Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

Lowassa aikana Richmond, asema alijiuzulu kwa heshima ya serikali na chama chake!

Naamini huyu jamaa Lowassa pmaoja na ubaya wake mengine anazushiwa
 
Kiwete kimyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!
Wana Magamba mwambieni Kiwete wenu ajibu mapigo ya Lowassa kama ana ubavu!
 
Usitake ncheke(FF)!Kama hao ni references zako, basi umepotea kabisa! Hao wana mambo yao binafsi na wala hayausiani na chama kabisa. Ukiongelea mgawanyiko ndani ya CCM halafu ukawataja hao unaonekana kama kituko.

Kituko nadhani ni wewe usiyetaka kukubali ukweli; acha fikra mgando mkuu! Ebu tuelezee mambo binafsi yanayosababisha hao watu kutaka kutoana roho!
 
Maselef shukrani sana kwa kuipenda Title yangu. Hata picha yangu bomba sema mvivu mmoja ajiitaye washawasha ameikopi kiasi cha kunidhalilisha. Naye ni gamba tena la kiakili. Tuendelee kujadili CCM inavyoendelea kubaka taifa letu huku fisadi mkuu Jakaya Kikwete akijifanya atapambana na magamba wakati yeye ndiye gamba kuu.
Duu ama kweli kamvisha gamba gumu mwanangu. Siamini haya maneno Lowasa ameyatapika. Kumbe Lowasa alikuwa amemfichia siri mwenzake lakini yakamfika aeona ngoja atue mzigo wa mtu mmoja ili wengi wafaidi.

Hata hivyo JK kupokea na kuzifanyia kazi simu za makatibu bila ya consultation ya aliyepewa dhamana hiyo ambaye ni Lowasa ilikuwa ni makosa JK aliyafanya. Kumbe JK alitakiwa awarudishe kwa Lowasa ili wasaidiane (Just imagining how things would be ethically/Utendaji) Nahao makatibu watakuwa wameshawishiwa na ROstam Aziz.

Ngoja tuone libeneke litakuaje.
 
Haya ndiyo yale magamba magumu ya kakakuona ambayo JK anayaogopa sana na hana ubavu wa kuyang'oa. Hapa yakiwa yanapongezana baada ya ushindi wa Dodoma.
 

Attachments

  • Magamba magumu.jpg
    Magamba magumu.jpg
    17 KB · Views: 52
simtetei Nape ila kuna jambo halijakaa sawa,hivi inawezekanaje Nape afanye kazi ya kuhubiri uvuaji wa gamba na mengineyo bila kuambiwa na wakubwa wake wa kazi? naona hii ni movie tu tunachezewa akili. Hapa pia naona cost ya kuwa na 'best friend',kikinuka lazima siri zote zimwagwe
 
Watanzania sasa amua wenyewe. Lowassa kwa mara nyingine amemshinda Kikwete je Bunge letu litaendelea kuchekelea kwa vile wote ni nyani wana mikia?
Haya chini ni maneno mazito aliyomwaga Lowassa akiamua kumwaga mboga baada ya Kikwete kutaka kumwaga ugali.

"Mwenyekiti utakumbuka kwamba mimi nilishaamua kuvunja mkataba wa Richmond mapema, lakini baada ya kukupigia simu ukiwa katika safari nje ya nchi ulisema tusubiri kwani ulikuwa umepata ushauri wa makatibu wakuu wa wizara, sasa leo hii ninahukumiwa nakuitwa fisadi kwanini?".

"Nilijiuzulu kuwajibika kwa ajili ya kuilinda Serikali yangu na kwa heshima ya chama changu, sasa kwanini leo nahukumiwa kwa jambo hili, tena natukanwa na wana CCM wenzangu na siyo wapinzani nchi nzima kwamba mimi eti fisadi?,"alinukuliwa akihoji Lowassa.

Kadhalika kada huyo wa CCM alinukuliwa akimkumbusha Rais Kikwete kwamba: "Mwenyekiti nikukumbushe mwaka 1997 kule Zanzibar, kina Mzee Daudi Mwakawago walikuja na mafaili yakiwa na tuhuma dhidi ya mtizamo hasi wa jamii dhidi yako, kwa hiyo wakati ule kama si busara za kina Mzee Mkapa (Benjamin) leo usingekuwa hapo ulipo".


All in all, ukweli unabaki pale pale kuwa wote wawili-Kikwete na Lowasa hakuna mwenye hekima. Hawafai kuwa viongozi wa watu. Kikwete ni dhaifu na LOwasa ni mwizi. Mungu atawahukumu kwa hukumu ya haki.
 
Maselef shukrani sana kwa kuipenda Title yangu. Hata picha yangu bomba sema mvivu mmoja ajiitaye washawasha ameikopi kiasi cha kunidhalilisha. Naye ni gamba tena la kiakili. Tuendelee kujadili CCM inavyoendelea kubaka taifa letu huku fisadi mkuu Jakaya Kikwete akijifanya atapambana na magamba wakati yeye ndiye gamba kuu.

hivi wewe unajua maana ya kupayuka.kama ulikosa username ungesema nikusaidie.You are not creative kama jina tu lakushinda
 
Mi cjui bana, maana lishanichosha sasa....hata hivyo, ,kuna jambo moja ambalo nalifahamu kwa 100% ambalo naweza kulisimamia hata The Hague. Nakumbuka aliwahi kusema : "Mheshimiwa Spika, Nimedharirishwa sana! Nimechafuliwa sana! Nimetukanwa sana! Lakini najua, tatizo ni uwaziri mkuu!"

Leo hii:
"
tatizo kubwa analolifahamu la vita ya sasa ni urais wa 2015."

