Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Huyu ndio mzuri sasa
Kuna watu akili itawajia

Sio mtu anaboronga tu
Mechi inayofuata anapata namba

Watu wanamlaumu Slot kwamba yupo harsh. Ila kutumia akili yake ya kawaida kuona kama ni kweli au la ni ngumu.

Slot alisema “Quansah hakuwa vizuri kipindi cha kwanza, alikosa aerial duels nyingi” je ni kweli au uongo?? Jibu ni kweli.
Wengi wamekaa na Klopp muda mrefu hawajawahi kuona Klopp akisema hivyo, ndio maana wanaona jamaa yupo harsh.

Ilikuwa rahisi Klopp kukaa ni kina Henderson, Milner, Keita, Thiago, Ox, Matip licha ya kuwa na viwango visivyoridhisha na wengine kuwa majeruhi wa kudumu. Mchezaji akikosea Klopp alizidi kumpa game time ili ajirekebishe kitu ambacho ukiwa kama Manager sio kizuri.

Slot ana namna yake ya kufundisha na kuhudumia wachezaji, yes anahitaji mchezaji awe attention muda wote wa mchezo, asipoteze umakini, which is somethimg good.
 
Hakuna tena yale ma hug [emoji847] ya Klopp. Slot ni kazi kazi hana bla bla. Kwa hili nasimama nae. Klabu kwanza mengine baadae. Klopp alitaka kua mwema kwa kila mtu wakati mwingine ilimgharimu mechi kwa kukosa ujasiri wa sub kama hizi.

YNWA

Tulishihudia kwa Henderson baada ya kuondolewa.

Klopp alizidisha ubaba sana, ikafika mahali wachezaji wakaona hata ikitokea nimeharibu next match nitakuwepo.

Kwa maamuzi haya ya Sub nafikiri sasa ni wakati wa wachezaji kujituma, hakuna mchezaji wa kocha. Ni kazi kazi.

Amezingua hata Vvd piga bench weka sub, hakuna kulea lea kimayai.

Halafu Trent hajazoea hii hali kwani miaka yake yote ya professional football anamjua Klopp hakuwahi kupitia hizi heka heka. Zabu anazofanyiwa sio kwamba hafai, ameharibu, hapana ni kwa ajili ya faida yake. Long season to go. Kingine Trent anaweza kumuhofia Bradley maana bwana mdogo hana masihara, no. Anaitaka sana which is good thing. Sasa hivi kidoooogo akiumia Trent pressure inakuwa kidgo kwa sababu ya Trent. Kitu kama hiki tunakiona kwa Pep, hata Slot alisema timu zingine kila no zina wachezaji wawili wawili, wengine hadi watatu position moja.

Hofu yangu ni DM na LCB,
 

Its a never ending cycle…!!!

Ili tujiulize ile LFC ambayo wengi hatukuiona ya 70’s 80’s na 90’s ilikuwaje?? Back to back cups waliwezaje??

Yes LFC ni kama dini hivi inaamini katiak misingi yake siku zote, lkn katika misingi yke kuna vile inaweza kufanywa na tuka shine.!!!

YNWA
 
Maombi yazidishwe kwa Nunez

Hehehehe kuna comment niliiona mahali dah.!!!

Ety “kila mtu kwa imani yake afanye jambo kwa ajili ya Nunez watu wa kwao wamuachie.”
Kuna wanaigeria wa LFC wamesema wapelekewe Nunez wakamtengeneze.

Jamaa ana kila kitu cha kumfanya awe mchezaji mzuri ila msingi wake hautimizi, (kufunga magoli). Anyway sisi shabiki zake tunasubiri under Slot atafanya nini?? Kisha nitakuja kurusha taulo au niendelee kupanda gari lake.
 

Yani jamaa ukimuangalia ana appearance ya Diego Folan na Calibre ya Fernando Torres lakini output ni ya Cristian Benteke.
 
Naomba huo ujumbe Mkuu hata screenshot yake.
Nunez ni wa kuombewa kwa kweli kuna clear chance aliikosa sijui alidhani yuko offside?
Na camera zikaelekezwa kwa Slot na Slot alionekana kuchukia
 
The MoNA tupe mtazamo wako mechi ya jana

Slotball.

