Uchaguzi 2020 Lissu anazidi kuumbuka, kila hoja anayoanzisha inaonekana haina mashiko kwa Watanzania

Uchaguzi 2020 Lissu anazidi kuumbuka, kila hoja anayoanzisha inaonekana haina mashiko kwa Watanzania

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Tanzania ya leo sio ile ya miaka ya nyuma ambayo watu wengi walikuwa hawawezi kupata habari kwa urahisi kama ilivyo hii ya leo. Miaka ya nyuma radio station ilikuwa moja tu na hata Tv stations hazikuwepo,pia radio stations za watu binafsi nyingi hazikuwepo,hivyo upatikanaji wa habari ulikuwa mgumu na hivyo ilikuwa rahisi kuwapotosha watu

Leo hii utampotosha nani? Karibu kila familia mijini na vijijini ina Tv set na kila mwanafamilia ana simu janja ambayo inauwezo wa kumpatia habari anayoyote anayoitaka. Kipindi hiki cha uchaguzi wananchi wanapata habari kwa urahisi sababu teknolojia imekuwa na hivyo kila hoja na sera za mgombea wananchi wanazipata.

Mgombea urais kwa Chadema, Tundu Lissu amekuwa akisikika kila mahala anapofanya kampeni zake kuwa rais aliyepo madarakani amefifisha mahusiano ya kidiplomasia na nchi jirani na mataifa ya nje. Kisa tu huwa hafanyi safari za nje mara kwa mara. Hii hoja amekuwa akisisitiza mno kiasi kwamba watu wamekuwa wakimshangaa.

Ziara ya rais wa Burundi ndugu Evarist Ndaishiaye imemuumbua huyu ndugu Tundu Lissu,maana kama nchi haina mahusiano mazuri ya kidiplomasia na majirani au mataifa ya nje rais wa Burundi angekuja leo Tanzania kufanya ziara ya kikazi ambayo ina manufaa makubwa kwa taifa letu? Kama Tanzania ina mahusiano mabaya na majirani zake Burundi ingeweza kufanya makubaliano ya kuanzisha mchakato wa kujenga kinu cha kuchenjulia nickel kwa pamoja na Tanzania? Mbali na ziara ya rais wa Burundi ambae amefanya ziara leo,je ziara ya rais Museveni? Sio uhusiano mzuri wa kidiplomasia na majirani?

Leo bomba la mafuta litapita hapa Tanzania na taifa letu litanufaika kimapato.Biashara baina ya Burundi na Tanzania kwa sasa ni zaidi ya bil 201. Je wakianza kuuza dhahabu mkoani Kigoma kwenye soko la dhahabu itakuwaje?

Mimi binafsi naona ndugu Lissu hakujiandaa kugombea urais vizuri na itakuwa jambo la ajabu wakazi wa mkoa wa Kigoma na Tanzania kwa ujumla kuchagua mtu ambae haoni mahusiano mazuri ya taifa letu na nchi za nje amabayo yanaliletea taifa letu manufaaa makubwa. Hii hoja potofu kuwa JPM amefanya mahusiano ya kimataifa kuwa mabaya ni sababu tosha kumnyima kura huyu mgombea maana ni muongo na mzandiki.
 
Mlimuandalia Lissu kifo. Sasa mnaona ni mzimu tu ndio unaomba Urais. Hamuamini! Jiwe walilolikataa waashi, ndilo linakuwa jiwe kubwa la pembeni.
Mimi binafsi naona ndugu Lissu hakujiandaa kugombea urais vizuri na itakuwa jambo la ajabu wakazi wa mkoa wa Kigoma na Tanzania kwa ujumla kuchagua mtu ambae haoni mahusiano mazuri ya taifa letu na nchi za nje amabayo yanaliletea taifa letu manufaaa makubwa. Hii hoja potofu kuwa JPM amefanya mahusiano ya kimataifa kuwa mabaya ni sababu tosha kumnyima kura huyu mgombea maana ni muongo na mzandiki.
 
Silly argument. Unataka kueleza umma huu kuwa sababu ya kuibiwa wakati wa Kikwete ni mahusiano mazuri ya kidiplomasia? Uongo mkubwa. Ukisimama mahakamani na hoja kama hizi, utafungwa bila kosa.
Tulikuwa na mahusiano mazuri ya kidiplomasia enzi za kikwete na walituibia sana kuanzia escrow, Iptl na Richmond .Hatutaki mtu hapa ni mbele kwa mbele
 
NAWAKUMBUSHA TU WAKUU.

Tanzania ni moja kati ya The Poorest Countries in the World (MASIKINI ZAIDI DUNIANI) inashika nafasi ya 8 kutoka chini. ( Focus economy 2019- 23)
MIAKA 60 YA UHURU.

CCM imetufikisha hapa
Tupo lower middle income economy, takwimu zako ni upuuzi. Hizo takwimu zinahusiana nini na mahusiano ya kidiplomasia ?
 
Mlimuandalia Lissu kifo. Sasa mnaona ni mzimu tu ndio unaomba Urais. Hamuamini! Jiwe walilolikataa waashi, ndilo linakuwa jiwe kubwa la pembeni.
Hoja hapa ni uhusiano mbaya wa kidiplomasia ambao Lissu alidai umeharibika,wakati ni uongo.
 
Silly argument. Unataka kueleza umma huu kuwa sababu ya kuibiwa wakati wa Kikwete ni mahusiano mazuri ya kidiplomasia? Uongo mkubwa. Ukisimama mahakamani na hoja kama hizi, utafungwa bila kosa.
Acha hasira,Lissu anasema JPM ameharibu uhusiano wa kidiplomasia kitu ambacho si kweli, hafai.
 
Back
Top Bottom