Lowassa aongea na vyombo vya habari; akataa kugusia suala la Richmond/DOWANS

Lowassa aongea na vyombo vya habari; akataa kugusia suala la Richmond/DOWANS

Wana JF,
Hawa jamaa wawili JK na EL wanajuana vizuri sana. Kumbukeni enzi zao za ''BOYS 2 MEN''!!!!
Kila kitu kiko wazi. EL na JK wanajaribu kucheza na akili za Watanzania kwa kufanya The Comedy Show. Hawa watu 2 watatusumbua sana huko tunakoenda. Mkutano wa jana ilikuwa ni gheresha tu na kuvuta masikio ya Wadanganyika!

Watu tulikuwa tuko roho juu kwamba pengine EL angechukua maamuzi magumu kama alivyodai Bungeni juzi kwa kufuata nyayo za rafiki yake RA wa Igunga. Lakini waaapi!!! Huo ubavu wa kuchukua MAAMUZI MAGUMU ANAO???Kwanza JK alishamwambia yeye atulize bori maana hakuna kitakachomtokea yeye na AC kuhusiana na KUJIVUA GAMBA. EL na AC wataendelea kupeta ndani ya Chama Cha Magamba. Kelele za Vuvuzela Nape ni danganya toto!!!

Yale yale ya RA. Kwamba unajivua gamba halafu kesho CCM hao hao wanakuja kuomba UWAFADHILI NA UWASAIDIE KUPIGA KURA! Hakuna cha kuvuana gamba baali ni usanii wa CCM wa kucheza na akili za Wadanganyika.

Kuna ASKOFU au Mchungaji wa Kanisa moja pale Dar aliwahi kutamka mwaka huu kwamba: LOWASSA ASIPOKUWA RAIS MWAKA 2015 MNIUE! Hizo habari ziliandikwa na magazeti mengi sana na sikumsikia EL akikanusha habari hizo. Hivi karibuni EL ameonekana akienda kwa Nabii Joshua wa Kanisa la Emmanuel huko Nigeria. Watu wamemwona kupitia kwenye Runinga ya Emmanuel TV akiombewa mara mbili. Habari za kuaminika ni kwamba HAYO NI MAANDALIZI YA URAIS MWAKA 2015! Rejea taarifa ya Askofu hapo juu.

Nihitimishe kwa kusema kuwa Kiwete na Lowassa wanajua kabisa nini wanakifanya ndani ya CCM na UVCCM. Kumbukeni kauli za EL kuwa yeye na JK hawajakutana barabarani. Kumbukeni walivyochukua Fomu za Kugombea Urais kwa mbwembwe mwaka 2005 na kufuatia uundaji wa Serikali ya JK 2005. Kumbukeni baada ya EL kujiuzulu Uwaziri Mkuu mwaka 2008 JK alitamka nini! Kwamba kilichompata rafiki yake EL ni ajali ya kisiasa.

Wazungu wanasema kuwa,''BIRDS OF THE SAME FEATHER FLOCK TOGETHER''. Kiwete na Lowassa hakuna wa kuwatenganisha.Hakuna cha UVCCM,hakuna cha Nape wala hakuna cha SS. Ni lazima EL aukwae Urahisi mwaka 2015!!!!
 
namsubiri nimpe kura yangu 2015 sijaona kama lowasa ikulu ni yake
 
Katika picha chache za Lowassa jana kwenye Luninga zetu ungeona tu kwamba alichokuwa anakisema sicho kilichokuwa moyoni mwake.
 
Pamoja sana, waambie hao masharo balo wa siasa zisizo na tija! Endelea kuongea tutajua mengi sana mkuu, na usitishike nao njia ni nyeuuuupeeee kwako kama nywele zako.
 
Ndugu zangu wana JF. Kwanza kabisa napenda kumshukuru na kumpongeza sana "INVISIBLE" kwa kutuhabarisha juu ya kilichokuwa kinaendelea Monduli, kabla na baada ya mkutano wake Mh. Edward Lowasa na waandishi wa habari leo.

