List ya Mastaa Bongo wanaoongoza kwa kupigilia Suti kali, Diamond kinara!

GadoTz

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2014
Posts
370
Reaction score
636
Vazi la suti ni vazi linaloheshimika sana duniani. Ni vazi pekee ambalo linavaliwa kwenye matukio makubwa na mtu kuonekana nadhifu. Leo nataka tuone mastaa sita wa hapa Bongo wanaoongoza kwa kupiga suti kali.

1.Diamond Platnumz : Kwa sasa unaweza kumuita Mr red carpet ,maana amemaliza karibia matukio yote ya kistaa duniani labda kabakiza tuzo za Oscar tu lol. Ndio msanii anayependeza akiwa kwenye suti kuliko celeb yoyote Tanzania.




2. Sheria Ngowi : Mbunifu wa mavazi, sio mtu wa kuonekana sana kwenye matukio mengi kama celebrities wengine, ila akitokea kwenye tukio lazima mtafutane. Suti za huyu jamaa ni simple ila zipo so classic.




3. B12: Mtangazaji namba moja kwenye maswala ya fasheni za pamba... Ni mtangazaji anayetupia suti kali kuwahi kushuhudiwa katika kizazi hiki. Kwa mahaba aliyonayo kwenye mitupio, mshikaji ana duka la pamba Born2shine. Akivaa suti, suti inakuwa inajisikia ipo nyumbani.



4. January Makamba: Rais mtia nia huyu, suti zinampenda kuliko yeye anavyozopenda, Ni mwanasiasa pekee anayejua suti classic haswa, angeingia ikulu, kina Obama lazima wangetubu kwenye mamikutano yao huko.



5. Ommy Dimpoz : moja ya viumbe wachache ambao suti haziwakatai. Akivaa suti utafikiri kazaliwa nayo.



6. Hemed PHD: Ukiangalia namna suti inavyotakiwa kumkaa mtu, basi PHD ni mmoja ya vijana wachache akiwa ndani ya suti lazima uikubali suti kwa ujumla... Suti zinamtoa chicha sana kuliko mavazi mengine.




 
Ungemtafutia picha nzuri huyo ommy dimpoz! Hizo sifa na hio koti alovaa wala haviendani!
 
Iyo top5 ni ya kwako umeiandaa au kuna shirika limetoa iyo kitu
 
ila kwa jux umezingua mdau inabidi ufanye editing mana ni aibu kutokuwepo
 
Jux anavaa vizuri ila hapa nazungumzia suti tu, Jux sio mtu wa suti mkuu.

sasa huyo diamond anazivaaa wapi yeye c kwenye matamasha hata jux ndo hivyo hivyo ila ngoja tuache maana sujui umetumia vigezo gani ila jux kwenye ktma alipiga suti moja kali
 
Angekuwa sio staa usingemfahamu

Angekuwa sio staa asingeonekana top 5 ya ccm

Angekuwa sio staa ata kwenye hii super list asingekuwepo.

1. Mimi na wewe au watu wengine kumfahamu mtu fulani hakumfanyi huyo mtu kua star, maana mimi na wewe pamoja na watu wengine tunamfahamu Sospeter Muhongo, je, ni star?

2. Kuoneka au kutokea kwenye top five ya ccm ndo kabisa hakumfanyi mtu awe star,

3. Yupo kwenye list hii sababu either ya mapenzi yako binafsi, au ume copy na kupaste toka sehemu ingine bila kupitia vizuri maana umechanganya wanamuziki, waigizaji na wanasiasa.. Sasa mwanasiasa anakuaga star tangu lini? Ma star mara nyingi wanajihusisha na maswala ya entertainment na sports.. ndo mana kuna football stars, rising music stars... sasa ushawahi sikia wapi political star..?
 
Mbona umemsahau mzee kingwendu jaman anastail awe namba 2 hapo
 
Huyu ndiyo babu yao hao wavaa suti wote....waige mfano hapaaaa
 
Hii list itabidi iwereversed kuleta mvuto japo wa kwanza asiwe wa mwisho,,japo nilichogundua ni kwamba aliepost siomfatiliaji wa mambo,coz kunawakuitwa jux jamaa kwa mwaka Jana ndie aliechukua namba 1 kwa macelebrity wa kuime ,kwa mavazi ya wakati..?!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…