Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

Mkuu THE ROMANTIC,

Stori yako haina ukweli wowote kwa kuangalia mtiririko wa matukio yenyewe mpaka Lowassa alipotangaza Bungeni kwamba amemwandikia barua Rais ya kuomba kuachia ngazi halafu pia kuna matatizo ya kikatiba, na hayo yote lazima yalikuwa yanajulikana kwa wote.

Mosi, Kwa kuwa Ripoti ilishasomwa Bungeni tayari, hakukuwa na uwezekano wa kutojadiliwa mpaka Bunge liahirishwe. Kwa hiyo hoja yako kwamba EL angeandika barua ya kuomba kujiuzulu then JK achelewe kuijibu, isingezuwia Bunge kuendelea na mjadala wa Ripoti. Kama JK alitaka kuizima hiyo ripoti basi lazima angewaita wabunge wa CCM hata kabla Bunge halijaanza ili kuweka mambo sawa na huo umekuwa ni utaratibu wao.

Pili, JK asingekuwa mjinga akubali kwamba Lowassa akatangaze Bungeni kwamba ameamua kujiuzulu halafu JK aje kumkatalia, ingewafanya wananchi wawe na mtazamo hasi kwa Rais wao.

Tatu, Waziri Mkuu akitangaza kujiuzulu, maana yake ni kwamba Baraza la Mawaziri linakuwa limevunjwa mpaka Waziri Mkuu Mpya atakapoteuliwa na kupitishwa na Bunge then ndipo Waziri Mkuu ashirikiane na Rais katika kuteua Mawaziri/Naibu Waziri. Hilo pekee linafanya shughuli za serikali Bungeni zisimame kwa muda mpaka Baraza la Mawaziri litakapoteuliwa na kuapishwa.

Kwa hiyo the whole stori haina mashiko.
 
Upuuzi tupu wanapigania matumbo yao na kulinda ufisadi wao, hawajaongea lolote kwa maslahi ya nchi na watanzania
 
Too early to conclude mkuu..

Siku hata wiki inaweza kubadili upepo wa siasa mbaya kabisa..sembuse 3 yrs

Na upepo ndio unamwelekea EL ile mbaya, yaani vuuuuuuuhh...!!! Kichama, makanisa, wenye fedha, watu binafsi, na zaidi zaidiii ww ni mtu mzima SOMA MEDIA HASA MAGAZETI, ALMOST YOTE YANAMWELEKEA EL KWA UZURI NA KUMPENDA, EL nomaaa
 
Ya kanu-kenya na Unip -zambia,
sasa yanatimia kwa Ccm -tanzania.

Sasa ccm ijipongeze kwa kuishi angalau kidogo zaidi ya mwasisi wake mzee wetu mpendwa Nyerere.
It cant leave longer.
It is over for ccm.
Time for change, it is inevitable.
It is all about history.
It is over now ccm, it is over , just take the last gulp of water and drop dead!
 
Ukituhumiwa au kuzungumzwa vibaya ..kipo chanzo... sasa tunapiga hatua moja mbele na kurudi tatu nyuma... Mzee Mkono aliifisadi BOT..mpaka Govana Ndullu aipoingia..leo ndo shahidi wa EL..Kweli?

Vimemo vya Richmond alivyovitaja Dr. Msabaha.. Uswahiba wake na Rostam Aziz uko kwenye uwanja gani? Na Je Maneno ya Mwal. juu ya EL.. "kijana mdogo - utajiri huu umeupata wapi?"

Tetesi ya mtoto wa EL kununua jumba UK -baba yuko safi?... Kweli EL alikuwa mchapa kazi lakini kuna maswali mengi juu ya uadilifu yake ambayo yako kizani na nadhani kwa jinsi alivyojiuzulu kwa kulinda heshima ya nchi alipaswa kujisafisha wakati ule ule na siio miaka kadhaa baadaye ambapo kuna machungu zaidi juu ya hali ya afya ya Dr. Mwakyembe inayosemekana ni matokeo ya mikono ya mafisadi!!!!
 
Lowassa angewajibu kamati ya Mwakyembe bungeni, au angewapeleka mahakamani, WaTanzania sio Mabwege tena, Suala la umeme lilikuwa la dharura iliyosimamiwa na Waziri Mkuu Mwenyewe sio Wasaidizi wake!

Pesa za Richmond zilibiwa kwa kutumia Sheria, So ni Sheria tu ndio inaweza kumsafisha Lowassa sio vikao vya chama. Kwa kusema kwake kwamba Wapinzani hawamsemi, anasema kwamba ameshawagawia mgawo or What? LOWASSA WATANZANIA WOTE SIO MABWEGE TENA!
 
