Lifahamu kiundani zao la Nyanya chungu (Ngogwe) na jinsi ya kulilima

Lifahamu kiundani zao la Nyanya chungu (Ngogwe) na jinsi ya kulilima

Heshima kwenu wanaJamvi Nimelima eka1 ya nyanya chungu na Mahindi Mabichi MVUMI KILOSA Morogoro nashukuru mazao yamekubali sana khs Nyanyachungu Inatakiwa kila wk nivune nakuuza zikikaa sana znabadilika Rangi inakuwa C ishu ss Tatizo nililo nalo nina Mteja 1 kwakweli ananiua Nimeona nije kwenu nikiamini hamtakosa chakunishauri Natanguliza shukrani wandugu!
Kwema mkuu? Bado unalima nyanya?
 
Thnx frend,,,! kwa ushauri ntaufanyia kz binafsi nimehamacka na KILIMO kupitia michango mbali mbali ya wadau wa Jukwaa hili Kwahiyo wale wote mnaoweka michango yenu ya mawazo humu mjue haipotei bure tunaifanyia kz naimekuwa msaada sana. Ikimpendeza MUNGU kuanzia mwezi July nitakuja Rasmi kuwashukuru waDAU wa Jukwaa hili Endeleeni kuBARIKIWA,,,!
mkuu habari, bado unafanya kilimo cha nyanya chungu?
 
Mimi nililima ngogwe maeneo ya tengeru kando ya barabara moshi Arusha, eneo ni kama nusu eka, ilikuwa 1998 mpaka nilipokwenda secondary 2001 mahitaji yote yalipatikana kutokana zao hili, nilichuma kila jumamosi na kuuza katika soko la tengeru, wastani ilikuwa ni mfuko wa salfet mkubwa kwa kila mchumo, sikutuia gharama yeyote kwani mbegu nilikuwa natengeneza mwenyewe maji yalikuwa bure mferejini, mbolea nilikuwa naweka ya kuku, sikuwahi kupiga dawa yeyote. Kwa kweli ngogwe ni zao la kuanzia kutafuta mtaji kama mtu una eneo la kulima na maji yapo.
Nampango wa kulima nyanya chungu apo Tengeru,siku si nyingi ,natumaini utanipa mwongozo wa kuanza adi mavuno,
Swali langu izo mbegu unazitengenezaje?
 
View attachment 1604040

Hatua za kufuata ukitaka kulima nyanya chungu
Nyanya Chungu ni zao la Kitropic linalotoa mazao yake kama matunda au kama mboga. Rangi ya matunda huwa kijani kibichi au kijani-njano, au njano-nyupe. Kuna aina mbalimbali za nyanya chungu ambazo ni ni nyanya chungu za asili na zingine ni chotara siyo chungu kama za asili.

Mazingira
Zao hili hustawi vizuri maeneo yenye baridi ya wastani na joto la wastani kuanzia nyuzi joto 25°C hadi 35°C, hupendelea udongo tifu tifu usiotwamisha maji na wenye rutuba. Kama utaweza kutumia mbolea za samadi na mboji au mbolea za asili pamoja , basi nyanya chungu hustawi vizuri sana.

Kuandaa shamba
Mbegu za nyanya chungu huandaliwa kwenye kitalu kwanza kabla ya kupelekwa shambani.

Maelekezo ya kuandaa kitalu cha nyanya chungu.
  • Chagua eneo la kuanzisha kitalu kwenye maeneo yanayopatikana maji kwa urahisi.
  • Inua udongo wa kitalu hadi kufikia kimo cha sm 20 na upana wa mita 1 na urefu wowote. Bonda bonda mabonge makubwa ya udongo ili kupata udongo laini.

- Weka mbolea ya asili iliyooza vizuri, changanya ndoo moja kubwa ya lita 20 ya mbolea hiyo kwa eneo la mita 1 kwa mita 1 (1 m2). Kwa hiyo kama tuta lako la kitalu lina urefu wa mita 5 na upana mita 1, utaweka ndoo 5 za mbolea za asili.

- Kama ni wakati wa kiangazi, mwagilia tuta lako kwa siku 3 mfululizo mpaka udongo uloane vizuri.

Kusia mbegu
Maelekezo ya namna ya kusia mbegu kwa usahihi
- Tengeneza vimifereji vyenye kina cha sm 2 kukatisha tuta, nafasi kati kimfereji kimoja na kingine ni sm 15 au nusu rula.

  • Sia mbegu zako ndani ya vimifereji hivyo, halafu funika na udongo laini.
  • Weka matandazo ya nyasi juu ya tuta ili kuzuia jua kali na matone ya maji ya moja kwa moja.
  • Mwagilia maji kitalu chako juu ya nyasi asubuhi na jioni kila siku. Ila inashauriwa kumwagilia kitalu chako maji wakati wa jioni.

  • Mbegu za nyanya chungu huota baada ya siku 10 hadi 14 tangu kusia. Baada ya mbegu kuota toa matandazo ya nyasi halafu yaweke matandazo hayo katikati ya mistari ya miche.
  • Tengeneza kivuli cha matandazo ya nyasi juu ya kitalu chenye kimo cha mita moja, kivuli hicho cha nyasi lazima kiwe kinapitisha mwanga wa jua walau kidogo ili kuruhusu mwanga kuifikia miche.

Kupandikiza miche shambani
Miche huwa tayari kuhamishiwa shambani baada ya mwezi mmoja hadi mwezi mmoja na nusu tangu mbegu kuota. Nafasi ya kupandikiza nyanya chungu ni mita 1 kwa mita 1 (yaani mita 1 shina hadi shina na mita 1 mstari hadi mstari)

Kabla ya kupandikiza miche chimba mashimo yenye ukubwa kiasi, weka samadi iliyooza vizuri kiasi cha mkono mmoja uliojaa, halafu fukia udongo kiasi. Baada ya kufukia udongo pandikiza mche wako, kila shimo mche mmoja. Kama ni kipindi cha kiangazi pandikiza wakati wa jioni, baada ya kupandikiza mwagili maji vizuri.

