Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

nec 2.jpg

Kalamu yangu nashika, shairi nakutungia
Kamanda umeongea, kiwingu umeondoa
Hukutaka kusinzia,makosa kuyarudia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Mwananchi nimesoma, la jana nilinunua
Machoya yakatuama, dukuduku umetoa
Uliyosema Dodoma, Kwakweli yanavutia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Richmond kupasua, mapema uligundua
Kikwete ukamwambia, mkataba kuondoa
Rais akakataa, nini alitegemea?
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Nape akashikilia, lile asilolijua
Mikoani kaambaa, uzushi kang'ang'ania
Jinalo kulichafua, wewe ukavumilia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Mapema nilitabiri, falsafa nikapinga
Magamba sikukariri, kuvuana sikuunga
Ukweli niliukiri, mantiki iso kunga
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Beti sita nakomea, kalamu naweka chini
Mengi nimeongelea, soma tena kwa makini
Yatazidi kutokea,kusini kaskazini
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa.

Shairi limetungwa na Nova Kambota Mwanaharakati,
+255717 709618
novakambota@gmail.com
www.novakambota.com
Tanzania, East Africa
Jumamosi, November 26, 2011

 
Big up Nova. You took back to old school primariiii kwa mwalimu mkuu wakati wa saba saba nk
 
Lowassa na ujanja wake wote eti nae bila ajizi aliamini na kuandika barua ya “kuigiza” kujiuzuru na kisha akaondoka kurudi Dodoma mjini usiku ule. [/QUOTE]

Unajua nini? Wote ni wajanja, lakini kuna tofauti kubwa sana kati ya mjanja aliekulia Monduli na mjanja aliyekulia Magomeni!!!

Dah!Nimecheka sana kuhusu hao wajanja na sehemu walikokulia
 
Kwa wale wanaoshangilia "ushindi" wa lowassa baada ya suala lake la kuvuliwa gamba pamoja na suala la Nape na chiligati anaowalalamikia kuzunguka nchi nzima "kumchafua" kutinga mikononi mwa kamati kuu,leo nataka kuwakumbusha kidogo kuhusu Jakaya ili huku mkifurahia "ushindi" pia mumfahamu sawa sawa muungwana jakaya ni mtu wa dizaini gani,sina lengo la kutia mchanga kwenye kitumbua chenu cha furaha la hasha ila nataka tukumbushane muijua siasa pia.Wandugu wapendwa mnajua ilikuwaje mpaka Lowassa akawa sio waziri mkuu.....

Kiufupi ni Kwamba Lowassa aliingizwa choo cha stendi na Jakaya!
Lowassa aliutema uwaziri mkuu anaoupenda mpaka leo kutokana na "utoto wa mjini" utapeli wa kisiasa wa Rais Kikwete kwa swahiba wake Lowassa, wala haikua "ajali ya kisiasa".

Mpango mzima ulikua hivi:

Bunge kupitia Kamati Teule ilisoma ripoti yake kupitia mwenyekiti wake, Dk. Harrison Mwakyembe. Hali ilikuwa tete Dodoma na hata Chamwino ambako Rais Kikwete alikuwa amejichimbia.
Baada ya kusomwa kwa ripoti, taarifa zinasema Lowassa alikwenda Chamwino kuonana na bosi wake ili kupanga mkakati wa kuzima maasi ya wabunge wa CCM waliokuwa wamesisimka ili kummaliza Lowassa, rais Kikwete na serikali yao.
Katika mazungumzo yao usiku ule, Rais Kikwete na swahiba wake huyo wa zamani; – Lowassa akapendekeza eti jk aende upesi kukutana na wabunge wa CCM ili kuwaonya wasiiangushe serikali yao, Jk baada ya "kupima" akastuka.
Ndipo yeye akaja na maarifa ya kimjini kwa kumwambia Lowassa aandike barua ya kujiuzuru, halafu yeye jk aicheleweshe kuijibu hiyo barua kwa makusudi mpaka Bunge lihairishwe ili kumpa nafasi yeye jk kama rais kuonana na wabunge wa CCM ili kuzima maasi ya wabunge kabla ya mkutano mwingine wa Buge wa Aprili haujafanyika Dodoma.
Lowassa na ujanja wake wote eti nae bila ajizi aliamini na kuandika barua ya "kuigiza" kujiuzuru na kisha akaondoka kurudi Dodoma mjini usiku ule. Yaliyotokea Chamwino baada ya Lowassa kuondoka inabakia kuwa siri ya Kikwete mwenyewe na aliokutana nao. Usiku wa manane wa siku hiyo, Rais Kikwete aliamua kuwa barua ile ijibiwe na kukubaliwa. Ni kinyume na makubaliano yake ya awali na Lowassa!

