Elections 2015 Lowassa kuzungumza na wanahabari baada ya kumaliza kikao kizito na familia pamoja na marafiki zake

Elections 2015 Lowassa kuzungumza na wanahabari baada ya kumaliza kikao kizito na familia pamoja na marafiki zake

Updates za JPM hizi hapa """1. Nyumba za Serikali
Kwa hakika hili ni doa kubwa sana kwa Magufuli. Ni katika kipindi alichokuwa Waziri wa Ujenzi (awamu ya 3) alishawishi kwa nguvu na msukumo mkubwa sana mpaka kufanikiwa uuzaji wa nyumba za serikali.

Hii hatua ya Magufuli halina tofauti na kile alichokiita CAG Professor Assad “Political Entrepreneurship”. Professor Assad mara baada ya kuingia madarakani alisema wazi kwamba mradi wa Magufuli wa kuuza nyumba za serikali ni ufisadi mkubwa sana. Professor Assad alizidi kusema ya kwamba alichokifanya Magufuli yalikuwa kwa manufaa yake binafsi na ilikuwa ni “personal political entrepreneurship”.

Katika uamuzi huo, Magufuli alienda mbali zaidi mpaka kugawa bure baadhi ya nyumba kwa ndugu zake na mahawara zake. Kwa mfano Dada Kabula ambaye ni mmiliki hewa wa Kebby’s Hotel iliyopo Mwenge/Bamaga jijini Dar es Salaam. Dada Kabula ambaye hajawai kuwa mtumishi wa umma tokea awamu ya kwanza mpaka leo hii Ocampo ninaposhusha huu uzi alifanikiwa kuhongwa nyumba mbili zenye Plot No. MSM/201 na Plot No. MK/521 (Mikocheni na Msasani).

Kwa hatua hiyo Magufuli aliliingiza serikali hasara kubwa sana, na hayo machungu mpaka leo hayajaisha na serikali bado linaendelea kubeba mzigo. Katika kipindi hiki tumeshuhudia watumishi wengi (Majaji, na watendaji wakuu, makatibu wakuu) wamekuwa wakiishi hotelini, huku gharama za vyumba zikiwa za hali ya juu sana almost dola 1200-1500 kwa mwezi ambayo ni sawa na Millioni 27 kwa mwezi; kwa mwaka ni Millioni 324 kwa mtumishi moja.



2. Ujenzi wa Barabara
Eneo hili ni sehemu nyingine ambayo Magufuli amekuwa akijipatia fedha haramu. Baadhi ya wafuasi wake wamekuwa wakijaribu kusema kwamba ni TANROADS ndiyo wahusika wakuu katika barabara na siyo Magufuli. Ingawa hoja yao siyo ya kweli na haina mashiko.

Kiutaratibu na sheria barabara utakiwa kuwa na upana (width) wa 6.5m ila imegundulika barabara nyingi kipindi hichi cha Magufuli zimekuwa zikijengwa kwa 5.7m to 6m na siyo 6.5m, je fedha za hizo baki 0.5m to 0.8m zinakwenda wapi, ni wazi fedha hizo uingia mifukoni mwa Magufuli na washirika wake wa Tanroads. Vile vile ni kipindi kirefu sasa Highway Economic Assessment ya miradi ya barabara imekuwa hazifanyiki kitu ambacho kinapelekea barabara zetu nyingi kuwa chini ya viwango. Utafiti wa Ocampo unaonyesha kwamba barabara kuwa chini ya viwango ni swala la makusudi ambapo waziri na wasimamizi wa miradi husika wanakula na kugawana fedha za miradi….


3. Sakata La Bomoa Bomoa
Ni jambo la wazi ya kwamba sheria zimetumgwa ili zifuatwe, lakini kuwa na ubinadamu au utu ni zaidi ya sheria. Ni Magufuli huyu huyu alipigwa stop na Mh. Rais pale alipoona Magufuli anakiuka wazi haki za binadamu. Ubomoaji wa nyumba zilizopo pembezoni mwa barabara umekuwa hauzingatii “UTU”. Ni jambo la wazi wanaanchi wengi waliobomolewa nyumba zao mpaka sasa wako katika hali ngumu ya maisha na hawana uelekeo baada ya kufanyiwa unyama usiyothimilika na Magufuli.

