Lowassa aongea na vyombo vya habari; akataa kugusia suala la Richmond/DOWANS

Hiyo hotuba tayari Absolom Kibanda alishamwandikia kwenye gazeti la leo la Tanzania Daima, for me there is nothing new than wasting our energy & time. am out on this thread.
 
Yaani aliwaita waandishi na vyombo vyao kuvionya tu na kutishia kuvichukulia hatua kwa "kumchafua?" Kweli mvi siyo busara -- kwake zimekuwa kama uchuro tu.

WHAT A SHAME!!!
 
Nimekubali msemo wake kuwa yeye na rais hawakukutana barabarani. Kwa hiyo urafiki mbele au kwanza watanzania na matatizo yao shauri yao
pili kumbe ikulu kunaendeka tu? na kweli hawa wawili wananufaika na matatizo yetu

Ni kweli mkuu. Mtu hayuko tayari kukubali kuwa alifanya makosa kwa umma. Tunahitaji mapinduzi ya kifikra na mfumo mzima wa utumishi wa umma.
 
Shukurani mkuu. Ila hapo sioni kipya.
 
Na hapo mwisho anapotaja changamoto mbali mbali zinazolikabili taifa -- hivi kimakusudi tu, au kwa kapitiwa -- kuacha kuitaja ile changamoto Namba 1 yaani UFISADI?
 
Lowassa Press conference has done nothing but reignite controvecy surrounding him. He would have been well adviced to( as Ole Ntimama said the other day) lay low like an envelope.
 


Mkuu uwezo wake umeishia hapo unakumbuka aliwai shidwa kumjibu mwanafunzi uelewa wasasa nimkubwa vingozi wetu wengi uwezo wao nifinyu haiingii akilini alicho kiongea kuwasumbuwa waandishi watu wamesitisha kazi kufuatilia nini atatamuka kumbe upupu wengi wamefilisika kisiasa
 



yle dogo wa ukerewe nakumbuka sana maana siku hiyo alivyonuna
 
Ndugu Dark City,naona EL na yeye ameshindwa kuchukua maamuzi magumu.

Naomba nitofautiane na wewe...EL keshachukua uamuzi mgumu sana labda kama watu hawauoni.

Hivi ni rahisi mtu kuvuta trigger ya silaha iliyokulenga kwenye paji lako la uso???? Sasa EL keshaanza taratibu kuivuta!
 

Na hajui kwamba kwa uelewa wao wa mambo mengi tu, waandishi sasa hivi wako hatua moja mbele ya wanasiasa. Hivyo wanasiasa ndiyo kila mara wanajikuta katika hali ya kutaka kujikosha mbele ya waandishi, kuwatisha au hata kuwahonga.

The press is always ahead!
 

Yeah! Press ndiyo kwa kiasi kikubwa zina-set agenda za wanasiasa!
 
Naunga mkono aliyoyaongea na style yake presentation maana mkutano au press cenference ameitisha yeye. Kama aliyosema siyo yale tuliotaka kusikia hatna haja ya kuyajadili na message will be sent to him.Lakini kama audience constituting waandihi wa habari na wengine walimsikiliza na kuuliza maswali na kusikia ambayo hawakurataji walikuwa na options kadhaa. Wangeondoka immediately after he had stated his position that questions be in the context of what he had presented. Basi angegoma zaidi wangenyanyuka na kuondoka kabisa huku wakimwacha ameduwaa. Pili Watanzania lazima tuwe serious na yale tunayotaka kusikia na kutoka kwa nani.

Haingii akilini kwamba mtanzania sensible alitaka EL afanye kama Wakatholiki ndani ya confession box kuwa nilikosa eno kadha wa kadha. EL kama ilivyo JK are both birds of the same feather na historia itakuja kusema.Tusiwe wasaarifu. Waliposhika madaraka kila zuri mfano amani na utulivu, mshikmano, hazina ya fedha za kigeni $3b, miundo mbinu ya barabara, uwanja mpya wa taifa, viwanda vichache vilivyobinafsishwa na kuendelea kuzalisha walivifanya kama ni mafanikio yao wala si ya chama au serikali zilizopita. Ilikwa ni nadra Mkapa na Nyerere kutajwa kwenye mazuri hayo labda Mzee Mwinyi peke. Kumbuka mpaka Mkapa alianza kuzomewa na watu kama ambaye hakuwahi kufanya jema lolote.

Lakini penye matatizo kama ukame, njaa, ukosefu wa umeme, mikataba mibovu ya madini, radar ya ndege na mengine hayo yalifanywa kuwa ni urithi mbaya wa wa serikali zilizopita. Sasa mtu ambaye alizoea propaganda za namna hii mnamtaka leo asimame ajipige kifua aseme nilikosa. Watu wa kukubali makosa na kusema yalifanywa kwa ubinadamu na kutoa wito wa kujirekebisha walikuwa ni kina Kambarage, Kaduma, Warioba na wengine lakini bahati mbaya Mwalimu ashatangulia mbele ya haki na waliokuwa hai badohawako ktk vyombo vya kimaamuzi.

