Lissu hana uwezo wa kuiongoza CHADEMA hata kwa mwezi mmoja tu. Ataipasua na kuigawa kwa mdomo wake usio na breki

Lissu hana uwezo wa kuiongoza CHADEMA hata kwa mwezi mmoja tu. Ataipasua na kuigawa kwa mdomo wake usio na breki

Aisee chawa ni chawa tu aya za juu umesimamia kwenye mada na kueleza fresh kabisa.
Ila paragraphs za mwishoni sasa ukaamua kuudhihirisha ule uchawa wako.

Yaani mada hata haukuhusiana na Samia lakini hukukubali hadi umemchomeka, kizazi cha hovyo sana hiki.
 
Sidhani CCM inamwogopa Lissu,wao wanamwona kama kituko.
Wamuogope kwa lipi wakati hao CCM waitawala nchi tokea uhuru,wao ndio wenye serikali yaani dola, wao ndio chama kikubwa kuliko chama kingine.Wao hawana tatizo la ukwasi kwani matajiri wakubwa ndio wadhamini wa CCM.
Acha kujishtukia hakuna aliyesema CCM wanamuogopa Lissu au mnamuogopa kweli.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kuiongoza CHADEMA siyo suala la Mihemuko wala Uropokaji wala ukurupukaji wala matamko wala makelele yasiyo na mpangilio.

Kuiongoza CHADEMA inahitaji Mwenyekiti aina Ya Mbowe Mwamba na Jabali la siasa za upinzani hapa Nchini.Mwenye utulivu wa akili na umakini,mwenye kujua wakati gani azungumze na wakati gani awe na subira, mwenye kujua kipi kizungumzwe kwenye vikao na kipi kisubiri wakati muafaka.

CHADEMA haihitaji Mtu aina ya lissu kuwa Mwenyekiti wake kwa sababu huyu mtu ni Mropokaji, mkurupukaji,mwenye Mihemuko,asiye na breki ya mdomo wala subira wala uvumilivu. Huyu lissu ukimpa chama hata kwa mwezi mmoja tu ataacha amekipasua,kukigawa ,kukivuruga na kukisambaratisha kwa mdomo wake.

Atatoa matamko yenye kuleta na kuchochea taharuki ,ubaguzi na hisia za kutengwa kwa baadhi ya wanachama.atapandikiza chuki kubwa sana kwa chama.mpaka kuisha kwa Mwezi mmoja atakuwa amekisambaratisha chama na hakutakuwa na umoja wa chama.

Chama kitagawanyika mapande mapande na kila mtu atakuwa msemaji wa chama na kila mtu atakuwa anafyatuka kivyake kwenye camera na vyombo vya habari.chama kitakosa nidhamu na utaratibu na hakutakuwa na wa kumheshimu wala kumsikiliza mwenzake.

Wana CHADEMA ni uamuzi wenu kusuka au kunyoa. Mkimchagua lissu mjue kuwa mmekiua na kukichimbia kaburi chama.Lissu hana uwezo wala hastahili kuongoza chama kama CHADEMA.Lissu ni wa kuongozwa na siyo kuwa mtu wa mwisho juu.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Acha wapasuane 🤣🤣🤣🤣🤣
 
Aisee chawa ni chawa tu aya za juu umesimamia kwenye mada na kueleza fresh kabisa.
Ila paragraphs za mwishoni sasa ukaamua kuudhihirisha ule uchawa wako.

Yaani mada hata haukuhusiana na Samia lakini hukukubali hadi umemchomeka, kizazi cha hovyo sana hiki.
Rais Samia ni Kama Maji usipoyanywa utayaoga tuuu.
 
Wewe muosha vyoo wa lumumba mambo ya chadema yanakuhusu nini mbona una kinyampwipwi
 
Back
Top Bottom