Elections 2015 Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!

Elections 2015 Licha ya kukubalika, Jina la Lowassa halitafika hata CC!

daaaah sijui ni uelewa wangu mdogo ama vipi ila kiukweli sijaona jambo kubwa alilolifanya lowasa hadi makundi yaandamane kwenda kwake.....
 
daaaah sijui ni uelewa wangu mdogo ama vipi ila kiukweli sijaona jambo kubwa alilolifanya lowasa hadi makundi yaandamane kwenda kwake.....

..kwani JK alikuwa amefanya jambo gani kubwa?

..mbona wananchi walimchagua, tena kwa kishindo?

..hizi ni siasa kibongo-bongo, rekodi/uwezo siyo kigezo cha kuchaguliwa nchi hii.

cc Mkandara, Kiranga, Pasco
 
Last edited by a moderator:
Mkandara,

..hii michezo Lowassa alianza kuifanya tangu mwaka 95.

..alipumzika hapa katikati ili kumpa nafasi JK kwa "makubaliano" maalum.

..sasa this time inaonekana Lowassa doesn't wanna take any chances.

..hivi kipenga hakijapulizwa mambo yako hivi. wakiruhusiwa ku-campaign itakuwaje?

cc Pasco, Gagnija, Nyamizi
Nakumbuka sana na bahati mbaya sijui hawa watu wa Lowassa wanafikiri sisi wajinga kiasi gani maana kila siku kazi kubwa ni kuwashambulia wagombea wenzake na maandalizi yao ni dhidi yake tu sio kwamba wanafaa kuwa viongozi. Sasa Lowassa alitaka kugombea peke yake hii nafasi au?

Kibaya zaidi basi kampeni zenyewe wanazifanya Kitaifa kana kwamba taifa zima ni CCM badala ya kujiandaa na uchaguzi wa chama. Huwezi kuwa chaguo la wananchi hata huna baraka za chama chako na kibaya zaidi wote wanaokwenda kumuomba achukue fomu sio hata wanachama wa CCM - huoni maajabu haya...

Hivi kweli akienguliwa atabakia vipi CCM nani atamshika mkono maana wagombea wengine woote kisha wapaka nani atamvumilia.Labda kweli anafikiri UKAWA watampokea au pengine sheria hiyo ya Mgombea binafsi ipo kwa sababu yake na Katiba Pendekezwa ndio hivyo inapigwa panga, yaani namhurumia kuliko anavyojitambua.
 
Sasa hako kakamati ka maadili ndiyo sauti ya wengi, basi wafanye hivyo!! Ni wazi, wakimwaga mboga na sisi tunamwaga ugali. Na kama mbwaa na iwe mbwaa! Kura zote zitakwenda UKAWA!
 
Mkandara,

..hii michezo Lowassa alianza kuifanya tangu mwaka 95.

..alipumzika hapa katikati ili kumpa nafasi JK kwa "makubaliano" maalum.

..sasa this time inaonekana Lowassa doesn't wanna take any chances.

..hivi kipenga hakijapulizwa mambo yako hivi. wakiruhusiwa ku-campaign itakuwaje?

cc Pasco, Gagnija, Nyamizi
Tutarajie vifo kwa baadhi ya watu.
 
Nikiangalia hali ilivyo na ndoto za lowassa za kukalia kiti cha urais toka enzi ya mwalimu. Ikitokea Ccm wakakata jina lake basi ni wazi hata maisha ya mzee huyu hayatokuwa na mdamrefu duniani

Mimi sio mungu ila kiuhalisia naona msungo mkubwa wa mawazo wa lowassa akikosa nafasi ya kuwa mgombea na msongo wa mawazo ni maradhi mabaya mno na huwa husababisha vifo vya ghafla.

Kamati kuu ya Ccm msaidieni EL aendelee kuishi bado ni kipenzi cha wengi pamoja na mapungufu yake kama binadamu.
 
Niliwahi andika kitu kama hiki na nikashambuliwa sana.Ngoja nione leo itakuwaje kwa upande wako.
 