Kutunza shamba
Mimea jamii ya mbogamboga ikiwemo nyanya chungu haipendi bugudha ya magugu shambani, kwa hiyo hakikisha unafanya palizi wakati wote kuakikisha magugu hayaathiri ustawi wa mmea.
Dhibiti magonjwa na wadudu mabalimbali wanaoathiri zao hili, kwa kutumia madawa mabalimbali na matumizi ya mbolea mbalimbali za kurutubisha mimea pale inapobidi na iwe ya kilimo hai.
KUVUNA

Nyanya chungu huwa tayari kuvunwa ndani ya siku 90 hadi 120 tangu kupandikiza. nyanya chungu inaweza kuvunwa mara 1 au mara 2 kwa wiki. Matunda ya nyanya chungu yanatakiwa kuvunwa kabla hayajabadilika rangi kutoka nyeupe kwenda njano mpauko.

matunda haya ya nyanya chungu yanaweza kusindikwa kuwa unga. Ili kusindika nyanya chungu kuwa unga fwata hatua zifuatazo;

  • Chagua nyanya chungu bora na zioshe kwenye maji
  • Kata kata nyanya chungu hizo kutengeneza vipande vidogo dogo, halafu tandaza vipande hivyo kwenye mkeka au turubai safi

  • Anika vipande hivyo vya nyanya chungu juani hadi vikauke.
  • Baada ya vipande hivyo kukauka vizuri, visage kwa kutumia kinu au mashine ya mkono mpaka viwe unga.

  • Tunza unga huo kwenye chombo kisafi ambacho hakingizi hewa.
  • Unaweza kutumia unga huo kwenye maharage, karanga, nyama na mboga zingine, mboga iliyowekwa unga huu wa nyanya chungu inakua tamu mno na inakua na virutubisho vya kutosha.

Wadau ahitaji kujua zaidi kuhu kilimocha nyanya chungu na jinsi ya kupata masoko

----

----


Wadau mbalimbali wachangia kuhusu zao hili la nyanya chungu

----

-----

----
napenda nyanya chungu haswa kama jina lilivyo nilikuwa nazipata enzi hizo kwa sasa nitapata wapi mana masoko mengi hakuna.
 
Heshima kwenu wanaJamvi Nimelima eka1 ya nyanya chungu na Mahindi Mabichi MVUMI KILOSA Morogoro nashukuru mazao yamekubali sana khs Nyanyachungu Inatakiwa kila wk nivune nakuuza zikikaa sana znabadilika Rangi inakuwa C ishu ss Tatizo nililo nalo nina Mteja 1 kwakweli ananiua Nimeona nije kwenu nikiamini hamtakosa chakunishauri Natanguliza shukrani wandugu!
Kwa heka Moja ulikuwa unavuna kiasi gani?
 
Uzi uendelee wadau,wale walio weza kulima waje na mrejesho tujifunze pamoja ili tuelimishane kwa undani na namna ya kukabiliana na changamoto zote zinazojitokeza.

Kuna kipengele cha muhimu sana hakijagusiwa na wadau, kwa asilimia kubwa,

1.Uangalizi kwenye hatua zote 4 za ukuaji
A.Ukuaji wa mwanzo kabisa -Establishment
B.Maendeleo ya ukuaji (Growth development)
C.Maua - Kutunga Matunda-Kuwa tayari kuvunwa (Flowering - Fruit set- maturity)
D.Mavuno(Harvesting)
2.Mahitaji na uwekaji wa Mbolea katika hatua zote 4
3.Muda sa hihi wa kuweka mbolea(idadi ya siku baada ya kupanda(Days After Transplanting)) na aina ya virutubisho vya mbolea vinavyohitajika na mmea huu kwa wanaopanda mashambani (N-Nitrogen,P-Phosphorus,K-Potassium,Ca-Calcium,Mg-Magnesium,S-Sulphur)
4.Magonjwa na dawa zake(viambata badaya ya majina ya dukani).

Kwa mwenye uelewa tunaomba ku share unachokijua.

Binafsi ni mkulima,na bandika hichi kidogo nlichofanikiwa kukijua katika harakati,

Ngogwe hizi tunazolima sisi kwa asilimia kubwa ni za group la "DB3" hasa hasa Gilo,
Zinahitaji udongo wenye rutuba nzuri ,mbolea za samadi na mboji (ng'ombe,mbuzi na kuku) ambazo zinakua na NPK(hapa hizi ndio Base dressing) ni sahihii sana pia mbolea za viwandani kwa namna moja ama ingine zinaweza hitajika sana hasa kwa wale wanaolima kwenye udongo wenye upungufu wa rutuba na watakao kosa samadi na mboji.
Ntaelezea mbolea hizi,
Ngombe na Mbuzi zinakaa muda mrefu shambani na kufanya udongo kua na rutuba kwa muda mrefu ukilinganisha na aina nyingine ya mbolea(hizi ziko katika mtindo (form) ya inogarnic Nitrogen na organic Nitrogen ambayo ipo kwenye mkojo na urea ambayo ipo kwenye mavi,hii huitaji kubadilika kua Nitrogen(N) alafu bacteria na enzymes watazibadili kwenye udongo ili iwe Nitrate NO3(mfumo ambao mmea utaichukua kwa haraka),kwa hiyo ni slow acting/release,ndo mana unashauriwa uweke week 2 ama zaidi kabla ya kuhamisha miche yako,
Mbolea ya kuku hii ina Nitrate tayari nyingi kwa hiyo ni nzuri kwa kipimo sa hihi kwa mahitaji ya haraka(fast release/acting) na haikai shambani muda ikishachukuliwa na mmea basi zoezi limeishia hapo,zingatia kwamba ukizidisha mbolea hii itaunguza mmea.

