Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
Mchakato wa kutafuta mgombea urais kwa tiketi ya CCM umeshakamilika, na mgombea aliyepatikana ni John Pombe Magufuli. Pamoja na hayo, ukweli unabakia kwamba katika mchakato wa kutafuta wadhamini, ni Edward Lowassa ndiye aliyeungwa mkono na wanachama na makada wengi wa CCM kuliko mgombea mwingine yoyote.
Edward Lowassa aliungwa mkono na wanachama karibia milioni moja wa Chama Cha Mapinduzi. Pamoja na jina la Edward Lowassa kutorudishwa na vikao vya ngazi za juu ya CCM, kuelekea uchaguzi mkuu, suala la Lowassa kupata wadhamini karibia milioni moja ni suala ambalo halitakiwi kuchukuliwa kimasihara au kubezwa, kote - ndani na nje ya CCM. Kwanini tunasema hivyo:
1. Wadhamini hawa karibia milioni moja ni mchanganyiko wa wanachama na viongozi wa ngazi mbali mbali wa CCM. Wanatoka katika kona mbalimbali za Tanzania. Ni hawa ambao kwa kawaida, ndio wanaochukuaga jukumu la kumbeba na kumnadi mgombea urais (CCM) baada ya jina la mgombea kupatikana.
2. Kwa kuzingatia historia inavyotueleza, upinzani umeweza kunyakua makada wengi wa CCM baada ya makada hao kuenguliwa majina yao na vikao vya juu vya chama, licha ya makada husika kukubalika na kuwa chaguo la wanachama na makada wengi wa ngazi za chini. Kilichofuatia ni kwamba, CCM ilikuja kupoteza majimbo kadhaa kwa upinzani.
Kama ilivyotokea huko nyuma kwa makada kadhaa kuenguliwa katika vinyanganyiro cha ubunge hivyo safari yao ya matumaini kuzimishwa na vikao vya juu vya CCM licha ya kukubalika na makada wengi wa ngazi za chini za CCM, hali hii imejitokeza kwa mara ya kwanza katika kinyanganyiro cha kutafuta mgombea urais (CCM) ambapo, Safari ya matumaini ya Edward Lowassa kubeba bendera ya CCM (urais) 2015, Safari hiyo imezimwa rasmi na vikao vya juu vya chama cha mapinduzi. Je:
· Edward Lowassa alikosea wapi katika safari yake ya matumaini ndani ya CCM?
Na iwapo itatokea akashawishika kuendelea na safari yake ya matumaini kupitia chama kingine cha siasa kama ilivyotokea kwa makada wengine walioenguliwa kwenye vinyanganyiro vya ubunge (CCM), ili kutimiza safari yake ya matumaini nje ya CCM, je:
· Edward Lowassa arekebishe wapi ili kufika safari yake ya matumaini nje ya CCM?
Edward Lowassa aliungwa mkono na wanachama karibia milioni moja wa Chama Cha Mapinduzi. Pamoja na jina la Edward Lowassa kutorudishwa na vikao vya ngazi za juu ya CCM, kuelekea uchaguzi mkuu, suala la Lowassa kupata wadhamini karibia milioni moja ni suala ambalo halitakiwi kuchukuliwa kimasihara au kubezwa, kote - ndani na nje ya CCM. Kwanini tunasema hivyo:
1. Wadhamini hawa karibia milioni moja ni mchanganyiko wa wanachama na viongozi wa ngazi mbali mbali wa CCM. Wanatoka katika kona mbalimbali za Tanzania. Ni hawa ambao kwa kawaida, ndio wanaochukuaga jukumu la kumbeba na kumnadi mgombea urais (CCM) baada ya jina la mgombea kupatikana.
2. Kwa kuzingatia historia inavyotueleza, upinzani umeweza kunyakua makada wengi wa CCM baada ya makada hao kuenguliwa majina yao na vikao vya juu vya chama, licha ya makada husika kukubalika na kuwa chaguo la wanachama na makada wengi wa ngazi za chini. Kilichofuatia ni kwamba, CCM ilikuja kupoteza majimbo kadhaa kwa upinzani.
Kama ilivyotokea huko nyuma kwa makada kadhaa kuenguliwa katika vinyanganyiro cha ubunge hivyo safari yao ya matumaini kuzimishwa na vikao vya juu vya CCM licha ya kukubalika na makada wengi wa ngazi za chini za CCM, hali hii imejitokeza kwa mara ya kwanza katika kinyanganyiro cha kutafuta mgombea urais (CCM) ambapo, Safari ya matumaini ya Edward Lowassa kubeba bendera ya CCM (urais) 2015, Safari hiyo imezimwa rasmi na vikao vya juu vya chama cha mapinduzi. Je:
· Edward Lowassa alikosea wapi katika safari yake ya matumaini ndani ya CCM?
Na iwapo itatokea akashawishika kuendelea na safari yake ya matumaini kupitia chama kingine cha siasa kama ilivyotokea kwa makada wengine walioenguliwa kwenye vinyanganyiro vya ubunge (CCM), ili kutimiza safari yake ya matumaini nje ya CCM, je:
· Edward Lowassa arekebishe wapi ili kufika safari yake ya matumaini nje ya CCM?
Edit Post

