Taaisi yoyote Duniani ina kitu kinaitwa Siri - sasa kama ni mkutano wa siri wewe unaanza kubwabwaja hadharani ili tukujuie wewe ni mkweli sana ama? Upo wapi uugwana wako?
Je unabakizaje sifa za kuwa kiongozi bora, Leo umetoa siri za mkutano wako na Mbowe na viongozi wa dini kesho utatoa za kamati kuu CDM na kesho kutwa utatoa za nchi.
Hata Serikali ina mambo ya siri ambayo hata ukifukuzwa hutakiwi kuita press na kuanza kubwabwaja, yanabakia yako ili kuilinda taasisi.
Usifikiri unamshambulia Mbowe, unaishambukia Taasisi mzima, yaani nyumba unayotegemea kuishi unaipopoa mawe.
CDM angalieni sana hii kitu.