Lowassa ana dhambi nyingine zaidi ya Richmond?

Haya hilo la RICHMOND ni dogo?
Na nisifa kuwa na kashfa hata moja ya kuangamiza taifa ?
Kama uelewi watu kama hawa kunanchi zinachinja kichwa
huwezi ukacheza na maslahi ya wananchi kienyeji kienyeji
 
Haya hilo la RICHMOND ni dogo?
Na nisifa kuwa na kashfa hata moja ya kuangamiza taifa ?
Kama uelewi watu kama hawa kunanchi zinachinja kichwa
huwezi ukacheza na maslahi ya wananchi kienyeji kienyeji

Kuna ugonjwa unaitwa myopia na mtoa thread hii ameonyesha moja ya dalili za ugonjwa huo!
 
Tatizo liliopo ni kwanini Bw Lowassa hajashitakiwa mahakamani kwa tuhuma hizo zote? Mh Lowassa is not above the law.Na kama wameshindwa kumshtaki wanaogopa nini au hakuna ushahidi wa kutosha kumfungulia mashtaka? Nani alaumiwe? Akisimama Lowassa akadai hizo ni siasa za maji taka yaani kuchafuliana majina kwani kila nikitaka kuwania Uraisi wabaya wangu wananipaka matope atakuwa amekosea? Bila kutumia nguzo ya mahakama na ikamweka hatiani Lowassa is still innocent na anayo haki ya kugombea the Highest Office of the Republic.
 
Mzee wa Watu kapumzika hana nia ya kuongembea uraisi......anakula kuku kwa mrija,
 
Mh.Umeandika kweli kweli!Je na wewe ulikuwa Unamshauri Vizuri mwalimu?Manake hata enzi ya Mwl siyo kwamba nchi ilikuwa ya Asali na Maziwa!
Hasa Swala Uchumi!umekuwa Ukidorora kadiri Umri wa Uhuru unavyoongezeka!
Si kwamba Mwl ndio 'Point of Ref' ya Kila Kitu?
 

Jasusi,

Muongezee na nyumba anazomiliki afrika ya kusini mojawapo aliwahi kupangisha kwa balozi wa tanzania south africa. Baba wa taifa alipogundua kidogo azimie kwa mshtuko. Kote anakopita Lowassa amefanya uharibifu hafai hata kuwa class monitor wa darasa. Aendelee na ubunge wake Monduli akimaliza akapumzike tu.
 
Footprints nyingine za huyu Lowasa alipokua Waziri wa Maji na Mifugo hizi hapa... Dont say you were not warned! Kila alipopita alihusishwa na kashfa... amebakiza kuwauza watanzania wenyewe tu sasa, ndio maana ana haha kwa huo Urais!

SOURCE: TANZANIA DAIMA( LA ENZI ZILEEEE.....KABLA MHARIRI HAJAENDA KUKUTANA NA LOWASA KAMA INAVYOSOMEKA HAPA CHINI, Hahahaa...)

Taarifa zilizoifikia Tanzania Daima Jumapili hivi karibuni, zinaeleza kuwa, Lowassa alitumia nafasi yake ya uongozi wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu, ya uwaziri wa Maji na Maendeleo ya Mifugo kununua eneo kubwa la Ranchi ya Taifa ya Mifugo ya Mzeri, iliyoko wilayani Handeni, mkoani Tanga.

Zinaeleza kuwa Lowassa anamiliki kitalu namba 645/5, huku majina ya watu wanaoonekana kuwa wamiliki halali wakiwa ni wengine, jambo linalotia shaka.

Taarifa zinaeleza kuwa maelezo ya wamiliki wa kampuni hiyo yaliyoko kwa Msajili wa Makampuni (BRELA) na yaliyo katika Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), yanaonyesha kuwa Kampuni ya Olospa, ndiyo mmiliki wa ranchi hiyo.

Baadhi ya viongozi wa NARCO waliozungumza na gazeti hili walieleza kuwa, wakati ranchi hiyo ikiuzwa kwa Kampuni ya Olospa, kitalu namba 645/5, hawakujua kama ilikuwa na uhusiano wowote na Lowassa.

Kwamba baada ya kuanza kuibuka kwa tetesi kuwa ranchi hiyo ni mali ya Lowassa, walianza kuwa na wasiwasi kuwa inawezekana hakuweka wazi uhusiano aliokuwa nao na kampuni hiyo kutokana na wadhifa aliokuwa nao wakati huo.

"Ni kweli imebainika kuwa Lowassa anamiliki block namba 645/5, na amekuwa akionekana huko mara kwa mara, lakini sisi hatukujua lolote wakati wa zoezi la kumilikisha maeneo hayo," alisema Mshauri Mkuu wa NARCO, Fabian Shempemba, ambaye wakati wa uuzaji wa ranchi hizo alikuwa Meneja Mkuu wa kampuni hiyo.