Nimeipitia kwa umakini sana hotuba ya Mh. Edward Lowasa aliyoisoma leo mbele ya waandishi wa habari jimboni kwake Monduli. IENISIKITISHA SANA. Sikutegemea kama Mh. Lowasa baada ya misukosuko yote hii, aendelee kuwa "muongo" kiasi hiki. Hili linanipa tabu kichwani mwangu na, hasa pale anaposema na kuonekana akiombewa na TB Joshua.

Sio kweli kama Mh. Lowasa hukuwahi kupanga kugombea Urais mwaka 2010. Mipango hii ulikuwa nayo na uliwashirikisha baadhi ya wenyeviti wa CCM wa mikoa kadhaa, wabunge na makatibu wa CCM wa mikoa kadhaa. (Majina na vituo vyao vya kazi tunahifadhi kwa sasa). Mipango yako hii ilikuwa inajulikana kwa viongozi mbali mbali ikiwa ni pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM.

Baada ya kuona maji ni marefu ktk kutekeleza mipango yako hiyo, ulimshawishi Waziri Mkuu mmoja mstaafu agombee na wewe ulikuwa tayari kumsaidia, tumshukuru mke wa Mheshimiwa huyo, kwani alimkatalia mume wake kata kata, na hata kutishia kuvunjika ndoa. Mama huyo alimwambia mumewe kuwa amtizame mbunge mmoja toka kanda ya ziwa aliyejiuzuru kwa kushawishiwa na kundi lako, na sasa anavyoteseka, maana hata nauli inamshinda.

Kumekuwa na mipango ya kupeleka ktk Halmashauri Kuu ya Chama ijayo hoja ya kutenganisha kofia ya Uenyekiti na Urais, HOJA hii inatoka kwako, na watu wako ndio wanayoiuza kwa wajumbe. Je, hizi sio hujuma kwa Mwenyekiti unayedai kuwa hamkukutana mitaani? Kuipeleka hoja hii ktk vikao vya Chama kunamsaidia nini Mwenyekiti wa Chama?

Hivi karibuni tumemshuhudia Kiongozi mmoja wa UVCCM akiwakemea VIONGOZI wake akiwa Arusha. Siku chache baadae ulimwita na kumpongeza kwa utumbo aliousema. Leo hii unatuambia kuwa eti huhusiki na mgogoro wa kisiasa mkoani Arusha, maneno hayo kawaambie wajinga, welevu wanajua nini kinachoondelea. Halafu umejichanganya ktk maelezo yako kwa kutoa rai kuwa UVCCM waachwe wafanye mambo yao Hivi hiki kinachoendelea UVCCM unaona kinafaa hata waachwe? Wote wanaeleta fujo ndani ya Chama na Jumuiya zake ni watu wako wa karibu, utakaaje kuwa nawe huhusiki? Mbona hatujasikia ukiwakemea waache ujinga wanaoufanya?

Mh. Lowasa, hivi ni kweli kuna kundi la watu wanaotaka kukugombanisha wewe na Rais au wewe na tamaa zako ndio unajigombanisha na Rais? Hivi utaacha lini uongo wa namna hii? Nilidhani ulipoenda kwa TB Joshua basi utaenda kuungama, kumbe sio vile hata kidogo. Tutamwambia Rev. Joshua azidi kukuombea angalau uache tabia ya kusema uongo.

Kusema ukweli hotuba yako ya leo imekera saana na hasa pale unapotumia nafasi zako mbali mbali ulizoshika na unazoshika kukinga maovu yako. Ulishindwa kujirekebisha tabia yako ulipopewa Uwaziri Mkuu na JK, ukatuingiza ktk RICHMOND. Baada ya kushinikizwa UJIUZURU ukadai bungeni kuwa umeonewa. Waziri Mkuu anaonewa na nani????? Nenda kawadanganye hao hao wenye njaa na walio tayari kuona Taifa lao linaingia ktk matatizo kwa ajili ya kukutetea.

