Uchaguzi 2020 Lissu umati usikudanganye, wengi hawajajiandikisha

Uchaguzi 2020 Lissu umati usikudanganye, wengi hawajajiandikisha

maccm yanakusanya wanafunzi kwa hiyo hao wanavitambulisho
 
Wafuasi wa CHADEMA na Lissu wamekuwa wakipagawa na kuota kwamba, uchaguzi wa October utawapatia ushindi na kwa mara ya kwanza toka tujipatie Uhuru nchi itaongozwa na upinzani.

Hii ni kutokana na Umati ambao umekuwa ukijitokeza kwenye kampeni za ugombea urais kwa mheshimiwa Tundu Lissu. Niwaambie wafuasi wa CHADEMA endeleeni kufurahia ngojera za mgombea wenu ila Urais mtaendelea kuusikia hadi 2925.

Sababu ya kwanza ni kwamba, watanzania wengi mnaowaona kwenye mikutano, hawajajiandikisha na hata hao waliojiandikisha, kwenye uchaguzi wa mwaka huu hawataamka kwenda kupiga hiyo kura kwa vile inajulikana wazi Mjomba Magu anarudi pale Chamwino na Magogoni.

Pili, vyama vya upinzani vyote vimeshapoteza mvuto kwa wananchi na kuikubali CCM na mgombea wake, kwa yale Serikali ya CCM iliyoyafanya na yanaonekana kwa macho na hata kuyagusa kwa mkono.

Tatu, Viongozi wa vyama vya upinzani wameshapoteza imani kwa wananchi na hasa Wasomi na waelewa wa mambo,ambao miaka michache iliyopita ndiyo tulikuwa tukiunga mkono mageuzi, kwa kuona CCM ni ya watu wasiojielewa. Kupotea kwa imani hii kumetokana na viongozi wenyewe wa vyama vya upinzani kufanya kama taasisi zao, na si za wananchi. Tazama Mbowe na Chadema, Zitto na ACT, hawana tofauti na Mzee Mrema wa TLP, au NCCR ya Mbatia.Ndiyo maana Dr Slaa aliyaona haya mapema akaamua kukaa pembeni.Chadema na wafuasi wenu msijidanganye.
Kwa hiyo unashauri Nini kifanyike?
 
Lissu amenifurahisha sana na ile hoja yake ya elimu.
to be honest sijawahi dhani kuna muafrika angewaza vile kuhusu elimu hivyo sina budi kumpa kura yangu.


Change my mind....
 
Ila wanaohudhuria fiesta la chama cha mashetani - CCM ndio wamejiandikisha?
Akili zako ni za kuvukia barabara tu
 
Afadhali huyu anayedanganywa na wingi wa watu kwenye kampeni kuliko mijizi inayojiandaa kuiba masanduku na kuchakachua kura! Tunafahamu Jiwe amedeploy maaskari wa TISS wa combat intelijensia wakafanya kazi haramu toka jana!
Onyo:
1. Kama uchaguzi huu ni mpango wa Mungu kukomboa watanzania kutoka katika gereza la kichaa wa chattle basi hawawezi kitu. Mpango wa Mungu hauingiliwi na chochote! na wote walioingilia waliuawa haraka sana.
2. Kwa kuzingatia nguvu ya Mungu nashauri wale mnajielewa jiepusheni na hii laana itakayowala haraka na vizazi vyenu.
3. Kwa nini mjihangaishe na kichaa ambaye hana nia njema na viumbe wa Mungu.

Kumbukeni:
Walioshambulia Tundu lissu wameshakatwa zaidi ya Nusu. Kuna kina Nyaulingo na juzi yule mtoa amri na mshauri mkuu wa mauaji ametangulizwa kuzimu ghafla kupitia Lupaso.
Achana na kupindisha haki mtaangamia!!
 
JPM wakati anapambana na Lowassa alipiga push-ups nyingi mara kadhaa, ulifahamu maana yake? Dhihaka kwa Lowassa kuhusu afya yake. Rhetorical language.

Wakati huu anapambana na amepigishwa magoti mara mbili akiomba kura, unajua maana yake??

