Local Transport Card: Hii itumike nchini pekee

Local Transport Card: Hii itumike nchini pekee

Nyongeza hapa mkuu. Matumizi ya NFC cards. Simu janja kibao sasahivi zina support NFC ilikuwa ni jambo rahisi sana kubeba card ni ishu za kizamani sana dunia iko kiganjani ulipo simu yako ipo na wewe ni kiasi cha kutengeneza app ya malipo iwe na IOS na android app. Plus POS zake, raia tuna download app tuna weka hela kwenye wallet za hii Local Payment App ina kuwa mwendo wa kutap simu zetu kwenye POS za watoa huduma kama daladala, mwendokasi, dukani etc. Hii inge punguza kasi sana, currently nilikuwa na pambana ku intergrate N card kwenye simu ili fail kz IOS zina issue dynamic keys while Ncard ni static hii ingekubali means card ya Ncard ningeacha tumia ningebaki na punch kwa kutumia simu yangu tu. Hii ingeleta mapinduzi makubwa sana kwenye cashless society kz karibu kila mtu sasa ana tumia android phone.
Achana na mambo ya kutumia simu kufanya malipo. Yaani malipo yote yanayohusu Usafiri wa Umma yawe kwa njia ya CARD tu. Mtoa huduma yeye anapaswa kuwa na kifaa cha kuscan ambacho hakiitaji INTERNET.
 
Lile Nyomi la Gongo la Mboto ndio uende na kadi yako?

Na kwa nchi hii iliyojaa ghilba na utapeli, wenye madaladala binafsi wanaweza jikuta wanadai pesa zao mpaka wasage meno.

Serikali ya nchi hii kwa kukwapua pesa za taasisi hasa kipindi cha campaign, itaenda kukwapua hizo pesa zote kutoka huko huko zinakupitia kama ni bank ama kwenye simu.
Tukubaliane tu. Hii itaondoa hizo changamoto. Unajua wawekezaji wanashindwa kuwekeza hususani sekta ya Usafiri wa umma sababu hakuna Data zinazoeleweka na kuaminika.

Kwa kupitia LTC (Local Transport Card) itavutiwa wawekezaji kwa uzuri na usawa.
 
Wataweza tu. Unajua mwanzo huwa mgumu.
Swali jepesi, unaweza vipi kufanya mawasiliano kwa njia ya simu pasipo Simu Card na Simu Kifaa. Hii ndio kitatakiwa kiwapate hao maafisa Usafirishaji.
Ninakutakia kila la kheri.
 
Wizara ya Uchukuzi ni lini sasa mtaanza huu mchakato wa kupunguza kero za usafiri kwa Umma hapa nchini!?
 
Hii ndio Tanzania, amani iwe nanyi !

Napendekeza tuwe na kitu kinachoitwa "LOCAL TRANSPORT CARD". Hii iwe kadi maalumu itakayo jazwa pesa kupitia mifumo ya kifedha ya hapa hapa nchini (Local Banks, Mpesa, Tigo Pesa, Z-pesa, Airtel Money Halopesa nk) na kutumika kwake iwe kwa scan pekee katika kutoa pesa kwenda kwenye vyombo husika (Magari au Kampuni ya Usafiri wa Umma).

Hii kadi (LTC) itumike katika vyombo vyote vya Usafiri wa Umma hapa nchini kuanzia Bodaboda, Bajaji, Daladala na Mabasi ya Mikoani.

1. Kwa kupitia njia hii itapunguza sana usumbufu katika usafiri wa Umma kuanzia Bodaboda, Bajaji, Daladala, Mabasi ya kwenda mikoani.