Nakushauri ukae kimya au la, utaumbuka kuliko unavyodhani. Utashinda mahakamani kuwashitaki waandishi wote wa habari, maana hata hao wanaokutetea itafika wakati watazidiwa nguvu na Umma. Mh. Lowasa, kubali tu kuwa tamaa zako ndio zimekufikisha hapo. Usichokonoe mengine ambayo watu walikuwa wameamua kukusitiri.

Points tupu anajidai kuhadaa umma wakati moto kauwasha mwenyewe anaona unataka kumuunguza anaanza kupayuka
 
Mimi kwa upeo wangu huwa najaribu kuchunguza kwa kina makosa ya lowasa katika uongozi lakini bado sijawahi kuona kosa kubwa ambalo linawazidi wengine maana kuna wenye makosa makubwa zaidi katika uongozi na bado wapo madarakani
Pia nimekuwa nikijaribu kufuatilia ufisadi wake kwa kweli ushahidi kamili hamna!! Hela alizonazo na mali ni za kawaida sana kwa mtu ambaye amefanya kazi sehemu nyeti za serikali kama yeye kwa muda mrefu namna hiyo ukilinganisha na wenzake
Lingine ni kwamba siyo siri Tanzania tumepoteza mwelekeo siku nyingi na kama tukiendelea hivi hatutakaa tuwe na maendeleo yetu wenyewe..... Bunge linatumia muda mrefu sana kufuatilia na kujadili nani kaiba nini au fulani ana mali gani badala ya kujadili matatizo ya wananchi.
Western country wanapokuja kuomba tenda nchini ukiwa mzalendo nawe umeomba hiyo tenda hua wanahonga waandishi ili uanze kuchafuliwa kuwa fedha na uwezo wako ni wa kifisadi and atlast mikataba ya uwekezaji wanapewa wageni na wazalendo walio na hela za kuwekeza nchini kwetu zinaozea kwenye mabank ya nchi za nje maana tanzania hamtaki kuwapa fursa za kuwekeza nyumabni....wakati umefika ndugu zangu tuwabebe wazalendo wawekeze mali zao ndani ya nchi ili kukuza ajira kwa vijana wetu na kuongeza mzunguko wa hela yetu.
Mwisho mzee lowasa kashastaafu uwaziri mkuu tumwache apumzike kwa amani na tutafute namna ya kumaliza matatizo yetu ya uchumi na si kelele za ufisadi kila siku.

Hivi Lowasa alistaafu au alijiuzuru???

Kama anataka kupumzika kwa amani si aachane na siasa ka RA!!
 
Hongera kwa kuamua kutoa dukuduku lako la moyoni kama tulivyoelezwa na vyombo vya habari kwamba leo (jana) Lowasa kutoa la moyoni. Sasa hayo uliyosema ndio ya kwako ya moyoni?, lakini dukuduku la mioyo ya watanzania ni kujua je zile kashfa zizungumzwazo kuhusu wewe Edward Lowasa mbona hukuzijibu na hicho ndicho watanzania walitegemea kukipata sio uende kuelezea kwenye kikao cha ccm, kwanza kwenye kikao cha ccm ndio ungeongea hayo uliyosema jana, ila mimi nilifikiri tuhuma wanazokutuhumu ndizo zingejibiwa. Hii inaonyesha kabisa umechanganyikiw a na tuhuma hizo na kunauwezekano ni kweli umehusika na hizo tuhuma. maana kama hukuhusika ungejibu tuu kwamba mimi si huki na Richmond au Dowans au Epa au nakadhalika. mbna ni rahisi sana kusema hayo maneno na wala si misamiati migumu, ingawa pia si mtihani kwamba lazima ujibu.
 