Sasa leo tena suala la lowassa baada ya kupata kibali cha NEC liko mikononi mwa kamati kuu ambamo lowassa hayumo!Na watu wake eti wanashangilia "ushindi" wa ice cream iliyowekwa juani huku jakaya akiwa tayari amejeruhiwa na kutajwa kwenye sakata la richmond na pia ikikumbukwa Jakaya hana tena cha kupoteza kwa kuwa hawezi tena kuwa rais!mi nawaomba msiwe wajinga kama jamaa yenu kwa mujibu wa mwalimi nyerere ambae alifahamu ujinga wake zamani kabla kabla ya jk kuja kuthibitisha kwa kumuingiza choo cha stendi!!!!!!!!!!!!!!!!!!



Acha hadithi za kutunga ww, kama barua ya kujiuzulu ilikubaliwa usiku wa manane, mbona hautuelezi nini kilimfanya EL kutangaza bungeni asubuhi yake kujiuzulu, na barua hiyo ya kukubaliwa EL kujiuzulu alipewa nani wakati hata spika wa kipindi hicho amewahi kukuaririwa akisema kujiuzulu kwa EL ndilo jambo lililomshtua mno kipindi cha uongozi wake- Hizi hadithi zenu za kutunga pelekeni huko vijiweni kwenu!!!
 
Mi siwaelewi kwahiyo mnataka kusema rais wa 2015 ni Lowassa na si DK Slaa tena??? Au tunaongelea wagombea tu

Tunaongelea rais! tumekuacha wapi mkuu?! ingawaje ni ngumu kumeza, inabidi ukubali hivyohivyo!!!! ukishindwa, fanya kama nilivyofanya mwenzio, hapa nilipo nina azam cola pembeni, kwa issue ngumu kumezeka kama hizo nashushia na hiyo ki2!!!
 
maumivu ya kichwa huanza pole poleeeee,mi napita zangu naelekea mmu,karibuni waungwana.
 
Nadhani tatizo la nchi yetu lipo kwenye kichwa. Na siyo kwenye vidole at sehemu nyingine
 
Watu kwa kucheza na maneno ni mahodari sana, hivi Lowassa kasema nini kuhusu Richmond zaidi ya kusema alimpigia simu Kikwete alipokuwa nje ya nchi akamwambia asubiri ushauri wa makatibu wakuu.

Hapo ndiyo Lowassa kasema Richmond ya Kikwete au ina husiana na Kikwete? Mnanshangaza!
 
Heee kumbe waberoya nae kaingia kichwa kichwa kuamini lowassa kweli amepona kuvuliwa gamba?!!basi watu yaelekea huwa hamfuatilii mambo!wabaya wote wa lowassa walikuwa wanaomba usiku kucha suala la kujivua gamba baada ya kushindikana kwa hiyari liachiwe kamati kuu lakini baada ya kupata kibali cha nec!sasa hapo nani mshindi mnavyodhani??wabaya wa lowassa ama lowassa??maana kibali kimeshatoka na watu mnajifanya mmesahau hiyo badala yake mmekazania kulia lia kwa lowassa ili jumba bovu lisimuangukie peke yake!haitasaidia alitakiwa azicheze karata zake vizuri suala hilo lizimwe kwa nec kugoma kutoa kibali,kachemsha kampa rungu mwenyekiti atambe na kamati kuu yake anayoimudu vyema!

Mkuu hujaelewa falsafa yangu

falsafa yangu CCM wote ni wezi.....nani wa kumvua gamba mwenzake?

Lowasa anapoweka wazi wizi wao yeye na rais wake ni chereko na furaha kwa wananchi...lakini ukitake side between Lowasa na Kikwete inaleta logic?? wote wezi "kuvua gamba" ni falsafa na maneno yaliyowekwa kukupumbaza wewe! RA si alijiuzulu, aliyemweka mbunge wa CCM Igunga ni nani? hawa wote wezi huwa tunawashangaa mnaposema EL fisadi na JK msafi,...au huyu ajivue gamba na yule aisjivue...Nape juzi amesemaje?? na wewe leo unasemaje??