Either wataalamu wengi pale wizarani katika mahojiano wanasema Magufuli hana tabia ya kufata sheria na utaratibu, wakitolea mfano swala la kuvunjwa kwa jengo la TANESCO (Ubungo) na jengo la Millenium Towers. Kwa hakika ni jambo jema sana kuwa na Rias kama JK aliyediriki kumpiga stop Magufuli, hivyo basi ni wazi anapaswa apate mtu wa juu yake katika kufanya maamuzi, ila yeye ndiyo akiwa mtoa maamuzi walai nchi tutaipoteza (Tafakari kwa kina).


4. Shelly Ya Mwanza
Tukizidi kukumbuka sakata la Shelly ya Mwanza ndipo tunazidi kujua jinsi gani Magufuli ni mtu wa kukurupuka na mtu mwenye chuki. Kwa chuki zake binafsi kipindi cha awamu ya 3 akiwa waziri wa ujenzi aliamuru kuvunjwa kwa Shelly ya bwana Mansoor (mbunge wa Kwimba) iliyopo maeneo ya madaraka misheni jijini Mwanza. Baada ya ukiukwaji huo wa sheria bwana Mansoor alienda mahakamani na kisha kushinda kesi na hukumu kutolewa kwamba serikali imlipe Mansoor mabillioni ya fedha, sababu kubwa zikiwa ni chuki na kisasi cha Magufuli……

5. Magufuli ni mtu mwenye kiburi, majivuno na hashauriki
Sifa zingine pekee za Magufuli ni mtu mwenye kiburi, majivuno na hashauriki kitu ambacho ni hatari sana kwa ustawi wa Taifa. Hayo mambo yamepelekea hata utendaji kazi wa watumishi wa chini kuwa mgumu sana. Watumishi chini ya wizara yake wanasema Magufuli ni mtu mwenye majivuno sana, ni mtu mwenye chuki na ni mtu asiyepokea ushauri wa mtu yeyote yule zaidi ya mke wake na Kabula…

6. Umiliki wa Kebby’s Hotel
Kebby’s Hotel ni hoteli iliyopo Mwenge/Bamaga upande wa kulia kama unaenda posta/mjini. Kwa muda mrefu mmiliki wa hoteli hiyo amekuwa akijificha katika mgongo wa mtu mwingine ila ukweli ni kwamba mmiliki halali wa hoteli hiyo ni John Pombe Magufuli na siyo Dada Kabula.

Umiliki wa Hoteli kubwa kama Kebby’s ambayo kulala ni zaidi ya dola 60-90 inaonyesha wazi kwamba Magufuli ni fisadi wa kimya kimya kama yule jamaa mwingine aliyepiga za Escrow na vibali vya sukari au yule aliyechimbia fedha za Ghadafi kwenye mahandaki.

7. Kuvunja Ndoa
Katika maandiko Matakatifu, Kumbukumbu la Torati 27: 14 imeandikwa alaaniwe yule amtamaniye mke wa nduguye au jirani yake. Ila kinyume na hayo maandiko Matakatifu Magufuli amediriki kumtamani mke wa jirani yake mpaka kupelekea kuvunja ndoa ya mtu.

Dada Kabula ambaye ni mmiliki hewa wa Kebby’s Hotel, awali alikuwa mke wa Januarius Maganga ambaye ni mtumishi mwandamizi katika makampuni ya IPP Media. Swali la kujiuliza kama Magufuli kadiriki kuvunja ndoa ya mtu angali ni waziri wa kawaida tu, je akiwa Rias itakuwaje? Jibu nafkiri unalo…. Na sitaki unipe jibu.

