Lini mara ya mwisho kumtamkia mzazi/mlezi wako nakupenda?

Lini mara ya mwisho kumtamkia mzazi/mlezi wako nakupenda?

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2018
Posts
21,711
Reaction score
35,644
Siku moja maza kaja kunitembelea kwangu, nikamtoa out tukala nyama akafurahi sana akaniambia Einstein mdogo wako wa mwisho siku moja aliniuliza "mama nlishawahi kukuambia NAKUPENDA?"

Akasema sikutaka kumkatisha tamaa nikamwambia umeshawahi mwanangu.

Dogo akasema "Mama NAKUPENDA"

Maza akasema machozi yalitoka mbele yake.

Wakati ananisimulia nikatafakari mimi mbona sikumbuki lini nilimtamkia neno hilo hata kwenye meseji?

Baada ya mwezi akafariki bila mimi kumtamkia NAKUPENDA MAMA hili deni linaniuma sana. Jana nimesafiri kutoka mkoani kuja Dar kumjulia hali baba ambaye yupo wodini anapigania maisha yake.

Nataka nikamwambie "BABA NAKUPENDA"before its too late.

Nauliza nyinyi hasa watoto wakiume lini umemwambia mzazi wako NAKUPENDA??

Wadada sometimes mnawezaga.

Muwe na jumapili njema watu wa Mungu.
 
Wote sijakaa nao utotoni hivo sikuwazoea. Mimi ndio yule leo kwa baba mdogo, kesho kwa aunt, keshokutwa kwa mjomba nimehama shule mara kadhaa. Hata kuongea nao kwa simu sio sana, mama nakaa siku nne sijaongea nae kama hakuna issue ila mzee hata mwaka sawa tu tena yeye kunipigia sijui lini mwisho
 
Wote sijakaa nao utotoni hivo sikuwazoea. Mimi ndio yule leo kwa baba mdogo, kesho kwa aunt, keshokutwa kwa mjomba nimehama shule mara kadhaa. Hata kuongea nao kwa simu sio sana, mama nakaa siku nne sijaongea nae kama hakuna issue ila mzee hata mwaka sawa tu tena yeye kunipigia sijui lini mwisho
Pole mkuu, ndio nature hio
 
Haya mambo bana hayaibuki tu from nowhere uanze kumwambia mzazi nakupenda, inategemea mzazi mwenyewe alivokupa hayo malezi, kuna wazazi kuambiana na mtoto hivo ni kawaida, kupigana busu n.k kuna wengine hayo mambo hayapo na hayajawahi kuwepo.

Mimi sikulelewa hivo, ila mimi ninawalea wanangu hivo nawabusu, nawaambia nawapenda tukiendelea kujaaliwa uzima hata baadae kusema mama nakupenda itakua ni kitu cha kawaida wala sio cha kuwaza kabisa.

Teh nawaza leo nikimwambia bi mkubwa nampenda nahisi atawaza "mwanangu ana nini jamani au ana matatizo, au mme anamtesa" 😁
 
Siku moja maza kaja kunitembelea kwangu, nikamtoa out tukala nyama akafurahi sana akaniambia Einstein mdogo wako wa mwisho siku moja aliniuliza "mama nlishawahi kukuambia NAKUPENDA?"

Akasema sikutaka kumkatisha tamaa nikamwambia umeshawahi mwanangu.

Dogo akasema "Mama NAKUPENDA"

Maza akasema machozi yalitoka mbele yake.

Wakati ananisimulia nikatafakari mimi mbona sikumbuki lini nilimtamkia neno hilo hata kwenye meseji?

Baada ya mwezi akafariki bila mimi kumtamkia NAKUPENDA hili deni linaniuma sana. Jana nimesafiri kutoka mkoani kuja Dar kujulia hali baba ambeye yupo wodini anapigania maisha yake.

Nataka nikamwambie "BABA NAKUPENDA"before its too late.

Nauliza nyinyi hasa watoto wakiume lini umemwambia mzazi wako NAKUPENDA??
Wadada sometimes mnawezaga.

Muwe na jumapili njema watu wa Mungu.
Mimi babayangu nikimwambia nakupenda anaweza nizingua sana aisee

Sijui hata ntaanzaje😀😀
 
Haya mambo bana hayaibuki tu from nowhere uanze kumwambia mzazi nakupenda, inategemea mzazi mwenyewe alivokupa hayo malezi, kuna wazazi kuambiana na mtoto hivo ni kawaida, kupigana busu n.k kuna wengine hayo mambo hayapo na hayajawahi kuwepo.

Mimi sikulelewa hivo, ila mimi ninawalea wanangu hivo nawabusu, nawaambia nawapenda tukiendelea kujaaliwa uzima hata baadae kusema mama nakupenda itakua ni kitu cha kawaida wala sio cha kuwaza kabisa.

Teh nawaza leo nikimwambia bi mkubwa nampenda nahisi atawaza "mwanangu ana nini jamani au ana matatizo, au mme anamtesa" [emoji16]
[emoji851][emoji851][emoji851][emoji851][emoji851] hadi wewe mkuu!!!!
 
Back
Top Bottom