzibar.
Ndaniya Jamhuri ya Muungano ipo Zanzibar na hofu kuwa maslahi ya Zanzibarhayatozingatiwa vyema ndani ya Jumuiya hayana msingi." Zanzibar haina uwezondani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa sababu mambo ya nje ni mambo yaMuungano.
Palikuwana mawazo kuwa hoja hii, kusema kweli, inahitaji swali, vipi, kwanza, jambo linakuwa la Muungano ili kuuondoa uwezo wa Zanzibar?

Uk.99:
Tatizo, kwa mujibu wa Zanzibar si suala la kutokuwa na madaraka tu kwa upande waserikali ya Muungano juu ya mambo yasiyokuwa ya Muungano ndani ya Jumuiya yaAfrika Masharaki. Tatizo kubwa zaidi ni kwamba miongoni mwa masuala 18yaliyoshughulikiwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki 4 tu ndiyo mambo ya Muungano.

Mkandara, jisomee kijarida ujionee mazingaombwe ya Muungano wa nchi inayoitwa Tanzania.

Mkandara ukisoma uk.90- 94 ndio utaelewa kuwa EAC, ushirika huu sio wa kibiashara na uchumi tu.

Kuhusu hatua ya mwisho ya shirikisho la kisiasa, katika Mkutano Usio wa Kawaida mwaka2004 Wakuu wa Nchi wa Kenya, Tanzania na Uganda waliazimia kuunda Kamati ya Kuharakisha Shirikisho la Afrika Mashariki. Kamati hiyo inayoongozwa na AmosWako iliwasilisha taarifa yake kwa Wakuu wa Nchi mwezi November mwaka huo huo katika Mkutano wa Sita wa Wakuu wa Nchi. Miongoni mwa mambo mingine, kamati hiyo ilitengeneza ratiba iliyotaka mambo yafuatayo:
a.Rasimu ya katiba ya shirikisho la Afrika Mashariki ifi kapo Desemba 2007
b.Kupitishwa katiba na mkutano wa Wakuu wa Nchi mwezi Januari 2009
c.Kura ya maoni kuhusu katiba ifi kapo Desemba 2009
d.Shirikisho la kisiasa lenye urais wa mzunguko ifi kapo 2010 na uchaguziwa rais ifi kapo 2013

Mw. Nyerere alishasema ni vyema tutakapokwenda EAC ni vyema kuingia huko na serikali mbili ,ya Tangayika na Zanzibar.
Ukaidi wetu, mbele ni giza tupu!



 
Kura hawataki wanasema na bara nao wapewe kura hiyo!

Swali usilotaka kujibu ni kuwa nini kinashindikana kutangaza kuwa muungano umekufa
1. Mna baraza la mapinduzi, kwani kazi yake ni nini?
2. BLW
3.Wabunge
4. Wananchi
5. Wahuni wa UAMSHO

Mkuu
Rudi kwenye post # 184.
 
Mkuu wangu
Hivyo kelele za wajomba sijui kina Jussa au UAMSHO haziwezi kubeba nafasi kubwa ya maamuzi ya Wazanzibar hadi mtuonyeshe kwamba Wazanzibar kwa vithibitisho hawautaki muungano nasi tutawapeni hiyo talaka.


Hivyo mkuu wangu mtu akitaka kutalakiwa hakuna sheria inayomlazimisha bwana kumpa ruksa mwanamke akaulize ndugu na jamaa zake hii ni kazi yake yeye mwenyewe na siku akifikia maamuzi ya kutalakiwa na kuiomba talaka kortini mume hana hila zaidi kuitoa talaka. Ama kwa upande mwingine sii mke anayetoa talaka, hututaki unaandika tu talaka maamuzi ya kufikia kuandika ni yako wewe sio kuomba ruksa kwa mke...
Mkuu Mkandara,

Katika Muungano wa (Tanganyika na Zanzibar)TAnZanIA nani ni bwana, nani ni mke na korti ni ipi/nani?
Na talaka ni nini? au talaka ni ipi?

Ukinifafanulia haya huenda nikapata masuali ya nyongeza ya kutaka kufahamu unazungumzia nini hapa.
 
Nonda,

..lakini hawa walishapiga kura ya maoni kuamua suala la serikali ya umoja wa kitaifa.


Lilianzia kwenye vikao vya CCM na CUF na likapata baraka la Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Muungano.