Eeeeeh; Kweli ukistajabu ya musa utaona ya filauni.Ndg yangu lowassa unasemwa kwa mambo yafuatayo:
Kwanza: Umefanya mbinu ya kuiibia serikali kupitia EPA ili kumweka Kikwete Madarakani ambaye ameshindwa kuongoza nchi leo kila mwananchi anasota, na kikwete anachekachekatu .
Pili. Umeliasababisha hasara Taifa kwa Kuingia Mikataba mibovu na Kitapeli ya Richmond na Hatimaye Dowans.Tatu umekuwa kamanda na master mind wa wizi serikalini ukimtumia Mwanasheria Andrew Chenge kuiibia serikali ya Watanzania na mengine mengi hayo ndo tunajua sisi na ndo tunayoyasema. Swala la kumhujumu raisi siyo letu, tena kama uanuwezo ungemtoa kabisa maana ameshindwakazi. wewe ulijitosa kumtetea apate kiti hicho kwa vile ulijua udhaifu wake ndo maana unasisitiza kuwa hamkufahamiana barabarani. kikubwa mnatakiwa wewe na swahiba wako mkae chini mtafakari muwaombe radhi watanzania kwa shida wanazo zipata.Usiwatishie waandishi sasahivi umechelewa watanzania tunahasira, na hilo mlijue wazi wanatamani wawakamate na kuwanyonga hadharani. Serikali imekosa heshima kwa tabia yake ya wizi na uonezi wa hadharani. Ebu fikiria mkuu wa wilaya ni mtu mkubwa na wa heshma serikalini lakini Watanzania walivyochoka na kukerwa na tabia wanadiriki kumkamata na kumpeleka polisi. Tumechoka na shida za mfumko wa Bei, umeme, njaa, maji safi hakuana. Hivi Hamuoni Hayaaaaaaaaaaaa aaaaaaaaaaaaaaa aaaaaaaaa!!!!!! !!!!!
 
Eeeeeh; Kweli ukistajabu ya musa utaona ya filauni.Ndg yangu lowassa unasemwa kwa mambo yafuatayo:
Kwanza: Umefanya mbinu ya kuiibia serikali kupitia EPA ili kumweka Kikwete Madarakani ambaye ameshindwa kuongoza nchi leo kila mwananchi anasota, na kikwete anachekachekatu .
Pili. Umeliasababisha hasara Taifa kwa Kuingia Mikataba mibovu na Kitapeli ya Richmond na Hatimaye Dowans.Tatu umekuwa kamanda na master mind wa wizi serikalini ukimtumia Mwanasheria Andrew Chenge kuiibia serikali ya Watanzania na mengine mengi hayo ndo tunajua sisi na ndo tunayoyasema. Swala la kumhujumu raisi siyo letu, tena kama uanuwezo ungemtoa kabisa maana ameshindwakazi. wewe ulijitosa kumtetea apate kiti hicho kwa vile ulijua udhaifu wake ndo maana unasisitiza kuwa hamkufahamiana barabarani. kikubwa mnatakiwa wewe na swahiba wako mkae chini mtafakari muwaombe radhi watanzania kwa shida wanazo zipata.Usiwatishie waandishi sasahivi umechelewa watanzania tunahasira, na hilo mlijue wazi wanatamani wawakamate na kuwanyonga hadharani. Serikali imekosa heshima kwa tabia yake ya wizi na uonezi wa hadharani. Ebu fikiria mkuu wa wilaya ni mtu mkubwa na wa heshma serikalini lakini Watanzania walivyochoka na kukerwa na tabia wanadiriki kumkamata na kumpeleka polisi. Tumechoka na shida za mfumko wa Bei, umeme, njaa, maji safi hakuana. Hivi Hamuoni Hayaaaaaaaaaaaa aaaaaaaaaaaaaaa aaaaaaaaa!!!!!! !!!!!

nne: bado yuko huru na kuwaita wandishi mpaka kwake monduli......wizi wa huyu jamaa ni very very unique.

fikiria tena na tena utagundua kuna tatizo sana upande wako..

maana kuna uwezekano angechukua mkeo ungeandika

sita: ulimchukua mke wangu na leo ninaumia sana

poor Tanzananian
 





*Akana kumhujumu rais, kuchochea UV-CCM
*Akwepa kuongelea Dowans, kujivua gamba
*Asisitiza hajakutana na JK barabarani


Na Waandishi Wetu, Arusha

ALIYEKUWA Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa amejitenga na tuhuma zilizogaa kuwa anaandaa mikakati ya kumhujumu
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, akisema atakuwa mtu wa mwisho kufikiria au kupanga njama hizo.

