Ligi yetu inazidi kupungua ubora kila mwaka. Timu dhaifu, hakuna ushindani

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Ni wazi sasa ligi yetu inazidi kukosa ubora, timu nyingi ukiacha Simba na Yanga, ni zinazidi kuwa dhaifu, angalia tu zinavyocheza mechi za ndani na za kimataifa.

Azam imetolewa na timu kibonde kutoka ligi dhaifu ya Ethiopia, Singida ambayo inaonekana ni bora imefungwa na JKU ya Zanzibar.

Watu wasijione wanapiga vibonde goli nyingi wakajisifu, kimataifa wanaweza kuishia tena raundi ya pili
 
Kimataifa ndiyo kipimo sahihi cha simba na yanga
 
Acheni wivu, mimi ni Mnyama nimevutiwa sana na juhudi wanazoonesha Yanga.

Tangu huko nyuma hatujawahi kuwa na msaada kimataifa wa timu kama Azam n.k.

Hongereni Yanga boli linatembea.

Simba tunashinda ila washabiki hatufurahii kiwango cha timu.
Ligi kila siku inaimarika ila Yanga inaimarika zaidi
 
Kameze wembe ili upunguze maumivu maana maumivu uliyonayo sidhani kama utapata usingizi leo
 
Nakuunga mkono, bado tuna safari ndefu
 
Iwe mikia ndio wamempiga 5. Ingekuwa ligi bora na timu iliyopigwa 5 imezidiwa tu mbinu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…