..sasa kinachowazuia kuitisha kura ya maoni kuhusu muungano ni nini?

CCM wana sera ya kwenda serikali moja na CUF wanasera ya kuleta serikali tatu.

Baada ya kuwepo serikali ya umoja wa kitaifa huko,wananchi wameachwa solemba, ndio vinatokea vikundi kama UAMSHO kupiga mayowe.

..my take ni kwamba viongozi wa Zanzibar, watu ambao wana uelewa kuhusu faida za muungano, wanaogopa matokeo ya kura ya maoni.

Hilo linawezekana likawa kama unavyosema na kwa hivyo, kitokee kikundi huku Tanganyika nacho kidai kura ya maoni ili kuwaunga mkono wazanzibari. Pia ni jambo jema kama sisi Watanganyika 40 milioni tunazijua hasara za muungano kudai kura ya maoni ili kuepuka hasara hiyo/hizo. Kwa nini kuendelea na biashara inayotuingizia hasara?

..also, kupigwa dana-dana kuhusu "kero za muungano" kunatokana na ukweli kwamba kwa hapa tulipofikia Zanzibar imepewa kila kitu, ukiwapa zaidi utavunja muungano. Makamu wa Raisi, na Waziri mwenye portfolio ya muungano, wote ni wa-Zanzibari lakini wameshindwa kupata suluhisho la "kero za muungano."

Kwa maoni yangu hao wapo hapo kuwakilisha matumbo yao na sio walalahoi wa Zanzibar. Wakijaribu kuwatetea jamaa zao, watanyang'anywa fupa.

..mwisho, kwanini hizi "kero za muungano" zimekuwa ni malalamishi ya wa-Zanzibari tu, mbona hatusikii jambo lolote lile kuhusu maslahi ya wa-Tanganyika??

Hili la mwisho hata mimi linanishangaza sana.
Sijui watanganyika wengi hatuelewi kuwa Muungano unatutia hasara au ndio tumezoea kuwa "kichwa cha mwendawazimu".

Wewe una fununu au uelewa wowote juu ya ukimya huu?
Ni ukondoo au maradhi ya kiharusi?
 
Unasema hakuna kiongozi wa bara(Tanganyika) anayeweza kuwazuia?

Umesahau wakati Jumbe alivyoshughulikiwa? Hali ya hewa imechafuka Zanzibar!
Jumbe hakutaka kuvunja muunga bali alitaka kuwepo kwa serikali tatu wajlkati ni chama kimoja tu ndicho kinaongoza nchi.. Na halikuwa swala wala wazo la baraza la Mapinduzi wala wananchi wa Zanzibar isipokuwa yeye mwenyewe kwa kuunga mkono na kusuka mbinu zote na kina Malecela. In fact ilikuwa against serikali ya Mapinduzi na ingekuwa baraka kwa bara isipokuwa leo kina Maalim Seif wanaitumia kama siasa ya kujitenga kwa sababu maamuma wengi hawajui undani wake. Serikali tatu ni kuiwekza bara kuwa na serikali yake kama ilivyo Zanzibar lakini hakuna litakalo ifaidisha Zanzibar maana mamlaka ya Kitaifa yangebakia ktk serikali kuu hivyo hakuna kitu watakacho faidika nacho Zanzibar, lakini kwa bara inahitajika na faida kwao. Wee waulize kina Maalim Seif kuundwa kwa seriikali tatu kutaibadilisha vipi Zanzibar?. Ni Ulaji tu mkubwa, Maalim Seif hana hoja zaidi ya kutumia mbinu ya kuwagawa wananchi kitu ambacho sii itikadi wala sera, plse usiingie mkenge wa kina Maalim Seif.
Zanzibar ina serikali kamili? Leo tunasema Zanzibar ina serikali kamili kwa ajili ya kukidhi utashi wa hoja?
Alaa kwani serikali kamili ni kitu gani?, sii mnayo katiba yenu, mnaye rais mwenye mamlaka ya kuchagua baraza la mawaziri na ambao ndio wasimamizi wakuu wa utendaji wa serikali hiyo kwani hilo hamna?. Labda rudi ktk katiba ya Jamhuri usome SURA YA NNE, halafu sura ya Tano ina zungumzia pia swala la Mahakama, sasa mmebakiziwa kitu gani kuunda serikali?
Umesahau Zanzibar ilipojiunga na OIC, au wakali ule haikuwa serikali kamili? Serikali kamili isiyotambulikana kimataifa?
Swala la kujiunga na OIC ni swala la bunge la muungano (foreign Affairs), nachoweza kusema ni kwamba Tulikosa watu na wajuzi wa kuwakilisha wazo hilo badala yake likapelekwa kama swala la kiimani bungeni kama mnavyojaribu kupitisha mahakama ya kadhi. Sheria na katiba inaweza kabisa kuwaruhusu kuwakilisha hoja hiyo lakini pia tukubali pale kunaposhindwa kwa kura ama uwakilishi mbaya. Tatizo lenu mnajenga hoja kupitia mgongo wa dini na kiimani wakati hili ni swala la kiuchumi na maendeleo na ndio maana hata Benki zisizochukua riba zilipata taabu sana kuingia nchini hadi ilipoelezwa kiuchumi. Na bahati mbaya Benki hizo zinakula riba kama kawa kwa kutumia jina la kugawana profit wakati ni riba ile ile unapewa ama wanachukua.
Miezi michache au mawiki yaliyopita, Balozi Sefu na wazanzibari wenzake (ujumbe wa serikali ya Zanzibar) walikwenda Israel, liliibuka suali hili:

