LIssu alikosea, Mbowe hakuvunja katiba kuwa mwenyeti kwa muda mrefu

LIssu alikosea, Mbowe hakuvunja katiba kuwa mwenyeti kwa muda mrefu

Ni lini Lissu amewahi kupendekeza kuweka ukomo kwenye uongozi wa chama cha chadema akakataliwa?

Kwanini anaisema katiba kwenye mkutano wa bayana/hadhara badala ya kutumia vikao vya chama?

Kama chadema wanataka chama chao kife, basi wamkumbatie Lissu.

Dunia nzima sasa hivi imekumbatia dialogue badala ya jino kwa jino kama kule Sundani kwa aikna RSF na Jeshi, DRC na M23, Urusi na Ukraine, nk. Lissu anataka nginjangija inayopoteza watu weeeengi na mali zao badala ya dialogue.
Hatutaki siasa za kumtumia nguvu tutapoteza maisha
 
Vijana wa kisasa mna vichwa vizito sana aisee, hebu nenda kareplay ile lecture utuonyeshe wapi Simba kasema Mwenyekiti Mbowe kavunja katiba au kamtaja tu. Tunajiuliza hizi div zero zinakua zinaongezeka deile wakati watoto wanaenda shule kila siku kwa nini? Kumbe hata kusikiliza tu hamjui sasa mtacompose nini namna hii?
Lissu anzisha chama chako uwe mwenyekiti.

Huhitaji D 2 kujua kama Lissu alikuwa anahalalisha yeye kuwa mwenyekiti ili kuondokana na mwenyekiti aliyekaa muda mrefu sana kuliko Mtei na makani. Mtei na Makani waliondoka wenyewe kwa utashi na uzee wao kukithili na kumwachijia kijana wao Mbowe apambane na mikikimikiki ya vyombo vya dola na walawala kwaajili yao. Lakini "they can not let chadema go to the dogs". Chadema ni kama kisima cha maji, chota maji tu kwa matumizi yako ya kunywa, kuoga, kuvua, au kuchambia basi, na kukiacha kisima cha watu palepale kikiwa safi. Chadema imekusaidia kuwa mbunge, kujenga majumba, kununua magari, kujenga mahotel na nk. kama umetosheka ondoka tu kaka na kuachana na chadema maana chadema ni mali ya mtu aliyewekeza mtaji wake. Yaani badala ya wengine kutumia viinua mgongo vyao kununua magari na kujenga hoteli wao waliamua kuwekeza katika kuanzisha chama cha siasa kwa manufaa yao. Mzee Mtei na makani walianzisha chadema, Rungwe alianzisha UMMA PARTY, kuna akina Dovutwa, Mapalala, Zitto, Prof. Kigoma malima nae alianzisha chake.
 
🔥🔥🔥🔥😂😂😂😂😂😂
CHADEMA Digital yawakana Wana CHADEMA.

Nimefurahi sana leo. Mamluki na vibaraka wa mabeberu(AKA Chadema Digital) wameanza kujionyesha. Wanawakana wana CHADEMA wa Mbowe na wa Lissu.

Muwashauri wauze sera. Alooo
Lissu anahitaji kukumbushwa kwamba chadema ni mali ya mtu binafsi, si kila mtu kwakutumia hotuba majukwaani anaweza kuwa mwenyekiti (engine) ya chadema. Akaanzishe chama chake kama alivyofanya Zitto.
 
Hatutaki siasa za kumtumia nguvu tutapoteza maisha
Siasa za kutumia nguvu ni siasa za kishamba (uncivilized) katika zama hizi. Shida yetu kubwa sio chama tawala bali mifumo inayoruhusu kiongozi kuiba na kubaki salama na mifumo mibaya ya uchumi na masoko ya kidunia. Wapinzani wamepata nafasi ya kutawala kule malawi, Zambia, Kenya, DRC, Burundi, Ethiopia, Libya, Iraq, Afghanistan, nk, lakini hali ya maisha ya wananchi huko imebaki ileile au chini zaidi. Huu ni ushahidi kuwa tatizo sio chama tawala.
 