EL anasema wezi wote wamefunguliwa mashtaka..yy kwa nini hajafunguliwa mashtaka?? hauoni tusi kwako wewe, CCM na serikali yako?? guys think ebo!
 
Mwenyekiti wa kamati ya maadili ni CHENGE au alishaondolewa??

Bado yupo, na kwa sasa anaandaa dodoso a.k.a questionaire kwa ajili ya watuhumiwa wa pande zote mbili-upande wa akina Nape na upande wa akina EL! Moja ya maswali yaliyopo kwenye dodoso hilo kwa upande wa akina EL ni:
Qn:1. Mheshimwa Waziri Mkuu Mstaafu, eti kweli inawezekana mtu kama wewe mweneye utumishi uliotukuka inawezekana kweli ukawa fisadi?! I can't believe it at all; is it true?
Instruction to answer this question is YES or NO!

Qn:2. Mr. Honarable Excellence Unquestinable Lawyer Ndugu Andrew Chenge; is it possible kweli kwa m2 kama mimi nisiwe na tujisent kama tule nje ya nchi wakati nina tung'ombe zaidi ya laki moja?

Instructions to answer: Strictly, my answer should be POSSIBLE or IMPOSSIBLE., over!

Na dodoso kwa Nape na wenzake!
Wewe nape a.k.a Vuvuzela mwenye roho ya korosho, roho mbaya mwenye kijicho na roho ya kwanini, kv tu babako alikufa maskini; Briefly, explain with vivid and strictly strong and unquestionable evidence approved by undoubtful lawyers, as to why u should not be fired from the part u fail u to submit the demanded evidence?!
 
Lowasa hana makosa, hakutendewa haki hata kidogo. Tuishi kwa kumuogopa Mungu, kama kuna kundi linapanga njama chafu mbele ya kiumbe cha Mungu kisicho na makosa, basi subiri uuone jinsi ukweli utakavyojitenga na uwongo. Nuru na giza havitakaa pamoja hata siku moja. Lowasa atashinda kwa hili nina hakika 110%
Mi nakuunga mkono ccm wasipo msimamisha lowasa inakula kwao
 
Sio kila mtu ana bei. Kama nyie mnauzika shauri lenu, msitusemee sisi.

Unafikiri issue ni kuuzika basi, issue ni kununulika! Unaweza usiuzike lakini ukanunulika! Tusiyemtaka waungwana sio asiyeuzika, bali asiyenunulika na kumweka kwenye kapu lako! Ukishakuwa waziri, say wa nishati na madini.; tayari unauzika kwa gharama yoyote ile.....sasa tunachotaka ni yule asiyenunulika kwa gharama yoyote ile!!!
 
Acha hadithi za kutunga ww, kama barua ya kujiuzulu ilikubaliwa usiku wa manane, mbona hautuelezi nini kilimfanya EL kutangaza bungeni asubuhi yake kujiuzulu, na barua hiyo ya kukubaliwa EL kujiuzulu alipewa nani wakati hata spika wa kipindi hicho amewahi kukuaririwa akisema kujiuzulu kwa EL ndilo jambo lililomshtua mno kipindi cha uongozi wake- Hizi hadithi zenu za kutunga pelekeni huko vijiweni kwenu!!!

dah mkuu kwan EL asubuhi ili alitangaza kujiuzulu?kwa kumbukumbu zangu MH EL alitangaza kuwa amesikitiswa sana ameonewa sana na amegundua kuwa wish ya kugrant ni UPM kwa hiyo MEMWANDIKIA BARUA YA KUJIZULU MH RAIS,naye ndo alikuwa anasubiriwa aridhie ua vinginevyo.vyanyuma ya pazia ndo hivyo vinavyosemwa mkuu
 
kwani Lowasa akitoswa kitatokea nini CCM zaidi ya majeraha kwa mwenyekiti
 
Inategemea, nyati kajeruhiwa na nani/na nini?, nionavyo mimi nyati kakeruhiwa na muwindaji hodari mwenye siraha nzito- bora nyati akimbie akafie mbali kuliko kujaribu kulipiza. Itakula kwake.
kwa hali ilivyo tete sasa na kwa mujibu wa mleta mada ni kuwa jk kajeruhiwa kweli. Na huyu jamaa akijeruhiwa huwa mbaya kuliko nyati. Lolote laweza tokea
 
Back
Top Bottom