link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...zanzibar-improve-agriculture.html#post3876713
Ukamili wa serikali kamili uko wapi hapo?
Mkuu wangu tatizo lako huelewi maana ya muungano wa serikali mbili tatu au hamsini.. wala hufahamu madaraka yanayoingia ktk umoja ama mtu pekee. Hili ni sawa na mkeo kwenda disco halafu anarudi nyumbani anakwambia Mkandara kamuahidi atampa mtaji wa kufungua duka Millenium tower ati kwa sababu she is independent...Kuna uhuru wa mke au hata mume ktk ndoa lakini uhuru huo una mipaka hata sisi bara tunalazimika ktk maswala kama kupitia kanuni za jamhuri ya muungano yaani ndio hatuwezi kabisa kufanya maamuzi ya kibara pasipo kuwashirikisha visiwani..Rais na hata baraza la Mapinduzi wanaelewa kwamba hakuna Tanganyika isipokuwa serikali ya muungano hivyo lazima Zanzibar wawe na sauti ktk mambo yote ya serikali ya Jamhuri utadhani mume wa Kikerewe.
Tunasema Zanzibar wanayo bendera yao. Lakini angalia bendera ipi inapepea katika ziara hiyo ya ujumbe wa serikali ya Zanzibar. Picha ya tano katika link hii https://www.jamiiforums.com/habari-...wa-smz-wazuru-israil-kwa-ziara-ya-kikazi.html

Ukamili wa serikali kamili uko wapi hapo?
Unarudia tena makosa yaleyalke ya kutoelewa nini maana ya Muungano, labda nikuulize wewe umewahi kuiona bendera ya Tanganyika ikipepea? umewahi kuiona bendera New York, au Michigan ikipepepea?
Bado utakaidi kuwa huu Muungano wa Tanzania (Tanganyika na Zanzibar) ni mazingaombwe? Serikali kamili ya Zanzibar inapeperusha Bendera ya Muungano? Au ndio ukamili wenyewe unaousema hapa?
Mkuu wangu sikaidi isipokuwa nawasikitikia sana Wazanzibar kkwa sababu wengi wenu hamna exposure zaidi ya kwenda Dubai mkaona jinsi Sultan wa nchi hizo walivyogawana kutawala, mwingine kachukua Shrja, Abushabi na kadhalika ndio mnafikiri ni muungano...Wewe tembea nchi zote zenye states ama zenye muungano halafu tuambie ni bendera gani hupepea..
Mkuu Mkandara sitaki nishuku uelewa wako lakini Zanzibar hakuna serikali kamili. Tuwasaidie , tuwape talaka wapate serikali kamili. Au tumeridhika na viini macho na usanii?
Hakuna kiini macho bali wewe mwenyewe unaota kengeza, miwani sio bei mbaya mkuu wangu..Zanzibar ni serikali na katiba imejieleza wazi kabisa jambo ambalo hulioni kwa bara. Nenda kaisome halafu jiulize kwa nini Wabunge wa Zanzibar huchagia pia bungeni ktk maswala ya Bara? Leo hii watu wanauliza kwa nini waziri fulani ni wa Zanzibar lakini amepewa madaraka bara. Hawa wote wanashindwa kuelewa kwamba hakuna serikali ya bara wala kitu bara isipokuwa serikali ya muungano ambayo hata rais anaweza kuwa Mzanzibar, waziri mkuu na bado Zanzibar ikawa na rais wake, baraza lake na kadhalika.. Kiini macho kipo bara ambako kuna uwezekano tukawa hatuna kiongozi hata mmoja juu isipokuwa makamu wa rais ambaye inalazimika kikatiba.

