Lissu ameulizwa kwanini ameongea sasa kuhusu rushwa za mama abdul na mwanaye anakuja kuongea sasa, amejibu hivi;
Nilihitaji kukusanya taarifa zaidi kabla sijangumza, kabla ya kuzungumza kwenye mkutano wa iringa may 2 aliandika ujumbe wa maandishi kwa wajumbe wote wa kamati kuu, akielezea juu ya tatizo la rushwa kwenye chama, rushwa ya abdul na mama yake, na kuvugwa kwa uchaguzi wao wa ndani.
Alipozungumza hapa alikuwa amepata taarifa za kutosha juu ya rushwa hiyo ya abdul na mama yake kuharibu uchaguzi, lakini alitengenezewa zengwe kwenye kamati kuu. Alipozungumza kwenye kikao hicho habari hizo hazijawahi kutolewa nje, wakisema Lissu aliomba msamaha, lakini si kweli, kama wanabisha watoe video.
Baada ya kikao hicho cha kamati kuu alipata habari za ziada, ilikuaje abdul akapelekwa na wenje, anasema habari ilianzia kwengine, ambako huko alisema wenje anammudu lissu maana ni marafiki, ndio wenje akampela abdul kwa lissu
Lissu anaongea haya club house December 23, 2024 pia unaweza kusikiliza kwenye XSpaces ya Sauti ya Watanzania