Nyerere katika moja ya hotuba zake aliwahi kutolea mfano sakata la waziri mdogo wa Uingereza aliye onekana na kimada barabarani. Kwa tamaduni za hao wenzetu huo ulikuwa ukosefu mkubwa wa maadili mpaka ikapelekea kufukuzwa kazi na waziri mkuu wa wakati huo.

8. Magufuli Hakifahamu Chama Vizuri
Ni jambo la wazi na ukweli usiopingika kwamba Taifa linatafuta Rais bora na kwa upande mwingine CCM kinatafuta mtu mwenye uwezo wa kushika kofia mbili kwa pamoja.

Magufuli ana utamaduni wa kutumia chama pale anapoitaji madaraka, ila pale tu anapoyapata hayo madaraka anakuwa ajiusishi na mkakati wowote wa kujenga chama. Historia inaonyesha Magufuli hajawahi kushika wadhifa au nafasi yoyote ile ndani ya chama, wanachama wa CCM wanauliza kwamba watamkabidhi vipi mtu asiye na background nzuri kwenye chama? Vile vile historia inaonyesha hajawahi kuchangia hata senti tano katika shughuli zozote zile zenye lengo la kujenga chama.

9. Sakata La Samaki
Katika muendelezo wa kukurupuka katika maamuzi, Waziri Magufuli mwaka jana tena aliliingiza Taifa na serikali kwa ujumla katika hasara nyingine. Ambapo serikali iliamuriwa na mahakama ilipe kiasi cha shilling Billioni 2.8 na kurudiha meli husika baada ya kukiuka sheria za kimataifa pale alipokamata Meli yenye vibali halali na iliyokuwa inafanya shughuli zake kihalali.

Sasa kama ni waziri wa kawaida anadiriki kuvunja sheria za kimataifa, Je akiwa Rais si ni wazi anaweza kulipelekea Nchi ikatengwa na jumuiya za kimataifa….. we need to think kwa umakini sana wakuu…..



10. Sakata La Kivuko
Dhana ya ubinadamu siyo kuvaa nguo au kulala kwenye nyumba bali ubinadamu ni pamoja na kuwa na hekima, busara na kauli nzuri kwa binadamu wenzako; cha kushangaza Magufuli alidiriki kutumia lugha iliyotafsiriwa kama tusi kubwa sana na wananchi wa Dar es Salaam, pale alipoowambia wapige mbizi wakitaka kwenda Kigamboni. Ni jambo jema kwa kiongozi kuwa na msimamo ila msimamo wake uendane na lugha nzuri, ya uungwana na ya ubinadamu. Ni wazi kauli hiyo iliwauzinisha sana na kukasirisha wananchi wengi Dar es Salaam. Ubinadamu na utu ni kitu cha bure na siyo cha ulazima, hivyo ilitegemewa Magufuli awe na kauli nzuri na yenye hekina na busara kwa wananchi husika.

11. Magufuli ni Mtu wa Visasi vya Hatari
Magufuli siyo mtu wa kawaida kabisa, ndani yake amejaa chuki na visasi. Ni mtu wa visasi vya ajabu, hii inanikumbusha alipogombea ubunge 1995 na bwana Ernest Nyororo. Baada ya kushindwa katika kura za maoni ila baadaye alipoteuliwa bila uwoga alianza kumshughulikia Nyororo mpaka ikampelekea Nyororo akapata shinikizo la moyo. Kumbuka Nyororo ni ndugu yake wa damu sasa sisi wengine itakuwaje, ni wazi hili jambo linaitaji tafakari ya kina. Kama ndugu yake anaweza kumshambulia kiasi hicho iweje watu wa kawaida….. Leo Ocampo nikiwa naandika huu uzi sisiti kusema ya kwamba hata hao viongozi wanaotaka Magufuli apitishwe naomba niwaambie kwa chuki na kisasi cha Magufuli kuna siku atawabadilikia tena sana sana. Huko mbeleni naomba msije mkasema Ocampo hakutuambia….. Nina hakika asilimia zaidi ya 100 Magufuli ana chuki na viongozi waandamizi wa sasa, chuki hiyo anasubiri kuilipiza muda ukifika….