Huu ushujaa wa kwenye key board umeleta matokeo gani?
Lissu alitolea mfano wa Mzee Mtei na Makani kuwa waliachia vijiti wengine ili kuhalalisha Mbowe kumuachia kijiti yeye pia. Hii mifano haisadifu hapa; kwanza alitakiwa kueleza kwanini Mzee mtei alimwachia kijiti Bob Makini wakati katiba haimlazimishi kuachia kijiti, kwanini Bob Makani alimwachia Mbowe kijiti wakati katiba ya chadema haikumlazimisha kuachia kijiti? Je, hawa wazee waliachia vijiti kwasababu zinazofanana au zinazotofautiana? na je, Mbowe aachie kijiti kwa Lissu kwa sababu zipi Mtei na Makani waliachia vijiti? Je, mazingira ya Mtei na Makani yaliyosababisha waachie vijiti yanafanana na haya ya Mbowe kuachia kijiti kwa Lissu? Je, sifa za kuachia kijiti ni zipi?
 
Ni lini Lissu amewahi kupendekeza kuweka ukomo kwenye uongozi wa chama cha chadema akakataliwa?
Wapi na lini amewahi kukosoa swala la kutokuwa na ukomo? Sababu kama ni ile kauli aliyoitoa wakati anatangaza nia pale hakukosoa bali alitoa directiin na sababu.
Kwanini anaisema katiba kwenye mkutano wa bayana/hadhara badala ya kutumia vikao vya chama?
Katiba ni nyaraka ambayo kila mtu anapaswa kuijua na kuwa nayo ndiyo unataka wakaiongelee chumbani? Wewe ni mtu serious kweli au caricature?
Kama chadema wanataka chama chao kife, basi wamkumbatie Lissu.
Lissu ameshakuja na comebacks kadhaa abazo zilirudisha CHADEMA kwenye mstari na nyingine zikaipa nguvu zaidi. Mfano wa Karibuni kabisa ni yale maridhiano fake, lile lilikuwa ndiyo kaburi la CHADEMA, ni Lissu ndiye aliyefanya game changing. Wewe tutajie mfano wa kitu alichowahi kukiua au wapi aliiyubisha na kuigharimu CHADEMA?
Dunia nzima sasa hivi imekumbatia dialogue badala ya jino kwa jino kama kule Sundani kwa aikna RSF na Jeshi, DRC na M23, Urusi na Ukraine, nk. Lissu anataka nginjangija inayopoteza watu weeeengi na mali zao badala ya dialogue.
Wapi Lissua aliongea habari za jino kwa jino? Kwenu nyie mtu kuwa na msimamo na kutoyumbishwa na chochote ndiyo mnaita 'Jino kwa Jino?' Naona akili zenu zina utoto na ujinga wingi sana.
Halafu duna ipi hiyo unayosema siku hizi inakumbatia Dialogue? Unaiongellea Vatican? Au Russia na Ukraine? Au Mali, au Burkina Faso? Au Iran? Israel? Yemen? Hezibollah? Hamas? Venezuella? Colmba? Haiti? Au unaongelea dunia gani?
 
Huu ushujaa wa kwenye key board umeleta matokeo gani?
Haujaleta matokeo yoyote...

Ndyomaana Lisu alionya kuhusu ‘mashujaa wa mtandaoni' kwamba hiyo mbinu haina manufaa na njia sahihi ni kuanzisha na kupambana kwa nguvu ya uma.
 
Tusichoke na dialogue, hata akina Nyerere waliwafukuza wakoloni nchini kwa dialogue huku wakiendelea kuimarisha chama chao cha TANU. Vyama vyetu vya upinzani viko imara kiasi gani kuweza kuiongoza nchi? Tuna viongozi wanaohamahama kila siku kutafuta maslahi binafsi. Chadema ina wabunge wangapi bungeni hata wakichaguliwa kwenda Ikulu leo, au wataishia kutangaza Martial Law kama yule rais wa Korea Kusini? Tuache kudanganya watanzania vyama vyetu vya upinzani haviko tayari kuliongoza taifa, hata ofisi za kueleweka kila mkoa havina, ni kama saccos tu kila kiongozi kujitafutia maisha binafsi.
Hoja yako ni dhaifu sana. Kwa hiyo, wewe unaona chama imara chenye sifa ya kuongoza serikali, sifa yake ni kuiba kura ili kishinde na wengine washindwe ili uone hawana sifa ya kuongoza serikali na si ushindani unafanya mshindi halali atangazwe, na anayeshindwa Kwa haki kubali.matokeo? Kwa mambo yanayofanyika dhidi vya vyama vya upinzani ni unfair kuviona kama bado havijajipanga, wakati huwa unaona nguvu inayorumika ya kuvidhibiti, hasa Chadema. Mtu yeyote mwenye akili timamu anaona hasa Chadema inadhibitiwa na CCM haidhibitiwi. Kwa mantiki hiyo, hakuna fair play. Labda hii ndiyo ingekuwa hoja yako kwamba kuwe na fair play ili Chadema na vyama vingine vya upinzani vijijenge zaidi na kuimariaha mfumo wa demokrasia nchini.
 