Alisema taratibu zilizokuwepo za kumilikisha ranchi ndogo za kibiashara kwa wafugaji wadogo, ziliipa madaraka ya kufanya maamuzi ya mwisho iliyokuwa Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo, wakati huo ikiwa chini ya Lowassa.

"Baada ya kukubaliwa na serikali mwaka 2002, kwamba ranchi za taifa zigawanywe vipande vidogo vidogo vya kibiashara na kumilikishwa Watanzania, NARCO tulipewa jukumu la kutangaza na kupokea maombi.

"Baadaye Bodi ya NARCO iliwasilisha mapendekezo yake wizarani kuhusu nani anafaa na nani hafai kumilikishwa ranchi hizo ndogo ndogo, halafu wizara ndiyo ilikuwa na mamlaka ya kuamua wamiliki," alisema Shempemba.

Shaka inayoelezwa hapa ni uwezekano wa Lowassa kuamua kununua ranchi hiyo kupitia Kampuni ya Olospa kwa sababu hakutaka kwa wadhifa aliokuwa nao kuhusika kwa namna yoyote na ununuzi wa ranchi.

Aidha, shaka nyingine inayojitokeza ni usiri uliopo kati ya Lowassa na Kampuni ya Olospa inayodaiwa kuwa licha ya kutambuliwa kama mmiliki wa ranchi hiyo na NARCO, jina la Lowassa halimo katika orodha ya wakurugenzi wa kampuni hiyo.

Kwamba katika misingi ya uadilifu wa uongozi, Lowassa alipaswa kutangaza mapema masilahi yake katika Kampuni ya Olospa ili asishirikishwe katika kujadili na kufanya maamuzi juu ya maombi ya kampuni hiyo ya kutaka kumilikishwa ranchi hiyo.

Akizungumza na gazeti hili wiki iliyopita kupitia simu yake ya kiganjani, Lowassa alikiri kumiliki ranchi hiyo na kueleza kwamba haoni kosa lolote kuwa mmiliki wa ranchi hiyo kwa sababu hapakuwa na sheria ya kumzuia kuinunua.

"Kwani kuna makosa yoyote mimi kununua hiyo ranchi? Sikiliza wee ……, wewe si ndiye uliyekwenda kwanza Wizara ya Mifugo kuhoji habari hizi wiki iliyopita?

"Sasa si vizuri kuzungumza haya mambo kwenye simu, nisubiri Dar es Salaam, nitarudi baada ya wiki moja, kwa sasa nipo safarini Monduli.

"Lakini njoo ukijua kuwa hiyo ilikuwa ni sera ya taifa ya kuzigawanya ranchi za taifa na mashamba makubwa ya mifugo ya umma, katika vipande vidogo vidogo na kuwamilikisha Watanzania wenye uwezo wa kufuga kisasa na kibiashara," alisema Lowassa.

Gazeti hili jana lilimtafuta Lowassa kama alivyoahidi ili kutoa ufafanuzi wa madai hayo na lilipompata kupitia simu yake ya kiganjaini alieleza kuwa atatoa ufafanuzi huo wiki ijayo.

"Nipo njiani narudi Dar es Salaam, nakuomba unipigie Jumatatu nitakuambia tukutane wapi ili tuongee kwa kina suala hilo, na ningependa uje na mhariri wako," alisema Lowassa.

Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumapili umebaini kuwa, Kampuni ya Olospa ilisajiliwa Julai 31, 1992, chini ya wakurugenzi wanawake watatu.

Taarifa zilizoko BRELA zinaonyesha kuwa wakurugenzi hao ni Ruth Mollel, Nengai King'ori Mollel na Olomutai Mollel.

Jina kamili la biashara la kampuni hiyo lililosajiliwa BRELA ni Olosipa Printers and Stationers Limited, ambayo ni kampuni inayofanya biashara za uchapishaji na uuzaji wa vifaa vya ofisini.

Shughuli za kampuni hiyo zinapingana na shughuli za biashara ya ranchi (kufuga na kuuza mazao ya mifugo), jambo ambalo linatia wingu zaidi la mashaka kuhusu kampuni hiyo kuuziwa ranchi hiyo.

Uamuzi wa kuzigawa ranchi za taifa katika vipande vidogo vya kibiashara na kuzimilikisha kwa Watanzania wazalendo, ulifikiwa na serikali mwaka 2002, na utekelezaji ulianzia kwa Ranchi ya Mkata (Morogoro), na kufuatiwa na ranchi ya Mzeri iliyogawanywa vipande 9, ambapo kipande kimoja (Block 645/5) ndicho kinachomilikiwa na Olosipa.
 
Huu ndio ujasiri anaouzungumzia mwl, UJASIRI WA KIFISADI. Lowassa hana limits, ni mtu hatari sana.
 