Hivi nikuulize mwanamke aliye olewa huwa hayupo huru na hana mamlaka yake kamili ndani ya ndoa hadi aachike?. Tatizo lako unaamini kwamba mwanamke huru ni yule ambaye hajaolewa, ukisha olewa basi huna uhuru tena kwa sababu ya utamadunin ulokukuza kwamba mke aloolewa ni mali ya mume. Fikra hizi mnaziingiza hadi ktk muungano wakati mko huru ktk kufanya mema kama miungano mingine yoote duniani.
 

Mkuu Mkandara

Quebec ilishawahi kuwa nchi huru hapo mwanzoni au ni jimbo tu la Canada?
Quebec wana uhusiano upi na Canada?
Quebec imeungana na nchi ngapi? Zipi hizo?

Link Quebec - Wikipedia, the free encyclopedia

Kama Canada ni Muungano, ni muungano wa aina ipi? Wanafata mfumo ,muundo upi?
Mfumo wao ni kama huu wetu wa mazingaombwe? Kiini macho?

Canada ina majimbo mangapi? Canada imeundwa na nchi ngapi?

Muungano wa Tanzania umeundwa na nchi ngapi? au majimbo mangapi?
Nitajie kwa majina nchi zilizounda Tanzanaia.

Kama hatuoni kura ya maoni juu ya muungano ni lazima iridhiwe na serikali ya Muungano ( sio serikali ya bara) ni wazi kuwa hatuelewi aina ya Muungano tulionao.

Pia tunasahau au hatuelewi kauli ya Rais wa Muungano anaposema uwepo au kutokuwepo kwa Muungano ni off-limit.
Mjadala /kelele tu kuwa wanataka kura ya maoni zinaleta sokomoko, je wazanzibari watakapoonesha kuwa sasa wanachukua unilateral decision, wale wanajeshi na vifaru vinavyopelekwa kule wakati wa uchaguzi mkuu si idadi yao itaongezwa maradufu?

Hata hivyo, wacha nikubaliane na wewe kwa mantiki ya hoja yako tu kuwa Wazanzibari wanao uwezo wa kuitisha kura ya maoni juu/dhidi ya Muungano lakini wanaogopa au wana sababu wanazozijua wenyewe.

Suali la kujiuliza ni: Je sisi watu milioni 40 tumeridhika na Muungano?

Je sisi watu milioni 40 hatunyonywi na watu laki tisa na nusu? Kama tunanyonywa na wanatutia hasara, je sisi hatutaki kuvunja Muungano?

Au hatutaki kupata maoni ya watu 40 milioni juu ya Muungano ambao unawapendelea wazanzibari?
Au Muungano huu hauwahusu watanganyika bali unawahusu viongozi wao tu?

Na hivi ni kwa nini hakuna kikundi/ watu huku Tanganyika kinachotaka mjadala wa wazi wa Muungano au kutaka kura ya maoni juu/ dhidi ya Muungano?

Hali hii ni ya kawaida kweli? Au tunapata faida gani na Muungano huu kiasi tusiwe tunaudadisi?
Au tunapenda kunyonywa? Au tunapenda kuwabeba Wazanzibari?

Kwa nini kura ya Maoni juu ya muungano si muhimu kwa mtanganyika?

