Live: KUTOKA BUTIAMA

NGULI

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2008
Posts
4,801
Reaction score
643
Leo watz wanakumbuka kifo cha baba wa Taifa Mwl Julius K. Nyerere.Butima ndiko kumbukumbuku zinafanyika kitaifa, viongozi mbalimbali wakitaifa wapo hapa, brudani za ngoma zinaendelea na wakati wowote mh! Rais wa Jamhuri ya Munnganio-Kikwete atafika hapa badi sijafahamu kama atalihutubia taifa katika kilele hichi. Ila kumbukumbu zimefana sana.

Na kama kuna sehemu yeyote watu wamekusanyika au kuna mdahalo wa kumuenzi mwl hata nje ya mipaka ya nchi yetu tungependa kujuzwa nini kinajiri huko.
 

Shida kubwa si ngoma na vinywaji, its about delivery! Wanaboa sana hao viongozi uchwara! Utakuta wameenda hapo na magari ya fahari, ambayo hata Mwalimu mwenyewe hakuwahi kuyaona au kuyapanda... Wamemuenzi Mwalimu kivipi?Wameipiga vita rushwa kivipi?Ni kwa kiasi gani wanaingia Ikulu kwa Usafi?Hapo kinachofanyika ni Ngonjera tu...yani kujiwekea fedha zaidi mifukoni kwa wale walio kwenye kamati za maandalizi... fyuuuuuu!!! Aibu!
 

Mkuu umekuwa mkali sn hapa, da! kweli unauchungu na hii nchi, mimi sio mzuri kwenye siasa nafikiri mpwa unafahamu, nimereport tu na baada ya kutuma hii thread net ilikata na hata hii post sijui kama utaisoma. Naona hapa ngonjera zimepamba moto watoto wako trained vizuri wametoa shoo kali ya martial arts nzuri.
 
Je hapo wanamuenzi kwa ukweli na kimatendo au ni unafiki tu??
 
Tumuenzi Nyerere kwa matendo na wala sio hizi sherehe na ngoma huku matendo yetu ni kinyume kabisa na aliyokuwa anasema Nyerere.
 
Kama kawaida yake Mkapa bila aibu lazima awepo kumkumbuka shujaa aliyefanikisha ulaji wake
 
Leo ni muhimu ahutubie alahiki ya watu sasa sijui kama hana uchovu tena wa safari
Natamani afufuke hapo alipo awakemee hao mafisadi kisha akalale kwa amani
 

nipe news kama uko huko Butiama nikupe salaam sangu kwa mama Nyerere umfikishie
 
Jamani achaneni na habari hizo za Butiama, mimi nina hasira hadi ninataka kupiga watoto wangu wanapofosi waendelee kuangalia hayo matumizi ya hela za serikali bila tija!...Mitumbo yao mikubwa mipana, kama magunia, na hawaoni aibu jinsi walivyo tofauti na wananchi wa kawaida...puuuuuhh!. Wananiboa mimi bana! Mikalio ndo usiseme.. Ukianzisha mada ya kujenga chuo kikuu hapo Butiama wataanza kuinamisha sura kama vile wanashikisha mtu ukuta!...sIWAPENDI HAO WANGEJUA...!
 
Pole pole kaka usije toboa macho watoto
 
Waziri Kapuya anataka kumkaribisha rais kuhutubia sijui ataongea nini,kwa sasa mh. anapumzika.Kapuya kisha ingiza mambo yake ya Simba sport clu kwa kuhoji kwanini haoni laki yake kwenye waimba halaiki bali rangi ya jangwani?????
 
Waziri Kapuya anataka kumkaribisha rais kuhutubia sijui ataongea nini,kwa sasa mh. anapumzika.Kapuya kisha ingiza mambo yake ya Simba sport clu kwa kuhoji kwanini haoni laki yake kwenye waimba halaiki bali rangi ya jangwani?????


leo akisimama kwenye juwa wanamvalisha pama ..wameshajifunza....!!!
....na naona wamemuwekea mike mezani ..ataamua mwenyewe kama aongee akiwa amekaa au amesimama....na lingine ni kutoa hotuba fupi na straight to the point amalize akae...

kuna haja ya kujali lakini hali yake nzuri!!
 
komba anaimba hapa ....jk amekuwa too emotional ...anaimba ...anasimama kuendelea kuimba!!
 
jk amekamata maji anapiga mafundo kudu kudu...nadhani anatafuta energy ya kuongea baada ya wimbo huu...
 
amepewa hotuba ...yupo busy ana i review....sidhani kama hii ni sababu ya kurefusha kidogo muda wa vikundi vya sanaa.....anapitia hotuba....[i guess hakupata muda wa kupitia kabla ya kuja kwenye hadhara]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…