Licha ya kuongoza kutoa wasomi wengi, ni kwanini Mwanza makao makuu ya kanda ya ziwa hawana Vyuo vikuu vya serikali

Licha ya kuongoza kutoa wasomi wengi, ni kwanini Mwanza makao makuu ya kanda ya ziwa hawana Vyuo vikuu vya serikali

Ni kweli kanda ya ziwa imetoa wasomi wengi sana. Hii inatokana na ulaji mzuri wa vichwa vya sato, sangara na kamongo + ugali wa mhogo&dona hupelekea mtoto kuwa na IQ kubwa...!!
Hilo suala la kukosa vyuo vikuu vya serikali ni vipaumbele na muono wa waasisi wa uongozi wa Nchi na kingine watu wa kanda ya ziwa hawana ubnafsi.

Ukiachana na UDSM na UDOM, vyuo vikuu vingine vilianza kama taasisi then vikapandishwa hadhi mpaka kufikia kuitwa universities.
 
Unapozungumzia Kanda ya ziwa ndiko wasomi wengi wanakotoka

Kagera

Mwanza (Hususan kisiwa cha ukerewe)

Mara


Mwanza ndio makao makuu ya mikoa ya kanda ya ziwa, Watu wa Kagera na Mara ni rahisi kufikia hapa lakini jiji hili la pili kwa ukubwa hapa nchini halina chuo kikuu, kwanini ?

Dar kuna UDSM na mkoa wa karibu Morogoro kuna chuo cha Mzumbe na Sokoine

Dodoma kuna UDOM

Mbeya kuna MUST na tawi la Mzumbe

Kwanini Mwanza hakuna chuo kikuu ?
SAUT
IFM
TIA
 
Hata hao wasomi (drs. na profs.) wengi wa ukerewe wana asili ya mkoa wa Mara hasa kabila la wajita na subtribes zake (wakara na waruri ). Anayebisha afanye utafiti wake halafu aje hapa na majibu.
1688667446085.png
 
afu umkute mambo yamenyooka hahahha wanakuaga na kujiona balaa
Nawajua vyema kabila la mama angu hilo nmekaa kiasi chake mkoa wa mara ...na uwakute makazini hawatoagi connection wale umkute kwa interview usitaraji unafuu wanakaa balaa
 
Mwanza ina wasomi wengi tangu lini?

Wasomi wapo

1.kilimanjaro
2.kagera
3.mbeya
Nitajie maprofessor wakichaga nikutajie maprofessor zaidi ya 50 wa kisukuma kwa vyuo vitatu tu vya SUA, BUGANDO NA MUHIMBILI.
 
Population ikoje usukumani vs uchagani
Wachaga wanapenda mambo ya fedha na wasomi wao wengi wapo CBE, IFM N.K na wasukuma utawakuta kwenye vitu vigumu kama medicine, uhandisi, veterinary medicine na mambo ya madini na kilimo SUA pekee faculty ya veterinary medicine ina maprofessor 10 wa kisukuma.
 
Kwani jamaa kaleta comparison,kuwa na wasomi wengi maana yake wapo waliosoma hiyo elimu ya juu wengi?

Au ndio superiority complexes za kikanda na kikabila zinakupa changamoto.

Issue kubwa kwake ni kwanini hakuna chuo kikuu cha serikali?Labda ungemsaidia ktk hilo.

Ndio maana bado tupo ktk nchi masikini zaidi duniani🤣🤣.
Mwanza ina wasomi wengi tangu lini?

Wasomi wapo

1.kilimanjaro
2.kagera
3.mbeya
 
Nyie Sgr inawatisha baba yenu yule aliwajengea 😁😁😁😁

Kwanza Mwanza ipi Ina wasomi wengi? Lini Wasukuma walienda shule wakaacha kuchunga ng'ombe?
Hawa watu wana umimi sana shujaa aliwapendelea sana hawaridhiki
 
Wachaga wanapenda mambo ya fedha na wasomi wao wengi wapo CBE, IFM N.K na wasukuma utawakuta kwenye vitu vigumu kama medicine, uhandisi, veterinary medicine na mambo ya madini na kilimo SUA pekee faculty ya veterinary medicine ina maprofessor 10 wa kisukuma.
Professor 10 relative to population number ya wasukuma ni kawaida sio wengi wa kutosha bado kazeni mwendo
 
Back
Top Bottom