Hivi kuna binadamu anaamini ccm ya leo inaweza kumkata lowassa:what::what::what:hivi hamjui Lowassa ndio ameishikilia ccm isianguke!
 
Niliwahi andika kitu kama hiki na nikashambuliwa sana.Ngoja nione leo itakuwaje kwa upande wako.

Nikiangalia hali ilivyo na ndoto za lowassa za kukalia kiti cha urais toka enzi ya mwalimu.Ikitokea Ccm wakakata jina lake basi ni wazi hata maisha ya mzee huyu hayatokuwa na mdamrefu duniani
Mimi sio mungu ila kiuhalisia naona msungo mkubwa wa mawazo wa lowassa akikosa nafasi ya kuwa mgombea na msongo wa mawazo ni maradhi mabaya mno na huwa husababisha vifo vya ghafla
Kamati kuu ya Ccm msaidieni EL aendelee kuishi bado ni kipenzi cha wengi pamoja na mapungufu yake kama binadamu.

Kwahiyo akabidhiwe nchi sababu ya kuogopa atakufa?? Jiulize anapambana kote kuingia ikulu ili awasaidie watanzania? Au mnataka kuigeuza Ikulu kuwa pango la wanyang'anyi?
 
Wanabodi,

Hii ni tetesi ya habari mbaya kwa wapenzi wa kipenzi cha watu, Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa kuwa pamoja na Mhe. Lowassa kuwa ndie mtu anayekubalika sana kuliko mtu mwingine yoyote ndani ya CCM, wale wasiolitakia mema taifa hili, wamepania kupanga njama za kumhujumu kwa kuhakikisha kuwa jina lake halitaingia hata ndani ya kikao cha CC kujadiliwa!, wamepanga kumchinjia baharini kwenye kamati ya maadili, itakayoyajadili majina wagombea kabla ya kuyaingiza kwenye Kamati Kuu, kujadiliwa!.

Lengo la hujuma hiyo ni kufuatia Lowassa kukubalika kupindukia, jina lake likifika tuu CC, hakuna wa kumkata, hivyo wahafidhina wa CCM, wanaounga mkono kambi ya mmoja wa wagombea, wameapa kuhakikisha jina la Lowassa, halivuki kisingiti cha kamati ya maadili, hivyo kumchinjia rasmi baharini, ili mgombea wao apete kwa mteremko!.

Naomba nisitaje chanzo cha habari hizi, kwa kutumia kanuni ya "the confidentiality of the source"
ila kwa vile hizi ni tetesi tuu, zitakapothibitika ndipo nitaweka source!.

Kama kawaida yetu jf, habari kama hizi ambazo hazijathibitishwa, zimeletwa humu hivi hivi zilivyopokelewa, ili wewe kama mwana jf, be the first to know!, na information is power!, hivyo kutoa fursa kwa wenye uwezo wa kuizuia hii mipango dhalimu inayopangwa, kutaka kuwakosesha Watanzaia mgombea kipenzi chao, chaguo la wengi, na mwenye uwezo usio tia shaka kuyamaliza matatizo yote ya taifa letu Tanzania.

Hii ni thread ya info tip, tuu, hivyo naomba nisiulizwe swali lolote kuhusu hii news tip for your info tuu.

NB. Chama cha Mapinduzi ni taasisi huru yenye uwezo wa kufanya shughuli zake kwa uhuru vile ambavyo wataona wenyewe inafaa, ikiwemo vigezo na jinsi ya kuwachagua wagombea wake, ila kwa sisi ambao ni wakereketwa wa mustakali mwema wa nchi hii, kamwe hatutakubali, kuona watu wenye uwezo na wanaokubalika na wengi, wakienguliwa kwa mizengwe tuu, kitu ambacho CCM imekuwa ikikifanya mara nyingu huko nyuma na labda ni kweli ndicho walichopanga kukifanya mwaka huu!, yaani CCM imekuwa ikiwaengua wagombea wazuri kwa mizengwe na ikabaki salama!, lakini this time, nimewasikia baadhi ya wana CCM kindakindaki, kuwa wamejiapiza, this time CCM ikimuengua chaguo lao kwa mizengwe, patachimbika!.