NB: Je kuna Magufuli Mwingine au ni huyu huyu?...............

Asanteni
Ocampo four"" mwaka huu wataisoma number ...

Mkuu kwa maana halisi na nyepesi ni kuwa jpm ni mtuhumiwa nambari moja wa kufuja mali za serikali?
 
Hongereni wale mlioshinda kule Dodoma, lakini pia poleni sana WANA WA EMAMNUEL NCHIMBI, KINGUNGE NGOMBALE MWIRU, SOFIA SIMBA NA ADAM KIMBISA.Faida za kuwa maarufu wa asili na maarufu wa kutengeneza zimejidhihirisha kwa kile kilichotokea Dodoma. Ni matokeo ya kuwa na hamu ya kweli ya kuwatumikia wanancgi na hamu ya kutengeneza ambayo hapana shana huambatana na matamanio ya kupita kiasi ya madaraka.
Nudgu zangu kuna taarifa ya kuwepo kwa Mkutano baina ya Edward Ngoyai Lowassa na wana Habari, nia na madhumuni kwa mujibu wa chanzo cha habari ni Lowassa kutaka kufukisha ujumbe kwa wafuasi wake kile anachodhani ni kutotendewa haki na vikao vilivyompa ushindi John Pombe Maghufuli kuwa mgombea wa Urais kupitia CCM hapo mwezi Oktoba, 2015.

Maswali yangu kwa Lowassa ni machache tu, anishawishi labda mimi na hata wengine ambao wanataka kuaminishwa kuwa bila Lowassa mchakato ule haukuwa na maana.
1. Lowassa anataka kutuambia kwamba Vikao vilivyofikia uamuzi wa John Pombe Maghufuli kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM si halali?
2.Kati ya Wagombea 37 walioachwa wakiwemo Makamu wa Rais, Mohamed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pindd na Waziri Mkuu msaafu(siyo aliyejiuzulu), Fredrick Tluway Sumaye, yeye ndiye alikuwa na sifa zote kwa maana ya uadilifu, uzoefu ndani ya chama na mwenye kuweka maslahi ya Chama na Taifa mbele kwanza na siyo maslahi binafsi kuliko wenzake?
3. Ni ukweli usiopingika kwamba Lowassa ndiye aliyetumia pesa nyingi kwenye mchakato huu kuliko wagombea wenzake inawezekana kabisa kiasi alichotumia kikawa zaidi ya mara 50 ya kiasi alichotumia John Pombe Maghufuli. Je hilo ndilo tatizo?
4. Haya yaliyotokea halisha wakuta aliyekiwa Katibu Mkuu wa Umoja wa nchi kuru za Afrika, OAU wakati huo, Dr. Salim Ahamed Salim, Makamu na Waziri Mkuu Mstaafu, Mzee john Samwel Malecela na hata Rais wa Sasa Jakaya Mrisho Kikwete. NIni cha ziada alichokuwa nacho Lowassa mpaka aanze kulalamika na tofauti ya waliomtangulia ambao kimsingi waliona CCM ni taasisi na siyo mali ya mtu na hivyo busara ikatawala na maslahi ya chama na Taifa kwa ujumla vikatawala? Lowassa ni mwadilifu, ni mchapakazi kuliko hao wazee, enzi za utumishi wao?

