Lindi: 13 wafariki katika ajali kati ya Coaster na Lori

Lindi: 13 wafariki katika ajali kati ya Coaster na Lori

Duh yaani tunazika watu wengi sana kwa ajali ya kugongana uso kwa uso na nyingi zikihusisha maroli lakini nobody cares government yenyewe ni kutoa rambirambi tu
 
Sio kwa ubaya ila nauliza dereva wa hiace kaponaje hapo ilihali ilikuwa ni head to head collission? Naona hapo mwisho wanasema amekamatwa kwa ajili ya mahojiano. HOW?
Hapo mbona mahesabu tu mshikaji. Yaani ile unaona dude limeegemea kwenu we unaenda upande wa lenyewe. Kitambo zipigane busu we uko zako mtaroni unazicheki tu kama mechi ya simba na yanga yani
 
Umeelewa lakini mantiki ya point yangu ya kwenye comment hiyo uliyonukuu??
Hata kama dereva angekuwa kipofu, endapo kama barabara hiyo ingejengwa kwa kuzingatia hayo masuala niliyoeleza wala ajali hiyo isingeweza kutokea, ingezuilika.

Tuta, Ukingo au gingi kubwa kati kati ya barabara vingeweza kuzuia magari yanayopishana kuweza kukaribiana na kugongana uso kwa uso. Tuta au gingi lingekuwa kizuizi 'barrier' cha kulizuia gari la upande mmoja wa barabara kuvuka na kwenda kulivamia gari linalopita upande wa pili wa barabara hivyo kuzuia ajali kutokea.
Hilo tuta halitoruhusu gari la nyuma kulipita gari la mbele over take. Hiyo hali inatakiwa tu pale penye njia nne na kuendelea
 
Ukichunguza kwa umakini Sana utagundua kwamba Kiini hasa cha mkasa huu ni uduni wa miundombinu ya barabara hapa Tanzania. Barabara ni nyembamba sana, 'lanes' za kupita magari hazijatenganishwa kwa matuta, kingo au magingi
Njia za London ni nyembamba kuliko hizi zetu na bado ni sehem salama sana kuendesha gari ,ukienda hapo Comoro ndio kabisa sio barabara ni njia na bado wako salama
Chanzo kikuu Cha ajali ni uzembe wa drivers kwa tz
Kwa miundo mbinu iliyopo drivers wakiamua pawe na zero accident basi itawezekana
 

Watu 13 wamefariki dunia na wengine sita kujeruhiwa kufuatia ajali ya basi dogo la abiria aina ya Toyota Hiace lililokuwa likitokea Somanga kuelekea Kilwa Mkoani Lindi kugongana uso kwa uso na lori la mafuta leo April 22,2024 katika Kijiji cha Somanga.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi, John Imori amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo katika barabara kuu ya Lindi - Kibiti ambapo amesema chanzo cha ajali ni Dereva wa lori kuhama upande wake na kuingia upande wa Hiace na kugongana uso kwa uso.

Majeruhi sita wanapatiwa matibabu katika Kituo cha Afya cha Tingi huku miili ya waliofariki ikihifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi.

Kamanda Imori amesema Mashuhuda wamesema Dereva wa lori amelewa na walimuona akiwa anayumba na kumgonga Mwendesha baiskeli kabla ya ajali hyo ya gari, hivyo atafanyiwa vipimo na ikibainika alikunywa pombe kupita kiasi atachukuliwa hatua “Dereva wa lori na wa Hiace wote tumewakamata kwa mahojiano”
Mungu awalaze mahala pema wanapostahili
 
Back
Top Bottom