2. Tutakuwa tumeondoa kabisa changamoto ya usumbufu kwa mwananchi kutembea na fedha nyingi atakapo kusafiri.

3. Tutaimarisha Usalama wa nchi kwa Serikali, Abiria na Wamiliki wa vyombo vya Usafiri.

4. TRA mtakusanya mapato yenu kwa njia rahisi sana sambamba na nyie halmashauri husika mliopo maeneo husika.

5. Tutakuwa watu waliostaarabika, tutalindana utu wetu na tutajipatia maendeleo kwa haraka.

NB

Local Transport Card (LTC) ni njia salama na sahihi kwa usafiri wa umma hapa nchini.
(Pia kwa kutumia tu mfano; Ikapendekezwa Tsh.10,000/= iwekwe kama kifungua akaunti na fedha hii haitarudishwa kabisa na abiria anapaswa awe na akiba isiyopungua kiasi flani kwenye akaunti yake ya kadi; kwa idadi ya watu milioni 40, unahisi sekta ya usafiri itajikusanyia mapato kiasi gani?, tuchukue hatua.)

Cc
TRA
LATRA
National Institute of Transport (NIT)
Dar es Salaam Institute of Technology (DIT)
Wizara ya Uchukuzi
TAMISEMI
Ofisi ya Waziri Mkuu
Ofisi ya Raisi

Karibu.
Hii tutafanikiwa kwa usahihi kama tutakuwa tunaipenda nchi yetu na tunaiwazia mema usiku na mchana.
Asante.
 
Hii ndio Tanzania, amani iwe nanyi !

Napendekeza tuwe na kitu kinachoitwa "LOCAL TRANSPORT CARD". Hii iwe kadi maalumu itakayo jazwa pesa kupitia mifumo ya kifedha ya hapa hapa nchini (Local Banks, Mpesa, Tigo Pesa, Z-pesa, Airtel Money Halopesa nk) na kutumika kwake iwe kwa scan pekee katika kutoa pesa kwenda kwenye vyombo husika (Magari au Kampuni ya Usafiri wa Umma).

Hii kadi (LTC) itumike katika vyombo vyote vya Usafiri wa Umma hapa nchini kuanzia Bodaboda, Bajaji, Daladala na Mabasi ya Mikoani.

1. Kwa kupitia njia hii itapunguza sana usumbufu katika usafiri wa Umma kuanzia Bodaboda, Bajaji, Daladala, Mabasi ya kwenda mikoani.

2. Tutakuwa tumeondoa kabisa changamoto ya usumbufu kwa mwananchi kutembea na fedha nyingi atakapo kusafiri.

3. Tutaimarisha Usalama wa nchi kwa Serikali, Abiria na Wamiliki wa vyombo vya Usafiri.

4. TRA mtakusanya mapato yenu kwa njia rahisi sana sambamba na nyie halmashauri husika mliopo maeneo husika.

5. Tutakuwa watu waliostaarabika, tutalindana utu wetu na tutajipatia maendeleo kwa haraka.

NB

Local Transport Card (LTC) ni njia salama na sahihi kwa usafiri wa umma hapa nchini.
(Pia kwa kutumia tu mfano; Ikapendekezwa Tsh.10,000/= iwekwe kama kifungua akaunti na fedha hii haitarudishwa kabisa na abiria anapaswa awe na akiba isiyopungua kiasi flani kwenye akaunti yake ya kadi; kwa idadi ya watu milioni 40, unahisi sekta ya usafiri itajikusanyia mapato kiasi gani?, tuchukue hatua.)

Cc
TRA
LATRA
National Institute of Transport (NIT)
Dar es Salaam Institute of Technology (DIT)
Wizara ya Uchukuzi
TAMISEMI
Ofisi ya Waziri Mkuu
Ofisi ya Raisi

Karibu.
Ni wazo zuri sana ila Napendekeza huo mfumo usitengenezwe na wazawa na wala usisimamiwe na wazawa mifumo mingi iliyo tengenezwa na wazawa ni kichefuchefu sana katika ufanisi wake

Unaweza kukuta mnapanga foleni masa mawili ku swap kadi kwenye mashine na mtandao unasumbua
 
Back
Top Bottom