Haya, tuendeleee...
Awali ulisema Gerrard alitakiwa na timu zote kubwa za Ulaya (hapa naamini ulimaanisha Bayern Munchën, R. Madrid, Barcelona, Manchester United, Juventus, na AC Milan.
Lakini hapo juu umeweka links za timu mbili tu! Hiyo ya SAF, umeona mwenyewe anasema hakumwona SG kama top player wa kuweza kucheza nafasi za Keano na Scholesy, pamoja na SG kutamba Anfield..
Sasa, bado naomba links za timu nyingine na links zinazoonyesha kukataa kwa SG...
Pili, hivi unafahamu hata lineup ya Liverpool siku ile Instabul? Maana unauliza kama Alonso alifanya nini msimu wake wa kwanza? Doh! Alonso alikuja Liverpool msimu wa 2004/05, msimu Liverpool waliposhinda UCL, na yeye kufunga moja ya magoli. Pia, unasahau mchango wa Luis Garćia aliyefunga magoli ya muhimu dhidi ya Rentboys?
Check lineup ya UCL Final 2005
UEFA Champions League 2004/05 - History - Milan-Liverpool Lineups ? UEFA.com
Wewe jamaa ni mweupe sana, nasema tena...soma historia ya timu yako vizuri...
Hakuna anayebisha kuwa SG ni mchezaji mzuri sana, ila kwa talents, techniques na sophistications, atasubiri sana kwa Scholesy. Na ushahidi ni kuliliwa kwake na waingereza ili arudi national team iliyokuwa bado na kina SG na FL!
Nimekuuliza, umesikia waingereza wanamlilia SG arudi national team?