Elections 2015 Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!

Elections 2015 Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!

Pasco hapa Lowassa anasoma ulichoandika - Lakini chukua hii kama unapenda! Ni bora tuwe na Raisi Fisadi ambaye ametuibia na amewekeza hapa Tanzania, kuliko tuwe na Mafisadi ambao wametuibia na wamewekeza Uswiss!
1907513_966068363427614_4736803703485890492_n.png
 
CCM wampige chini ili njia ya UKAWA kuingia magogoni iwe rahisi, maana jamaa anaonekana kajipanga sana akipitishwa kugombea hakuna wa kumzuia. CCM wataturahisishia kazi kama watamchinjia mbali huyu kiumbe
 
Mwaka huu tutavunja record nyingine duniani FISADI awe raisi ?Tanzania my country akitaka aupate uraisi namshauri EL awe muwazi atuaambie hadharani deal la Richmond alipiga na nani huko CCM hiko ndo kizingiti kinachomwangamiza
Wewe ni kanyoka ktk pori lenye minyoka hivyo huna madhara yoyote kwa mnyama kama swala kwa kuwa kummeza huwezi.ishu ya richmond unauliza leo wakati alitolea ufafanuzi mkutano mkuu ulotaka kumpoka madaraka jk ndipo mkapa akamuokoa jk.wewe leo unaendelea kubwabwaja
 
Jambazi mkuu nchini tanzania awe raisi? Fisadi number moja nchini...lowasa akigombea uraisi na akapata watanzania wote tawaona hawana akili
 
Lowasa labda awe rais wa Yanga Africa ya jangwani lakini si urais wa Tanzania .
Huo hataupata kamwe.
 
Muhimu ni kuiombea nchi yetu amani mwaka uu wa uchaguzi.mwisho wananchi wataamua.MUNGU IBARIKI TANZANIA.MUNGU WABARIKI WATANZANIA
 
We Pasco Wee!Acha Ku2zuga Nyie Ndo Mwala Hela Za Mzee Wa Watu Na Kawatuma Kupost V2 Kama Hv Jf! Dogo Mda Ndo Huu Piga Hzo Hela Usimwachie Fisadi Huyo. Na Akismama Tu Ukawa Yetu Njia Nyeupeee Magogoni!
 
Mimi mwenyewe CCM ndakindaki na katika kitu naomba ni Lowassa akatwe asiwe Rais. Waheshimiwa hakikisheni Lowassa hafiki popote.
Sema akatwe asiwe mgombea kupitia CCM. Hata asipokatwa hatakuwa Rais wa nchi hii
 




NB. Chama cha Mapinduzi ni taasisi huru yenye uwezo wa kufanya shughuli zake kwa uhuru vile ambavyo wataona wenyewe inafaa, ikiwemo vigezo na jinsi ya kuwachagua wagombea wake, ila kwa sisi ambao ni wakereketwa wa mustakali mwema wa nchi hii, kamwe hatutakubali, kuona watu wenye uwezo na wanaokubalika na wengi, wakienguliwa kwa mizengwe tuu, kitu ambacho CCM imekuwa ikikifanya mara nyingu huko nyuma na labda ni kweli ndicho walichopanga kukifanya mwaka huu!, yaani CCM imekuwa ikiwaengua wagombea wazuri kwa mizengwe na ikabaki salama!, lakini this time, nimewasikia baadhi ya wana CCM kindakindaki, kuwa wamejiapiza, this time CCM ikimuengua chaguo lao kwa mizengwe, patachimbika!.

Pasco
Hapo nilipoweka red ni kama am reading something about someone here!! naanza kuhisi nikirudia kusoma mara tatu naweza anza pata taarifa za ziada kumbe!!
 
Pasco nimejawa na maono mabaya sana juu ya matukio yatakayotokea kama sehemeu ya mchakato wa kuelekea uchaguzi Mkuu. Miongoni mwa yale ninayoombea yasitokee ni misiba mikubwa ya ghafla na vilema vya kudumu (Kiharusi,.... ) kutokana na mishtuko ya mambo "ndivyo sivyo". Tukifika June, 2015 salama nitapumuua kidogo.

