Uchaguzi 2020 Lissu na Urais 2020: Fursa na Changamoto

Uchaguzi 2020 Lissu na Urais 2020: Fursa na Changamoto

Sorry sio mwanasiasa. Lakin kuja hapa kushtaki as if ww na Mungu mnaishi nyumba moja, umepotea.
Mungu si kikaragosi cha siasa.. haamuliwi na mtu anaamua mwenyewe.
Hakuna ajuae kesho yetu, tumuachie Mungu afanye maamuz yake.. lakin si kuwa msemaji wake.
But kilio na maombi ya wengi ubadili maamuzi ya Mungu.Mungu ujibu maombi ya wengi.
 
Asante sana....

Na hiki kinachoitwa huyu ni "presidential material" na huyu siyo "presidential material" ni cha kushangaza kidogo...

Na maana ya hawa ni kuwa "all presidential material personnels" wapo na lazima watokane na CCM tu. Huu ni upogo mwingine was watu wenye mawazo na dhana hizi......

Tangu Uhuru 1961 hadi leo (about 60 years) Tanzania imeongozwa na "the so called presidential material personnel" wanne na huyu aliyepo ni watano...!

What did they do? How much did they do to change Tanzania from worse to better?

Kwa maoni yangu wamefanya kidogo sana. Tanzania kwa umri wa miaka 60 sasa ya uwepo wake kama taifa huru, hatukupaswa kuwa hapa kimaendeleo, KIJAMII na KIUCHUMI....

Na Tanzania kama tukimfananisha na binadamu kwa umri wake wa miaka 60 maana yake ndiyo MTU huyu anajifunza kutembea sasa badala kuwa ameshaoa, kuzaa na kupata na wajukuu.....!!

Tatizo la nchi yetu siyo MTU kuwa "presidential material" ama kutokuwa. Tatizo ni mfumo wetu wa kikatiba na kisheria ndiyo kikwazo cha kupiga hatua za haraka za maendeleo yetu ya kijamii na kiuchumi....

Tukikubali na kukaa pamoja kama taifa kufanya reforms za nguvu za kisheria na kikatiba, tutaona Tanzania mpya ktk kipindi kifupi sana...
Watu huwa wanachotwa akili kirahisi sana; huwa inaibuliwa misemo ambayo ukiitazama vizuri haipo practicable, but utashangaa linaibuka kundi la watu ku support hiyo misemo, hili tatizo limesababishwa na kuzileta tabia za ushabiki wa Simba na Yanga kwenye siasa, wanadhani siasa ni kama mpira!.

Na bahati mbaya wenye hilo jukumu la kufanya hizo reforms hawako tayari, wameendelea kuegemea mawazo yao yaliyokwisha feli siku nyingi ambayo hayajatusogeza popote, hivyo wanaendelea kutuzubaisha na misemo yao, na mbaya zaidi sisi tunajikuta tunaanza kuizoea.
 
Mungu sijawahi kuaamini utendaji wake hata siku 1 maana haeleweki

kwa hiyo wataka kusema yeye ndiye aliye muweka jiwe madarakani
Ni chaguo la Mkapa na lubuva na si la Mungu. Wa Mungu utenda na kutii amri za Mungu,yaani usiuwe, usiseme uongo,mpende jirani yako,
 
Vipi baba yako na mama yako kijijini nao walipewa vipande vingapi?
Bibi yangu kafariki juzi kaniachia kadi ya CHADEMA na ni msukuma wa malampaka kabla ya kufa kasema mjuu wangu hiki ndiyo chama ata ukifa njaa unapigania haki ni sawa.
 
Namkubali sana lissu lakini bila kupepesa lisu sio presidential
Mara kumi wapinzani kama wamekosa mtu wamweke zito
 
Hapo kwenye THREATS" kuna upogo kidogo kwenye hoja yako. Na nafikiri labda hata wewe kidogo ufahamu wako kwenye baadhi ya mambo uko tenge kidogo....

Mimi nikukosoe kwenye eneo moja tu na mengine watasema wengine...

#Lissu na maendeleo jimboni kwake
- Kwamba hajaleta maendeleo jimboni, watu wake masikini na social services kwa ujumla ni hovyo

- Ukamalizia kwa kusema "Charity begins at home"

MASWALI KWAKO;

1. Hivi ni nani hasa wa kupeleka maendeleo ktk jimbo la uchaguzi lolote? Mbunge au serikali?

2. Nafahamu kazi ya mbunge kubwa ni kupeleka kero ama mahitaji ya watu wake huko bungeni/serikalini kwa ku - shout ili kero fulani zitatuliwe kibajeti au kisera....