Lissu alitolea mfano wa Mzee Mtei na Makani kuwa waliachia vijiti wengine ili kuhalalisha Mbowe kumuachia kijiti yeye pia. Hii mifano haisadifu hapa; kwanza alitakiwa kueleza kwanini Mzee mtei alimwachia kijiti Bob Makini wakati katiba haimlazimishi kuachia kijiti, kwanini Bob Makani alimwachia Mbowe kijiti wakati katiba ya chadema haikumlazimisha kuachia kijiti? Je, hawa wazee waliachia vijiti kwasababu zinazofanana au zinazotofautiana? na je, Mbowe aachie kijiti kwa Lissu kwa sababu zipi Mtei na Makani waliachia vijiti? Je, mazingira ya Mtei na Makani yaliyosababisha waachie vijiti yanafanana na haya ya Mbowe kuachia kijiti kwa Lissu? Je, sifa za kuachia kijiti ni zipi?

..wakati Chadema inaanzishwa katiba yao ilikuwa na kipengele cha ukomo wa uongozi.

..hapo katikakati waliondoa kipengele hicho kwasababu kilikuwa kinawaletea changamoto ktk kupata viongozi kwasababu chama kilikuwa kichanga.

..Lissu amejenga hoja kwamba Chadema imeshakua na changamoto za kupata wagombea haziko tena hivyo anapendekeza ukomo wa uongozi urejeshwe.
 
Kama chadema wanataka chama chao kife, basi wamkumbatie Lissu.
Kinyume chake nidyo chadema itakufa. Maana kupitia sakata hili ndiyo kila mtu atajiridhisha kuwa "Chadema ni mali ya Mbowe".
 
Haujaleta matokeo yoyote...

Ndyomaana Lisu alionya kuhusu ‘mashujaa wa mtandaoni' kwamba hiyo mbinu haina manufaa na njia sahihi ni kuanzisha na kupambana kwa nguvu ya uma.
Nimeishaeleza humu mara kadhaa kuwa hapa Tanzania wanasiasa waliokuwa na watu ni wawili tu nao ni Nyerere na Maalim Seif basi. Kwa sasa hakuna hata mwanasiasa mmoja wa upinzani au CCM mwenye watu hivyo Lissu akiwa mmoja wao hana impact yeyote katika kulazimisha jambo. Kenya kila mwanasiasa ana watu ila wanatofautiana idadi tu ndiyo maana wanaweza kuleta impact kwa suala lolote. Uganda Bob Wine ana watu.

Bila watu ambao mwanasiasa anaweza kuwaagiza waingie barabarani na wakaingia, mwanasiasa huyo ni mbwa koko tu hawezi sababisha jambo lolote la kisiasa litekelezwe na walio madarakani.

Hao wanaojidai nguvu ya umma nguvu yao ipo katika key boards tu.

Nimesema hata hii slogan NO REFORMS NO ELECTION ni kama slogan zingine muda ukifika uchaguzi utafanyika tu hakuna key board warrior atakayejitokeza kuzuia uchaguzi.
 
Ni lini Lissu amewahi kupendekeza kuweka ukomo kwenye uongozi wa chama cha chadema akakataliwa?

Kwanini anaisema katiba kwenye mkutano wa bayana/hadhara badala ya kutumia vikao vya chama?

Kama chadema wanataka chama chao kife, basi wamkumbatie Lissu.