Tatizo mnajiunga JF na mnaanza kutembe hapo hapo bila hata kutambaa, unataka mtu akuweke nini hapa tafuta taarifa wewe mwenyewe, acha uvivu wa kusoma kuna kila aina ya taarifa humu JF nyinye ambao kazi yenu ni kujadili mnachokiona na mnauliza hata mambo mliyoyakalia ndio mnaturudisha nyuma kama Taifa.

Haya mambo unayouliza umeyakalia humu JF watu wameyajadili miaka kadhaa iliyopita yapo humu bure ni kusoma tu! Uvivu tu, sijui hata kama unaweza kushika Jembe kama kusoma tu huwezi.
 
Kule kwemye Hifadhi ya wanyama pori ya Gombe, kuna kiongozi wa sokwe anayetawala sasa.Kiongozi huyu alimpindua aliyepita kwa kisingizio kuwa alikuwa dikteta. Hata hivyoi utaratibu wa sokwe hawa, mawindo yote ya sokwe raia ni lazima yapelekwe kwa huyu kiongozi,yeye ndio anao uamuzi ama wa kula mawindo yote, ama kugawa kwa raia wake na raia wapi awagawie!Huyu kiongozi wa sasa eti ni nafuu kuliko aliyemtangulia,na utaratibu huu hajaubadilisha, ukiwinda ni lazima mawindo upeleke kwake pia! Lakini eti ana unafuu kuliko aliyemtangulia! Hiyo ni Hifadhi ya Gombe.

Lowasa na wengine huko CCM wanafanana kitabia na hawa viongozi wa sokwe wa Gombe. Wote watachukua tu kwanza wao na watachagua wa kuwagawia mawindo kwa utaratibu usio shirikishi! Ila Lowasa anawazidi moja kubwa, anao ujasiri wa kutuongoza kuelekea kwenye mafanikio ya kiuchimi na kijamii kuliko wenzake wote ukiwaweka pamoja.Hiyo ni Tz

Dhambi kubwa aliyonayo EL ukiacha ya Richmond ni kuwa wenzake wanaifananisha safari ya Zuma kuelekea Urais wa Afrika Kusini-na safari yake: atashinda!
 
Ukitumwa siku zote tafakari kwa kina juu yaujumbe uliopewa ukiona hauna mashiko kwa future ya Taifa nibora ukae kimya.jf siyo yamatusi Bali niukweli Daima
 
capt lowasa tafadhali uone aibu,achana na urais huna sifa na una kashfa nyingi
 

Hebu chukua mfano wa mchezo wa mpira wa miguu. Mchezaji anapofanya madhambi uwanjani mwamuzi anaweza kumpa onyo kwa kadi ya njano, lakini kama mchezaji huyo atafanya madhambi mengine anaweza kupewa kadi nyingine ya njano ikiufatiwa na kadi nyekundu hivyo kwenda nje ya uwanja. Hata hivyo endapo yale madhambi ni mabaya mno mchezaji anaweza kupewa kadi nyekundu moja kwa moaja na kwenda nje ya uwanja. Hii scenario ya pili ndiyo hiyo inamhusu EL.
 
Mvua za Kutengeneza Kutoka bara la Asia zikajaze Mtera maji! muhahahahahahaha
 

Yaelekea uko nyuma ya matukio au unafanya makusudi,ninakushauri kwamba pitia historia yake yote alikowahi kufanya kazi kisha nenda kafanye uchunguzi utamgundua huyu ni nani na amefisadi nini na utashangaa na roho yako,kwaujumla jamaa ni mchapakazi sana tena sana tatizo lake mali zilizombele yake haziachi hata ufanyeje, nenda AICC,Wizara zote alizofanyia kazi mpaka anajiuzuru utapata taarifa zaidi ya tani mia hivi.ukianza na wizara ya Ardhi ni vizuri zaidi.
 


Ni kweli Tanzania kuna siasa za unafiki, kuna wanafiki wengi na uzushi mwingi. Lakini kwa mtu mwenye akili timamu, Lowassa hata kuwa Waziri Mkuu lilikuwa tatizo, si dogo kubwa. Mfano tunao, tena wazi kabisa tuliona ufisadi katika u-PM wake,tunajua kabisa kuwa akiwa PM tena nini kitafanyika, leave alone urais, ambao akiupata atafanya "makubwa zaidi". Barua ya Mzee Samuel Kasori hapa JF si mara ya kwanza kuonekana, na yaliyosemwa yote hayajawahi kukanushwa, even worse baada ya kuwa PM alifanya zaidi ya yale yaliyomo kwenye barua. Tutakuwa wapumbavu sana kama tunafikiiri EL atatufaa, tunatakiwa kufikiri kwenda mbele, sio style hii ya reverse.
Bonga
 
lowasa mwacheni jamaani awe raisi wetu tuondokane na viongoz maneno tunataka watendaji
 
lowasa mwacheni jamaani awe raisi wetu tuondokane na viongoz maneno tunataka watendaji
 
lowasa mwacheni jamaani awe raisi wetu tuondokane na viongoz maneno tunataka watendaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…