Pasco
Pasco kweli nawe ni mweupe kanuni za ccm hakuna mahali kamati ya maadili inaweza kugusa kukata jina la mtu wao wanapeleka maoni yao ya kimaadili kamati kuu ndo inapendekeza majina umedanganywa
 
pasco umehaidiwa unikuru mkuu wa itakayokuwa ikulu ya lowasa au?nasikia tayari mshaanza kugawana vyeo.kila la kheri mkuu
 
pasco umehaidiwa unikuru mkuu wa itakayokuwa ikulu ya lowasa au?nasikia tayari mshaanza kugawana vyeo.kila la kheri mkuu

Sasa kinachowasha ni nini? Kukatwa kwa jina la Lowasa? Kwani mmesahau kuwa mtoto wa rais alishasema kuwa rais wa nchi hii hataweza kutokea kanda ya Kaskazini? Kwani tangu alipoitoa kauli hiyo akiwa uvccm iliwahi kukanushwa na mtu yeyote ndani ya uvccm au wa ndani ya ccm? So kutopitishwa kwa jina LA Lowasa ni utekelezaji wa kauli hiyo iliyoonyesha ubaguzi wa kikabila na kikanda, japo ccm watajaijutia.
 
Sasa kinachowasha ni nini? Kukatwa kwa jina la Lowasa? Kwani mmesahau kuwa mtoto wa rais alishasema kuwa rais wa nchi hii hataweza kutokea kanda ya Kaskazini? Kwani tangu alipoitoa kauli hiyo akiwa uvccm iliwahi kukanushwa na mtu yeyote ndani ya uvccm au wa ndani ya ccm? So kutopitishwa kwa jina LA Lowasa ni utekelezaji wa kauli hiyo iliyoonyesha ubaguzi wa kikabila na kikanda, japo ccm watajaijutia.

Mkuu nimejitahidi kadri niwezavyo kurudia mara nyingi changio lako lakini bado sijapata mantiki yoyote ya kuniquote..msaada tafadhali yamkini waweza kuwa na maana iliyojificha.
 
Wanabodi,

Hii ni tetesi ya habari mbaya kwa wapenzi wa kipenzi cha watu, Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa kuwa pamoja na Mhe. Lowassa kuwa ndie mtu anayekubalika sana kuliko mtu mwingine yoyote ndani ya CCM, wale wasiolitakia mema taifa hili, wamepania kupanga njama za kumhujumu kwa kuhakikisha kuwa jina lake halitaingia hata ndani ya kikao cha CC kujadiliwa!, wamepanga kumchinjia baharini kwenye kamati ya maadili, itakayoyajadili majina wagombea kabla ya kuyaingiza kwenye Kamati Kuu, kujadiliwa!.

Mtoa habari wangu amesema kamati ya maadili ya CCM, itamchinja Lowassa kwa kumpa alama za chini kabisa kuliko wagombea wengine wote ili kuirahisishia kazi Kamati Kuu ambayo inatakiwa lazima itoke na majina matano kuyaingiza Halmashauri Kuu, ambapo mgombea rasmi wa CCM ameishachaguliwa, hivyo hili zoezi la kutangaza nia na kuomba uteuzi ni kwa lengo la kukamilisha tuu taratibu.

Sifa za Wagombea Watano watakao pitishwa na CC kuingia tano bora ya NEC ni hawa...
1. Mgombea mmoja mwanamke
2. Mgombea mmoja Muislamu
3. Mgombea mmoja kutoka Zanzibar
4. Mmoja wa Mawaziri Wakuu ambaye ameandaliwa kama kingio la huyo aliyeshachaguliwa!
5. Mgombea aliyeshachaguliwa kuipeperusha bendera ya CCM.