Tukisema tuna kundi la mafisadi tutakuw tumekosea?
 
Kalamu yangu nashika, shairi nakutungia
Kamanda umeongea, kiwingu umeondoa
Hukutaka kusinzia,makosa kuyarudia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Mwananchi nimesoma, la jana nilinunua
Machoya yakatuama, dukuduku umetoa
Uliyosema Dodoma, Kwakweli yanavutia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Richmond kupasua, mapema uligundua
Kikwete ukamwambia, mkataba kuondoa
Rais akakataa, nini alitegemea?
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Nape akashikilia, lile asilolijua
Mikoani kaambaa, uzushi kang'ang'ania
Jinalo kulichafua, wewe ukavumilia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Mapema nilitabiri, falsafa nikapinga
Magamba sikukariri, kuvuana sikuunga
Ukweli niliukiri, mantiki iso kunga
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa

Beti sita nakomea, kalamu naweka chini
Mengi nimeongelea, soma tena kwa makini
Yatazidi kutokea,kusini kaskazini
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa.

Shairi limetungwa na Nova Kambota Mwanaharakati,
+255717 709618
novakambota@gmail.com
www.novakambota.com
Tanzania, East Africa
Jumamosi, November 26, 2011

Source: MJENGWA BLOG
 
Lowassa ame-prove kuwa hakuna msafi ndani ya uongozi wa CCM; kila mmoja ana gamba lake, wengine wana makubwa na wengine wana madogo tu. Ingawa hatujuia kulikuwa na nini ndani ya mafaili ya Paul Sozigwa kuhusu Kikwete, kutokana na maadili ya Mzee sozigwa nina imani kuwa yalikuwa sahihi na kwa kitendo cha Mkapa kumtetea Kikwete mwaka huo 1997 basi aliimarisha uongozi usiowajibika ndani ya CCM.
 
Lowassa angewajibu kamati ya Mwakyembe bungeni, au angewapeleka mahakamani, WaTanzania sio Mabwege tena, Suala la umeme lilikuwa la dharura iliyosimamiwa na Waziri Mkuu Mwenyewe sio Wasaidizi wake! Pesa za Richmond zilibiwa kwa kutumia Sheria, So ni Sheria tu ndio inaweza kumsafisha Lowassa sio vikao vya chama. Kwa kusema kwake kwamba Wapinzani hawamsemi, anasema kwamba ameshawagawia mgawo or What? LOWASSA WATANZANIA WOTE SIO MABWEGE TENA!

Njia pekee ya JK kukisafisha chama ni kuacha uchaguzi wa 2015 uwe huru na haki. Kusiwe na chakachua wala scramble of voters register. CCM ikiwa nje ya madaraka japo kwa miaka miatano tu kupe wote watapukutika na kukiacha chama kikiwa safi kabisa. As long as CCM imeshikilia mshipa wa aorta wa Tabzania na kujinyoyea taratiibu ni dhahiri kupe hawataisha as long as blood is still flowing towards their mouths.
 
Lowassa angewajibu kamati ya Mwakyembe bungeni, au angewapeleka mahakamani, WaTanzania sio Mabwege tena, Suala la umeme lilikuwa la dharura iliyosimamiwa na Waziri Mkuu Mwenyewe sio Wasaidizi wake! Pesa za Richmond zilibiwa kwa kutumia Sheria, So ni Sheria tu ndio inaweza kumsafisha Lowassa sio vikao vya chama. Kwa kusema kwake kwamba Wapinzani hawamsemi, anasema kwamba ameshawagawia mgawo or What? LOWASSA WATANZANIA WOTE SIO MABWEGE TENA!
Mbona aliunguruma kwenye kikao cha magamba?

Hii ina maana he will never be held accountable under magamba.

Umeona alivyochezewa mchezo Nape?

Huo ni upande wa magamba.
 
kalamu yangu nashika, shairi nakutungia
kamanda umeongea, kiwingu umeondoa
hukutaka kusinzia,makosa kuyarudia
jibu umetupatia, viva kamanda lowassa

mwananchi nimesoma, la jana nilinunua
machoya yakatuama, dukuduku umetoa
uliyosema dodoma, kwakweli yanavutia
jibu umetupatia, viva kamanda lowassa

richmond kupasua, mapema uligundua
kikwete ukamwambia, mkataba kuondoa
rais akakataa, nini alitegemea?
jibu umetupatia, viva kamanda lowassa

nape akashikilia, lile asilolijua
mikoani kaambaa, uzushi kang'ang'ania
jinalo kulichafua, wewe ukavumilia
jibu umetupatia, viva kamanda lowassa

mapema nilitabiri, falsafa nikapinga
magamba sikukariri, kuvuana sikuunga
ukweli niliukiri, mantiki iso kunga
jibu umetupatia, viva kamanda lowassa

beti sita nakomea, kalamu naweka chini
mengi nimeongelea, soma tena kwa makini
yatazidi kutokea,kusini kaskazini
jibu umetupatia, viva kamanda lowassa.