Je, unadhani Lissu ktk umri wake wote wa ubunge hakutimiza wajibu huu muhimu wa uwakilishi kwa watu wake waliomchagua kwa awamu mbili?

3. Kila Jimbo la uchaguzi Tanzania lazima limo ndani ya halmashauri fulani ya jiji, manispaa, mji, ama wilaya na mkoa fulani. Huko wako viongozi kibao wa serikali mathalani DC, DEDs, RCs DSO, na wengine wengi tu ambao kiuhalisia hawa ndiyo ma - in charge wa shughuli za kijamii na maendeleo ya siku kwa siku ktk maeneo yao ya kiutawala....

Ndo tuseme hawa wote wanakuwa hawaoni kuwa eneo fulani ktk vijiji, miji, ama kata na wilaya kwa ujumla wananchi hawana maji, shule, kituo cha afya nk hadi tu wamsubiri mbunge?? Ni nini nafasi na uwepo wao kama lawama zinakwenda kwa mbunge? Kwa akili yako unadhani hii ni sawa?

MWISHO:
Kwa mfumo wetu wa utawala wa kisiasa na kijamii, ni ngumu kwa mbunge asiyetokana na chama kilicho madarakani na mkosoaji mkubwa wa serikali hiyo, jimbo lake la uchaguzi likapata bajeti ya maendeleo ktk miradi mbalimbali...

Kwa sababu kwa mfumo wa utawala wetu ukiwa mbunge wa upinzani na ukataka jimbo lake lipate favour, basi lazima u - compromise na utawala wa serikali iliyopo...

Ktk hali hii na kwa "nature" ya mtu kama Tundu Lissu huyu kamwe hawezi ku - compromise na Rais John Pombe Magufuli na CCM na ni bahati njema kuwa na wewe mwenyewe umelisema hili ktk uchambuzi wako kwanini yuko hiyo, is a person with his own and unquestionable stands...!!

Ndivyo ilivyokuwa kwa Tundu Lissu. Na kuthibitisha hili, immediately baada ya jimbo kupata mbunge yule wa Viti maalumu - CCM (Miraji Mtaturu) - chama cha Rais aliyeko madarakani hata kabla mbunge huyo kusimama bungeni kusema lolote, haraka haraka Rais Magufuli aliamuru pesa bilioni kadhaa ziende jimboni kwa Lissu kwa ajili ya mradi fulani wa maji...!!

Unasemaje hapo? Hiyo SWOT analysis yako inafaa kweli kufanya kazi ktk mazingira hayo??... Ukiitumia na kuja na conclusion yoyote, utakuwa hujitendei haki mwenyewe na nafsi yako....!!
Kongole Ndugu kwa kumpa za USO,tunafahamu kitendo cha kukosekana kwa maendeleo katika Jimbo LA Singida Mashariki linafanana na majimbo mengine mengi kama siyo yote Tanzania Bara,yawe CCM ama upinzani hali hazitofautiani sana.Tujiulize tatizo huwa ni wabunge?Bajeti zinazopitishwa Bungeni zinapelekwa kwa usawa nchi nzima?Je,CDM au Lissu ndiyo wanakusanya kodi nchi hii? Tunafahamu kuwa maendeleo ya nchi huletwa kwa kodi na mwenye jukumu hilo LA kukusanya na kugawa fedha za maendeleo ni serikali iliyoundwa na chama kilichoshinda katika uchaguzi halali wa kidemokrasia(CCM ?).
Swali,nani alitakiwa kupeleka maendeleo huko Singida Mashariki?Kama hayakupelekwa nani walipaswa kuwajibika kwa kuwakosesha wana Singida Mashariki haki yao ya huduma tangia Uhuru wa nchi hii?
Nionavyo mimi hiyo hoja haiwezi kuwa kikwazo cha Mh Lissu kutostahili kugombea Urais wa JMT.
Tusiwapangie Watanzania Rais wamtakaye,ndiyo maana Katiba imeweka utaratibu wa uchaguzi wake kila baada ya miaka mitano.
 
Mikutano inazuiwa kwa sababu hamtumii akiri kufikiri ila mnatumia matumbo yenu kuwaza uhakifu,
Lazima mzuiwe tu, ahkuna namna.
Hivi umeandika lugha gani hii, nimejitahidi kuelewa lakini nimeshindwa. Inawezekana ulikuwa na maoni mazuri tu, ila lugha uliyotumia kufikisha ujumbe haieleweki.
 
Back
Top Bottom