Lowassa aache kutudanganya bwana, angekuwa msafi kiasi hicho angekuwa lulu kwa wapinzani, kwa Chadema ambao kwenye Orodha ya Mafisadi walioisoma pale Mwembe Yanga jina lake limo au hata ACT ambako kauli mbiu yao ni "MUHIMU SIYO MADARAKA, BALI UZALENDO", Chama ambacho sharti moja wapo la kuwa mwanachama wake ni lazima ukataje mali ulizo nazo, LOWASSA atatumia siku ngapi kutaja mali zake ili awe na uhalali wa kiwa mwanachama wa kweli wa ACT kama kweli wanamaanisha? Mrema ni mfano mzuri wa mwadilifu aliyetoka CCM kwenda NCCR tukaona athari zake kwa CCM na siyo Lowass ambaye ameanza kwanza na kupoteza kabisa na kupoteza Kauli mbiu ya baadhi ya vyama kwa kufadhili mikutano ikiwa ni hatua ya kujitengenezea mazingira ya kukubalika lakini baada kuyafunika macho ya viongozi wa vyama hivyo kwa UTANDO wa buibui ili wasahau kuwa nao walikuwa wapingaji wakubwa wa ufisadi wake huko nyuma.
 
Mwanasiasa Edward Ngoyai Lowassa ambaye yupo katika sintofamamu na chama chake CCM atazungumza na waandishi wa habari leo au kesho nyumbani kwake Masaki jijini Dar es salaam iwapo atawahi kumaliza kikao na familia yake.

Taarifa kutoka kwa marafiki wa karibu wa mtoto wa Lowassa Fredy Lowassa ambaye alikuwa kiungo muhimu katika kampeni zake za kuelekea Urais kwa tiketi ya CCM zinaarifu kuwa Lowassa alianza kwa kufanya mazungumzo ya kina na familia yake huku katika kikao hicho Watoto wake wote wakihudhuria lakini pia wakwe zake akiwemo Sioi Sumari na kukubaliana baadhi ya mambo.

Mambo yanayodaiwa kukubaliwa na wanafamilia hao ni kwamba wawe tayari kumfuata katika chama chochote atakachoamua kuelekea, huku akishindwa kubainisha ni wapi atakapoelekea kwani alisisitiza kuwa hawezi kuhama au kutangaza uamuzi wowote pasipo kushauriana na marafiki zake wa karibu.

Hivi sasa waandishi wa habari wamefika nyumbani kwake Masaki hata hivyo wameombwa kuondoka na kuwa na subira kwani Lowassa bado anafanya mazungumzo na marafiki zake muhimu. mashuhuda kutoka eneo la tukio wanadai moja kati ya magari ya watu waliopo Nyumbani kwa Lowassa yameonekana kuwa ni yavmwenyekiti wa ccm wanawake taifa Sophia Simba, Lawrance Kago Masha, Adam Kimbisa, Emmqnuel Nchimbi, Mwenyekiti wa vijana taifa ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Donge zanzibar Sadifa Khamis, Hussein Bashe, Absolomon Kibanda, Khamis Mgeja(mwenyekiti ccm Shinyanga) Msukuma(mwenyekiti ccm Geita), Na Mgana Msindai(mwenyekiti CCM Singida).

===================

UPDATE: 12:40hours

Lowassa kaahirisha kuongea hadi taarifa zaidi itakapotolewa
.

Hana ubavu wa kukihama hilo lichama. Akijaribu tu ndo mwanzo wakuanza kumulikwa na biashara zake zilizo nyuma ya pazia. Akubalianae na matokeo. Bado hata akilazimisha kukihama chama ndo atajichoresha zaidi yatafumuka na yauvunguni,na ule umati wengine ilikuwa upepo na ushabiki tu.
 
Naona bado haamini Cinema ilivyoisha, anaendelea kungojea boti at the airport
 
Hana ubavu wa kukihama hilo lichama. Akijaribu tu ndo mwanzo wakuanza kumulikwa na biashara zake zilizo nyuma ya pazia. Akubalianae na matokeo. Bado hata akilazimisha kukihama chama ndo atajichoresha zaidi yatafumuka na yauvunguni,na ule umati wengine ilikuwa upepo na ushabiki tu.

ccm ni km freemason tu ukiwakiuka wanakumeza
 
Ili kuinusuru CCM ilitakiwa wamshauri asigombee kabisa kwa sababu yote haina ahueni kwa CCM ama angepitishwa, au alivyotemwa.
 
