Lugha asili, Makabila, Mila na Utamaduni wa Mtanzania vinafutika kwa kasi sana

Lugha asili, Makabila, Mila na Utamaduni wa Mtanzania vinafutika kwa kasi sana

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Niko kijijini kabisa huku ndanindani. Nimekuja kumzika bibi yangu aliye fariki akiwa na miaka 97 lakini akiwa bado mrembo na nguvu zake.

Kilichonuogopesha na kunishangaza, mimi wakati nakua, tulikiwa hatujui Kiswahili, tunabonga tu lugha yetu ya asili, huku tukisimuliana hadithi za Masala Kulangwa na Shing'weng'we, Kalukalanje, Ng'wanakapolo na simulizi nyingine nyingi.

Michezo yetu ilikuwa ya kiasili kabisa kutokana na mazingira yetu, mashindano ya nyimbo, kulima, kuendesha baiskeli na mitumbwi.

Shule tulivishwa bango shingoni kwa kushindwa kuongea Kiswahili. Na hata mtu asiyejua kuongea lugha ya Kibujibuji na kuongea Kiswahili pekee alioneka kama ametoka sayari ya Pluto huko.

Leo niko kijijini, watoto hawajui tena Kibujibuji, wanaongea Kiswahili, hata kanisani mahubiri sio ya kilugha tena. Hata lile bango lilioandokwa ungea Kiswahili tu tulilokuwa tukivishwa shingoni halijulikani hata lilikopotelea.

Kwa heshima na taadhima, naiomba wizara yenye dhamana ya kutunza tamaduni zetu iliangalie hili.

Sio lugha tu inayopotea inayopotea kwa kasi, ila pia vyakula vyetu, matambiko, aina ya malezi na kila kitu chetu kinapotea kwa kasi.

Tuendako tutakuja kuwa taifa lisilo na mila na tamaduni, kila kitu chetu kitapotea na tutatawaliwa kiutamaduni na mataifa makubwa
 
Culture is dynamic,


YESU NI BWANA NA MWOKOZI!
Umeshawahi kusikia habari za Ng'wanamalundi na miujiza yake?

Mi nashindwa kuwaelewa Waafrika.
Mji mtakatifu wa Waarabu uko Uarabuni Mecca and Madina, mji mtakatifu wa Wachina uko China, mji Mtakatifu wa Waroma uko Vatican Rome Italia, mji mtakatifu wa Wahindi uko hukohuko India 🇮🇳. Mji mtakatifu wa Wayahudi uko Jerusalem Uyahudini.

Inakuwaje sisi weusi hatuna miji yetu mitakatifu? Hata tukisema mji wetu mtakatifu utasikia Maka na Madina au Jerusalem, nani katuroga?

⁰Wachagga wako very determined, mji wao mtakatifu ni Moshi na kila mwisho wa mwaka huenda huko kuhiji.

Wachaga msiache kudumisha mila zenu kwa maneno ya masimango kutoka kwa watu wasio na utamaduni, wanaojiona utamaduni ulioletwa na Wazungu na Waarabu ndio utamaduni bora kuliko wa asili yao.
 
Umeshawahi kusikia habari za Ng'wanamalundi na miujiza yake?

Mi nashindwa kuwaelewa Waafrika.
Mji mtakatifu wa Waarabu uko Uarabuni Mecca and Madina, mji mtakatifu wa Wachina uko China, mji Mtakatifu wa Waroma uko Vatican Rome Italia, mji mtakatifu wa Wahindi uko hukohuko India 🇮🇳. Mji mtakatifu wa Wayahudi uko Jerusalem Uyahudini.

Inakuwaje sisi weusi hatuna miji yetu mitakatifu? Hata tukisema mji wetu mtakatifu utasikia Maka na Madina au Jerusalem, nani katuroga?

⁰Wachagga wako very determined, mji wao mtakatifu ni Moshi na kila mwisho wa mwaka huenda huko kuhiji.

Wachaga msiache kudumisha mila zenu kwa maneno ya masimango kutoka kwa watu wasio na utamaduni, wanaojiona utamaduni ulioletwa na Wazungu na Waarabu ndio utamaduni bora kuliko wa asili yao.
miss chuga na Miss Natafuta hebu njoo tuyajenge
 
Umeshawahi kusikia habari za Ng'wanamalundi na miujiza yake?

Mi nashindwa kuwaelewa Waafrika.
Mji mtakatifu wa Waarabu uko Uarabuni Mecca and Madina, mji mtakatifu wa Wachina uko China, mji Mtakatifu wa Waroma uko Vatican Rome Italia, mji mtakatifu wa Wahindi uko hukohuko India 🇮🇳. Mji mtakatifu wa Wayahudi uko Jerusalem Uyahudini.

Inakuwaje sisi weusi hatuna miji yetu mitakatifu? Hata tukisema mji wetu mtakatifu utasikia Maka na Madina au Jerusalem, nani katuroga?

⁰Wachagga wako very determined, mji wao mtakatifu ni Moshi na kila mwisho wa mwaka huenda huko kuhiji.