Dunia nzima sasa hivi imekumbatia dialogue badala ya jino kwa jino kama kule Sundani kwa aikna RSF na Jeshi, DRC na M23, Urusi na Ukraine, nk. Lissu anataka nginjangija inayopoteza watu weeeengi na mali zao badala ya dialogue.
Kweli tupu Lisu alikosea sn
 
Kinyume chake nidyo chadema itakufa. Maana kupitia sakata hili ndiyo kila mtu atajiridhisha kuwa "Chadema ni mali ya Mbowe".
CHADEMA haitakufa na itaendelea kuwa na wanachama na mashabiki; dola iliishashindwa kuiua CHADEMA kwa kutumia mifumo na vyama vibaraka kikiwemo ACT.

Baada ya uchaguzi wao wa kitaifa Januari 2025 wagombea uchaguzi maslahi wote watakaokuwa wameshindwa watatimka na Mbowe kwa kuwa atashinda ataendelea kuipaisha zaidi CHADEMA.

CCM itaendelea kuzuia uchaguzi halali usifanyike kwa kuengua zaidi ya asilimia 50 ya wagombea wa CHADEMA na pia kura bandia na kutomtangaza mshindi kwani hapo ndipo salama yake ilipolala.
 
CHADEMA haitakufa na itaendelea kuwa na wanachama na mashabiki; dola iliishashindwa kuiua CHADEMA kwa kutumia mifumo na vyama vibaraka kikiwemo ACT.

Baada ya uchaguzi wao wa kitaifa Januari 2025 wagombea uchaguzi maslahi wote watakaokuwa wameshindwa watatimka na Mbowe kwa kuwa atashinda ataendelea kuipaisha zaidi CHADEMA.

CCM itaendelea kuzuia uchaguzi halali usifanyike kwa kuengua zaidi ya asilimia 50 ya wagombea wa CHADEMA na pia kura bandia na kutomtangaza mshindi kwani hapo ndipo salama yake ilipolala.
Basi sawa. Wacha tuone, muda utaongea mkuu. Hofu yangu ninkwamba Mbowe akishinda tena uenyekiti atabakia mpweke kama Lipumba na CUF yake.

Hata hivyo, wengine tunaishia kusema tu kuwa "yetu macho".
 
Huu ushujaa wa kwenye key board umeleta matokeo gani?
Iko hivi, kuna mwamba aliwafungia kabisa msifanye siasa na kweli mlikuwa hamfanyi siasa. mara paaaap!! akaja mtu akawafungulia mfanye siasa na bado akaja na 4Rs zake na R moja ikahusu maridhiano na nyingine ikiwa mabadiliko. Mtu wa hivi alipaswa kupokelewa na kukumbatiwa na watu wa upinzani ambao ni smart, wenye akili, wenye maarifa, wenye heshima, wenye uelewa, wazalendo, na wenye nia njema na nchi yao. Kilichotokea ni kwamba baada ya kufunguliwa kufanya siasa basi yalifunguliwa matusi, kejeli, hasira za matukio ya nyuma, vurugu na ujuaji mwingi uliopitiliza kana kwamba hawajui kwamba katiba hii inampa nguvu kubwa Rais aliyeko madarakani ya kufanya yasiyo na idadi bila kuhojiwa wala kuulizwa na chombo chochote ndani ya nchi. Wangekubali kujishusha, kuheshimu, kuwa wasikifu na kukumbatia siasa zenye staha za kuheshimu mamlaka, demokrasi, uchumi, utamaduni wetu na mustakabali wa taifa letu lazima kungetokea a "win-win" and "lose-lose" situation.

Kipaumbele chetu lazima liwe taifa na sio demokrasia. Tujenge taifa lenye matumaini hata kama "demokrasia" hakuna. China na Urusi mambo yao yanakwenda bila kujali sana mambo ya demokrasia. Siku hizi hata Ulaya na markani hakuna demokrasia wala haki. mahakama zinatumika vibaya na watawala na chaguzi zao pia wanazilalamikia kutokuwa free and fair. Tuunde kitu chetu kitakachotuvucha bila kung'ang'ania uhuru wa kutukana viongozi, ushoga na maandamani ambayo tunahua lazima yatasababisha usumbufu kwa watu, uporaji, majeruhi na vifo.
 
Back
Top Bottom