Lonely Me...... Nimefiwa na baba yangu

Lonely Me...... Nimefiwa na baba yangu

Pole Bujibuji kwa kupoteza mzazi...mungu ailaze roho yake mahali pema peponi
 
Bujibuji, ilinipita hii niungane na wapwaz na binamz wote kukupa pole na pia kukuombea kwa Mungu akuvushe kataika wakati huu mgumu wa majonzi
 
tumeumbwa kwa udongo, mavumbini tutarudi, pole sana mpendwa
 
Wenzangu wana JF, nasikitika kuwajulisha kuwa nimefiwa na baba yangu mdogo, ambaye tulikuwa tumeshibana naye sana, na alikuwa ndiye baba yangu pekee aliyenijali na kunitunza tangu alipofariki baba yangu mzazi.
Nimeachwa mpweke sana, na kesho natarajia kwenda Usukumani kwa ajili ya maziko.
Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu.

Mkuu bujibuji Pole sana, imeniuma utadhani ni mimi, japo niliachwa na wazazi wangu wote wawili ningali mdogo. La msingi mtumaini Mungu siku zote, hasa katika kipindi hiki kigumu cha majonzi. Mungu akutie nguvu na akuwezeshe.
 
Pole na safari njema ufike salama huko usukumani
 
Mungu awatangulie, safarini kwenda usukumani, pole sana Bujibuji.
 
Pole sana mkuu hiyo inatukumbusha sisi pia kujiandaa kwani dote tutarudi kwa muumba uwe na moyo mkuu
 
Mkuu BujiBuji, pole sana.Mungu akupe nguvu za kuhimili kipindi hiki. Daima kila mwanadamu atapitia hiyo hatua.
 
pole sana,tuko na niaba!mungu amrehemu baba mdogo
 
Wenzangu wana JF, nasikitika kuwajulisha kuwa nimefiwa na baba yangu mdogo, ambaye tulikuwa tumeshibana naye sana, na alikuwa ndiye baba yangu pekee aliyenijali na kunitunza tangu alipofariki baba yangu mzazi.
Nimeachwa mpweke sana, na kesho natarajia kwenda Usukumani kwa ajili ya maziko.
Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu.

Pole sana Buji
 
Pole sana bujibuji, mungu awatie nguvu wafiwa wakati huu mgumu, tuko pamoja mkuu!
 
Back
Top Bottom