Akizungumza na wandishi wa habari nyumbani kwake Monduli, Arusha jana, Bw. Lowassa alisema kuwa amemuunga mkono Rais Kikwete kwa dhati kwa muda mrefu na kushirikiana naye katika harakati nyingi za kifikra na za kiuongozi katika ngazi mbalimbali kwa miaka mingi.

Uamuzi wake kukutana wandishi wa habari jana, alisema hauna makusudi ya kuzozana na vyombo vya habari wala kwenda kinyume na utamaduni wa kimaadili wa chama chake, bali kutoa ufafanuzi na angalizo kwa pande hizo mbili ambazo zinaguswa na matukio yanayoendelea kutokea.

Bw. Lowassa ambaye alikataa katakata kuzungumzia masuala yanayoendelea kuvuma kwa sasa, ya Richmond, Dowans wala falsafa ya kujivua gamba ndani ya CCM, akiahidi kuyazungumzia wakati mwingine, alisema kumhusisha na tuhuma za kumhujumu rais ni mambo ya kipuuzi, kizushi na yenye malengo machafu.

Akifafanua tuhuma hizo zilivyo, Bw. Lowassa alisema wahusika wanavitumia vyombo vya habari na wamefikia hatua ya kudai kwamba ameanza kuandaa orodha ya kile wanachokiita madhambi ya Rais Kikwete, ambayo amepanga kuyasoma wakati wa kikao kijacho cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.

"Ninaamini kwa dhati kabisa kwamba, waandishi wa habari wanaofuatilia kwa karibu na kwa umakini mwenendo wa masuala ya kisaiasa nchini wanatambua kwamba, watu wanaopenyeza taarifa hizi katika vyombo vya habari wanafanya hivyo kwa malengo ya kufikirika na kujisafishia njia kisiasa.

"Ni jambo lisiloingia akilini kunihusisha na kile kinachoitwa mikakati ya kumhujumu rais au chama ambacho mimi ni kada wake wa muda mrefu, mbunge anayetokana na chama hicho hicho na mtu anayeiongoza Kamati nyeti ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na zaidi ya yote kiongozi wa ngazi mbalimbali za kisiasa na kiserikali nilizowahi kushikilia.

"Kuhusu hili, napenda kusema kwa uwazi kwamba, mbali ya ukweli kuwa sijapata kufikiria hata mara moja kuhusu hicho wanachokiita mabaya au madhambi ya rais, sina, wala siijui hiyo wanayoitaja kuwa ni orodha ya mabaya ya namna yoyote dhidi ya Rais Kikwete.

"Mbali ya ukweli kwamba huo ni uongo wa wazi, silika yangu kama mwanasiasa na mtu mwenye dhamana kubwa kwa watu wa Monduli na kwa taifa langu, haiwezi kamwe kunituma nianze kupanga mikakati ya kumhujumu kiongozi wetu mkuu au chama ambacho kimenilea na mimi mwenyewe nikakitumikia kwa uadilifu na kwa juhudi kubwa pengine kuliko ilivyo kwa hao wazushi.

Bw. Lowassa alikwenda mbali hadi kuzungumzia urafiki kati yake na Rais Kikwete: "Nilipatana kulisema hili na leo nalirudia tena. Mimi na Rais Kikwete hatukukutana barabarani."

Aliongeza: "Tangu serikali ya awamu ya nne iingie madarakani kuna kundi la watu limekuwa likifanya juhudi kubwa kunigombanisha na rais wakitumia kila aina ya hoja za kupikwa. Kundi hilo ... ndilo ambalo mwaka juzi lilipenyeza ndani ya chama chetu na katika jamii hoja kwamba nilikuwa nimejipanga kugombea urais kwa tiketi ya chama chetu katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana," alisema Bw. Lowassa.

"Mwenyekiti wetu wa Taifa, Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete hawawezi kamwe kuamini, kushawishiwa na propaganda chafu zinazoendeshwa na kikundi kidogo cha wanasiasa hao.