Eti Pasco mfano Mzee wetu akavuka dalaja, ana mpango gani wa kumuwezesha kumudu ukubwa wa zoezi la kupanda majukwaa walau 7 kwa siku?
 
Last edited by a moderator:
Huwa nashindwa kupata jibu sahihi na jepesi kuhusu Lowasa na wafuasi wake. Kwa muda mfupi sana amejidhihirisha kuwa si mkweli na ni tapeli na hafai kuaminiwa katika nafasi ya urais wa nchi yetu. Na hii imejidhirisha pale aliposhiriki pamoja na kufungiwa na chama chake kwa kuanza kampeni mapema lakini bado alikusanya watu kwa kutumia fedha zake makundi kwa makundi kwa nyakati tofauti na kuwaita mahala alipo na kujitathiminisha kuwa anapendwa sana na wananchi na eti wanamtaka agombee urais na kuwa hawezi kuwazuia watu wanaofika kwake kumtaka agombee urais.

Ukitaka kujua kuwa huu ni utapeli na michezo ya kuigiza jipe majibu sahihi ya maswali haya: -

1. Ni kwa njia gani watu zaidi 100 waweze kukusanyika kwa wakati mmoja wakasafiri toka mikoa ya mbali bila ya kupanga, kuchanga fedha kwa ajili ya safari kwa ajili ya kula, kulala na kujikimu na wasiwe na taarifa ya kule waendako kama watamkuta mwenyeji wao au la na wakasafiri bila hofu na kumkuta mwenyeji wao na kukamilisha dhumuni lao kwa wakati stahiki bila ya kukwama popote pale?

2. Je ni wakati wote Lowasa pale Monduli na nyumbani kwake Dodoma huwa ana waandishi wa habari ambao wako tayari kwa mapokezi yoyote yale hata yale yasiyo na taarifa?

3. Je ni wakati wote Lowasa huwa ameandaa hafla za mapokezi kwa wageni wanaozidi kiasi kikubwa hivyo pale Monduli na Dodoma katika makazi yake bila ya kuwepo taarifa za awali za maandalizi ya mapokezi?

4. Kwa nini kuwepo na taarifa za kukanusha kuhusu wanaojitokeza nyumbani kwake kuwa ni wawakilishi wa taasisi/jamii fulani badae viongozi husika wa taasisi/jamii hukanusha na ukweli kudhihiri kuwa si wawakilishi kama ilivyoelezwa awali?

5. Je waendesha bodaboda toka Mbarali Mbeya zaidi ya kilometa 600 wamewezaje kusafiri na kurudi umbali mrefu hivyo kwa gharama zake binafsi ikiwemo mafuta, kula na kulala?

Usisahau kuwa kipato chao ni cha chini na ni aghalabu kumkuta bodaboda anayeweza kujigharamia umbali mrefu hivyo bila ya matarajio yoyote.

Majibu sahihi ya maswali haya yanakupa aina ya mtu tunaelazimishwa kuwa anapendwa sana na wengi kuwa si mkweli na hafai kuwa kiongozi wa juu wa taifa hili na ni wa kuogopwa kama ukoma hata kama anafedha nyingi za kununua watu kiasi gani bado hatufai.

My take:
Naamini CCM itatutendea haki watanzania kwa kutuletea mgombea asiye mtapeli wala mpenda madaraka na asiye na makundi na asiye na kashfa ya kifisadi wala ya rushwa.
 
Pasco, kama hutajali naomba untajie majina ya wajumbe wa kamati ya maadili ya ccm
 
There he goes....!!!! EL...2015..!!!

No qns...we made our mind....ni Lowassa 2015...period..!!

CCM...sio wapuuzi kiasi hicho, eti wakate jina kwa mtu kama EL...kwani KIZURI CHAJIUZA....

So EL...ana uzika..na ndio maana hata UKAWA wako shocked...as well wapinzani wa EL ndani ya CCM wako paralyzed...hawajaui cha kufanya...!!!

EL....SAFARI YA MATUMAINI ..inaendelea...!!
 
CHANZO NI WHATSAPP SCREEN SHOTS TOKA KWA PRINCE

Mchan mwema
 
Back
Top Bottom