Liquid Asset (FD, Bonds, UTT) v/s Fixed Asset (Nyumba ya Kupangisha)

Liquid Asset (FD, Bonds, UTT) v/s Fixed Asset (Nyumba ya Kupangisha)

Hivi hizi TB huna zinacompounding effect? Mfano Nina 85 M now nikiweka for 25 years nitavuna kiasi gani kwa wastani?
Its not true compounding, you are reinvesting payouts into new bonds, earning multiple interest payments like compound interest.
 
UTT nibora zaidi kwasababu ina compaund interest , yani faida unayoipata leo nayo pamoja na mtaji vitazalisha faida kesho. Pia vipande vinaongezeka bei . Nyumba ya milion 20 kupata bei ya lakimbili kwa mwezi nichangamoto sana . Sana sana kodi ni elfu 60 hadi laki kwa mwezi
Inategemea umewekeza wapi,chanika hakuwezi kuwa sawa na sinza au kimara
 
Treasury bonds 25 years @ 16% , then reinvest gawio lako na ukiweza ongeza 1 m kila mwaka, baada ya 5 years itakuwa na 50m, 10 years 120m na 25 years utakuwa na 1.2 billion 😂, kumbuka no taxes, kazi ngumu na inflation very unpredictable
Hizi hesabu nitazipiga Tena. Maana naona kama sijazielewa hivi.
 
Eneo i.e location.
Siyo dar yote master sebule ni 100,000
Nafaham hilo mkuu,
Ila amini kuna maeneo hiyo bei ipo. Yaani kachumba kamoja tu chenye choo ndani ni laki moja. Hapo hakuna sebule wala jiko.

Mimi ninaishi maeneo hayo hivyo nafaham nilichiandika.
 
Mkuu hii liquid assets ukiweka mfano mil 3,4,5 je kila mwezi utakuwa unapokea sh ngapi na ni bank Gani
Mkuu liquid assets ziko za aina 3. Kwanza ni fixed deposits ama amana za akiba za benki. Hii unaweka hela yako bank kwa muda flani, mnakubaliana riba wamayokulipa. Hii riba yake inatofautiana kwa benki na benki na kwa kiasi ulichonacho. Wewe ukienda na 2m riba utakayipewa sio sawa na atakaeenda na 500m. Mara nyingi riba zake ni ndogo kama una kiasi kidogo cha pesa.

Liquid assets nyingine ni hisa, hati fungani za serikali ama za makampuni binafsi. Tukianza hisa, hizi wanauza soko la hisa la Dar es Salaam. Hii unanunua sehemu ya umiliki wa kampuni flani mfano crdb, kwa maana kwamba thamani ya crdb ikipanda basi na thamani ya hela yako inapanda, zikishuka na thamani ya hela yako inashuka na unaweza kufilisika kabisa. Kwa Tanzania bado soko la hisa ni changa sana mimi binafsi sishauri mtu labda kama una mabilioni ya shilingi.

Kwenye hati fungani, iwe ya serikali ama ya kampuni binafsi hii muuzaji, ama mkopaji anaweka dau la riba, kwamba nataka unikopeshe kwa 12%. Ni wewe uamue ukopeshe ama uache., take it or leave it,haina majadiliano. Ukiamua kuikopesha serikali ama shirika basi unakua unalipwa riba kwa robo mwaka ama nusu mwaka. Yaani kila baada ya miezi 3 wakakuwekea riba yako ama kila baada ya miezi 6.

Liquid assets ta tatu ni collective investment scheme (CIS) ambapo kwa Tanzania ziko 2, ya kwanza ni mifuko ya hifadhi ya jamii. Hii ni kwa watumishi na wanachama. Hii kwa wanachama ni lazima. Ya pili ni CIS ya hiyari kama UTT, hii ni kwamba unawapelekea hela yako wataalam wafanye uwekezaji kwa niaba yako, wao ndio watafte fursa za kuwekeza kisha wawekeze hela yako halafu faida inayopatikana mnagawana riba. Pia hii nadhani wanagawa riba kwa mwezi, robo mwaka na kuendelea.

So ukielewa aina ya liquid assets ndio utaelewa wapi kuna faida kubwa. Obvious CIS na hati fungani zina faida kwa Tanzania kuliko fixed deposits unless una hela nyingi sana hivyo uwe na bargaining power kubwa.
 
