LilOmmy wa Times fm muda utazungumza

mayowela

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2014
Posts
2,125
Reaction score
1,753
Jina la kitambulisho Ommary Rajabu Saleh Tambwe al maarufu Lilommy jamaa yuko kwenye tasnia kwa muda tangu enzi yuko Voice of Tabora (V.O.T) fm, Kiufupi anakipaji cha kutangaza,production,Graphix design, kuchana (kurap) kiufupi kajaaliwa

Nakumbuka kipindi yuko Tabora alikuwa ni Dj baadae akaanza kutangaza kipindi cha mchana cha Bongo Rhymes then akakibadili jina na kukiita Extra ordinary pia alikuwa na studio kama sikosei ilikuwa inaitwa Lunatic production.

Miaka ya 2008-2009 alipata ubalozi kutoka mtandao wa simu wa Zantel na hapo ndipo mambo yalianza kubadilika, kama masihala akaibuka mjini na milango ikafunguka zaidi pale Times fm, na kwa sasa ni moja kati ya watangazaji wa moto sana anazidi hadi wale walioko kwenye media kubwa ambao wengi wao majina yana wabeba na sio kipaji halisi.

Wengi wanaweza wakawa wamekuona na wakahisi sehemu ulipo sio sahihi, mimi nasema Times ni sehemu sahihi kwa sasa sidhani kama una nafasi ya utangazaji tu pale naamini una nafasi ingine pia ki utawala, Endelea kujenga jina na ipo siku wasio kuelewa watakuelewa ikiwa muda umewatupa mkono.

Ongeza chochote kwa Lilommy, wakuzua aka wamacausative aka ORST the king of Saturday show The PlayList
 
Jamaa yuko poa , interview zake anazofanya na wasanii anakuwa amemfanyia msanii research ya kutosha kwanza na kumuuliza maswali watu wanayotaka kusikia yakiulizwa.. ni mtu wa Tabora kumbe?
Sikiliza interview yake na Fid Q hapo,
 
Jamaa yuko poa sanaas

Sent from my TECNO-Y3+ using JamiiForums mobile app
 
Jamaa yuko poa , interview zake anazofanya na wasanii anakuwa amemfanyia msanii research ya kutosha kwanza na kumuuliza maswali watu wanayotaka kusikia yakiulizwa.. ni mtu wa Tabora kumbe?
Yaah wa Tabora
 
M huwa naikumbuka show aliyokuwa anaifanya pale VOT FM Extra ordinary show around 2008
 
The guy knows what he is doing and he's multi talented,asilewe Tu sifa
 
Ni kweli jamaa yupo vizuri sana

Sent from my TECNO-Y3+ using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…