NEC itawapigia kura, ambapo mgombea tajwa, ataongoza kwa kura nyingi atasindikizwa na mgombea mmoja mmoja Mwanamke kutoka Zanzibar na Yule Waziri Mkuu Kingio, ambapo kwenye Mkutano Mkuu, wale wagombea wasindikizaji wawili watajitoa hivyo mgombea huyo kupaswa bila kupingwa kisha Wajumbe wa Mkutano Mkuu watapiga kura zuga tuu na matokeo, atakuwa amechaguliwa kwa asilimia 99%, na hiyo asilimia 1% itakayo mkataa ni kuzungia tuu kuwa CCM demokrasia!.

Lengo la hujuma hiyo ni kufuatia Lowassa kukubalika kupindukia, jina lake likifika tuu CC, hakuna wa kumkata, hivyo wahafidhina wa CCM, wanaounga mkono kambi ya mmoja wa wagombea, wameapa kuhakikisha jina la Lowassa, halivuki kisingiti cha kamati ya maadili, kwa kumchinjia rasmi baharini kwa kumpa maksi za chini, ili mgombea wao apete kwa mteremko!.

Naomba nisitaje chanzo cha habari hizi, kwa kutumia kanuni ya "the confidentiality of the source"
ila kwa vile hizi ni tetesi tuu, zitakapothibitika ndipo nitaweka source!.

Kama kawaida yetu jf, habari kama hizi ambazo hazijathibitishwa, zimeletwa humu hivi hivi zilivyopokelewa, ili wewe kama mwana jf, be the first to know!, na information is power!, hivyo kutoa fursa kwa wenye uwezo wa kuizuia hii mipango dhalimu inayopangwa, kutaka kuwakosesha Watanzaia mgombea kipenzi chao, chaguo la wengi, na mwenye uwezo usio tia shaka kuyamaliza matatizo yote ya taifa letu Tanzania.

Hii ni thread ya info tip, tuu, hivyo naomba nisiulizwe swali lolote kuhusu hii news tip for your info tuu.

NB. Chama cha Mapinduzi ni taasisi huru yenye uwezo wa kufanya shughuli zake kwa uhuru vile ambavyo wataona wenyewe inafaa, ikiwemo vigezo na jinsi ya kuwachagua wagombea wake, ila kwa sisi ambao ni wakereketwa wa mustakabali mwema wa nchi hii, kamwe hatutakubali, kuona watu wenye uwezo wa uongozi, wa kulibadili taifa hili kuwa nchi ya neema, na wanaokubalika na wengi, wakienguliwa kwa mizengwe tuu, kitu ambacho CCM imekuwa ikikifanya mara nyingi huko nyuma na ikabaki salama, hivyo kama ni kweli hiki ndicho walichopanga kukifanya this time!, hakitabaki sala!. Yaani CCM imekuwa ikiwaengua wagombea wazuri kwa mizengwe na ikabaki salama!, lakini this time, nimewasikia baadhi ya wana CCM kindakindaki, kuwa wamejiapiza, this time CCM ikimuengua chaguo lao kwa mizengwe, patachimbika!.

Pasco

Leo ndio kipenga cha CCM kinapulizwa!, hivyo hizi tetesi au zitathibitika au kuwa dismissed!.

Pasco
 
kuacha kumchagua mtu mwenye nguvu ya umma na pesa na marafiki wakubwa ni jambo la hatari sana kwa nchi yeyote, isitoshe, ameshaonyesha nia, labda wangemzuia kabla, lakini sasa is too late.

Wamechelewa sana... Watu wengi wanawazia mwaka huu tu, 2020 si mbali Lowassa akikosa, 2020 ndo atakuwa kashaanzisha chama chake mwenyewe.

Lowassa ana mbinu za sasa na baadaye, anajua siasa kuliko unavyodhani ,na NEC iseje ikajidanganya kumwacha. Kwani kiongozi ajaye atakuwa na wakati mgumu sana, anyway muda utaamua. Yetu macho...
 
Lazima kufuata taratibu na sheria kwani kama hana sifa ataachwa tu na kama akiachwa na kuleta fujo sheria zipo na lazima kufuata utawala wa sheria.
 
Back
Top Bottom