Note: Zao hili linaweza kuota bila kuweka chochote,hapa ina maanisha udongo ilipo ota umejitosheleza,

Hapa tunaongelea kwa wale wanaotaka kulima kibiashara wakilenga mazao mengi na ya uhakika.

Tuendelee

Mbolea za viwandani,
Mmea wa nyanya chungu(ngogwe) huhitaji mbolea ya Nitrojeni na Phosphorus kwa kukua vizuri na imara na Pottasium kwa matunda (Nitrogen inaleta makuzi,majani,shina na kusaidia photosynthesis-upumuaji,lakini isiwekwe kwa wingi sana, nitrojeni ikiwa nyingi na ikiwekwa mara kwa mara huleta majani mengi na kufanya mmea kua na msitu,hii hupunguza mazao sana,pia mmea huhitaji phosporus kwa wingi katika hatua hizi za awali baada ya kuhamisha miche ili kuleta mizizi bora na mingi pia imara ambayo huwezesha mmea kuchukua chakula katika udongo ikiwemo hiyo nitrogen,pia husaidia kinga ya mmea kwa magonjwa,
Kwa hizi za viwandani inashauriwa kuweka mbolea pembeni ya mmea(side dressing) baada ya week 2(hapa mmea unakua umeshajishika chini vizuri na kuanza kutoa majani mengine mapya) weka mbolea shambani zenye uwiano sawa wa NPK isiyo ya kiwango cha juu mfano (10:10:10, 12:12:12) hata zenye kupungua kidogo na kuongezeka kidogo hazina tatizo mfano 11:14:10(kama zipo)
Utarudia mbolea wakati maua yana anza,utaweka mbolea zenye nitrojeni ya chini zaidi na Potassium ya juu kidogo mfano 5:10:20 etc,Calcium(CaO na Magnesium(MgO),zikiwa na O maanza yake ni oxides(kwamba zinayeyuka kwenye maji -soluble) zitahitajika,Calcium Nitrates(Ca(NO3)2) kama CAN ina Nitrogen 26-27%,Nitrabor,CALCINIT etc zenye N 13-15.5% na 25-27% CaO hizi nusu ya nitrogen ni ni slow release na nusu ni fast acting (kuna mbolea nzuri zenye michanganyiko inayofaa direct kama Minjingu Pamba(white diamond hii ina N,P,K,S,Mg,CaO),kuna Mbolea za kampuni OCP,Kuna mbolea za Yara(Nitrabor) hii ina 15.4 N(nusu N na nusu NO3-inayochukuliwa haraka na mmea) pia ina Boron kidogo,na aina zingine zenye majina tofauti tofauti. Tafadhali zingatia mbolea ina virutubisho(nutrients) gani na sio jina tuu ili mradi,
Utaendelea na mbolea za maji (Foliar) zenye Potassium kubwa(K 35-60%) kila baada ya siku 10-14 kama Multi K,Master Fruiter etc,alafu utarudia tena mbole za punje,NPK(Nitrogen ya wastani,phosporus ya chini kabisa na potassium ya juu zaid ya zote)kila baada ya siku 21-30
Utazingatia muonekano wa mmea kwa macho ili uweke mbolea sa hihi na kiwango sa hii hii,utakua pia unapiga mbolea za maji za kwenye majani(foliar),wakati huu phosporus haihitajiki kwa wingi kwa kua mizizi ishajishika vizuri katika hatua ya awali.

Kuna booster nyingi na nzuri,zenye virutubisho vingi vikuu(NPK),vya kati(Ca,Mg,S) na vya chini(Fe,Mn,Cu,Zn,B,Mo),pendelea zile zenye virutubisho vya kawaida na vya ziada pamoja,kuna zingine zina pendelewa sana lakini zinaivisha matunda haraka(mfano Vigmax) iwekwe mwanzoni wakati wa maua na sio wakati wa mavuno,kuna mbolea kama Max Green na zingine zipo vizuri(tukichambua zina virutubisho gani tutampoteza kabisa mkulima).

Mbolea za chenga chenga hizo nlizotaja (NPK,CaO,MgO,S) ni muhimu sana,alafu unaweza endelea na mbolea za juu za majani(hizi zote zinafanya kazi haraka sana kwa maana ya matokeo yake),zingatia maelezo ya kila mbolea kwenye vibandiko vyake.

Napokea maswali kwa hapa nlipo elezea,maswali yaliyoshiba na yenye uelewa ndani yake,sio maswali yasio na kichwa wala mguu i.e mtu anataka lima eneo flani,mkoa flani labda anauliza soko,soko kafanye research mwenyewe mazingira unayoweza yafikia.

NB:TUSIKARIRI,TUELEWE (ni nini na kwa nini)

Kwa wale wavivu wa kuuliza unaweza toa kiasi gani kwa ekari wakati hajui tofauti ya ekari na hekta wasituchoshe (~2.5 ekari ndo 1 hekta),4047m² ni ekari ama kibongo bongo 70mx70m - 4900m²,hii ntaijibu kwa mfumo unao eleweka.
Kwa upandaji wa 60cm mche hadi mche na 100cm kwa mstari hadi mstari maana yake kwa ekari moja ya 4900m² utakua na miche ~8,150-8,200
kwa mbegu hizi za kawaida za mashamba ya nje (OPV) na aina ya "DB3" unaweza toa kwa wastani wa mavuno yote kwa msimu usio pungua ukubwa wa eneo kwa square meter x 0.01,mfano eneo lako ni robo ekari,tuseme 1000m² - 1250m² utazidisha kwa 0.01 upate debe 10-12.5 wastani wa mavuno yako yoote kwa msimu wako,
Mwanzo wa mavuno utaweza kutoa debe 60 kila mchumo(itapanda mpaka debe 75 na kushuka mpaka 30 kutokana na mazingira,uangalizi,usimamizi na ulishaji wa virutubisho,wadudu na magonjwa).