Majibu sahii ya nini kijiri Richmond/Dowans na sasa Syombion anayo JK kama Rais maana anavyo vyombo vya kumsaidia kujua japo ashasema hajui. Polisi, usalama wa taifa, jeshi, PCCB, Tume ya maadili na ofisi ya rais.Sasa kuendelea kujificha chini ya kivuli cha siwajui ni kujidhalilisha na kuwatusi watanzania. Richmond/Dowans wamekuwa wakilipwa bilions of shs, sasa were we paying the ghosts? JK atuambie kuhusu haya na EL ambaye yuko nje ya vyombo vya maamuzi na kwa kuwa kuna vyombo vingi chini yake Rais jibu litakalotoka hapo tutajua pumba zipi na mchele upi. Lakini itoshe kusema yeye ndiye aliyebariki mitambo ya dowans wapewe symbion na kuzalisha umeme.sasa jiulize utaruhusu kitu cha mtu usiyemjua anunue mtu mwingine? kama ni hivyo hamna maana ya kuwa na mtu kama huyu as rais na vyombo hivi vikienedelea kuripoti kwa wahusika wanahitaji kupimwa.

Majibu mengine ya Richmond/Dowans anayo Sitta Samweli aliyekwa spika wakati huo. Alianzisha mchakato wa kuipeleleza richmond/dowans na ripoti kutolewa na jinsi alivyozima mjadala huo ni ishara ya kifisadi. Huwezi kuanzisha jambo leneye gharama in terms of perdiem kwa wajumbe na na nauli ya kwenda na kurudi nje ya nchi na muda mwingi wa bunge kuongelea swala hilo halafu ukalizima bila majibu na utarajie watu wakuenzi hapana. Ssita asipojitokeza waziwazi na kusema tutasema aliutaka uwaziri mkuu wa EL.Haitoshi kusema wasilipwe, ni wahuni, ni mkataba batili... Hayo kila mtanzania mwenye akili alishajua.Tuanataka atwambie sababu ya kuzima mjadala bila solution for interest of mother tanzania.Haoni kuwa alifanya hivyo na wao wakapata greenlight ya kutumia mahakama kutaka fidia?

Mwingine ni Mwakyembe na timu yake watuambia waliyofich Kulinda heshima ya serikali na sio taifa na kumwogopa Mungu ni yapi? Hivi serikali gani yenye hesima kuliko umma? Heshima hiyo imetoka wapi? Serikali itapita lakini taifa alipiti.Wana deni hawa maana wasingefanya filtering on what to report huenda kesi ya Dowans huko ICC isingepata nguvu.

Tuungane kulazimisha majibu na suluhu yenye manufaa kwa taifa na liwe ni fundisho kwa serikali zijazo. Mungu atutangulie wote wenye mapenzi mema na nchi
 
Nimepoteza muda wangu kukodolea macho thread hii tangu page ya kwanza hadi ya mwisho. Ninachoona hapa ni uharo ule ule wa kimagamba. Hakuna jipya
 
Kuhusu hoja ya kujenga viwanda na hasa domestic industries hilo halina ubishi.Ni hoja nzito ambayo tumekuwa tukiipigia kelele kila siku.Hata hivyo alipokuwa waziri mkuu hakufanya hayo

Pia kitu ambacho nimegundua,mkakati wake mkubwa ni kupata attention ya vvoters block ambayo mtaji wake mkubwa ni vijana.Ni lazima sasa tujipange sawasawa kwa sababu huyu jamaa anatafuta fursa ya kujiweka karibu zaidi na vijana.

Pia amejionyesha ni mtu wa mikakati kwa sababu hajataka kuongelea mambo sensitive ambayo yangekuwa ni suicide pact.ameyaacha strategically pengine kutokana na kikao kijacho cha NEC.Hataki ku-twist rebellion intuition waliyo nayo wajumbe wa NEC. He he Heeee! CCM mnayo kazi,mkitoka hapo mtakutana uso kwa uso na radical movement ya chadema na vijana!
 
Tunakusiliza mwenye maamlaka ya juu humu JF
 
Gamba au si gamba Mh Lowasa kama mtanzania ana haki ya kupiga au kupigiwa kura. Mpaka hapo haki hiyo itakapobatilishwa na mahakama au vikao husika vya chama chake hatupaswi kumuhukumu humu jamvini. Na hata chama chake kikimkatalia nna uhakika katiba mpya itampatia haki hiyo kupitia mgombea binafsi
 
invisible nakuomba ukae uipangilie vizuri hii habari coz haina mwanzo kati na mwisho.au kwasababu ameshamaliza kuongoa mwambie wa jikoni akupe copy ya aliyoyasema naamini kawagawia copy.over
Invisible aliyeshasema ile ni update tu na kwa mpangilio usubiri kesho kwenye magazeti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…