Wachaga msiache kudumisha mila zenu kwa maneno ya masimango kutoka kwa watu wasio na utamaduni, wanaojiona utamaduni ulioletwa na Wazungu na Waarabu ndio utamaduni bora kuliko wa asili yao.
Haika sana...in Chaga voice
 
Mkuu Bujibuji ni kweli kabisa lugha zetu za asili zinatoweka kwa kasi ya ajabu...hata December tukienda nyumbani Moshi makanisani hatuimbi tena zile nyimbo za kichaga wala mahubiri ya kichaga kila kitu ni kiswahili tofauti na zamani.
Watu wengi hawawezi ongea lugha ya nyumbani muda mrefu bila kuweka maneno mengi ya kiswahili.
 
Umeshawahi kusikia habari za Ng'wanamalundi na miujiza yake?

Mi nashindwa kuwaelewa Waafrika.
Mji mtakatifu wa Waarabu uko Uarabuni Mecca and Madina, mji mtakatifu wa Wachina uko China, mji Mtakatifu wa Waroma uko Vatican Rome Italia, mji mtakatifu wa Wahindi uko hukohuko India 🇮🇳. Mji mtakatifu wa Wayahudi uko Jerusalem Uyahudini.

Inakuwaje sisi weusi hatuna miji yetu mitakatifu? Hata tukisema mji wetu mtakatifu utasikia Maka na Madina au Jerusalem, nani katuroga?

⁰Wachagga wako very determined, mji wao mtakatifu ni Moshi na kila mwisho wa mwaka huenda huko kuhiji.

Wachaga msiache kudumisha mila zenu kwa maneno ya masimango kutoka kwa watu wasio na utamaduni, wanaojiona utamaduni ulioletwa na Wazungu na Waarabu ndio utamaduni bora kuliko wa asili yao.
At least hii ya kurudisha watoto mwisho wa mwaka kula sikukuu na wananzengo inawajengea picha ya kujua asili yao. Japo si rahisi kwa sasa kutafuta pesa na kudeal na mambo hayo lakini kwa uchache wake kizazi chetu cha kwanza kinaweza kujifunza kupitia kujifunza kwa ku-experience.
Kuna rafiki yangu kwa uraia ni mmarekani na mfaransa kwa maana ya his last generation(parents) lakini bado ana-refer zaidi ya nchi tatu za ulaya nje ya ufaransa kwa maana ya mababu na mabibi zake. Anajua walau lugha nne za asili yake
 
Mkuu Bujibuji ni kweli kabisa lugha zetu za asili zinatoweka kwa kasi ya ajabu...hata December tukienda nyumbani Moshi makanisani hatuimbi tena zile nyimbo za kichaga wala mahubiri ya kichaga kila kitu ni kiswahili tofauti na zamani.
Watu wengi hawawezi ongea lugha ya nyumbani muda mrefu bila kuweka maneno mengi ya kiswahili.
Bahati mbaya sijapata nafasi ya kuuishi utamaduni wangu, Lugha mama yangu ni kiswahili. Pamoja na hayo nimeamua mimi binafsi kujifunza utamaduni wangu (kabila) kujua asili yangu. Msukumo ulitokea baada ya kujifunza kwa wenzetu wayahudi, wahindi na baadhi ya familia zilizopo hapa Tanzania ila kwa asili ni wajerumani pamoja wako globalized lakini wanajua kila kitj kuhusu vizazi vyao 11 vilivyopita
 
Mkuu Bujibuji ni kweli kabisa lugha zetu za asili zinatoweka kwa kasi ya ajabu...hata December tukienda nyumbani Moshi makanisani hatuimbi tena zile nyimbo za kichaga wala mahubiri ya kichaga kila kitu ni kiswahili tofauti na zamani.
Watu wengi hawawezi ongea lugha ya nyumbani muda mrefu bila kuweka maneno mengi ya kiswahili.
Kuna haja ya makanisa kutenga ibada zinazoongozwa kwa lugha asilia. Mbona makanisa mengi yana ibada ya Kiingereza?
 
Kuna haja ya makanisa kutenga ibada zinazoongozwa kwa lugha asilia. Mbona makanisa mengi yana ibada ya Kiingereza?
Kabisa mkuu ....zamani walikua na utaratibu wa jumapili moja ibada kufanyika kwa kiswahili ..jumapili inayofuata ilikua kichaga ,inayofuatia tena kiswahili...hivyo hivyo inazunguka.Ila sasa hivi hamna huo utaratibu kabisa.
 
Kabisa mkuu ....zamani walikua na utaratibu wa jumapili moja ibada kufanyika kwa kiswahili ..jumapili inayofuata ilikua kichaga ,inayofuatia tena kiswahili...hivyo hivyo inazunguka.Ila sasa hivi hamna huo utaratibu kabisa.
Hata Mungu aliyeumba lugha zote pale mnarani Babeli hafurahishwi na lugha zake kuuliwa na mwanadamu kwa makusudi
 
Umeshawahi kusikia habari za Ng'wanamalundi na miujiza yake?

