DOKEZO Limeshafika ghorofa ya 13 na linaendelea, lakini nguzo kama njiti za kiberiti

DOKEZO Limeshafika ghorofa ya 13 na linaendelea, lakini nguzo kama njiti za kiberiti

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
38,920
Reaction score
44,970
Picha hapo chini inajieleza, jengo lipo Kariakoo, limefika ghorofa kama 13 hivi na bado naona kuna nondo zimetokeza hapo juu kuashiria kwamba floor bado zinaendelea juu.

Sasa unaweza kuta michoro ya structural engineer imespecify mwisho ghorafa 10, lakini mwenye jengo anaamua tu kuongeza zaidi kwa tamaa ya pesa. Maana zile nguzo ni nyembamba sana na jengo lenyewe ni jembamba kama mlingoti.

Pia wanasema jengo moja hadi jingine inabidi paachwe nafasi walau ya kupumulia, sasa hilo jengo ni kama linataka kugusa hili lingine, kwa ukaribu huu, hata moja moto ukiwaka lazima la pili lishike moto.

Mamlaka zinazohusika zifanye ukaguzi ili lisije likaleta madhara na mwishowe tukapeperusha bendera nusu mlingoti.

Screenshot_2019-08-30-11-38-45.png
 
Mkuu, fanya issue zako, mambo ya watu achana nayo, unaweza ukawa na very limited facts kwenye hilo jambo
Na ndio maana nimetoa angalizo, maana kuna jengo lilishawahi kuanguka kule posta na watu walikufa, na wahusika waliwekwa ndani na hatimae wakaachiwa, lakini waliopoteza maisha ndio imetoka,sasa kama naona kitu ambacho hata kwa macho tu kinatia shaka inabidi wahusika wakajiridhishe.
 
Na ndio maana nimetoa angalizo, maana kuna jengo lilishawahi kuanguka kule posta na watu walikufa, na wahusika waliwekwa ndani na hatimae wakaachiwa, lakini waliopoteza maisha ndio imetoka,sasa kama naona kitu ambacho hata kwa macho tu kinatia shaka inabidi wahusika wakajiridhishe.
Mkuu, mambo ya ujenzi hayapimwi kwa macho, embu jiongeze kidogo.
 
Mkuu, fanya issue zako, mambo ya watu achana nayo, unaweza ukawa na very limited facts kwenye hilo jambo
Umejuaje kama hiki alichokileta sio moja ya issue zake? Maybe hizi ndio kazi zake kwa hiyo usimjudge sana.

BTW kwa huo muonekano wa hizo nguzo ni kweli jengo linatia shaka uimara wake.

Cc Unforgetable
 
Haya mambo hayafanywi kienyeji enyeji tu. Lazima mtu awe na permit na authorization kutoka kwa mamlaka husika; na engineer anakuwa ame approve michoro ya hilo jengo kuwa ujenzi huo ni salama. Kama hujui kitu unauliza ufahamishwe...

Mchana mwema!
 
Picha hapo chini inajieleza, jengo lipo Kariakoo, limefika ghorofa kama 13 hivi na bado naona kuna nondo zimetokeza hapo juu kuashiria kwamba floor bado zinaendelea juu.

Sasa unaweza kuta michoro ya structural engineer imespecify mwisho ghorafa 10, lakini mwenye jengo anaamua tu kuongeza zaidi kwa tamaa ya pesa. Maana zile nguzo ni nyembamba sana na jengo lenyewe ni jembamba kama mlingoti.

Mamlaka zinazohusika zifanye ukaguzi ili lisije likaleta madhara na mwishowe tukapeperusha bendera nusu mlingoti.

View attachment 1193373
Mmh ila kweli hizo nguzo ni nyembamba kweli wahusika wanatakiwa kupita kufanya ukaguzi.
 
Unaweza ukawa na hoja lakini Strength haipimwi kwa unene Wa beam! ingefaa ukaweka structure ikoje ili tuichambue!

Note: Jengo linaweza kuwa na column/beam nyembamba lakini zikawa ni nyingi ili kufanya load distribution kuwa safe!.

Kwahiyo ipendeze sasa kuangalia structure kwanza kabla ya kulaumu
 
Back
Top Bottom