Kuhusu matuko ya UVCCM
"Kama hiyo haitoshi, wanasiasa hao hao baada ya kulitumia jina langu kama ajenda yao ya uzushi wa kila namna, sasa wameanza kunihusisha hata na matukio ya kisiasa kama yale yaliyotokea majuzi tu hapa Arusha.

"Ndugu wanahabari baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu sasa, nimeamua kuanza kuchukua hatua mbalimbali za kisiasa na kisheria ambazo anamini zitatoa majibu sahihi dhidi ya wale wote walio nyuma ya ajenda hizi chafu, kwa lengo la kuweka kumbukumbu sawia ndani ya chama changu na kwa jamii nzima ya Watanzania ambao kwa muda mrefu wamelishwa mambo mengi ya kizushi na wakati mwingine ya hatari dhidi yangu.

Hatua kwa vyombo vya habari
"Tayari nimepanga kuanza kuwasiliana na kuwasilisha malalamiko yangu kwa mamlaka husika zinazosimamia mienendo ya kimaadili na weledi wa kitaaluma wa vyombo vya habari kama vile Msajili wa Magazeti na Baraza la Habari Tanzania.

Alisema kama hiyo haitoshi, baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu ameanza kufikiria na kujipanga kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa habari na wahariri ambao kwa makusudi wameamua kutumia vibaya uhuru wa habari ambao serikali imeutoa.

Alisema kuwa anaamini wote wanakubaliana kuwa uhuru usio na nidhamu ni fujo.

Mbunge huyo, aliwataka viongozi wenye mawazo ya namna hiyo kutambua kwamba, muda adhimu wanaoutumia kubuni na kuzusha uongo kila kukicha mbali ya kuwavunjia heshima wao wenyewe unavidhalilisha vyombo vya dola ambavyo vinafanya kazi kubwa kuhakikisha hujuma za namna yoyote dhidi ya viongozi na taifa zinadhibitiwa.

Alisema kuwa akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ya Bunge na mtu aliyepata kuwa Waziri Mkuu anatambua na kuiheshimu kwa dhati kazi hiyo kubwa inayofanywa kwa weledi mkubwa na taasisi mbalimbali za dola zenye wajibu wa kuhakikisha ulinzi na usalama wa viongozi na taifa kwa ujumla.

Uchumi, ajira kwa vijana
Akizungumzia hali ya uchumi, Bw. Lowassa alisema kuwa uchumi wa dunia upo taabani na Tanzania inakabiliwa na hali mbaya, kwani shilingi inazidi kuporomoka vibaya na mfumuko wa bei unazidi kuelekea kubaya zaidi.

Aliongeza kuwa kuna tatizo kubwa la ajira kwa vijana, na wengi wao wamekuwa wakiishi katika hali ngumu, jambo ambalo alilitafsiri kuwa ni sawa na kukali bomu la muda na litasababisha kuvunjika kwa amani, hivyo akashauri kutafuta suluhu ya mambo hayo.

Katika mapendekezo yake, Bw. Lowassa alisema serikali ikope fedha ijenge viwanda ambavyo vitaweza kuajiri vijana wengi nchini.
 
nne: bado yuko huru na kuwaita wandishi mpaka kwake monduli......wizi wa huyu jamaa ni very very unique.

fikiria tena na tena utagundua kuna tatizo sana upande wako..

maana kuna uwezekano angechukua mkeo ungeandika

sita: ulimchukua mke wangu na leo ninaumia sana

poor Tanzananian

Indepentent Thinker Waberoya.
Mkuu, umejichimbia wapi wewe mtu muhimu sana humu jamvini
 
hapa ndipo napochukia watu aisee
kuna watu wana viburi vya uzima
i hope iko siku isiyo na jina.......
 
Huyu jamaa anajimaliza mwenyewe! yani awatoe waandishi kote huko kisha awapige bit badala ya kuongea mambo muhimu kama Richmond
 
Miminilimshauri EL vitu vinchache na vyepesi, ujue ndugu zangu katika zunguka zangu nimegundua sisi watz ni watu wepesi sana wa kusamehe huyu bwana mkubwa tungemsamehe kama;

1.Aongee ukweli kuhusu richmond, dowans etc etc kwani siasa sasa zimeshapita muda wa kuspin mambo ulikua ule 2008 siyo sasa, na kiusanii alie kidogo kama Mathieu Kerekou kule Benin mwaka 91 alisamehewa kwa mabaya yake na akaja kuwa rais wa kuchaguliwa miaka iliyokuja

2. Asapoti sera zenye maslahi kwa taifa kama katiba mpya na ahadi kuzitekeleza kwa pamoja na wapinzani na wananchi wote kwa ujumla.