Natanguliza heshima za dhati kwa mwenye uzi huu Kubota ,hizi elimu zinasaidia sana kama upako vile,tusichoke kuwa ng'amua watakao kua tayari na wenye uelewa.

Nawasilisha
 
Uzi uendelee wadau,wale walio weza kulima waje na mrejesho tujifunze pamoja ili tuelimishane kwa undani na namna ya kukabiliana na changamoto zote zinazojitokeza.

Kuna kipengele cha muhimu sana hakijagusiwa na wadau, kwa asilimia kubwa,

1.Uangalizi kwenye hatua zote 4 za ukuaji
A.Ukuaji wa mwanzo kabisa -Establishment
B.Maendeleo ya ukuaji (Growth development)
C.Maua - Kutunga Matunda-Kuwa tayari kuvunwa (Flowering - Fruit set- maturity)
D.Mavuno(Harvesting)
2.Mahitaji na uwekaji wa Mbolea katika hatua zote 4
3.Muda sa hihi wa kuweka mbolea(idadi ya siku baada ya kupanda(Days After Transplanting)) na aina ya virutubisho vya mbolea vinavyohitajika na mmea huu kwa wanaopanda mashambani (N-Nitrogen,P-Phosphorus,K-Potassium,Ca-Calcium,Mg-Magnesium,S-Sulphur)
4.Magonjwa na dawa zake(viambata badaya ya majina ya dukani).

Kwa mwenye uelewa tunaomba ku share unachokijua.

Binafsi ni mkulima,na bandika hichi kidogo nlichofanikiwa kukijua katika harakati,

Ngogwe hizi tunazolima sisi kwa asilimia kubwa ni za group la "DB3" hasa hasa Gilo,
Zinahitaji udongo wenye rutuba nzuri ,mbolea za samadi na mboji (ng'ombe,mbuzi na kuku) ambazo zinakua na NPK(hapa hizi ndio Base dressing) ni sahihii sana pia mbolea za viwandani kwa namna moja ama ingine zinaweza hitajika sana hasa kwa wale wanaolima kwenye udongo wenye upungufu wa rutuba na watakao kosa samadi na mboji.
Ntaelezea mbolea hizi,
Ngombe na Mbuzi zinakaa muda mrefu shambani na kufanya udongo kua na rutuba kwa muda mrefu ukilinganisha na aina nyingine ya mbolea(hizi ziko katika mtindo (form) ya inogarnic Nitrogen na organic Nitrogen ambayo ipo kwenye mkojo na urea ambayo ipo kwenye mavi,hii huitaji kubadilika kua Nitrogen(N) alafu bacteria na enzymes watazibadili kwenye udongo ili iwe Nitrate NO3(mfumo ambao mmea utaichukua kwa haraka),kwa hiyo ni slow acting/release,ndo mana unashauriwa uweke week 2 ama zaidi kabla ya kuhamisha miche yako,
Mbolea ya kuku hii ina Nitrate tayari nyingi kwa hiyo ni nzuri kwa kipimo sa hihi kwa mahitaji ya haraka(fast release/acting) na haikai shambani muda ikishachukuliwa na mmea basi zoezi limeishia hapo,zingatia kwamba ukizidisha mbolea hii itaunguza mmea.

Note: Zao hili linaweza kuota bila kuweka chochote,hapa ina maanisha udongo ilipo ota umejitosheleza,

Hapa tunaongelea kwa wale wanaotaka kulima kibiashara wakilenga mazao mengi na ya uhakika.

Tuendelee

Mbolea za viwandani,
Mmea wa nyanya chungu(ngogwe) huhitaji mbolea ya Nitrojeni na Phosphorus kwa kukua vizuri na imara na Pottasium kwa matunda (Nitrogen inaleta makuzi,majani,shina na kusaidia photosynthesis-upumuaji,lakini isiwekwe kwa wingi sana, nitrojeni ikiwa nyingi na ikiwekwa mara kwa mara huleta majani mengi na kufanya mmea kua na msitu,hii hupunguza mazao sana,pia mmea huhitaji phosporus kwa wingi katika hatua hizi za awali baada ya kuhamisha miche ili kuleta mizizi bora na mingi pia imara ambayo huwezesha mmea kuchukua chakula katika udongo ikiwemo hiyo nitrogen,pia husaidia kinga ya mmea kwa magonjwa,
Kwa hizi za viwandani inashauriwa kuweka mbolea pembeni ya mmea(side dressing) baada ya week 2(hapa mmea unakua umeshajishika chini vizuri na kuanza kutoa majani mengine mapya) weka mbolea shambani zenye uwiano sawa wa NPK isiyo ya kiwango cha juu mfano (10:10:10, 12:12:12) hata zenye kupungua kidogo na kuongezeka kidogo hazina tatizo mfano 11:14:10(kama zipo)
Utarudia mbolea wakati maua yana anza,utaweka mbolea zenye nitrojeni ya chini zaidi na Potassium ya juu kidogo mfano 5:10:20 etc,Calcium(CaO na Magnesium(MgO),zikiwa na O maanza yake ni oxides(kwamba zinayeyuka kwenye maji -soluble) zitahitajika,Calcium Nitrates(Ca(NO3)2) kama CAN ina Nitrogen 26-27%,Nitrabor,CALCINIT etc zenye N 13-15.5% na 25-27% CaO hizi nusu ya nitrogen ni ni slow release na nusu ni fast acting (kuna mbolea nzuri zenye michanganyiko inayofaa direct kama Minjingu Pamba(white diamond hii ina N,P,K,S,Mg,CaO),kuna Mbolea za kampuni OCP,Kuna mbolea za Yara(Nitrabor) hii ina 15.4 N(nusu N na nusu NO3-inayochukuliwa haraka na mmea) pia ina Boron kidogo,na aina zingine zenye majina tofauti tofauti. Tafadhali zingatia mbolea ina virutubisho(nutrients) gani na sio jina tuu ili mradi,
Utaendelea na mbolea za maji (Foliar) zenye Potassium kubwa(K 35-60%) kila baada ya siku 10-14 kama Multi K,Master Fruiter etc,alafu utarudia tena mbole za punje,NPK(Nitrogen ya wastani,phosporus ya chini kabisa na potassium ya juu zaid ya zote)kila baada ya siku 21-30
Utazingatia muonekano wa mmea kwa macho ili uweke mbolea sa hihi na kiwango sa hii hii,utakua pia unapiga mbolea za maji za kwenye majani(foliar),wakati huu phosporus haihitajiki kwa wingi kwa kua mizizi ishajishika vizuri katika hatua ya awali.

