Liberata Mulamula: Rais Samia alipanga kukutana na wapinzani lakini ratiba zikaingiliana

Liberata Mulamula: Rais Samia alipanga kukutana na wapinzani lakini ratiba zikaingiliana

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Kuna kitu kimoja ambacho nakichukia kupita kiasi katika maisha yangu ya U-Tanzania. Hiki ni kauli za Polisi au wanasiasa pale ambapo wanajaribu kuficha au kupotosha ukweli ambao ukiwekwa wazi wananchi wataona wanavyokiuka haki za msingi za Watanzania, wanavyokandamiza demokrasia au hata wanavyofanya uhalifu kama wanasiasa au polisi.

Nadhani mmesikia kauli za polisi za "waliuwawa katika mapambano makali ya silaha na polisi na hakuna askari aliyejeruhiwa", "aliuwawa na kitu cha ncha kali tunafanya uchunguzi", "alikufa kwa kujaribu kuruka toka kwenye gari akiwa na pingu" nk.

Na pia kauli za wanasiasa kama "kama hutaki tozo nenda Burundi"; "kama huna nauli piga mbizi"nk.

Sasa leo nimekutana na kauli ya Waziri wa Mambo ya Nchi za nje, Liberata Malamula, akijaribu kueleza kwa nini mkutano kati ya Raisi Samia na wapinzani haukutokea. Anasema "Raisi Samia alipanga kukutana na wapinzani lakini ratiba zikaingiliana". Hivi huu mkutano ulikuwa ufanyike kwa muda gani, miezi sita mfululizo?

Ni wazi kwamba hawa watu wanapotoa hizi kauli wanaona sisi Watanzania ni wajinga, hatuna akili na tanakubali lolote tutakaloambiwa.

Kwa kiingereza huwa ni falsafa ya "insulting Tanzanians' intelligence"

Napenda kwa mara nyingine niwaambie Polisi na Wanasiasa jambo moja, kwamba mtitutukane Watanzania, msidhani kwamba hatuna akili, na msione upole wetu na utunzaji wetu wa hali ya amani nchini kuwa ni watu ambao tupotupo tu kama mazezeta. Uvumilivu wa kutukanwa una mipaka yake, na mnatutukana sana kwa hizi kauli zenu.

Hizi ni kauli zinafanya niwachukie wanasiasa na polisi kwa kiwango cha juu kabisa, kwa kuwa ni kauli ambazo naziona kama matusi kwa Watanzania. Ninavyozitafsiri mimi ni kwamba mnatoa kauli kama hizo eidha kwa kuwa nyie hamna uwezo wa kufikiri, au kwa kuwa mnadhani sisi Watanzania hatuna uwezo wa kufikiri. Jitafakarini sana. Tanzania ya 2021 sio Tanganyika ya 1961. We are not naive - you are disgustingly naive.
 
kuna siku itafika tu huu ujinga wa wanasiasa na police utafika kikomo cjui mataga wataweka wapi sura zao cku hyo....cjui ni lini lakin ipo tu cku yao ujinga ukishatoka kwa baadhi ya watanzania tutaongea lugha moja.

wait and see
 
Alikutana na Shibuda ndiye muakilishi wa vyama vya upinzani
 
Ni aibu kubwa sana kutumia neno ratiba ilikuwa ngumu.
Kati ya huyo mmarekani na upinzani nani alitangulia kuomba kukutana na Rais.

Hii ni dharau kwa watanzania.
Mulamula siyo figure ya matamko ya siasa,alitakiwa awe kwenye idara/kurugenzi za wizara huwa haeleweki.What is America is back?
 
Wameanza kutoka mafichoni,hili la raisi kukutana na Upinzani mbowe ameliuliza mara nyingi mbona hawakujibu?

Baada ya Mabeberu kuuliza ndio wanajitokeza na majibu ya Uongo uongo,wanadhani sisi ni chekechechea?

Anaposema ratiba iliingiliana,iliingiliana na ipi?hio ratiba ya kukutana na wapinzani ilipangwa ni lini na je pande husika zilijulishwa kwamba kuna muingiliano?
 
Kuna kitu kimoja ambacho nakichukia kupita kiasi katika maisha yangu ya U-Tanzania. Hiki ni kauli za Polisi au wanasiasa pale ambapo wanajaribu kuficha au kupotosha ukweli ambao ukiwekwa wazi wananchi wataona wanavyokiuka haki za msingi za Watanzania, wanavyokandamiza demokrasia au hata wanavyofanya uhalifu kama wanasiasa au polisi...
Kinachoweza kuingilia ratiba ya rais ni NATURAL issues pekee...!! Mengine yote yanapangwa...
 
Kuna kitu kimoja ambacho nakichukia kupita kiasi katika maisha yangu ya U-Tanzania. Hiki ni kauli za Polisi au wanasiasa pale ambapo wanajaribu kuficha au kupotosha ukweli ambao ukiwekwa wazi wananchi wataona wanavyokiuka haki za msingi za Watanzania, wanavyokandamiza demokrasia au hata wanavyofanya uhalifu kama wanasiasa au polisi...

Hiyo ni kujaribu kujitosheleza kimasomaso. Uzuri sterling huwa hafi.

Wacha tusubiri
 
Kuna kitu kimoja ambacho nakichukia kupita kiasi katika maisha yangu ya U-Tanzania. Hiki ni kauli za Polisi au wanasiasa pale ambapo wanajaribu kuficha au kupotosha ukweli ambao ukiwekwa wazi wananchi wataona wanavyokiuka haki za msingi za Watanzania, wanavyokandamiza demokrasia au hata wanavyofanya uhalifu kama wanasiasa au polisi...
Rais awe makini. Wananchi walipigia kura ccm kwa hivyo kelele za chadema zisije kufanya ccm kutetereka kwa malengo yake. Chadema wanadai kuongoza wakati walishindwa kwenye uchaguzi. Hili samia awe makini kabisa.

Asifikiri akikutana na chadema wataacha malengo yao ya kutumwa na mabeberu kudai katiba ya kiliberali na serikali tatu ili muungano uvunjike.

Chadema wanataka katiba itakayotoa mwanya kwa wenye nacho kuweza kununua haki bila uoga. Wanataka katiba ambapo matajiri na wanasheria wataweza kuuza na kununua haki bila uoga. Huo ndio msingi uliyojificha wa demokrasia ya kiliberali kwa sisi afrika. Wamagharibi wanapenda tuwe na serikali legelege corrupt za kutimiza maslahi yao.
 
hata katika familia wewe kama mwanaume ndiyo baba wa nyuma sasa lazima utakuwa na taratibu zako na ratiba zako na vipaumbele vyako hawezi mtu yoyote kukupangia kwamba anza na hiki kwanikulikuwa na uharaka gani wa kuanza kuongea na wapinzani? au hata angeanza kuongea nao wangefaidika na nini?

Hizo ndiyo haraka ambazo hazinaga maana walizonazo chadema mngesubiri muone kama mpaka mwaka unaisha hajawaita kuongea naye? au nyie mwaka ni kama miaka kumi au mnapoteza nini msipoongea na rais?

Uvumilivu ni kitu kizuri sana CHADEMA ndiyo wataliangamiza taifa kwa uroho wao wa madaraka maana hata wakipewa hayo madaraka wanayoona hayapo hawawezi kuyaleta kwa maneno lazima watu wafanye kazi tu no way
 
Back
Top Bottom