Mkutano wa nini? mtaelewa tu kuwa mkutano ni wa nini ? mwaka huu kura hazitaibika
 
Golden chance ya Lowasa ilikuwa ni vikao vya CCM na vingemkubali basi angetimiza ndotoye ta urais .Sasa kwa kuwa kakosa huko asifanye kosa la kuhama. Atajutia maamuzi hayo mpaka anakufa .Yeye atulie, apewe uwaziri na astaafu kwa heshima. In business tunashauri mtu uwe na calculated risk sasa yeye Ali invest beyond calculated risk. Si Kila mshindani hushinda, kama amefeli vikaoni vya CCM huko kwa plan B au C ataangukia pua pia. Loss is common in any investment, learn from it and move forward.
 
Hongereni wale mlioshinda kule Dodoma, lakini pia poleni sana WANA WA EMAMNUEL NCHIMBI, KINGUNGE NGOMBALE MWIRU, SOFIA SIMBA NA ADAM KIMBISA.Faida za kuwa maarufu wa asili na maarufu wa kutengeneza zimejidhihirisha kwa kile kilichotokea Dodoma. Ni matokeo ya kuwa na hamu ya kweli ya kuwatumikia wanancgi na hamu ya kutengeneza ambayo hapana shana huambatana na matamanio ya kupita kiasi ya madaraka.
Nudgu zangu kuna taarifa ya kuwepo kwa Mkutano baina ya Edward Ngoyai Lowassa na wana Habari, nia na madhumuni kwa mujibu wa chanzo cha habari ni Lowassa kutaka kufukisha ujumbe kwa wafuasi wake kile anachodhani ni kutotendewa haki na vikao vilivyompa ushindi John Pombe Maghufuli kuwa mgombea wa Urais kupitia CCM hapo mwezi Oktoba, 2015.

Maswali yangu kwa Lowassa ni machache tu, anishawishi labda mimi na hata wengine ambao wanataka kuaminishwa kuwa bila Lowassa mchakato ule haukuwa na maana.
1. Lowassa anataka kutuambia kwamba Vikao vilivyofikia uamuzi wa John Pombe Maghufuli kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM si halali?
2.Kati ya Wagombea 37 walioachwa wakiwemo Makamu wa Rais, Mohamed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pindd na Waziri Mkuu msaafu(siyo aliyejiuzulu), Fredrick Tluway Sumaye, yeye ndiye alikuwa na sifa zote kwa maana ya uadilifu, uzoefu ndani ya chama na mwenye kuweka maslahi ya Chama na Taifa mbele kwanza na siyo maslahi binafsi kuliko wenzake?
3. Ni ukweli usiopingika kwamba Lowassa ndiye aliyetumia pesa nyingi kwenye mchakato huu kuliko wagombea wenzake inawezekana kabisa kiasi alichotumia kikawa zaidi ya mara 50 ya kiasi alichotumia John Pombe Maghufuli. Je hilo ndilo tatizo?
4. Haya yaliyotokea halisha wakuta aliyekiwa Katibu Mkuu wa Umoja wa nchi kuru za Afrika, OAU wakati huo, Dr. Salim Ahamed Salim, Makamu na Waziri Mkuu Mstaafu, Mzee john Samwel Malecela na hata Rais wa Sasa Jakaya Mrisho Kikwete. NIni cha ziada alichokuwa nacho Lowassa mpaka aanze kulalamika na tofauti ya waliomtangulia ambao kimsingi waliona CCM ni taasisi na siyo mali ya mtu na hivyo busara ikatawala na maslahi ya chama na Taifa kwa ujumla vikatawala? Lowassa ni mwadilifu, ni mchapakazi kuliko hao wazee, enzi za utumishi wao?