Brentford walijaribu sana kutushambulia but we were combact enough hawakuwa na madhara sana.

Ubora wa Alisson, Ibou, Vvd, Gravern, pass makini za Trent, Runs za Szobo, ziliwafungua Brent, vizuri tu. Magoli mazuri, la kwanza counter, la pili flowing move, good timing, good decisions kwenye magoli yote.

Mimi ni muumini wa double pivot, sana kwa sababu inasadia kutunza energy ya kiungo wako no. 6 na kuwa na watu wawili katikati.

Bado wachezaji wanahangaika na system ya Slot ila pole pole inawaingia.

Vvd na Ibou waliwin aerial duels nyingi sana, 2nd balls tuliziwin nyingi sana. Ikarahisisha maisha ya timu kwa ujumla wake.

Mtu naona tunahitaji mbadala wake ni Robertons ule upande wake upo very weak ukianza na yeye mwenyewe, ana struggle sana. Robbo alishamaliza mpira ma LFC since 2022/2023, injuries ya za last season zimemmaliza. He is not the same.

Uzuri sasa hivi kila mtu anatekeleza wajibu wake, hakuna mtu kuhangaika na jukumu la mtu.

Slot naona anavyomtumia Trent huenda tukamfaidia sana offensively na defensively kwa sababu hamtumii kuingia ndani zaidi anamuacha akae pembeni, zaidi which is good hata mkishambuliwa space inakuwa ndogo.

Slot sio attack attack coach kuna muda anacotrol mchezo with less intensity ili ku save energy ya wachezaji wake na kupunguza Spaces, kupunguza makosa yatokanayo na counter za opponents. Which is good thing, kuna muda ni bora kulinda moja ulilopata kuliko kuhangaikia mengine ambayo pengine unaweza kukosa.

Kuna njia nyingi za ku defense na moja wapo ni possession with low intensity, less counter, stay focused kwenye patterns, na combination plays.

Combination play ni mchanganyiko wa patterns na namna ya kucheza kuna muda inakuwa diamond, triangle, rectangular, passing through players, individual dribbling n.k hii inasaidia kumchanganya mpizani wako asijua unatumia nini.

Kuna muda Salah alikuwa anagonga 1.2 anaondoka, kuna muda Trent aliingia katikati, na 1,2 yeye na Szobo, kuna muda through dribbling, kuna muda tulikuwa, 4–2-4 kwenye kukaba, kuna muda 4-4-2 kwenye kuzuia. Baada ya goli la pilia tukapiga Slot ball with flowing movements waohh, just waooh..!!!

It’s a second match, binafsi gari la Slot nilishapanda muda tu, mengine mambo ya pira.

Gravern kwenye no. 6 anaicheza vizuri mno, mno, weakness yake ni tackling kama ile aliyoifanya jana unaona he is not expert kwenye mambo hayo akaishia kupata njano. Bradley, Konate hawa ndio wataalamu wa Tackling pale LFC, timing yao nzuri sana.
Namba nzuri kwa mtu ambaye sio natural 6.


Tukio lililoshika hatamu mechi ya jana. Nilipenda Slot alivyomfuata jana Trent baada ya kuonesha kutoridhishwa na kufanyiwa sub dk zile, Na hata alivyolijibu swali hilo kuhusu tukio lile.


Trent he is a world class player, kikubwa akubaliane na hali, na aendelee kupiga kazi, Anfield inamkubali sana na LFC inamtegemea kwenye ubora wake, (quality passes, long and shot passes, long and short ranges). Kipimo kizuri ni next match vs Utd at OT.

Its too early ila tuna enjoy every moment we have under Slotball. He might be our Bob Paisley

Best luck to us
Up reds
YNWA
 
Pavel Durov, the Russian-born CEO of encrypted messaging app Telegram, was arrested at at Le Bourget airport in France over the weekend, amid allegations about offences related to the service, according to AFP.

While Telegram says its CEO has "nothing to hide", French media reports suggest the billionaire executive remained in custody into Sunday as authorities investigate allegations of fraud, drug trafficking, organised crime, terrorism promotion and cyber-bullying related to the messaging platform. No formal charge sheet has yet been published
Kafanyaje?
 
