Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mimi hata bechi asingekaaNilimweka benchi kwenye kikosi changu, mishabiki ya Utopolo ilinishambulia mno.
Leo hii wameufyata yaani...Tunenda na Mpole.
Umeona eee hahhhhhahaKuna mod ni yanga au mshamba humu JF
NimeshangaaaImekuwaje.. Uzi wa Kumtetea mwaka mzima wameufyeka?!
Kinyume chake, line 2 akaamua kumnyima goli lake la wazi kabisa kwa kumhukumu kuotea! Na marudio yakaonesha wazi Mfungaji (Mayele) hata hakuwa katika nafasi ya kuotea!Itatafutwa penati ya mchongo hapo kilazima mpaka mchizi atie kamba
Mikiaa, 😂😂😂😂😂😂😇Wanajulikana kuwa ni watalaamu wa kusakata Kabumbu Nchini Tanzania lililothibitishwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika CAF, Mnyama Mkali Mwituni Simba SC, leo Juni 29, 2022 yupo ugenini kwenye Dimba la Majimaji kupambana na Mbeya Kwanza FC katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ambapo leo inafikia kikomo kwa Timu zote kujitupa kwenye viwanja tofauti kucheza michezo ya mwisho.
Matokeo ya leo kati ya Mbeya Kwanza FC dhidi ya Simba SC hayawezi kuathiri kwa vyovyote msimamo wa Ligi Kuu, ambapo Mbeya Kwanza FC tayari ameshashuka daraja rasmi huku Simba SC akijihakikishia nafasi ya pili
Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10:00 Jioni.. Usikose Ukaambiwa
Kulipewa Mwana...Kulitaka Mwana
View attachment 2276502
======
05' Mpira umeanza Uwanja wa Majimaji kwa kila timu kucheza mpira nzuri.
10' Hakuna timu imeona lango la wenzake, huku Simba wakimiliki mpira, lakini Mbeya Kwanza wanatibua mipango yote ya Simba SC
15' Kennedy anamrudishia golikipa Beno, lakini anaukosa na mpira unaambaa ambaa unatoka nje, ilikuwa nafasi nzuri kwa Mbeya Kwanza kufunga
Free Kick kuelekea Mbeya Kwanza FC, inapigwa kulee lakini mpira unaokolewa na mabeki wa Kwanza FC
20' Beno anafanya balaa anaokoa hatari ambayo almanusura Mbeya Kwanza wapate bao, mpira imetoka nje na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao.
25' Kassim anakosa nafasi nzuri ya kufunga ilikuwa Shambulizi kali kuelekea Mbeya City, mpira wake umepaa juu ya lango.
30' Jaribio la maana sana, kwa Mbeya Kwanza lakini mpira wa Mpepo unagonga mwamba wa juu na kurudi Uwanjani.
Simba wanajibu Counter mbele kuleee lakini Kibu anakosa nafasi nzuri ya kufunga kwa mpira kuokolewa, ilikuwa nafasi murua hii.
35' Mhilu anapiga pasi hafifu kwa mlengwa, ambayo inakuwa kama chakula kwa mabeki wa Kwanza FC kuokoa.
42' Simba wanashindwa kutumia nafasi nzuri ya kufunga kwa mpira uliopigwa na Kibu kuambaa ambaa eneo la hatari na kuokolewa na beki wa Kwanza FC.
45+1' Kuelekea kuwa mapumziko ambapo hakuna timu imeona lango la wenzake.
Naaam mpira ni mapumziko | Mbeya Kwanza FC 0-0 Simba SC
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Majimaji, huku mapema tu Simba wakikosa kutumia nafasi ya kufunga huku wakipata Kona mbili ambazo hazikuzaa bao.
53' Nyoni anapiga free kick kuelekea Kwanza FC, lakini golikipa anatokea na kudaka bila wasiwasi.
59' Jimmy anakosa nafasi nzuri ya kufunga, baada kupiga shuti dhaifu na mpira kuokolewa.
Almanusura Kwanza FC waandike bao, kama angekuwa makini mchezaji Richard angefunga
65' Simba wanapata Free Kick eneo nzuri na wanashindwa kutumia nafasi hiyo.
66' Kwanza FC wanakosa nafasi tena baada ya mchezaji kuwa 50+50 na golikipa Beno, lakini mpira unaokolewa na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao.
75' Timu zote zinacheza kwa kushambulia kwa zamu huku mabeki wakiwa imara kwa pande zote mbili
Kibu yupo chini akipatiwa matibabu baada ya kupata rabsha, ameinuka mpira unaendelea
83' Ametoka Mhilu na nafasi yake imechukuliwa na Bocco.
88' Kwanza FC wanashindwa kutumia nafasi ya kufunga, ilikuwa Shambulizi kali kuelekea lango Simba
90+2' Kuelekea kumalizika kwa mchezo, milango bado ni migumu hakuna mbabe.
Free Kick anapiga Chuku, Ooooh mpira unaokolewa na Gadiel, ilikuwa nafasi murua kujipatia bao dakika hizi za mwisho.
Naaam mpira umekwishaaaaaa ambapo Timu zote zimetoka sare, zimegawana alama.
FT: Mbeya Kwanza FC 0-0 Simba SC
...... Ghazwat...
WameufyekaImekuwaje.. Uzi wa Kumtetea mwaka mzima wameufyeka?!
Ona sasa! Mnashindwa hata kuhonga ili kuifunga timu ambayo haina cha kupoteza! Yaani ilishajishukia daraja kitambo!Hongera mpole
Sema Hongera Mpole wa Simba.Hongera mpole
SafiiFT: Yanga SC 1-0 Mtibwa Sugar
Mtibwa Sugar itacheza mechi ya mtoano na Tanzania Prisons kuwania kubaki Ligi Kuu
Mshamba kweli ,uzi wa kutetema mwaka mzima bila kiatu una tatizo gani ,heri angeunganisha yaani kaufyekaUmeona eee hahhhhhaha
Makosa ya kibinadamuKinyume chake, line 2 akaamua kumnyima goli lake la wazi kabisa kwa kumhukumu kuotea! Na marudio yakaonesha wazi Mfungaji (Mayele) hata hakuwa katika nafasi ya kuotea!
Bila shaka Waamuzi wanatakiwa kuwa fair bila shaka. Uzembe na kuendekeza ushabiki maandazi, kunawashushia hadhi ndani na hata nje ya mipaka yetu.
Hatumtegemei mfungaji mmoja!!Leo Mayele amewajambisha Utopolo
Hili jambo halikubaliki kwenye soka [emoji16]