Ligi ya Mabingwa Afrika | Uwanja wa Taifa, Dar: Simba SC 1-1 UD Songo. Simba yatolewa kwa faida ya goli la ugenini iliyopata UD Songo

Ligi ya Mabingwa Afrika | Uwanja wa Taifa, Dar: Simba SC 1-1 UD Songo. Simba yatolewa kwa faida ya goli la ugenini iliyopata UD Songo

We are Simba...This is Simba...miaka kumi mfululizo sisi ndio tutakuwa mabingwa....back to back..IGA UFE ...hii ni level nyingine...sisi ndio timu bora tukifuatiwa na Azam..nawachukia mno gongowazi..Kambi yetu ni South Africa na siyo Morogoro ambako wachezaji kambini wanagombea chips na mihogo...tutaanza kuokota mataji kama ngao ya jamii...target yetu mwaka huu ni kufika nusu fainali kwenye michuano ya CAF..
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Simba Sports Club wekundu wa msimbazi wametupwa nje ya klabu bingwa barani Afrika na klabu ya UD SONGO kutoka nchini Msumbiji.

Klabu hiyo kutoka kati kati mwa jiji la Dar Es Salaam iliacha gumzo kubwa kipindi cha dirisha la usajili ikichukua wachezaji kutoka Brazili, Sudani na Congo.

Lakini mungu si Athumani Simba imetupwa nje mapema tu, je unadhani klabu hiyo ilifanya maamuzi sahihi ya usajili au ilikuwa ikikurupuka kufanya usajili kila ilipotimu saa saba mchana ??!
 
Kwa kweli mimi kama Simba Damu tangia babu wa mama na babangu, nashukuru kwa kweli manake tumekufa kishujaa kuliko tungejifanya ujuaji halafu tukaenda kula gwala gwala mwisho wa safari. Sisi ndio Simba bhana! Tuna pua kali za kunusa hatari iliyo mbeleni kuliko ilivyo kawaida!! Mwaka huu CAF wamtafute mwingine wa kwenda kula hamsa hamsa, lakini sio sisi shubamiti zao!!!

Kwanza tulishanusa nia ovu ya CAF ya kutaka tumpandishe pandishe ndege Kibabu chetu Kagere ili achoke mapema wakatu keshajichokeail!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]my ribs
 
Si unaona yaliyotokea Shadeeya? Tatizo Wabongo tumezoe kudanganyana na kusifiana uongo matokeo yake tunajihisi tuna uwezo kuwazidi wengine kumbe tunatakiwa kuongeza jitihada
Na tatizo watu wanapenda zile kauli sukari tu Ses yaani ukiwa mkweli wanakuona mamluki.
 
Back
Top Bottom