Sooner or later
"Babaz Maaskofu, nimedharirishwa sana , nimechafuliwa sana, nimetukanwa sana! lakini kubwa ninalofahamu kwa vita hii ya sasa ni Unaibu Katibu Mkuu wa UN!"

nimedharirishwa
= nimedhalilishwa
 
Lowassa mwizi tu anawaleeza nyie mlokuwepo chama na kumwona kwenda kanisani basi mnafikiri mtu mzuri sana..Kama yeye alikuwa mkweli kwa nini asiwahutubie Umma mzima wa Watanzania badala yake anaenda katika mikutano ya chama! anajua huko mmejaa masaburi watupu. Kikao cha chama CC wanatokea watu wanafokea wengine as if wao ni Miungu!..damn.

Yeye alikuwa waziri mkuu na sii katibu wa chama, hakuwahi kupendwa na Nyerere hadi leo hii wananchi hawampendi pengine huko kwenu CCM. Halafu naweza sema ni jambazi lililokubuhu yaani anatuondolea watu tu kila mwaka. Kesho sintoshangaa Nape mgonjwa anatakiwa kupelekwa India..

pole ndugu! Umesikia yaliyomkuta Six?
 
Wacha hasira mkuu Lowasa anaonekana ana mengi ya kutueleza ila ukumbuke mwanasiasa huongea ukweli kwenye jina lake tuu na sio hoja zake na mengineyo...lowasa haitaji huruma za jk bali jk ndio anahaha atamfadhili vipi lowasa kwa kufichiana siri...ikumbukwe kama jk angejiuzulu yeye ingekuwa balaa zaidi ndio maana akamuomba lowasa abebe adhabu yake ili aweze kujilinda na kumlinda yeye siasa mchezo wa hila

True 100%...Lowasa kaongea maneno waiyopanga na JMK ayaseme then yawe mbeleko ya JMK kuzima hoja ya Ufisadi wa Richmond, lakini bado Lowassa ana kazi kubwa ya kutueleza utajiri mkubwa alionao uliowahi kuhojiwa na Baba wa Taifa Nyerere aliupata vipi? Na ile ndoto yake ya zile mvua za kutengeneza toka Thailand zilitumia Tsh ngapi?
 
watu mnadhani kuwa dhambi ya lowasa ni dowans, hivyo akisafisgwa downns atabaki malaika. huhu ni jambazi, anahusika mengi kuanznia alivyokuwa nkurugenzi A.I.C.C, ALIVYOKUWA WAZIRI WA ARDHI KAWAULIZE WANANFUNZI WA ARDHI UNIVERSITY JINSI ALIVYOTAFUNA POSHO ZAO AKIWA NA KATIBU MKUU WAKE, NI DIKTETA NA AKIPEWA UONGOZI ATBADILISHA UONGOZI NA KUTAWALA MILELE , JIULIZENI KUHUSU LILE FAILI ALILOLETA NYERERE KWENYE KUCHUJA WAGOMBEA WA URAIS 1995 LILIKUWA NA NINI KUHUSU LOWASA, ACHENI KUWA MYOPIC
 
Hadi sasa Lowassa njia nyeupeeee for Presidential candidate wa CCM 2015, na 7bu zipo wazi, read this
1. Mkapa alifurahia wakati Lowassa anaongea, meaning Ben is supporting EL, signs are clear
2: Sumaye, another powerful political leader & rich dude, wazi wazi anam support Lowassa tena kasema wakina Nape na Chilligati wachukuliwe hatua
3. Mzee Kingunge yupo 100% upande wa Lowassa, na ni baada ya kujua ukweli halisia kuhusu tuhuma dhidi ya EL are fake, publicized tu.
4: Hapa niseme JK yupo na Lowassa 100% na hawezi kuongea hadharani kwa nafasi alionayo sasa, ila dalili na matendo yapo clear, JK hadharani hajawahi mshutumu EL hata siku moja, hadi sasa ni marafiki....
5: EL ana support ya all rich dudes, Rostam, Karamagi, Chenge, na support kubwa hasa si kwa hawa financial power house wa CCM bali Wanachama wa CCM wanampenda saaaana, yaani leo NEC, CC, na wajumbe wa mikoa wa CCM, Lowassa ni lulu, signs are clear
6: Makanisani Roman Catholic & Lutheran churches EL kashamaliza kazi, wanampenda na wengine mfano mzee wa upako, Anthony Lusekelo wazi wazi anampigia kampeni mapemaaaa.....

What i see now & days to come-----
EL hana mpinzani CCM hadi sasa, na wazee wa CCM tayari wamemkubali, EL ni Field Marshall wa siasa za hapa TZ na atashinda Urais, ngojeni muoneee....
 
Hivi kuyataja makosa ya wengine ndio kujisafisha? Huyu EL hata aoshwe na sabuni kiasi gani hasafishiki!
 
kuna mtu anajua juu ya file la kina mzee mwakawago lilikuwana tuhuma gani?
 
Mkuu mimi namlaumu JK kwa kuendelea kumpa free airtyme huyu jamaa, yaani alikuwa na nafasi mfano last year wangetoa jina lake kwenye ubunge, next kama walivyofanya kwenye kuwaondoa kwenye CC. Halafu wangemsongesha mahakamani awe bize huko.

Sasa inavyoonyesha JK anaplay uungwana na huyu jambazi ambaye will stop at nothing kutimiza his personal dreams. JK amechelewa kiasi kwamba lolote litakalomtokea EL kwa sasa kuhusu tuhuma za ufisadi itaonekana JK anamwandama.

Politics is so dirty!!!!!!!! Hivi unafikiri ingekuwa ni Mkapa EL angethubutu kubwabwaja maneno kama hayo?
nashauri tuzungumze hoja zaidi badala ya kutanguliza na kuanika chuki zetu dhidi ya watu.
 
Back
Top Bottom