Dk 60,Yanga wanapata kona.
Dk 57, Yanga wanafanya mabadiliko, anaingiaGeofrey Mwashiuya, anatoka Deus Kaseke ambaye alikuwa upande wa winga wa kushoto.
Dk 55, Kangwa wa Azam anapata nafasi ya kupiga shuti kali langoni mwa Yanga lakini Dida analidaka.
Dk 53, Azam wanafanya shambulizi lingine lakini kipa wa Yanga, Deo Munis 'Dida' anaokoa.
Dk 50, Azam wanapiga pasi nzuri kuanzia katikati ya uwanja, wanalifikia lango la Yanga lakini mshambuliaji Thomas anashindwa kutumia nafasi anayopata, mabeki wa Yanga wanaokoa.
Dk 47, Mchezo umeanza kwa kasi ndogo, bado timu zote zinaonekana kusomana.
Kipindi cha pili kimeanza.