Lita 1,000 za maji kuuzwa mpaka Tsh 60,000 mgao wa maji mradi wa ‘watu wakubwa’ Serikarini?

Lita 1,000 za maji kuuzwa mpaka Tsh 60,000 mgao wa maji mradi wa ‘watu wakubwa’ Serikarini?

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Kadri siku zinavyoenda mgao wa maji unazidi kuwa mkali, na kwa sehemu kubwa maji hayatoki kabisa zaidi ya wiki mbili na wengine mpaka tatu.

Bei ya maji tunayouziwa mtaani inatisha, kwa jinsi gharama za maisha zilivyopanda tutafika kweli? Dumu moja la lita 20 linauzwa 1,000 mpaka 2,000, lita 1,000 hali ndiyo mbaya kabisa, huku bei inacheza kwenye sh 40,000 mpaka sh 60,000.

Kwa hali hii ni kama vile kuna mtu/watu wanaodhibiti maji yaendelee kutokupatikana ili waendelee kufaidika kwa manufaa yao yenyewe.

Hali ni mbaya, fanyeni kitu, mgao huu unatugharimu sana, hapo hujagusa gharama za bando zinazopanda kila siku pamoja na mgao wa umeme.

Wadau huko mbele kunaendeka kweli?
 
Moto huko milimani wachome wengine matokea yake ndio muwauzie serikalini...maji hamna mnataka dawasa wachote maji ya chooni wawauzie
 
Mlifanya party na mkanyeshwa mbuzi bia alipoondoka mwendazake kawaachia nchi yenu sasa mnapiga piga kelele za nini tulieni dawa iwaingie mpaka 2025 mtapauka kama wauza mikaa kanyaga twende mama hakuna kurudi nyuma.
 
Back
Top Bottom