Lukuvi, mbio za sakafuni huishia ukingoni; jitafakari

Lukuvi, mbio za sakafuni huishia ukingoni; jitafakari

sammosses

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2011
Posts
1,687
Reaction score
1,111
Lukuvi ana tatizo gani na mh. Samia rais wa JMT!! Alipomtoa kwenye uwaziri alisema anataka awe mshauri wake, lakini hakufafanua mshauri wa nini, watu wakapaza sauti kuwa Mama kavunja katiba kwa kumteua, likasemwa sana likapita.

Lukuvi kagombea U-NEC nao kaangukia pua, si ajabu kwa giant kama Lukuvi, nguli wa siasa za nyanda za juu kusini kudondoka, ila kina stusha ni ghafla mno. Shida iko wapi au kuna sehemu alikosea!!!

Kubwa nalo liona wanasiasa wengi hawajui kusoma alama za nyakati, hii hugharimu sana maisha yao ya kisiasa kuishia pabaya. Hawataki kung'atuka mpaka wajumbe waonekane siyo watu wazuri!!!

Mh Lukuvi mbio za farasi huishia ukingoni, rudi kwa mzee mwenzio Mzindakaya muulize aliona nini ambacho wewe umeshindwa kukiona!! Kwa heshima uliyojijengea ni wakati sasa wa kuachia vijana wewe ubaki kuwa mshauri, mbona Mark Mwandosya kaweza wewe na timu ya kina Wassira inashindwa nini!!!
 
Mimi naona tusiishie kwa Mheshimiwa William Lukubi pekee! Isipokuwa kwa chama chote cha ccm!!

Tuachieni nchi bhana. Yaani kuanzia mwaka 1977, mpaka leo bado mnatutawala tu kinguvu!! Hata wananchi pia wamewachoka. Waachieni wengine nao tuone watakachofanya.
 
Kila nikikumbuka Bilioni 7 za royal tour na deni la taifa lilivyopaa na mnasema bila haya mtaendelea kopa.. Haki tena mtu kama Lukuvi ni wa muhimu sana kwa sasa...
emoji3.png
Hahahq
 
Lukuvi ana tatizo gani na mh. Samia rais wa JMT!! Alipomtoa kwenye uwaziri alisema anataka awe mshauri wake,lakini hakufafanua mshauri wa nini,watu wakapaza sauti kuwa Mama kavunja katiba kwa kumteua,likasemwa sana likapita...
Kwa hiyo akafukuwe Kaburi la Marehemu Mzindakaya na kumuuliza hayo??muache Marehemu Christin Mzindakaya apumzike kwa amani
 
Back
Top Bottom