Kuna booster nyingi na nzuri,zenye virutubisho vingi vikuu(NPK),vya kati(Ca,Mg,S) na vya chini(Fe,Mn,Cu,Zn,B,Mo),pendelea zile zenye virutubisho vya kawaida na vya ziada pamoja,kuna zingine zina pendelewa sana lakini zinaivisha matunda haraka(mfano Vigmax) iwekwe mwanzoni wakati wa maua na sio wakati wa mavuno,kuna mbolea kama Max Green na zingine zipo vizuri(tukichambua zina virutubisho gani tutampoteza kabisa mkulima).

Mbolea za chenga chenga hizo nlizotaja (NPK,CaO,MgO,S) ni muhimu sana,alafu unaweza endelea na mbolea za juu za majani(hizi zote zinafanya kazi haraka sana kwa maana ya matokeo yake),zingatia maelezo ya kila mbolea kwenye vibandiko vyake.

Napokea maswali kwa hapa nlipo elezea,maswali yaliyoshiba na yenye uelewa ndani yake,sio maswali yasio na kichwa wala mguu i.e mtu anataka lima eneo flani,mkoa flani labda anauliza soko,soko kafanye research mwenyewe mazingira unayoweza yafikia.

NB:TUSIKARIRI,TUELEWE (ni nini na kwa nini)

Kwa wale wavivu wa kuuliza unaweza toa kiasi gani kwa ekari wakati hajui tofauti ya ekari na hekta wasituchoshe (~2.5 ekari ndo 1 hekta),4047m² ni ekari ama kibongo bongo 70mx70m - 4900m²,hii ntaijibu kwa mfumo unao eleweka.
Kwa upandaji wa 60cm mche hadi mche na 100cm kwa mstari hadi mstari maana yake kwa ekari moja ya 4900m² utakua na miche ~8,150-8,200
kwa mbegu hizi za kawaida za mashamba ya nje (OPV) na aina ya "DB3" unaweza toa kwa wastani wa mavuno yote kwa msimu usio pungua ukubwa wa eneo kwa square meter x 0.01,mfano eneo lako ni robo ekari,tuseme 1000m² - 1250m² utazidisha kwa 0.01 upate debe 10-12.5 wastani wa mavuno yako yoote kwa msimu wako,
Mwanzo wa mavuno utaweza kutoa debe 60 kila mchumo(itapanda mpaka debe 75 na kushuka mpaka 30 kutokana na mazingira,uangalizi,usimamizi na ulishaji wa virutubisho,wadudu na magonjwa).

Natanguliza heshima za dhati kwa mwenye uzi huu Kubota ,hizi elimu zinasaidia sana kama upako vile,tusichoke kuwa ng'amua watakao kua tayari na wenye uelewa.

Nawasilisha
Mkuu ni foliar fertilizer gani nzuri kwa matunda kutokana na uzoefu wako
 
Uzi uendelee wadau,wale walio weza kulima waje na mrejesho tujifunze pamoja ili tuelimishane kwa undani na namna ya kukabiliana na changamoto zote zinazojitokeza.

Kuna kipengele cha muhimu sana hakijagusiwa na wadau, kwa asilimia kubwa,

1.Uangalizi kwenye hatua zote 4 za ukuaji
A.Ukuaji wa mwanzo kabisa -Establishment
B.Maendeleo ya ukuaji (Growth development)
C.Maua - Kutunga Matunda-Kuwa tayari kuvunwa (Flowering - Fruit set- maturity)
D.Mavuno(Harvesting)
2.Mahitaji na uwekaji wa Mbolea katika hatua zote 4
3.Muda sa hihi wa kuweka mbolea(idadi ya siku baada ya kupanda(Days After Transplanting)) na aina ya virutubisho vya mbolea vinavyohitajika na mmea huu kwa wanaopanda mashambani (N-Nitrogen,P-Phosphorus,K-Potassium,Ca-Calcium,Mg-Magnesium,S-Sulphur)
4.Magonjwa na dawa zake(viambata badaya ya majina ya dukani).

Kwa mwenye uelewa tunaomba ku share unachokijua.