Telegram abides by EU laws, including the Digital Services Act — its moderation is within industry standards and constantly improving," the company said in a statement.

Based in Dubai, Telegram Messenger is one of the top five most downloaded apps in the world, according to the company. In 2024, it passed 900 million monthly active users.

The Russian embassy in Paris issued a statement saying it had asked for clarifications about the arrest, but had not heard back from the French side.

Read more: Best UK mortgage deals of the week

The arrest has sparked an outcry online among proponents of privacy and encryption, with figures such as Tesla (TSLA) CEO Elon Musk coming out to support him. Musk posted a clip on X of Durov being interviewed with the text #FreePavel.

Meanwhile, the co-creator of cryptocurrency ethereum (ETH-USD) Vitalik Buterin wrote: "This looks very bad and worrying for the future of software and comms freedom in Europe."

Whistleblower Edward Snowden also said the arrest was "an assault on the basic human rights of speech and association."

He added: "I am surprised and deeply saddened that Macron has descended to the level of taking hostages as a means for gaining access to private communications. It lowers not only France, but the world."

The price of toncoin (TON11419-USD), the cryptocurrency associated with Telegram, which people can use as an in-app form of payment, dove about 13% following the news.
 
Wachezaji wapo zaidi ya 20 ukiweka na vijama wa Academy sasa huyu Trent ananuna nini wakati hizi sub zina manufaa kwa wote. Yeye atulie tuli Slot haangalii jina anataka mfumo ueleweke na utekelezwe bila bla bla...

Henderson, Salah, Milner, Mane hawa wote wakipewa sub enzi ya Klopp ilikua muda mwingine ni aibu maana wana react kama mwisho wa dunia...

Slot mapema asome hii picha ili kuwatuliza vichwa hawa wachezaji...

Nina imani na Slot.

YNWA
 
😝😝😝😝Yaani FSG na akina Gillett ni full vimeo aisee ni balaa sijui ni nuksi ipi ... Ipo hivi team ikiwa kwenye peak ndio wamiliki hua wanacheki vipaji na kuongezea nguvu wale waliopo klabuni , ukijiuliza kwa nini Barcelona, Real Madrid, Manchester City, Bayern nk hawachezi mbali na makombe ni kwa sababu wanajicho la vipaji kwa bei yoyote kusudi kuwe na continuity uwanjani.. Tulikua kwenye peak 2019 na 2020 yaani pale ilifaa FSG kuingia sokoni full throttle kusudi sasa kua kikosi kipana sana cha kutetea UCL na EPL lakini FSG walidhani miujiza ya Klopp inatosha kuleta ubingwa na mwishowe tupo hapa Klopp hoi kaona kisha nini kupata ma presha na Yankees akasepa na sasa ni Slot.

Bila uwekezaji kikosini ubingwa tutausikia kwa wengine...

Angalau naona kidogo Slot anaweza kubadili huu upepo japo sijui kama atapata huo muda. Nimeona ameanza kwa kuona kuna kesho bila Allison akichoka yafaa kuwe na mbadala wake na naona kipa wa Valencia wanasepa nae mazima dogo Giorgi Mamardashvili. Haya ndio kilio chetu kwamba mapema kuwe na like for like ili kua na kikosi cha kuleta ushindani mashindano tofauti...

Wangekua wana react mapema wale usingemuona Mjapan Liverpool 😀😀lakini kwa kua hua ni zima moto tegemea kuona akina Mjapan wengi wengi... I mean unauza aje injini ya timu Fabihno bila kua mbadala wake aisee...

Hao unaosema vipaji mmh dirisha nilo wameuzwa haswa tena kwa faida kubwa tu lakini kusajili ndio wanajifanya eti hakuna wachezaji wenye ubora zaidi ya tulionao yaani wanatuona kama hatuna macho...

Hivi dokta unaamini kabisa FSG wangetoa 110m+ kwa Caicedo, hii ni mbinu tu ya kibiashara kutuaminisha kwamba they tried lakin hakuna kilichowezekana🤣🤣hii ni moja ya mbinu FSG hutumia sana case study Valverde wa Real Madrid, Mbappe, Caicedo, nk nk...

YNWA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…