Lowassa aache kutudanganya bwana, angekuwa msafi kiasi hicho angekuwa lulu kwa wapinzani, kwa Chadema ambao kwenye Orodha ya Mafisadi walioisoma pale Mwembe Yanga jina lake limo au hata ACT ambako kauli mbiu yao ni "MUHIMU SIYO MADARAKA, BALI UZALENDO", Chama ambacho sharti moja wapo la kuwa mwanachama wake ni lazima ukataje mali ulizo nazo, LOWASSA atatumia siku ngapi kutaja mali zake ili awe na uhalali wa kiwa mwanachama wa kweli wa ACT kama kweli wanamaanisha? Mrema ni mfano mzuri wa mwadilifu aliyetoka CCM kwenda NCCR tukaona athari zake kwa CCM na siyo Lowass ambaye ameanza kwanza na kupoteza kabisa na kupoteza Kauli mbiu ya baadhi ya vyama kwa kufadhili mikutano ikiwa ni hatua ya kujitengenezea mazingira ya kukubalika lakini baada kuyafunika macho ya viongozi wa vyama hivyo kwa UTANDO wa buibui ili wasahau kuwa nao walikuwa wapingaji wakubwa wa ufisadi wake huko nyuma.
Punguza maneno mengi. Cc tupo tayari kuungana na lowassa. Nyinyi mmeshamkataa sasa acheni kumfatafata. Kumkataa mumkatae kisha mumzuie asihame. Shame on you. Lowassa Ni MTU pekee aliyekuwa na uwezo wa kuubadilisha mfumo mbovu uliowekwa na ccm. Acheni kumtisha. MTU anapendwa na wananchi mnasema amehonga. Nano mwenye uwezo wa kuhonga taifa? Tuko nyuma ya lowassa. Sijawahi kuwa nwana ccm lakini kwa hill am supporting lowassa. In fact mmemzalilisha na kumuita mla rushwa bila kumpeleka mahakani. Kwani mkapa hakuiba? Aliwezeje kumiliki mashamba na kiwanda cha miwa. Kikwete hakuiba? He mwinyi yuko safi?
 
Haamini kilichotokea...ila Mwenyezi Mungu ametuhurumia. Huyu jamaa na yule aliyeanza ku practise urais wote wangetuyeyusha tu. Bora amechukua huyu arrogant atupige ngumi tufanye kazi na kujenga Taifa.
 
Lowasa hataweza kuhama ccm kamwe! Anajua mambo mengi aliyoyafanya na wanayofanya huko ccm ya kufichiana! Kudhubutu kuhama ndo mwisho wake utafika kisiasa. Lakin maombi yangu ahame ccm ili maandiko yatimie.
 
Enemy of my enemy is my friend.Upinzani una kila Sababu ya kushirikiana na Lowassa.
 
Mzee Lowassa

Natumaini unaendelea kujikongoja baada ya a bitter defeat. Lakini nikukumbushe - haya pia yatapita. Mwisho wa siku yote yatapita.

Kumbuka -Jambo la muhimu kuliko yote kwa mtu yoyote ni familia. Bado unayo familia yako iliyo kuwepo na itakayokuwepo.

Kumbuka - Bwana ndio mchungaji wako hutapungukiwa na chochote

Madhumuni ya barua hii ni kukumbusha kile kitabu maarufu cha THE ART OF WAR BY SUN TZU.

Katika kitabu kile Tzu anaandika kuwa, you must know how to choose your battles and you must choose your battles carefully. Sio kila vita lazima upigani. Zingine ziache zipite.

Katika issue hii ya urais, you have won some battles and you have lost battles. But overall you are loosing the WAR.

Nakushauri uache sasa. Usiendelee kupigana. You are loosing the WAR!

Iache vita hii ipite Mzee.
Nadhani sio vizuri kum-discourage mtu ambaye ana ndoto na anaona inawezekena. Muache apigane. Akishinda je? Na akishindwa tume ndo itasema Lowassa umepoteza, sisi wa pembeni tumwache apigane, sio vizuri kuingilia ndoto za watu. Imagine dying without trying your dream, na hali ulikuwa na uwezo wa kuipigania? Mi nadhani mumwache aamue mwenyewe kwamba hapa nimeshindwa.
 
Back
Top Bottom