3. atangaze mali zake itamuondelea yale yaliyosemwa na baba wa taifa na itamvua gamba kuonekana ni mtu anayeweza kuleta serikali ya kizalendo

4. Aanze kutembea tembea na kutoa misaada ya hapa na pale kurudisha imani kidogo..sasa huyu ataua Rais wa Monduli au Tz, wiki 2 hazipiti yuko monduli ah!
 
Ila ana moyo of all the things vilivyomtokea na yanayoendelea kuzungumzwa juu yake bado ana guts za kusimama mbele ya vyombo vya habari na kuongea.
Uraisi jamani ni noma watu wanaupigania by all means possible!
 
Du! Nchi yangu Tanzania nakupenda. Inatia shaka sana,pamoja na kutoeleza watanzania kuhusu mambo mengi yeye utata kuhusu yeye El. Ndugu anaongelea kero zinazo wagusa wa Tz na haswa vijana.kwa kuongelea kukopa na kuanzisha viwanda ili ajira zipatikane.SWALI LANGU NI VIPI ANAONGELEA VIWANDA WAKATI NISHATI YA UMEME NI TATIZO HIVYO VIWANDA VITAENDESHA NA NINI? Kwa mtazamo wangu naona muda umempita EL WATZ WAMEJUA NA WAMEBADILIKA NI VEMA AAChane na mdudu siasa kwani alikwisha chafuka. JE ANAWEZA AKAMWAMINISHA NANI KTK ULIMWENGU HUU WA SAYANSI NA TEKINOLOGIA KWAMBA KWASABABU ALIKUWA NIGERIA ASINGEWEZA FAHAMU YALIYO KUWA YANATOKEA ARUSHA! Wakati utafika mambo yatakua wazi haita jalisha mlikutana wapi. Nb.: hekima nikuwa mkweli na kuutafuta ukweli kwa njia yoyote iwayo na sio kukaa kimya. Mungu ibariki Tanzania na watu wake.
 
Sasa kama hakutaka kuzungumzia masuala ya Richmonduli, ambayo tulitaka kuelewa msaimamwake,kwa nini aliwaita waandishi? Anataka tusikie anayotaka yeye? Aache upuuzi! Ipo siku ataLAZIMIKA kuyajibu hata kama ni katika mahakama, kama sio nchini, basi kwa OKAMPO!
 
1. 1995 Kikwete alivyoenda kuchukua fomu naye wakiwa angani kwenye ndege Lowassa naye akasema anataka kuchukua fomu. Haingii akilini kama si msaliti ni nini?pamoja na hayo JK alimsamehe baada ya usuluhishi chini ya Samwel Sitta. lakini akazua jipya Bwana Lowassa.

2. Akiwa waziri mkuu akaitisha jopo la wapambe wake Dodoma na kupanga mikakati ya kutwaa Urais 2010 akisema "huyu mswahili term moja inamtosha" hili liliuuma sana JK akamuita Msuluhishi Mzee Sitta akasema "niaachie kwanza ana machafu mengi sana" Lowassa akachunguzwa kashfa ya Richmond akatolewa uwaziri mkuu.

3. Ugomvi mzito wa kifamilia Fred Lowassa na Bashe wametumia vyombo vya habari kuchafua familia ya JK. HASA Ridhiwani na mama Salma . Urafiki wa Fred na Ridhiwan umevunjika kabisa. Fred kajilimbikizia mali kipindi kifupi ili kufuta holo kamtengenezea zengwe Ridhiwani. watoto na wazazi sasa hawapataniii.

(To be Continued....)
STAY ON TUNE!!!
 
Back
Top Bottom