Mkuu liquid assets ziko za aina 3. Kwanza ni fixed deposits ama amana za akiba za benki. Hii unaweka hela yako bank kwa muda flani, mnakubaliana riba wamayokulipa. Hii riba yake inatofautiana kwa benki na benki na kwa kiasi ulichonacho. Wewe ukienda na 2m riba utakayipewa sio sawa na atakaeenda na 500m. Mara nyingi riba zake ni ndogo kama una kiasi kidogo cha pesa.

Liquid assets nyingine ni hisa, hati fungani za serikali ama za makampuni binafsi. Tukianza hisa, hizi wanauza soko la hisa la Dar es Salaam. Hii unanunua sehemu ya umiliki wa kampuni flani mfano crdb, kwa maana kwamba thamani ya crdb ikipanda basi na thamani ya hela yako inapanda, zikishuka na thamani ya hela yako inashuka na unaweza kufilisika kabisa. Kwa Tanzania bado soko la hisa ni changa sana mimi binafsi sishauri mtu labda kama una mabilioni ya shilingi.

Kwenye hati fungani, iwe ya serikali ama ya kampuni binafsi hii muuzaji, ama mkopaji anaweka dau la riba, kwamba nataka unikopeshe kwa 12%. Ni wewe uamue ukopeshe ama uache., take it or leave it,haina majadiliano. Ukiamua kuikopesha serikali ama shirika basi unakua unalipwa riba kwa robo mwaka ama nusu mwaka. Yaani kila baada ya miezi 3 wakakuwekea riba yako ama kila baada ya miezi 6.

Liquid assets ta tatu ni collective investment scheme (CIS) ambapo kwa Tanzania ziko 2, ya kwanza ni mifuko ya hifadhi ya jamii. Hii ni kwa watumishi na wanachama. Hii kwa wanachama ni lazima. Ya pili ni CIS ya hiyari kama UTT, hii ni kwamba unawapelekea hela yako wataalam wafanye uwekezaji kwa niaba yako, wao ndio watafte fursa za kuwekeza kisha wawekeze hela yako halafu faida inayopatikana mnagawana riba. Pia hii nadhani wanagawa riba kwa mwezi, robo mwaka na kuendelea.

So ukielewa aina ya liquid assets ndio utaelewa wapi kuna faida kubwa. Obvious CIS na hati fungani zina faida kwa Tanzania kuliko fixed deposits unless una hela nyingi sana hivyo uwe na bargaining power kubwa.
Nimekupata sana
 
Nafaham hilo mkuu,
Ila amini kuna maeneo hiyo bei ipo. Yaani kachumba kamoja tu chenye choo ndani ni laki moja. Hapo hakuna sebule wala jiko.

Mimi ninaishi maeneo hayo hivyo nafaham nilichiandika.
Jenga nyumba ya kupangisha. Kwa 20m unaweza kujenga 2 in 1 simple chumba kimoja kimoja jiko na sebule. Na kama eneo lako ndio unavyosema huwezi kukosa 200,000 per month. I'm talking from experience niko site sasa hivi.
 
Njoo sehemu, nikuoneshe kisha nitakwambia kwa nilijenga kwa mbinu gani?
Mkuu nawashangaa wanaosema haiwezekani. Ndio shughuli naifanya sasa hivi. Simple rental units. Kabla haijaisha watu wanaulizia.
 
Mkuu nawashangaa wanaosema haiwezekani. Ndio shughuli naifanya sasa hivi. Simple rental units. Kabla haijaisha watu wanaulizia.
Kuna maeneo yako hot kinoma, haswa kigamboni yetu, ujenzi bado unaambiwa pameshajaa.
Ukiwa na uzoefu na ujenzi, una koneksheni za mafundi wazuri na unaishi nao vizuri, ujenzi sio kichomi kabisa.
 
Nafaham hilo mkuu,
Ila amini kuna maeneo hiyo bei ipo. Yaani kachumba kamoja tu chenye choo ndani ni laki moja. Hapo hakuna sebule wala jiko.

Mimi ninaishi maeneo hayo hivyo nafaham nilichiandika.
Hayo maneno, kiwanja kitakuwa na thamani kuliko jengo.
Yàani kiwanja Cha 25m, nyumba 20m.
 
Hayo maneno, kiwanja kitakuwa na thamani kuliko jengo.
Yàani kiwanja Cha 25m, nyumba 20m.
Sahihi kabisa,
Maeneo ya Sinza, Makumbusho, Kijitonyama vyumba ni bei hiyo. Sio kiwanja kipya, bali ni eneo liko wazi tu lakini kuna nyumba za pembeni.
 
Back
Top Bottom