LIVE: Tanzania Primier League (TPL)... Simba SC dhidi ya Kagera Sugar moja kwa moja kutokea uwanja wa Uhuru, Dar es salaam.

LIVE: Tanzania Primier League (TPL)... Simba SC dhidi ya Kagera Sugar moja kwa moja kutokea uwanja wa Uhuru, Dar es salaam.

Dawa ya kagera sugar ni Golikipa mwingine pamoja na ulinzi na si manura na zana nitashangaa sana msimu ujao manura akiendelea kuaminiwa kama golikipa namba moja wa Simba pamoja na zana kubakia.
Ubingwa tutachukua lakini si kwa kufedheheshwa kiasi hiki na timu ileile, hii inamaanisha mbinu zao dhidi ya Simba ni bora zaidi na hatujawahi kuwafanyia kazi ipasavyo
Hapa wakulaumiwa ni shabalala, beki unatulizia mpira golini uyu dogo anatakiwa awe anaingia km sub
 
Manula naye ni tatizo zaidi ya ZANA. Wasiojua mpira wanamlaumu Mohamed Husein kwa kosa la Manula. Manula kwa nafasi yake alikuwa anaona uwanja vizuri kuliiko Mohamed Husseni kwa hiyo aliona wazi Mohamed Huseni hana adui nyuma yake yeye alikwenda kufanya nini ndani ya hatua sita wakati beki wake hakuwa na adui yeyote karibu? Kwa nini asingemuita kwa sauti halafu akaenda kuudaka ule mpira mbele yake? Na ni beki gani atakayeacha mpira umpite wakati hajui nyuma kuna nani? Iwapo Manula angetulia golini kusingekuwa na madhara yoyote.

Pia kuna haja ya makocha kumwelekeza Manula na wakati mwengine kumkumbusha kurudi golini. Magoli asilimia 95 aliyofungwa kwenye champions league and hata ligi ya ndani huwa anakuwa amesogea mbele na kuliacha goli. Hata juzi goli la Coastal Union lilikuwa hivyo hivyo. Na vizuri zaidi kumleta kipa mwingine mwenye viwango ili ampe changamoto.

Lakini face to face na washambuliaji Manula nampa credit zake kwani hapa bongo hakuna anaemfikia.
 
Back
Top Bottom