Binafsi ni mkulima,na bandika hichi kidogo nlichofanikiwa kukijua katika harakati,

Ngogwe hizi tunazolima sisi kwa asilimia kubwa ni za group la "DB3" hasa hasa Gilo,
Zinahitaji udongo wenye rutuba nzuri ,mbolea za samadi na mboji (ng'ombe,mbuzi na kuku) ambazo zinakua na NPK(hapa hizi ndio Base dressing) ni sahihii sana pia mbolea za viwandani kwa namna moja ama ingine zinaweza hitajika sana hasa kwa wale wanaolima kwenye udongo wenye upungufu wa rutuba na watakao kosa samadi na mboji.
Ntaelezea mbolea hizi,
Ngombe na Mbuzi zinakaa muda mrefu shambani na kufanya udongo kua na rutuba kwa muda mrefu ukilinganisha na aina nyingine ya mbolea(hizi ziko katika mtindo (form) ya inogarnic Nitrogen na organic Nitrogen ambayo ipo kwenye mkojo na urea ambayo ipo kwenye mavi,hii huitaji kubadilika kua Nitrogen(N) alafu bacteria na enzymes watazibadili kwenye udongo ili iwe Nitrate NO3(mfumo ambao mmea utaichukua kwa haraka),kwa hiyo ni slow acting/release,ndo mana unashauriwa uweke week 2 ama zaidi kabla ya kuhamisha miche yako,
Mbolea ya kuku hii ina Nitrate tayari nyingi kwa hiyo ni nzuri kwa kipimo sa hihi kwa mahitaji ya haraka(fast release/acting) na haikai shambani muda ikishachukuliwa na mmea basi zoezi limeishia hapo,zingatia kwamba ukizidisha mbolea hii itaunguza mmea.

Note: Zao hili linaweza kuota bila kuweka chochote,hapa ina maanisha udongo ilipo ota umejitosheleza,

Hapa tunaongelea kwa wale wanaotaka kulima kibiashara wakilenga mazao mengi na ya uhakika.

Tuendelee

Mbolea za viwandani,
Mmea wa nyanya chungu(ngogwe) huhitaji mbolea ya Nitrojeni na Phosphorus kwa kukua vizuri na imara na Pottasium kwa matunda (Nitrogen inaleta makuzi,majani,shina na kusaidia photosynthesis-upumuaji,lakini isiwekwe kwa wingi sana, nitrojeni ikiwa nyingi na ikiwekwa mara kwa mara huleta majani mengi na kufanya mmea kua na msitu,hii hupunguza mazao sana,pia mmea huhitaji phosporus kwa wingi katika hatua hizi za awali baada ya kuhamisha miche ili kuleta mizizi bora na mingi pia imara ambayo huwezesha mmea kuchukua chakula katika udongo ikiwemo hiyo nitrogen,pia husaidia kinga ya mmea kwa magonjwa,
Kwa hizi za viwandani inashauriwa kuweka mbolea pembeni ya mmea(side dressing) baada ya week 2(hapa mmea unakua umeshajishika chini vizuri na kuanza kutoa majani mengine mapya) weka mbolea shambani zenye uwiano sawa wa NPK isiyo ya kiwango cha juu mfano (10:10:10, 12:12:12) hata zenye kupungua kidogo na kuongezeka kidogo hazina tatizo mfano 11:14:10(kama zipo)
Utarudia mbolea wakati maua yana anza,utaweka mbolea zenye nitrojeni ya chini zaidi na Potassium ya juu kidogo mfano 5:10:20 etc,Calcium(CaO na Magnesium(MgO),zikiwa na O maanza yake ni oxides(kwamba zinayeyuka kwenye maji -soluble) zitahitajika,Calcium Nitrates(Ca(NO3)2) kama CAN ina Nitrogen 26-27%,Nitrabor,CALCINIT etc zenye N 13-15.5% na 25-27% CaO hizi nusu ya nitrogen ni ni slow release na nusu ni fast acting (kuna mbolea nzuri zenye michanganyiko inayofaa direct kama Minjingu Pamba(white diamond hii ina N,P,K,S,Mg,CaO),kuna Mbolea za kampuni OCP,Kuna mbolea za Yara(Nitrabor) hii ina 15.4 N(nusu N na nusu NO3-inayochukuliwa haraka na mmea) pia ina Boron kidogo,na aina zingine zenye majina tofauti tofauti. Tafadhali zingatia mbolea ina virutubisho(nutrients) gani na sio jina tuu ili mradi,
Utaendelea na mbolea za maji (Foliar) zenye Potassium kubwa(K 35-60%) kila baada ya siku 10-14 kama Multi K,Master Fruiter etc,alafu utarudia tena mbole za punje,NPK(Nitrogen ya wastani,phosporus ya chini kabisa na potassium ya juu zaid ya zote)kila baada ya siku 21-30
Utazingatia muonekano wa mmea kwa macho ili uweke mbolea sa hihi na kiwango sa hii hii,utakua pia unapiga mbolea za maji za kwenye majani(foliar),wakati huu phosporus haihitajiki kwa wingi kwa kua mizizi ishajishika vizuri katika hatua ya awali.

Kuna booster nyingi na nzuri,zenye virutubisho vingi vikuu(NPK),vya kati(Ca,Mg,S) na vya chini(Fe,Mn,Cu,Zn,B,Mo),pendelea zile zenye virutubisho vya kawaida na vya ziada pamoja,kuna zingine zina pendelewa sana lakini zinaivisha matunda haraka(mfano Vigmax) iwekwe mwanzoni wakati wa maua na sio wakati wa mavuno,kuna mbolea kama Max Green na zingine zipo vizuri(tukichambua zina virutubisho gani tutampoteza kabisa mkulima).

Mbolea za chenga chenga hizo nlizotaja (NPK,CaO,MgO,S) ni muhimu sana,alafu unaweza endelea na mbolea za juu za majani(hizi zote zinafanya kazi haraka sana kwa maana ya matokeo yake),zingatia maelezo ya kila mbolea kwenye vibandiko vyake.

