Loan Board mnatutesea Watoto. Jitahidini kwenda na muda

Loan Board mnatutesea Watoto. Jitahidini kwenda na muda

JF Member

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2014
Posts
7,914
Reaction score
10,793
Nashauri kama hari ndio hii basi vyuo visiwe vinafunguliwa hadi pale Loan Board inapokamilisha ugawaji wa mikopo na kuhakikisha kila anayestahili kupata amepata na kisha kutangaza kufunga dirisha la kupanga mikopo.

Wanafunzi wanateseka hawajapewa mikopo/accommodation huku masomo yameshaanza, yaani watoto wa masikini wako chuo hawajui watakula nini, wana tembea tembea tu na kuomba omba kwa watu. Mtoto ametoka Kigoma/Bukoba/Katavi/Mara/Songea kaja hapa Dar hajui anakula nini. Huu ni unyanyasaji.

Kuna wengine wameshindwa kutoka nyumbani kwenda vyuoni wakisubiri uhakika wa loan board iwapo itawapangia mikopo ama lah. Wengine wako radhi kuahirisha mwaka wasubiri Loan Board iwapangie mikopo.

Ushauri kwa Serikali: Databae ya wanafunzi wanaomaliza form six mnazo mapema kabisa. Fanyeni mpango muwape mikopo wote ama mshushe ada ili watoto wajilipie kama ilivyo kwa form six. Punguzeni ubaguzi kwenye Elimu.
 
Nashauri kama hari ndio hii basi vyuo visiwe vinafunguliwa hadi pale Loan Board inapokamilisha ugawaji wa mikopo na kuhakikisha kila anaestahili kupata amepata na kisha kutangaza kufunga dirisha la kupanga mikopo.

Wanafunzi wanateseka hawajapewa mikopo/accommodation huku masomo yameshaanza, yaani watoto wa masikini wako chuo hawajui watakula nini, wana tembea tembea tu na kuomba omba kwa watu. Mtoto ametoka Kigoma/Bukoba/Katavi/Mara/Songea kaja hapa Dar hajui anakula nini. Huu ni unyanyasaji.

Kuna wengine wameshindwa kutoka nyumbani kwenda vyuoni wakisubiri uhakika wa loan board iwapo itawapangia mikopo ama lah. Wengine wako radhi kuahirisha mwaka wasubiri Loan Board iwapangie mikopo.


Ushauri kwa Serikali: Databae ya wanafunzi wanao maliza form six mnazo mapema kabisa. Fanyeni mpango muwape mikopo wote ama mshushe Ada ili watoto wajilipie kama ilivyo kwa form six. Punguzeni ubaguzi kwenye Elimu.
Kutowapa wanafunzi mikopo kwa wakati na kuwapa kiduchu ambacho hakiwezi kukidhi gharama za chuo ikiwemo ada, accomodation na meal allowance inaonyesha serikali kuzidiwa na mzigo wa wanafunzi na hivyo basi ningeshauri utaratibu wa zamani wa kutoa ufadhili kwa wanafunzi waliodahiliwa kwenye vyuo vya umma urudi.
 
Kwa hiyo hujui kwamba moja ya jukumu la serikali ni kuwapa raia wake elimu, vilaza mnasumbua sana....
Nina watoto wanasoma chuo, high school, sekondari na msingi kwa gharama zangu. Naitegemea Serikali kwa ajili ya miundombinu ya elimu. Lakini kwa ajili ya karo, matumizi ya wanangu na mambo mengine, nahusika mwenyewe! Wewe ambaye sio kilaza endelea kuisubiria Serikali ikusaidie.
 
Nashauri kama hari ndio hii basi vyuo visiwe vinafunguliwa hadi pale Loan Board inapokamilisha ugawaji wa mikopo na kuhakikisha kila anaestahili kupata amepata na kisha kutangaza kufunga dirisha la kupanga mikopo.

Wanafunzi wanateseka hawajapewa mikopo/accommodation huku masomo yameshaanza, yaani watoto wa masikini wako chuo hawajui watakula nini, wana tembea tembea tu na kuomba omba kwa watu. Mtoto ametoka Kigoma/Bukoba/Katavi/Mara/Songea kaja hapa Dar hajui anakula nini. Huu ni unyanyasaji.

Kuna wengine wameshindwa kutoka nyumbani kwenda vyuoni wakisubiri uhakika wa loan board iwapo itawapangia mikopo ama lah. Wengine wako radhi kuahirisha mwaka wasubiri Loan Board iwapangie mikopo.


Ushauri kwa Serikali: Databae ya wanafunzi wanao maliza form six mnazo mapema kabisa. Fanyeni mpango muwape mikopo wote ama mshushe Ada ili watoto wajilipie kama ilivyo kwa form six. Punguzeni ubaguzi kwenye Elimu.
Nasikia safarii wamelamba 30% zakutosha! Alafu wanatuambia imetolewa mikopo mara 2 ya awamu ya 5.
 
