Mr the dragon
JF-Expert Member
- Apr 14, 2017
- 1,937
- 3,718
Guess what!!!!!!!!!!!!!!?
Nimemiss zile siku naamka asubuhi natoka nje naanza kukamua maziwa then mida ya saa mbili napata ugali mkubwa na maziwa yaliyopekechwa "masuke" kwa kisukuma.Kisha naelekea huko milimani kuchunga ng'ombe mpaka jioni ndio unarudisha mifugo nyumbani.
Huko malishoni Ni mwendo wa kuwinda sungura ukiwa na mbwa Kama ni kipindi Cha mvua.Au ndege aina ya "ndingwa" ukitumia rungu na manati.Usiombe ujisahau ng'ombe wakavamia shamba la mtu, baadae ukakutwa na mwenye shamba bakora utakazo chezea usiombe.
Namaanisha yale maisha ya kwenda shule siku mbili kwa wiki nyingine ni shambani na kuchunga.Shule iko umbali wa zaidi kilometre kumi lakini tunaenda kwa mguu.Kabla hujaenda shule unatafuta kiporo cha ugali na mgagani unakigonga then ndio unaenda shule.
Mliozaliwa Kariakoo and the likes I know you can't come across to imagine this kind of life.But we countrysiders we lived those kind of life on nothern Simiyu.
Kipindi hicho kila akifa mtu sisi tunaamini amerogwa, haiwezekani kufa bila kurogwa.Kiswahili tumekijua shuleni, sisi darasani ulikuwa mwendo wa "nyanoko, "lushindo loko".Sekondari huwa wanavalishwa madude ya "Swahili speakers",Lakini sisi tulivalishwa pembe la ng'ombe kwa "Sukuma speakers" sijui kosa letu ni nini wakati kilugha ndio tulikimudu vyema.
Maisha ya disko ikitokea kuna sehemu mtu kaoa au kaolewa.Nyimbo zinazopigwa hutamsikia Michael Jackson, P square au Juma nature.Ni mwendo wa ng'wana Kanundo,Saida Karoli,Budagala na Maringita.
It was very funny days I missed as a legend, though nisingependa mwanangu ayapitie.The rest is history
Nimemiss zile siku naamka asubuhi natoka nje naanza kukamua maziwa then mida ya saa mbili napata ugali mkubwa na maziwa yaliyopekechwa "masuke" kwa kisukuma.Kisha naelekea huko milimani kuchunga ng'ombe mpaka jioni ndio unarudisha mifugo nyumbani.
Huko malishoni Ni mwendo wa kuwinda sungura ukiwa na mbwa Kama ni kipindi Cha mvua.Au ndege aina ya "ndingwa" ukitumia rungu na manati.Usiombe ujisahau ng'ombe wakavamia shamba la mtu, baadae ukakutwa na mwenye shamba bakora utakazo chezea usiombe.
Namaanisha yale maisha ya kwenda shule siku mbili kwa wiki nyingine ni shambani na kuchunga.Shule iko umbali wa zaidi kilometre kumi lakini tunaenda kwa mguu.Kabla hujaenda shule unatafuta kiporo cha ugali na mgagani unakigonga then ndio unaenda shule.
Mliozaliwa Kariakoo and the likes I know you can't come across to imagine this kind of life.But we countrysiders we lived those kind of life on nothern Simiyu.
Kipindi hicho kila akifa mtu sisi tunaamini amerogwa, haiwezekani kufa bila kurogwa.Kiswahili tumekijua shuleni, sisi darasani ulikuwa mwendo wa "nyanoko, "lushindo loko".Sekondari huwa wanavalishwa madude ya "Swahili speakers",Lakini sisi tulivalishwa pembe la ng'ombe kwa "Sukuma speakers" sijui kosa letu ni nini wakati kilugha ndio tulikimudu vyema.
Maisha ya disko ikitokea kuna sehemu mtu kaoa au kaolewa.Nyimbo zinazopigwa hutamsikia Michael Jackson, P square au Juma nature.Ni mwendo wa ng'wana Kanundo,Saida Karoli,Budagala na Maringita.
It was very funny days I missed as a legend, though nisingependa mwanangu ayapitie.The rest is history