Napokea maswali kwa hapa nlipo elezea,maswali yaliyoshiba na yenye uelewa ndani yake,sio maswali yasio na kichwa wala mguu i.e mtu anataka lima eneo flani,mkoa flani labda anauliza soko,soko kafanye research mwenyewe mazingira unayoweza yafikia.

NB:TUSIKARIRI,TUELEWE (ni nini na kwa nini)

Kwa wale wavivu wa kuuliza unaweza toa kiasi gani kwa ekari wakati hajui tofauti ya ekari na hekta wasituchoshe (~2.5 ekari ndo 1 hekta),4047m² ni ekari ama kibongo bongo 70mx70m - 4900m²,hii ntaijibu kwa mfumo unao eleweka.
Kwa upandaji wa 60cm mche hadi mche na 100cm kwa mstari hadi mstari maana yake kwa ekari moja ya 4900m² utakua na miche ~8,150-8,200
kwa mbegu hizi za kawaida za mashamba ya nje (OPV) na aina ya "DB3" unaweza toa kwa wastani wa mavuno yote kwa msimu usio pungua ukubwa wa eneo kwa square meter x 0.01,mfano eneo lako ni robo ekari,tuseme 1000m² - 1250m² utazidisha kwa 0.01 upate debe 10-12.5 wastani wa mavuno yako yoote kwa msimu wako,
Mwanzo wa mavuno utaweza kutoa debe 60 kila mchumo(itapanda mpaka debe 75 na kushuka mpaka 30 kutokana na mazingira,uangalizi,usimamizi na ulishaji wa virutubisho,wadudu na magonjwa).

Natanguliza heshima za dhati kwa mwenye uzi huu Kubota ,hizi elimu zinasaidia sana kama upako vile,tusichoke kuwa ng'amua watakao kua tayari na wenye ue

Uzi uendelee wadau,wale walio weza kulima waje na mrejesho tujifunze pamoja ili tuelimishane kwa undani na namna ya kukabiliana na changamoto zote zinazojitokeza.

Kuna kipengele cha muhimu sana hakijagusiwa na wadau, kwa asilimia kubwa,

1.Uangalizi kwenye hatua zote 4 za ukuaji
A.Ukuaji wa mwanzo kabisa -Establishment
B.Maendeleo ya ukuaji (Growth development)
C.Maua - Kutunga Matunda-Kuwa tayari kuvunwa (Flowering - Fruit set- maturity)
D.Mavuno(Harvesting)
2.Mahitaji na uwekaji wa Mbolea katika hatua zote 4
3.Muda sa hihi wa kuweka mbolea(idadi ya siku baada ya kupanda(Days After Transplanting)) na aina ya virutubisho vya mbolea vinavyohitajika na mmea huu kwa wanaopanda mashambani (N-Nitrogen,P-Phosphorus,K-Potassium,Ca-Calcium,Mg-Magnesium,S-Sulphur)
4.Magonjwa na dawa zake(viambata badaya ya majina ya dukani).

Kwa mwenye uelewa tunaomba ku share unachokijua.

Binafsi ni mkulima,na bandika hichi kidogo nlichofanikiwa kukijua katika harakati,

Ngogwe hizi tunazolima sisi kwa asilimia kubwa ni za group la "DB3" hasa hasa Gilo,
Zinahitaji udongo wenye rutuba nzuri ,mbolea za samadi na mboji (ng'ombe,mbuzi na kuku) ambazo zinakua na NPK(hapa hizi ndio Base dressing) ni sahihii sana pia mbolea za viwandani kwa namna moja ama ingine zinaweza hitajika sana hasa kwa wale wanaolima kwenye udongo wenye upungufu wa rutuba na watakao kosa samadi na mboji.
Ntaelezea mbolea hizi,
Ngombe na Mbuzi zinakaa muda mrefu shambani na kufanya udongo kua na rutuba kwa muda mrefu ukilinganisha na aina nyingine ya mbolea(hizi ziko katika mtindo (form) ya inogarnic Nitrogen na organic Nitrogen ambayo ipo kwenye mkojo na urea ambayo ipo kwenye mavi,hii huitaji kubadilika kua Nitrogen(N) alafu bacteria na enzymes watazibadili kwenye udongo ili iwe Nitrate NO3(mfumo ambao mmea utaichukua kwa haraka),kwa hiyo ni slow acting/release,ndo mana unashauriwa uweke week 2 ama zaidi kabla ya kuhamisha miche yako,
Mbolea ya kuku hii ina Nitrate tayari nyingi kwa hiyo ni nzuri kwa kipimo sa hihi kwa mahitaji ya haraka(fast release/acting) na haikai shambani muda ikishachukuliwa na mmea basi zoezi limeishia hapo,zingatia kwamba ukizidisha mbolea hii itaunguza mmea.

Note: Zao hili linaweza kuota bila kuweka chochote,hapa ina maanisha udongo ilipo ota umejitosheleza,

Hapa tunaongelea kwa wale wanaotaka kulima kibiashara wakilenga mazao mengi na ya uhakika.