Tunabeba mzigo mzito( Zanzibar) au vipi? Hatutaki kupumzisha mabega yetu?
Kwa nini tuko kimywa sana? Hatupigi ukelele" mnatuumiza" au hatuumii?
Nilijua tu huelewi maana ya Muungano! na itakuwa taabu sana kukuelemisha zaidi. Quebec ni nchi yenye serikali kamili na wanayo bendera yao, Premier ambaye ni kama Dr.Shein wanalo bunge lao, wana exercise constitutional powers in their own right isipokuwa ktk maswala ya Muungano.
Sikuelewi unapoulizia MAJIMBO ni mangapi una maana gani?.. Maana MAJIMBO kwa Canada ndio nchi yaani kama vile zilivyo States za Marekani na kila jimbo lina bendera yake na viongozi wake acha mbali viongozi wa Jamhuri yao. yaani kuna wabunge wa Quebec tu na wapo pia wabunge wa kutoka Quebec ktk bunge la Jamhuri yao (Federal -Taifa), vivyo hivyo kwa majimbo yote.

Hivyo kuna Majimbo 10 na territory 3, majina yake fanya ku google mkuu wangu tusipoteze muda. Quebec wana uhusiano kama ilivyo Zanzibar lakini ktk muungano wao hakuna jimbo hata moja lenye mamlaka ya chini kama Tanganyika. Mfumo wao ni sawa na serikali tatu tukifanya, tofauti na wetu ambao kama tutaufanya uwe wa serikali tatu basi bila shaka Zanzibar itakufa kama ilivyokufa Quebec maana haijulikani kabisa zaidi ya Canada na ndio maana hujui kwamba Quebec ilikuwa nchi huru iliyojiunga kuunda Canada. Nina hakika huko Tanzania, watu wanajua majina ya miji tu ya Canada au hata Marekani ukianza kuwatajia Majimbo au states wanashindwa kuelewa maana hawajawahi kuyasikia isipookuwa zile wanazoziona sana ktk mtandao wakati wa uchaguzi.
 

Mkuu Mkandara.

Umepata uvivu kusoma kijarida: shirikisho ndani ya shirikisho?
Link hii hapa http://www.kituochakatiba.org/index2.php?option=com_docman&task=doc_view&gid=1208&Itemid=27

Ukurasa wa 95-96 utakutana na hii:

Hitimisho lililofikiwa kutokana na maelezo hayo ni kuwa katika uhusiano wa kimataifa kinachotambuliwa ni Jamhuri ya Muungano. Ndani inaweza kuwepo serikali yaZanzibar na Muungano, lakini nje ipo Jamhuri ya Muungano tu. Kwa hiyo
vilevile, Zanzibar katika hali hiyo haina uwezo wa kujadiliana au kufanyamazungumzo kimataifa. Hivyo, serikali ya Muungano inaingiliana na serikali nyingine na vyama vya kimataifa kwa jina la Jamhuri ya Muungano, pamoja na Zanzibar.Hii inahusu vile vile mambo ambayo si ya kisiasa, ya kifedha, ya kiuchumi na michezo, pamoja na shughuli za jumuiya za kiraia kama wale walioohojiwa wanavyoeleza. Hii nipamoja na Umoja wa Mataifa.

Ukurasa 98-99:
Kuhusiana na Jumuiya ya Afrika Mashariki, kwa sababu ya yote mawili, katiba ya Jamhuri yaMuungano na Mkataba wa Afrika Mashariki, Zanzibar si mwanachama rasmi kwasababu Jumuiya ,kama ilivyoelezwa, ni Jumuiya ya nchi na Zanzibar si nchi. "Hakunamwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anayeitwa Zanzibar.
Ndaniya Jamhuri ya Muungano ipo Zanzibar na hofu kuwa maslahi ya Zanzibarhayatozingatiwa vyema ndani ya Jumuiya hayana msingi." Zanzibar haina uwezondani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa sababu mambo ya nje ni mambo yaMuungano.
Palikuwana mawazo kuwa hoja hii, kusema kweli, inahitaji swali, vipi, kwanza, jambo linakuwa la Muungano ili kuuondoa uwezo wa Zanzibar?

Uk.99:
Tatizo, kwa mujibu wa Zanzibar si suala la kutokuwa na madaraka tu kwa upande waserikali ya Muungano juu ya mambo yasiyokuwa ya Muungano ndani ya Jumuiya yaAfrika Masharaki. Tatizo kubwa zaidi ni kwamba miongoni mwa masuala 18yaliyoshughulikiwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki 4 tu ndiyo mambo ya Muungano.

Mkandara, jisomee kijarida ujionee mazingaombwe ya Muungano wa nchi inayoitwa Tanzania.

Mkandara ukisoma uk.90- 94 ndio utaelewa kuwa EAC, ushirika huu sio wa kibiashara na uchumi tu.