Mi nashindwa kuwaelewa Waafrika.
Mji mtakatifu wa Waarabu uko Uarabuni Mecca and Madina, mji mtakatifu wa Wachina uko China, mji Mtakatifu wa Waroma uko Vatican Rome Italia, mji mtakatifu wa Wahindi uko hukohuko India [emoji1128]. Mji mtakatifu wa Wayahudi uko Jerusalem Uyahudini.

Inakuwaje sisi weusi hatuna miji yetu mitakatifu? Hata tukisema mji wetu mtakatifu utasikia Maka na Madina au Jerusalem, nani katuroga?

⁰Wachagga wako very determined, mji wao mtakatifu ni Moshi na kila mwisho wa mwaka huenda huko kuhiji.

Wachaga msiache kudumisha mila zenu kwa maneno ya masimango kutoka kwa watu wasio na utamaduni, wanaojiona utamaduni ulioletwa na Wazungu na Waarabu ndio utamaduni bora kuliko wa asili yao.
Sawa, ila ninajua jambo moja kwa hakika: THE HOLY BIBLE IS A WORD OF GOD, ALMIGHTY!.

Yerusalemu ni mji wa mfalme mkuu. Israeli imetokana na jina 'Yakobo' ambaye ni mtoto wa Ibrahimu. Mungu aliamua kumchagua Ibarahimu kuwa mtu ambaye baraka zote za dunia zitapitia kwake. MWANZO 12:1--- . Mila za Kristo ndizo mila halisi alizoziamuru Mungu kupitia Neno lake lililoandikwa (Biblia).

Kweli hubaki kuwa kweli hata kama huiamini.


YESU NI MFALME WA WAFALME
 
Sawa, ila ninajua jambo moja kwa hakika: THE HOLY BIBLE IS A WORD OF GOD, ALMIGHTY!.

Yerusalemu ni mji wa mfalme mkuu. Israeli imetokana na jina 'Yakobo' ambaye ni mtoto wa Ibrahimu. Mungu aliamua kumchagua Ibarahimu kuwa mtu ambaye baraka zote za dunia zitapitia kwake. MWANZO 12:1--- . Mila za Kristo ndizo mila halisi alizoziamuru Mungu kupitia Neno lake lililoandikwa (Biblia).

Kweli hubaki kuwa kweli hata kama huiamini.


YESU NI MFALME WA WAFALME
Ukristo ulienezwa kwa namna ya ushetani. Uuaji, ubakaji ulawiti nk.
Hadi leo kanisa Katoliki limegubikwa na kashfa kibao zisizo na idadi za ulawiti wa watoto wadogo wa kiume
 
Umeshawahi kusikia habari za Ng'wanamalundi na miujiza yake?

Mi nashindwa kuwaelewa Waafrika.
Mji mtakatifu wa Waarabu uko Uarabuni Mecca and Madina, mji mtakatifu wa Wachina uko China, mji Mtakatifu wa Waroma uko Vatican Rome Italia, mji mtakatifu wa Wahindi uko hukohuko India 🇮🇳. Mji mtakatifu wa Wayahudi uko Jerusalem Uyahudini.

Inakuwaje sisi weusi hatuna miji yetu mitakatifu? Hata tukisema mji wetu mtakatifu utasikia Maka na Madina au Jerusalem, nani katuroga?

⁰Wachagga wako very determined, mji wao mtakatifu ni Moshi na kila mwisho wa mwaka huenda huko kuhiji.

Wachaga msiache kudumisha mila zenu kwa maneno ya masimango kutoka kwa watu wasio na utamaduni, wanaojiona utamaduni ulioletwa na Wazungu na Waarabu ndio utamaduni bora kuliko wa asili yao.
Mji mtakatifu wa wachaga ni moshi 😄😁😆😅😅🤣🤣😂
 
Ukristo ulienezwa kwa namna ya ushetani. Uuaji, ubakaji ulawiti nk.
Hadi leo kanisa Katoliki limegubikwa na kashfa kibao zisizo na idadi za ulawiti wa watoto wadogo wa kiume
Kutokuipenda/ kuiamini imani fulani kusikupe uhalali wa kuichafua.
Je hayo ndiyo yanayofundishwa makanisani ama ni tamaa na kukengeuka kwa hao wanaoyafanya hayo?? Hakuna dini inakosa watu watendao matendo mabaya hasa wale wanaoonekana kua ni mfano wa kuigwa, lakini hayo si yafundishwayo ni tamaa na akili zao fyatu zinawatuma kufanya hayo.

Dhambi ya watu kadhaa usiibebeshe kwa jumuiya nzima.
 
Mkuu Bujibuji ni kweli kabisa lugha zetu za asili zinatoweka kwa kasi ya ajabu...hata December tukienda nyumbani Moshi makanisani hatuimbi tena zile nyimbo za kichaga wala mahubiri ya kichaga kila kitu ni kiswahili tofauti na zamani.
Watu wengi hawawezi ongea lugha ya nyumbani muda mrefu bila kuweka maneno mengi ya kiswahili.
Hayo mambo yanaenda kizazi kwa kizazi kizazi chako cha nne kuanzia sasa sidhani kama watajua hicho kilugha chenu wote tutaongea lugha moja kiswahili
 
Back
Top Bottom