Mataga Tafuta thamani ya X......
 
Lowassa alipigiwa mpaka deki katika barabara aliyokatiza kule Mwanza ulipo fikra siku ya uchaguzi akabaki akishangaa.
Kura alizopewa Lowassa na NEC sio zile alizopigiwa na wananchi.

Kulikuwa na massive vote rigging probably hata NEC wenyewe hawajui nini hasa kilitokea. Phillipo unalijua hili mzee!
 
Lowassa alipigiwa mpaka deki katika barabara aliyokatiza kule Mwanza ulipo fikra siku ya uchaguzi akabaki akishangaa.

Watanzania ni sawa sawa na “wajumbe”, wanaweza kukukarimu mpaka ukajiona unaishi mawinguni.


Je matokeo yalikuwaje ukilinganisha na matokeo ya chaguzi zilizowahi kufanyika?

Kuna baadhi ya nchi mgombea akishinda kwa kura chini ya 60% uchaguzi unarudiwa maana wanachukulia mshindi atakuwa hajakubalika na wengi.
Wanatakaga atleast 60% chini ya hapo uchaguzi unarudiwa [emoji108][emoji108]

Kwa hiyo yalopita si ndwele tugange yajayo wala hainahaja ya kutamba sababu kama ilivyoelezwa!

Lowasa alitisha!
 
Wafuasi wa Magu wajiandijishe au la.Yeye ataendelea kuwa Raisi,hakuna mjinga atakatekubali kuweka nchi Rehani kwa vyama visivyojitambua.Hata Tume ya uchaguzi ikosee na kumtangaza mgombea wenu ndiye mshindi,Tundu Lissu atapinga na kwenda mahakamani kwamba Tume imekosea yeye hakustahili kushinda,hayupo tayari kuwa Raisi maana hajajiandaa.Anaelewa kabisa anachofanya kwenye hizo kampeni ni maigizo ya Futuhi.
Eti hajajiandaa, muulize magu kama 2015 alijiandaa
 
Prapaganda za kipumbavu sana.
Vijana wamejiandikisha kwa hasira sana,
Wewe jifariji tu.
Mlishasema upinzani kufikia 2020 utakuwa haupo
Sasa ivi mnajinyea, mnakuja na hoja nyepesi eti wengi hawajajiandikisha.
 
Kumbe ndomana nw mnataman kusuguliwa co???
Lowassa alipigiwa mpaka deki katika barabara aliyokatiza kule Mwanza ulipo fikra siku ya uchaguzi akabaki akishangaa.

Watanzania ni sawa sawa na “wajumbe”, wanaweza kukukarimu mpaka ukajiona unaishi mawinguni.
 
Acha ubashiri wa waganga wa kienyeji.Wewe ulikagua mifuko ya wahudhuriaji kwamba hawana vitambulisho?Kwa taarifa yako vijana wengi wamejiandikisha ili kupata vitambulisho kwa ajili ya maisha yao ya kila siku.Ili upate kitambulisho Cha NIDA kwa ajili ya Kupata line ya simu ,njia rahisi Ni kuwa na kitambulisho Cha kura.Sasa kwa hesabu zako watanzania wangapi hawana line za simu?
Ukiwa Lumumba buku7 uwezo wa kufikiri unapungua Sana!
 
Hii mbinu yenu ni ya kitoto kabisa na mojawapo ya mbinu za kuhalalisha wizi wenu na unyang'anyi wa matokeo.

Kwani kwenye mikutano yote ya CCM huwa mnakagua kwanza waliojiandikisha ndio wahudhurie?

Subiri 28/10 muone mambo. Majizi nyie.
 
Kura alizopewa Lowassa na NEC sio zile alizopigiwa na wananchi.

Kulikuwa na massive vote rigging probably hata NEC wenyewe hawajui nini hasa kilitokea. Phillipo unalijua hili mzee!
Story za vijiweni Lowassa hakuwa na utayari wa kupewa nchi, kimwili hakuwa imara hakuna aliyeiba kura ni maneno ya kujifariji ya mitaani.
 
Back
Top Bottom