Tuendelee

Mbolea za viwandani,
Mmea wa nyanya chungu(ngogwe) huhitaji mbolea ya Nitrojeni na Phosphorus kwa kukua vizuri na imara na Pottasium kwa matunda (Nitrogen inaleta makuzi,majani,shina na kusaidia photosynthesis-upumuaji,lakini isiwekwe kwa wingi sana, nitrojeni ikiwa nyingi na ikiwekwa mara kwa mara huleta majani mengi na kufanya mmea kua na msitu,hii hupunguza mazao sana,pia mmea huhitaji phosporus kwa wingi katika hatua hizi za awali baada ya kuhamisha miche ili kuleta mizizi bora na mingi pia imara ambayo huwezesha mmea kuchukua chakula katika udongo ikiwemo hiyo nitrogen,pia husaidia kinga ya mmea kwa magonjwa,
Kwa hizi za viwandani inashauriwa kuweka mbolea pembeni ya mmea(side dressing) baada ya week 2(hapa mmea unakua umeshajishika chini vizuri na kuanza kutoa majani mengine mapya) weka mbolea shambani zenye uwiano sawa wa NPK isiyo ya kiwango cha juu mfano (10:10:10, 12:12:12) hata zenye kupungua kidogo na kuongezeka kidogo hazina tatizo mfano 11:14:10(kama zipo)
Utarudia mbolea wakati maua yana anza,utaweka mbolea zenye nitrojeni ya chini zaidi na Potassium ya juu kidogo mfano 5:10:20 etc,Calcium(CaO na Magnesium(MgO),zikiwa na O maanza yake ni oxides(kwamba zinayeyuka kwenye maji -soluble) zitahitajika,Calcium Nitrates(Ca(NO3)2) kama CAN ina Nitrogen 26-27%,Nitrabor,CALCINIT etc zenye N 13-15.5% na 25-27% CaO hizi nusu ya nitrogen ni ni slow release na nusu ni fast acting (kuna mbolea nzuri zenye michanganyiko inayofaa direct kama Minjingu Pamba(white diamond hii ina N,P,K,S,Mg,CaO),kuna Mbolea za kampuni OCP,Kuna mbolea za Yara(Nitrabor) hii ina 15.4 N(nusu N na nusu NO3-inayochukuliwa haraka na mmea) pia ina Boron kidogo,na aina zingine zenye majina tofauti tofauti. Tafadhali zingatia mbolea ina virutubisho(nutrients) gani na sio jina tuu ili mradi,
Utaendelea na mbolea za maji (Foliar) zenye Potassium kubwa(K 35-60%) kila baada ya siku 10-14 kama Multi K,Master Fruiter etc,alafu utarudia tena mbole za punje,NPK(Nitrogen ya wastani,phosporus ya chini kabisa na potassium ya juu zaid ya zote)kila baada ya siku 21-30
Utazingatia muonekano wa mmea kwa macho ili uweke mbolea sa hihi na kiwango sa hii hii,utakua pia unapiga mbolea za maji za kwenye majani(foliar),wakati huu phosporus haihitajiki kwa wingi kwa kua mizizi ishajishika vizuri katika hatua ya awali.

Kuna booster nyingi na nzuri,zenye virutubisho vingi vikuu(NPK),vya kati(Ca,Mg,S) na vya chini(Fe,Mn,Cu,Zn,B,Mo),pendelea zile zenye virutubisho vya kawaida na vya ziada pamoja,kuna zingine zina pendelewa sana lakini zinaivisha matunda haraka(mfano Vigmax) iwekwe mwanzoni wakati wa maua na sio wakati wa mavuno,kuna mbolea kama Max Green na zingine zipo vizuri(tukichambua zina virutubisho gani tutampoteza kabisa mkulima).

Mbolea za chenga chenga hizo nlizotaja (NPK,CaO,MgO,S) ni muhimu sana,alafu unaweza endelea na mbolea za juu za majani(hizi zote zinafanya kazi haraka sana kwa maana ya matokeo yake),zingatia maelezo ya kila mbolea kwenye vibandiko vyake.

Napokea maswali kwa hapa nlipo elezea,maswali yaliyoshiba na yenye uelewa ndani yake,sio maswali yasio na kichwa wala mguu i.e mtu anataka lima eneo flani,mkoa flani labda anauliza soko,soko kafanye research mwenyewe mazingira unayoweza yafikia.

NB:TUSIKARIRI,TUELEWE (ni nini na kwa nini)

Kwa wale wavivu wa kuuliza unaweza toa kiasi gani kwa ekari wakati hajui tofauti ya ekari na hekta wasituchoshe (~2.5 ekari ndo 1 hekta),4047m² ni ekari ama kibongo bongo 70mx70m - 4900m²,hii ntaijibu kwa mfumo unao eleweka.
Kwa upandaji wa 60cm mche hadi mche na 100cm kwa mstari hadi mstari maana yake kwa ekari moja ya 4900m² utakua na miche ~8,150-8,200
kwa mbegu hizi za kawaida za mashamba ya nje (OPV) na aina ya "DB3" unaweza toa kwa wastani wa mavuno yote kwa msimu usio pungua ukubwa wa eneo kwa square meter x 0.01,mfano eneo lako ni robo ekari,tuseme 1000m² - 1250m² utazidisha kwa 0.01 upate debe 10-12.5 wastani wa mavuno yako yoote kwa msimu wako,
Mwanzo wa mavuno utaweza kutoa debe 60 kila mchumo(itapanda mpaka debe 75 na kushuka mpaka 30 kutokana na mazingira,uangalizi,usimamizi na ulishaji wa virutubisho,wadudu na magonjwa).

Natanguliza heshima za dhati kwa mwenye uzi huu Kubota ,hizi elimu zinasaidia sana kama upako vile,tusichoke kuwa ng'amua watakao kua tayari na wenye uelewa.

Nawasilisha
Barikiwa sana
 
Mkuu ni foliar fertilizer gani nzuri kwa matunda kutokana na uzoefu wako
Hebu chambua hapo juu kwa nlichokieleza upate uelewa mzuri then ndo tuje kwenye majina ya Foliar(zipo nyingi sana),kuna kipengele nime elezea cha kuzingatia..yaani uletewe foliar 10 tafauti basi kwa uelewa wa hapo juu utaweza chagua nzuri kuliko zote(zingatia zenye virutubishe vya ziada (Trace Elements T.E),same price with extra nutrients.
 
Back
Top Bottom