Lissu aiomba Mahakama itupilie mbali Kesi ya Uchochezi dhidi ya Askofu Machumu Maximilian Kadutu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima

Lissu aiomba Mahakama itupilie mbali Kesi ya Uchochezi dhidi ya Askofu Machumu Maximilian Kadutu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Wakili wa mshtakiwa Askofu Machumu Maximilian Kadutu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Jijini Dar es Salaam, Tundu Antipas Lissu ameiomba Mahakama itupilie mbali shauri la Kesi ya Uchochezi dhidi ya Askofu huyo kwa madai kuwa halina mashiko.

Kwenye shauri hilo la jinai, Namba 19525, Mwaka 2024, Askofu Kadutu au Askofu Mwana Mapinduzi anadaiwa kutamka maneno ya uchochezi katika mkutano wa siasa, uliofanyika siku ya Jumatatu, Mwaka huu, Kijiji cha Ibaga wilaya Mkalama Mkoani Singida, hali iliyoelezwa na Wakili wa Serikali Almachius Bagenda.

Wakili huyo wa Serikali amesema ni kosa linaloweza kujenga chuki kwa Wananchi dhidi ya askari na Serikali yao, kutokana na uchochezi huo.

Kutokana na hali hiyo, Wakili Tundu Lissu, amemwomba Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi, wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Singida, Allu Nzowa, kupitia shauri dogo alilofungua mahakamani hapo, kutupilia mbali kesi hiyo, hoja iliyoibua malumbano ya kisheria, kutoka kwa wakili wa Serikali, Bagenda.

Hakimu Nzowa, ameahirisha hadi Desemba 2, 2024, atakapotoa uamuzi, juu ya pingamizi lililowekwa na upande wa utetezi, kupinga kuendelea kusikilizwa kwa shauri hili, linalomkabili Askofu Kadutu.
 
Wakili wa mshtakiwa Askofu Machumu Maximilian Kadutu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Jijini Dar es Salaam, Tundu Antipas Lissu ameiomba Mahakama itupilie mbali shauri la Kesi ya Uchochezi dhidi ya Askofu huyo kwa madai kuwa halina mashiko.

Kwenye shauri hilo la jinai, Namba 19525, Mwaka 2024, Askofu Kadutu au Askofu Mwana Mapinduzi anadaiwa kutamka maneno ya uchochezi katika mkutano wa siasa, uliofanyika siku ya Jumatatu, Mwaka huu, Kijiji cha Ibaga wilaya Mkalama Mkoani Singida, hali iliyoelezwa na Wakili wa Serikali Almachius Bagenda.

Wakili huyo wa Serikali amesema ni kosa linaloweza kujenga chuki kwa Wananchi dhidi ya askari na Serikali yao, kutokana na uchochezi huo.

Kutokana na hali hiyo, Wakili Tundu Lissu, amemwomba Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi, wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Singida, Allu Nzowa, kupitia shauri dogo alilofungua mahakamani hapo, kutupilia mbali kesi hiyo, hoja iliyoibua malumbano ya kisheria, kutoka kwa wakili wa Serikali, Bagenda.

Hakimu Nzowa, ameahirisha hadi Desemba 2, 2024, atakapotoa uamuzi, juu ya pingamizi lililowekwa na upande wa utetezi, kupinga kuendelea kusikilizwa kwa shauri hili, linalomkabili Askofu Kadutu.
SHIDA YA WATUMISHI WA MUNGU KUWA WANASIASA NDIYO HILO WASITAKE HURUMA WAPAMBANE NA KESI
 
Back
Top Bottom