Ludovic Uttoh: Kama Kodi ni kwa maendeleo ya Nchi kwanini Wabunge hawakatwi wakati nao wanalipwa Mshahara kama wengine?

Ludovic Uttoh: Kama Kodi ni kwa maendeleo ya Nchi kwanini Wabunge hawakatwi wakati nao wanalipwa Mshahara kama wengine?

Ubinafsi uliopitiliza na ndo hao wamepitisha tozo uku wamesinzia ......
 
Huyu si ndo alikuwa CAG.

Anyways. Tufanye alisahau kuhoji mda ule.
Licha kuwataka wabunge walipe kodi kwa kila kipato wanachoingiza, pia si sahihi kwa wabunge kulipwa posho za kuhudhuria bungeni, wakati mishahara yao inalipwa kwa kazi mbalimbali, ikiwemo kuhudhuria vikao vya bunge.

Wafanyiwavyo wabunge ni sawa na kuwalipa walimu, madakari na watumishi wengine wa umma malipo ya kuhudhuria eneo lao la kazi, juu ya mishahara ya o ya kila mwezi, na Wasilipwe mafao ya kustaafu baada ya miaka mitano, bali wasubiri kufikisha miaka 60 ya lazima au 55 ya hiari kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine wa umma.
 
Si wabunge tu,hata viongozi wengine wengi hawakatwi why?
 
CAG Mstaafu, Ludovic Uttoh amesema hakuna sababu za kwanini Wabunge wa #Tanzania hawalipi Kodi licha ya kwamba wana Mishahara kama walivyo Watumishi wengine wanaokatwa Kodi.

Uttoh amesema "Siku zote msingi wa Kodi ni Usawa na wala kodi haitakiwi kuwa na Matabaka. Ikiwa tunasema tunalipa Kodi kwa maendeleo ya Nchi ni kwanini Wabunge hawakatwi?"

Akieleza zaidi, amesema hafahamu kama kuna Nchi nyingine Duniani ambayo Wabunge wake hawalipi kodi. Kwanza logic ya kufanya hivyo haipo".
Wabunge wa Tanzania ni ma PARASITE(strictly facultative)
Hayana uchungu na nchi hii zaid ya mamtumbo yao wakiongozwa na lile bichwa DAFU dukai
 
Wabunge Waanze kukatwa
Yanahubiri uzalendo huku yenyewe yakiishi kikupekupe. Upuuzi mtupu !! Yanadai hayajui vyanzo vya kodi Huku yenyewe yakilipwa bila kukatwa Kodi,chanzo kimojawapo ni kodi ya mishahara. Wanaopata vijicenti wanakatwa kodi Huku wao na mamilioni yao hawakatwi kodi. Ni aibu , aibu, aibu !!!!
 
Back
Top Bottom