shairi limetungwa na nova kambota mwanaharakati,
+255717 709618
novakambota@gmail.com
www.novakambota.com
tanzania, east africa
jumamosi, november 26, 2011

source: mjengwa blog


kweli mlijipanga...mliandaa mpaka ngonjera na mashairi kumpongeza jamaa kwa kusema tu "alipiga simu"!!!!pongezi nyingine bwana...hivi huyo mwanaume wenu wa shoka (kwa mujibu mwenzenu mmoja-sofia simba)anawalipa kiasi gani na kwa style gani wenzetu na sisi tuje huko????na hapo bado kakaenu kubenea j5!kazi hiyo kuizuia kamati isimchinje mshkaji baada ya kupewa kibali cha kufanya hivyo na nec juzi!
 
Mkuu THE ROMANTIC,

Stori yako haina ukweli wowote kwa kuangalia mtiririko wa matukio yenyewe mpaka Lowassa alipotangaza Bungeni kwamba amemwandikia barua Rais ya kuomba kuachia ngazi halafu pia kuna matatizo ya kikatiba, na hayo yote lazima yalikuwa yanajulikana kwa wote.

Mosi, Kwa kuwa Ripoti ilishasomwa Bungeni tayari, hakukuwa na uwezekano wa kutojadiliwa mpaka Bunge liahirishwe. Kwa hiyo hoja yako kwamba EL angeandika barua ya kuomba kujiuzulu then JK achelewe kuijibu, isingezuwia Bunge kuendelea na mjadala wa Ripoti. Kama JK alitaka kuizima hiyo ripoti basi lazima angewaita wabunge wa CCM hata kabla Bunge halijaanza ili kuweka mambo sawa na huo umekuwa ni utaratibu wao.

Pili, JK asingekuwa mjinga akubali kwamba Lowassa akatangaze Bungeni kwamba ameamua kujiuzulu halafu JK aje kumkatalia, ingewafanya wananchi wawe na mtazamo hasi kwa Rais wao.

Tatu, Waziri Mkuu akitangaza kujiuzulu, maana yake ni kwamba Baraza la Mawaziri linakuwa limevunjwa mpaka Waziri Mkuu Mpya atakapoteuliwa na kupitishwa na Bunge then ndipo Waziri Mkuu ashirikiane na Rais katika kuteua Mawaziri/Naibu Waziri. Hilo pekee linafanya shughuli za serikali Bungeni zisimame kwa muda mpaka Baraza la Mawaziri litakapoteuliwa na kuapishwa.

Kwa hiyo the whole stori haina mashiko.
"Mosi, Kwa kuwa Ripoti ilishasomwa Bungeni tayari, hakukuwa na uwezekano wa kutojadiliwa mpaka Bunge liahirishwe. Kwa hiyo hoja yako kwamba EL angeandika barua ya kuomba kujiuzulu then JK achelewe kuijibu, isingezuwia Bunge kuendelea na mjadala wa Ripoti. Kama JK alitaka kuizima hiyo ripoti basi lazima angewaita wabunge wa CCM hata kabla Bunge halijaanza ili kuweka mambo sawa na huo umekuwa ni utaratibu wao."

Bunge kupitia Kamati Teule ilisoma ripoti yake kupitia mwenyekiti wake, Dk. Harrison Mwakyembe. Hali ilikuwa tete Dodoma na hata Chamwino ambako Rais Kikwete alikuwa amejichimbia.

Baada ya kusomwa kwa ripoti, Lowassa alikwenda Chamwino kuonana na bosi wake ili kupanga mkakati wa kuzima maasi ya wabunge wa CCM waliokuwa wamesisimka ili kummaliza Lowassa, rais Kikwete na serikali yao.(huu ndio umedai umekua utaratibu wao si ndio?)

Katika mazungumzo yao usiku ule, Rais Kikwete na swahiba wake huyo wa zamani – Edward Lowassa – "walipima" upepo na kuona pendekezo la Lowassa kuwa rais aende upesi kukutana na wabunge wa CCM ili kuwaonya wasiiangushe serikali yao, lilionekana halifai kwa hofu ya mihimili hiyo miwili kuingiliana.kwa hiyo mzee hilo walilifikiria lakini joto la wabunge lilikua kali mno!

