Ligi Kuu Bara | Mbeya Kwanza FC Vs Simba SC | Uwanja wa Majimaji | Juni 29, 2022

Ligi Kuu Bara | Mbeya Kwanza FC Vs Simba SC | Uwanja wa Majimaji | Juni 29, 2022

Itatafutwa penati ya mchongo hapo kilazima mpaka mchizi atie kamba
Kinyume chake, line 2 akaamua kumnyima goli lake la wazi kabisa kwa kumhukumu kuotea! Na marudio yakaonesha wazi Mfungaji (Mayele) hata hakuwa katika nafasi ya kuotea!

Bila shaka Waamuzi wanatakiwa kuwa fair bila shaka. Uzembe na kuendekeza ushabiki maandazi, kunawashushia hadhi ndani na hata nje ya mipaka yetu.
 
Wanajulikana kuwa ni watalaamu wa kusakata Kabumbu Nchini Tanzania lililothibitishwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika CAF, Mnyama Mkali Mwituni Simba SC, leo Juni 29, 2022 yupo ugenini kwenye Dimba la Majimaji kupambana na Mbeya Kwanza FC katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ambapo leo inafikia kikomo kwa Timu zote kujitupa kwenye viwanja tofauti kucheza michezo ya mwisho.

Matokeo ya leo kati ya Mbeya Kwanza FC dhidi ya Simba SC hayawezi kuathiri kwa vyovyote msimamo wa Ligi Kuu, ambapo Mbeya Kwanza FC tayari ameshashuka daraja rasmi huku Simba SC akijihakikishia nafasi ya pili

Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10:00 Jioni.. Usikose Ukaambiwa

Kulipewa Mwana...Kulitaka Mwana

View attachment 2276502

======

05' Mpira umeanza Uwanja wa Majimaji kwa kila timu kucheza mpira nzuri.

10' Hakuna timu imeona lango la wenzake, huku Simba wakimiliki mpira, lakini Mbeya Kwanza wanatibua mipango yote ya Simba SC

15' Kennedy anamrudishia golikipa Beno, lakini anaukosa na mpira unaambaa ambaa unatoka nje, ilikuwa nafasi nzuri kwa Mbeya Kwanza kufunga

Free Kick kuelekea Mbeya Kwanza FC, inapigwa kulee lakini mpira unaokolewa na mabeki wa Kwanza FC

20' Beno anafanya balaa anaokoa hatari ambayo almanusura Mbeya Kwanza wapate bao, mpira imetoka nje na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao.

25' Kassim anakosa nafasi nzuri ya kufunga ilikuwa Shambulizi kali kuelekea Mbeya City, mpira wake umepaa juu ya lango.

30' Jaribio la maana sana, kwa Mbeya Kwanza lakini mpira wa Mpepo unagonga mwamba wa juu na kurudi Uwanjani.

Simba wanajibu Counter mbele kuleee lakini Kibu anakosa nafasi nzuri ya kufunga kwa mpira kuokolewa, ilikuwa nafasi murua hii.

35' Mhilu anapiga pasi hafifu kwa mlengwa, ambayo inakuwa kama chakula kwa mabeki wa Kwanza FC kuokoa.

42' Simba wanashindwa kutumia nafasi nzuri ya kufunga kwa mpira uliopigwa na Kibu kuambaa ambaa eneo la hatari na kuokolewa na beki wa Kwanza FC.

45+1' Kuelekea kuwa mapumziko ambapo hakuna timu imeona lango la wenzake.

Naaam mpira ni mapumziko | Mbeya Kwanza FC 0-0 Simba SC

Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Majimaji, huku mapema tu Simba wakikosa kutumia nafasi ya kufunga huku wakipata Kona mbili ambazo hazikuzaa bao.

53' Nyoni anapiga free kick kuelekea Kwanza FC, lakini golikipa anatokea na kudaka bila wasiwasi.

59' Jimmy anakosa nafasi nzuri ya kufunga, baada kupiga shuti dhaifu na mpira kuokolewa.

Almanusura Kwanza FC waandike bao, kama angekuwa makini mchezaji Richard angefunga

65' Simba wanapata Free Kick eneo nzuri na wanashindwa kutumia nafasi hiyo.

66' Kwanza FC wanakosa nafasi tena baada ya mchezaji kuwa 50+50 na golikipa Beno, lakini mpira unaokolewa na kuwa Kona ambayo haikuzaa bao.

75' Timu zote zinacheza kwa kushambulia kwa zamu huku mabeki wakiwa imara kwa pande zote mbili

Kibu yupo chini akipatiwa matibabu baada ya kupata rabsha, ameinuka mpira unaendelea

83' Ametoka Mhilu na nafasi yake imechukuliwa na Bocco.

88' Kwanza FC wanashindwa kutumia nafasi ya kufunga, ilikuwa Shambulizi kali kuelekea lango Simba

90+2' Kuelekea kumalizika kwa mchezo, milango bado ni migumu hakuna mbabe.

Free Kick anapiga Chuku, Ooooh mpira unaokolewa na Gadiel, ilikuwa nafasi murua kujipatia bao dakika hizi za mwisho.

Naaam mpira umekwishaaaaaa ambapo Timu zote zimetoka sare, zimegawana alama.

FT: Mbeya Kwanza FC 0-0 Simba SC

...... Ghazwat...
Mikiaa, 😂😂😂😂😂😂😇
 
Hongera mpole
Ona sasa! Mnashindwa hata kuhonga ili kuifunga timu ambayo haina cha kupoteza! Yaani ilishajishukia daraja kitambo!

Hivi tajiri yenu Moo ana hela za majini, au!!
Mbona mwenzake GSM anatembeza tu bahasha, timu inachukua mpaka ubingwa! Yaani anatembeza bahasha mpaka kwenye timu yenu! Lakini yeye yupo yupo tu.
 
Kinyume chake, line 2 akaamua kumnyima goli lake la wazi kabisa kwa kumhukumu kuotea! Na marudio yakaonesha wazi Mfungaji (Mayele) hata hakuwa katika nafasi ya kuotea!

Bila shaka Waamuzi wanatakiwa kuwa fair bila shaka. Uzembe na kuendekeza ushabiki maandazi, kunawashushia hadhi ndani na hata nje ya mipaka yetu.
Makosa ya kibinadamu

Nikama tu ioe ambayo mayele aliunawa mpira halafu penati ikaenda jangwani

Namna ambavyo tulitafsiri hicho kitendo ilifaa tutumie busara hizo hizo na kwenye hili lililofanyika leo
 
Back
Top Bottom