Kuhusu hatua ya mwisho ya shirikisho la kisiasa, katika Mkutano Usio wa Kawaida mwaka2004 Wakuu wa Nchi wa Kenya, Tanzania na Uganda waliazimia kuunda Kamati ya Kuharakisha Shirikisho la Afrika Mashariki. Kamati hiyo inayoongozwa na AmosWako iliwasilisha taarifa yake kwa Wakuu wa Nchi mwezi November mwaka huo huo katika Mkutano wa Sita wa Wakuu wa Nchi. Miongoni mwa mambo mingine, kamati hiyo ilitengeneza ratiba iliyotaka mambo yafuatayo:
a.Rasimu ya katiba ya shirikisho la Afrika Mashariki ifi kapo Desemba 2007
b.Kupitishwa katiba na mkutano wa Wakuu wa Nchi mwezi Januari 2009
c.Kura ya maoni kuhusu katiba ifi kapo Desemba 2009
d.Shirikisho la kisiasa lenye urais wa mzunguko ifi kapo 2010 na uchaguziwa rais ifi kapo 2013

Mw. Nyerere alishasema ni vyema tutakapokwenda EAC ni vyema kuingia huko na serikali mbili ,ya Tangayika na Zanzibar.
Ukaidi wetu, mbele ni giza tupu!



Nisome kitu gani ikiwa mwandishi mwenyewe kisha kosea kiswahili?.. Neno SHIRIKISHO haliwezi kuwa na maana sawa na MUUNGANO, hili neno la shiriki linakupa tu kuhusishwa inaweza kuwa ktk jambo zuri au baya wakati muungano mnakuwa kitu kimoja kama ndoa..Hivyo mwandishi aliposema tu shirikisho tayari kakosea na sina sababu ya kumsoma zaidi aidha anataka upotosha au hajui anachokizungumzia kati ya Mke na hawala kuwapa uhalali sawa. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar sio sawa kwa aina yoyote na Ushirika wa EAC..
 
Mkuu Mkandara,

Katika Muungano wa (Tanganyika na Zanzibar)TAnZanIA nani ni bwana, nani ni mke na korti ni ipi/nani?
Na talaka ni nini? au talaka ni ipi?

Ukinifafanulia haya huenda nikapata masuali ya nyongeza ya kutaka kufahamu unazungumzia nini hapa.
Chaguo lako wataka kuwa mume au mke?.. Labda nikupe hadithi ya EMBE..

Unajua Embe ni tunda tamu sana lenye kokwa ndani yake na huwezi kuliita embe pasipo kokwa maana ndoo kiini cha kuwepo embe lenyewe. Sasa inapotokea embe kuingiwa mdudu mara zote hukaa ktk kokwa lakini hufanya ulaji wake ktk nyama za embe na kurudi mafichoni mwake kujipunzisha. Ni rahisi sana kwa mtu kusema embe limeingia mdudu, lakini sii rahisi pia kusema kokwa limeingia mdudu maana ndiko makazi yake lakini siku zote watu wanatazama embe sehemu zinazoliwa..

Zanzibar ndilo kokwa na kina Seif mkuu wangu ndoo yule mdudu aloingia ktk embe, washikeni mashati hao wanaojificha ndani ya kokwa wakati wakila Bara. Maswala ya muungano hata canada au Marekani yanaamuliza Ottawa au Washington, state ya California au jimbo la Ontario hawana mamlaka ya kudai maswala yanayohusu Muungano wa nchi hiyo isipokuwa kupitia bunge la muungano.
 
Let em go...binafsi sioni faida wala hasara ya" Pemba na Unguja" kujiengua kwenye muungano na kuiacha Tanganyika...Thereinafter niunge mkono wazo la wataalamu,wafanyabiashara,wanasiasa na wengine wengi wenye nafasi katika serikali ya muungano kutoka (warudi Pemba & Unguja) na niende mbali zaidi kwa kupendekeza hata waliooana wapeane talaka ili kila mmoja arudi upande wake na km wataona inafaa kurudiana wafuate taratibu za uhamiaji! Muungano usiwe sababu ya wachache wenye hila,agenda binafsi na roho zao mbaya kuhatarisha maisha na mali za wengi wanaotumia muda wao mwingi kujitafutia kesho yao!
 
Back
Top Bottom