"Tatu, Waziri Mkuu akitangaza kujiuzulu, maana yake ni kwamba Baraza la Mawaziri linakuwa limevunjwa mpaka Waziri Mkuu Mpya atakapoteuliwa na kupitishwa na Bunge then ndipo Waziri Mkuu ashirikiane na Rais katika kuteua Mawaziri/Naibu Waziri. Hilo pekee linafanya shughuli za serikali Bungeni zisimame kwa muda mpaka Baraza la Mawaziri litakapoteuliwa na kuapishwa."

Jibu la haya maneno yako meeeengi hili hapa...hatima ya yote uliyoyasema bado ni juu ya rais kukubali au kukataa uamuzi wa kujiuzuru waziri mkuu wake!
 
kama hii ni kweli ina maana na jk naye ajiuzulu kwa sababu alimzuia lowasa kufuta mkataba huohuo unaosema ndio ulisababisha lowasa ajiuzulu?

dah!
Hivi hamkumsikia lowassa alichosema au mnafanya makusudi,hakusema alizuia bali alitaka kupata ushauri wa wataalam kwanza kwa kuwa yeye lowassa si mtaalam ni mwanasiasa kama yeye JK, wale makatibu wakuu wadau ndio wataalam wenyewe,kwa kuwa katibu mkuu chini yake ana wakurugenzi wa idara n.k ambao ni wasomi wa fani husika mbona hamuelewi vitu rahisi namna hiyo?

Mnadhani mawaziri na wakuu wa mikoa kwa kuwa wanaonekana kwenye tv ndio wanafanya kila kitu hapo kwenye vote husika? Mikoani wapo makatibu wakuu wa mikoa kwa ajili ya kumsaidia mwanasiasa ambae ni mkuu wa mkoa, na wizarani wapo makatibu wakuu wa wizara kwa ajili ya kuwasaidia wanasiasa ambao ni mawaziri!

Haya maamuzi yote mkiona wanayatangaza mawaziri ni baada ya ushauri wa wataaam wadau!ndio mana mi nikiona mnamshangalia lowassa kwa kusema tu alipiga simu eti avunje mkataba siwaelewi wala simuelewi huyo mwanaume wenu wa shoka alikua anataka kusema nini hasa!

Kwamba rais hakupaswa kujipa muda wa kuwasikiliza wataalam na badala yake amsikilize yeye mwanasiasa mwenzake au? Hii nchi imefika hapa kwa wanasiasa kufanya maamuzi bila kuwashirikisha wataalam!tatizo la "mwanaume wa shoka" kila kitu yeye anakijua ndio mana wenzake wanamuingiza mkenge kwa ujuaji!
 
Hivi bado wanajadiliwa kina Richmond, EL, Kikwete, na RA. Hawa ni wahujumu wa uchumi ambao wanastahili kwenda jela na kazi ngumu.

Waendelee kutafuna pesa za walipa kodi lakini adhabu yao inakuja. Anayewalinda anajulikana na siku zake zinahesabika.
 
Lakini twende mbele turidi nyuma... kuna lipi geni haswa ambalo leo hii limetushtua sana.. Dr.Slaa aliwapeni list ya Mafisadi na tukaambiwa yote yaliyokuwemo tukabisha na kumwita mdini sasa haya ya vikao vya CCM ndio tunategemea kuupata ukweli kutoka huko?

Hivi kweli Lowassa hawezi shtakiwa bila idhini ya rais? hawezi kuitwa bungeni na kamati ya bunge kuhoijiwa kama raia kutokana na ushahidi mdogo uliopo maanake MarekaniUK na nchi zote zilizoendelea ikitokea tuhuma kama hizi mshitakiwa huitwa na wale wenye ushahidi mdogo huitwa pia wakahojiwa hadi kieleweke. Kama atakutwa na makosa bunge hukabidhi kesi hiyo vyombo vya sheria..

Majuzi tu tuliona wale ma CEO wa Mabenki wakiitwa, Shell Bp, Mwenye gazeti la uzushi wote hawa wakiitwa bungeni na kuhojiwa iweje kwetu kila mkosa maadam ni kiongozi wa serikali basi akijiuzulu imetosha! Na maadam hatuna ushahidi basi hawezi shtakiwa wala kujibu tuhuma hizo bungeni?

...Kina Rostam, Meghji, Karamagi, Msabaah na wengineo wote leo wanatucheka na kuweka mfano mbaya sana wa uongozi kwamba ukishikwa pabaya jiuzulu tu utakuwa msafi na mambo yanakwisha.
 
"......they have a wish which i am going to grant. ni uwaziri mkuu......."
 
Back
Top Bottom