Nina watoto wanasoma chuo, high school, sekondari na msingi kwa gharama zangu. Naitegemea Serikali kwa ajili ya miundombinu ya elimu. Lakini kwa ajili ya karo, matumizi ya wanangu na mambo mengine, nahusika mwenyewe! Wewe ambaye sio kilaza endelea kuisubiria Serikali ikusaidie.
Kwa hiyo serikali isifanye wajibu wake kwa kuwa unavyo vijisenti vya kusomesha wanao! kwa nini unafikiria kwamba kila mtu anao uwezo kama ulio nao wewe, unazidi kuthibitisha ukilaza mkuu bora upige kimya...
 
Unazaa watoto ili baadae uilalamikie Serikali eti haijawasomesha? Huu ujinga utaisha lini k wa Watanzania?
Mpumbavu Mkubwa Wewe....!!! Kama Wewe umebarikiwa kuwa na chochote Usiwadhihaki Wasiokuwa nacho...!! Hiyo ni Mikopo Siyo Bure..!! Pia wasiotegemea Mikopo wapo na Wapo Kimya Maana Walijiandaa. Tumia Akili Siyo Makamasi
 
Kwa hiyo serikali isifanye wajibu wake kwa kuwa unavyo vijisenti vya kusomesha wanao! kwa nini unafikiria kwamba kila mtu anao uwezo kama ulio nao wewe, unazidi kuthibitisha ukilaza mkuu bora upige kimya...
Kuna madaraja ya watu. Maskini wanaohitaji kweli msaada wa Serikali. Kuna wenye uwezo wa kuchangia kiasi na Serikali ikachangia kiasi na wa mwisho ni walio na uwezo kuwalipia watoto wao bila kuhitaji msaada wa Serikali. Tatizo letu Watanzania hatupendi kujipambanua. Tunapenda dezo. Hapa Jijini Mwanza, niliishawahi kuona familia ipo chini ya Mpango wa Kusaidia Kaya Maskini unaosimamiwa na TASAF wamekuja na gari binafsi ya familia kuchukua fedha za kujikimu na umaskini. Wewe ni miongoni mwao?
 
Mpumbavu Mkubwa Wewe....!!! Kama Wewe umebarikiwa kuwa na chochote Usiwadhihaki Wasiokuwa nacho...!! Hiyo ni Mikopo Siyo Bure..!! Pia wasiotegemea Mikopo wapo na Wapo Kimya Maana Walijiandaa. Tumia Akili Siyo Makamasi
Mimi wakati nasoma nilichukua mkopo wa asilimia 40%. Zingine nikawa nabangaiza (nafanya umachinga) mtaani. Sasa hivi nina miaka minne nimemaliza mkopo, lakini waliokuwa wanapambana kupata asilimia 80% au 100% bado wanapambana kumaliza deni na malalamiko kibao! Tujifunze kujibana na sio kulalamikalalamika tu!
 
Kuna madaraja ya watu. Maskini wanaohitaji kweli msaada wa Serikali. Kuna wenye uwezo wa kuchangia kiasi na Serikali ikachangia kiasi na wa mwisho ni walio na uwezo kuwalipia watoto wao bila kuhitaji msaada wa Serikali. Tatizo letu Watanzania hatupendi kujipambanua. Tunapenda dezo. Hapa Jijini Mwanza, niliishawahi kuona familia ipo chini ya Mpango wa Kusaidia Kaya Maskini unaosimamiwa na TASAF wamekuja na gari binafsi ya familia kuchukua fedha za kujikimu na umaskini. Wewe ni miongoni mwao?
Mzee tulia basi, serikali inapotimiza wajibu wa kuelimisha watu haiangalii unatokea familia ya aina gani.......kuna nchi hadi ngazi ya chuo kikuu elimu ni bure, labda mzee tukuulize kwa nini unafikiri serikali inapata hasara kwa kutoa pesa za kusomesha wanafunzi, maana inaonekana zinakuuma sana.....
 
Kuna dogo karudisha mpira kwa kipa (karudi home) huku (ngoreme)
 
Mzee tulia basi, serikali inapotimiza wajibu wa kuelimisha watu haiangalii unatokea familia ya aina gani.......kuna nchi hadi ngazi ya chuo kikuu elimu ni bure, labda mzee tukuulize kwa nini unafikiri serikali inapata hasara kwa kutoa pesa za kusomesha wanafunzi, maana inaonekana zinakuuma sana.....
Ninachojaribu kuwaambia hapa ni kwamba, kama Watanzania tutajitambua basi wale watoto ambao kweli wanahitaji msaada wa mikopo wataipata ya kutosha kabisa!!

Ila mikopo haitoshelezi kwasababu ya tamaa ta baadhi ya Watanzania wenzetu. Kama una uwezo wa kumsomesha mwanao kwanini ung'ang'anie mikopo ya Serikali na kuwafanya wenye uhitaji wa kweli kukosa?

Nimalizie kwa kukwambia Dogo ya kwamba, mimi nitauza hata parachichi maadam nguvu ninazo ili kisomesha wanangu na hela ambayo wangepata wao wapewe wengine wenye uhitaji wa kweli. Kama umenielewa, natanguliza shukrani!
 
Back
Top Bottom